Elections 2015 Kampeni CCM: Ndugai ampiga mgombea mwenzake, azimia na kukimbizwa hospitali huko Kongwa

Elections 2015 Kampeni CCM: Ndugai ampiga mgombea mwenzake, azimia na kukimbizwa hospitali huko Kongwa

1. Huyo daktari pole yake kwanza. . . . .Lakini unamrekodi mtu bila.ruhusa yake nawe huna tahadhari yeyote as if unampiga mwanao picha ya birthday??!!!
2. Unaambiwa leo utanikoma bado tu. . . . .nimecheka hapo alipokuwa akikusanya nguvu. . . . Nguvu zipi kwa mtu mzima kama yule??!!!

Anyways. . . . Sheria ichukue mkondo wake kama rushwa na cheo kitamlinda ikumbukwe kuwa "corrective measures" zimekuwepo kabla ya mahakama. . . . . . . .

Anatekeleza amri halali ya waxiri Mkuu aliyepinda aloitoa bungeni wakati ndugai akiwa naibu spika.Wapigwe tu hakuna NAMBA na akirudia apigwe tu!
 
Sheria ichukue mkondo wake haiwezekani mtu akajichukulia sheria mkononi namna hiyo
Hili linatutia doa wana CCM na tusikubali chama kuchafuliwa na watu wenye tamaa ya madaraka kama Ndugai
 
Aliyekuwa Naibu Speaker Job Ndugai amempiga Fimbo ya Kichwani Mtia nia Dkt Joseph Chilongani eneo la Kata ya Ugogoni na amekimbizwa Hospitali ya Kongwa
Mkuu wa Wilaya na Katibu wa CCM Kongwa wamekimbilia huko kumuona !!!!!!!


Hatimaye Mheshimiwa Ndugai amechimbia kaburi la kisiasa baada ya kumshambulia Mgombea mwenzake aitwae Dr Joseph Elieza Chilongani kwa gongo katika mkutano wa kuomba kupigiwa kura za maoni CCM

Hayo yametokea leo mnamo saa saa 10 jioni katika kitongoji cha ugogoni mjini Kongwa.

Katika kile kinachoonekana ni kuishiwa sera na kutumia ubabe na ukorofi ili kutetea nafasi yake ya kugombea ubunge wa Jimbo la Kongwa, Mheshimiwa Naibu Spika wa Bunge La Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Kongwa alipiga kwa gongo ambalo amekuwa akitembea nalo huku wasimamizi wa uchaguzi wakifumbua macho kitendo cha mgombea kutembea na silaha hiyo kwenye kampeni.

Inadaiwa na mtu aliyefuatilia kwa karibu tukio hilo mkutanoni kuwa Kuna mgombea mmojawapo (mkazi wa Kongwa aitwaye ngatunga) Alisimama kuuza sera zake na kudai kuwa Kongwa kuna madini jimbo halijafaidika na chochote kutoka kwa wachimbaji wa madini... Mara moja Ndugai alimtishia kuwa anyamaze la sivyo angemuonesha kazi kwa kile anachodai kuwa ni kuongea upuuzi..

Wakati wagombea hao wakiendelea kujibizana suala hilo ndipo ghafla mheshimiwa alipomuona Mmojawapo wa wagombea aitwaye Dr Joseph Chilongani ameshika simu na kutahamaki kuwa alikuwa akimrekodi kwa kuvunja taratibu.

Ndipo Job Ndugai alipoamka na kumwambia "Tena wewe nilikuwa nakutafuta siku nyingi sana, unanirekodi na makamera yako na leo utanitambua mimi ni nani."

Mara Ndugai akakusanya nguvu na kumpiga Dr Chilongani kwa fimbo hiyo. aidha hata baada ya kuanguka chini Ndugai alimfuata na kumrukia kumkanyaga tumboni akiwa na hasira na nia ovu ya kutaka kumdhuru zaidi..

Baadae wananchi walipata hasira na kutaka kumshughukilia kwa kichapo Mbunge huyo na ndipo alipopanda haraka gari lake haraka na kukimbi Eneo la Tukio..Inasadikiwa yule mgombea mwingine alijaribu kumnyanyua Dr. Pale chini, jambo ambalo baadhi ya wananchi walilichukulia ni kama kutaka kumdhuru zaidi hivyo walianza kumpa kichapo huyo mgombea mwengine kiasi hadi watu wengine walipoamulia.. Baada ya tukio hilo ovu mkutano ulivurugika.

Ndugu zake Dr. Chilongani kwa kusaidiana na watu walimbeba akiwa amezimia na kumkimbiz hospital baada y kupata PF 3 toka polisi.

Hadi reporter anaondoka hospitalini Dr alikuwa bado hajazinduka na madaktari walikuwa wanaendelea na harakati za kuokoa maisha ya mgombea huyo.

Shuhuda mmoja wa tukio anasema kuwa tukio hilo lilirekodiwa na pengine ushahidi huo utatumika katika kumuengua Ndugai katika kinyanganyiro cha ugombea ubunge kwa ticket ya CCM hasa baada ya watia wengine kuweka pingamizi mara mbili lakini bado uongozi wa chama ulikuwa unafumbia macho.

