Kampuni 3 zapigwa faini ya Tsh. Milioni 158.8 kwa kutumia vibaya Taarifa Binafsi za Wananchi

Kampuni 3 zapigwa faini ya Tsh. Milioni 158.8 kwa kutumia vibaya Taarifa Binafsi za Wananchi

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
1695754175513.png

Kampuni hizo ni pamoja na Mulla Pride Ltd, iliyopigwa faini ya Tsh. 50,404,970. Taasisi hii inamiliki 'App' za kutoa huduma za Mikopo za FairCash na KeCredit, imebainika kutumia Taarifa Binafsi za Wateja ili kudai Madeni .

Pia, kuna Klabu ya Starehe ya Casa Vera Lounge ambayo imekutwa na Kosa la Kuchapisha mtandaoni bila Idhini Picha za mteja wakati akipata burudani ndani ya Baa hiyo. Italipa faini ya Tsh. 31,344,267.

Nyingine ni Taasisi ya Elimu ya Roma iliyoko Uthiru, Nairobi ambayo imebainika kuchapisha mtandaoni bila idhini za Wazazi/Walezi, picha za Watoto. Italipa faini ya Tsh. 77,089,955.

Wakati hayo yakitokea Nchini Kenya, ni mambo yanafanyika hapa Nchini na umetambua yanakiuka Haki ya Faragha?
 
sasa hapo Wathiliwa wanafaidika na nini au wanapewa mgao ?

au Watu wanajaza matumbo yao tu ?
 
Back
Top Bottom