Baadhi ya wanachama wa CCM walidai kuwa kama haki itatendeka Ndugai atakuwa amejichimbia kaburi la kisiasa na kushuhudia KIAMA CHAKE RASMI KATIKA SIASA ZA JIMBO LA KONGWA..

The beginning of an end. Maskini ccm wamelewa pombe ya madaraka.
 
Alifikiri bado yuko bungeni akiwafokea na kuwakemea akina Lisu.
Unyenyekevu kwa hawa ma ccm ni ndoto. Duu huyu akikatwa huku ataibukia wapi kwa staili hii ya kutumia mgongo?

Kwa mtindo huo wa kupiga watu hakuna atakayempokea hata CCM wameshamchoka
Nadhani ipo haja ya kukinusuru chama kwa jimbo la Kongwa kwa kumuengua huyu jamaa vinginevyo wananchi watafanya maamuzi magumu
 
Msibishe jambo ambalo hata wewe pia huna uhakika nalo,
ndugu Joseph E Chilongani ni amepigwa kweli, na mpaka sasa kalazwa hosptali ya wilaya kongwa, na hali yake bado si nzuri,

kwa hali hii Ndugai inabidi achukuliwe hatua kali za kisheria kwa kitendo hicho, na asitake kuchukua madaraka kwa ubabe, kwanza wanakongwa wengi tumemchoka na ccm yake,
 
Habari wanaJF

Hali si hali kwa baadhi ya vigogo wa ccm kutetea ubunge wao hali inayosababisha haya yote tunayoyashuhudia

Nirudi kwenye mada
Kutoka jimbo la kongwa katika kampeni ya uchaguzi wa kuteuliwa kupeperusha bendera ya ccm ngazi ya ubunge uchaguzi mkuu,
mh. Job Ndugai amemshambulia kwa fimbo hadi kupoteza fahamu mgombea mwenzake katika nafasi hiyo bw. Joseph Chilangane hali hiyo ilitokea baada ya mgombea mwingine aliyekuwa mtumishi wa halmashauri akijinadi akisema nipeni nafasi hii nikaondoe ufisadi uliokithiri pale halmashauri unaoingozwa na mbunge atakayemaliza muda wake hapo october 20 Mh. Job ndugai.

Akijibu tuhuma hizo mh. Job Ndugai alisema yeye ndo mwenye uwezo tu wa kuondoa ufisadi huo na huyo anaesema atamaliza ufisadi halmashauri alikuwa mfanyakazi hapo alishindwaje kumali??

Akiwa anazungumza aligundua mgombea mwenzake bw. Joseph Chilangane anamrecord ndipo alipomgeukia na kumshambulia kwa fimbo hadi kupoteza fahamu na kukimbizwa hospitali ya wilaya ya Kongwa na kupata matibabu.


Upepo umezidi kumbadilikia mh.Job Ndugai hatua inayoonesha kupigwa chini kura za maoni maana amekuwa akizomewa kila anapopita na kufanya mkutano


Job Ndugai+Steven Wassira (Tyson)
 
CCM wana kazi mwaka uu wanaanza kuuana wenyewe. Huko Arumeru Sioi kapigana na mgombea mwenziwe John D.
 
Hivi ni kwa nini vitendo vya uvunjifu wa amani vitokee,kwani ni lazima uwe mtawala au kiongozi siku zote.Je nitakuwa sahihi kusema viongozi tulio nao wanaona ni wao tu lazima waongoze.Mh.Rais ajaye nikuombe utuletee sura mpya TOTALLY katika serkali yako,piga chini kabisa wa sasa hivi.
 
Hivi ukichokwa na wananchi hujijui? Kitendo cha kuzomewa tu kilitodha kumfanya ajiweke pembeni.. watu wana uchu wa madaraka mpaka wanageuka wanyama.. hawatufai!!!
 
Kuna msemo unaosema "nguruwe wakiingia shambani wakala na kushiba huanza kupigana bila kukumbuka kwamba shamba lina mwenyewe" Sasa wabunge wa chama tawala wamesahau kwamba nchi hii wenye nayo ni wapiga kura waliowachagua
badala yake wao wanajifanya ni wamiliki wa nchi hii.

Tujiulize hivi kweli huyu anayemjeruhi mwenzie anapigania kutumikia watanzania kweli au tumbo lake?
Hawa ndio waliotuiletea katiba pendekezwa na Sheria mpya ya mafuta na gesi wakijinadi kwamba wao ni
wazalendo baada ya wapinzani kususa michakato na kutoka.sasa watanzania tujionee wenyewe na kufanya hukumu stahiki.
 
Huyu Ndugai anapiga kampeni za kibabe
Ni vema wakamuengua mapema kwa vitendo vyake hivi vya kuhatarisha amani kwenye mikutano ya kampeni
 
Simpendi kweli ndugai nafurahi sana jinsi anavyojichimbia kabuli lake
 
Back
Top Bottom