Kampuni nyingi za Wachina unakuta Ni share ya watu hata 500

Lazima tuwe km kenge/mijusi kwenye msafara wa mamba,.watu tunapenda "matokeo mazuri" bila kufanya kitu/jambo LA kuleta matokeo hayo mazuri ambayo kila mtu ana ndoto nayo,..uvivu,ubinafsi/umimi,roho mbaya,kutaka kuwa juu ya mwezake na mengine kama hayo yanatufanya tusipige hatua kwenda mbele....lakini wenzetu hayo kwao ni sumu,.wasomi wanaungana wanafanya "tija" kwetu ndio hivyo tena kila mtu anataka kuonekana yeye ndio kafanya, yeye ndio yeye huku nguvu kazi yenyewe moja,itawezekana vipi kufanikiwa???
 
Umeongea ukweli mtupu mkuu,.
 
Mimi pia lilinikuta kama hili,.tulipanga mipango yetu vizuri kabisaaa mpaka eneo la kufanyia biashara yetu lilipatikana ajabu mwanzoni tuu nilimuona mwenzangu ana shida hasa kwenye muda,.nikahisi pengine sababu ya familia maana ameolewa na kupata mtoto nikavumilia hilo, baadae hali ikazidi kuwa mbayaa ukimuambia leo basi tufanye hivi au njoo eneo la tukio utamsikia "ooh ujue baba jaden ana wivu sana," shenz taip nikaona ananzingua huyu mara "ooh wewe fanya tuu kwenye kugawana Ww utapata asilimia nyingi" nikaona ntapoteza muda wangu hapa ukizingatia eneo la tukio lilikuwa karibu na anapoishi yeye tofauti na mm,....aah watz sisi sio poa asee!!!!
 
Uko sahihi,sisi kinachotugharimu ni ubinafsi wa mali...
 
1. Uono wa mbali.
2. Uthubutu
3. Uvumilivu
4. Juhudi
5. Uaminifu
6. Ushirikiano

Mkikutana watu wa5 mna vyote hivyo hakika mtasonga mbele... Hamna kazi inayoingiza hela ya lelemama lazkma jasho liwatoke.. Katika kila kikundi huitaji kiongozi mathubuti kusonga mbele na kamwe ushirikiano wa wengi hauwezi kuwa nguvu sawa....
 
Wabongo kwa visingizio visivyo na kichwa wala miguu hatujambo. Nilishasema sitaki tena ushirika na mtu
 
Tatizo kubwa ninaloliona huku kwetu ni uaminifu na kujituma. Sehemu zingine duniani kuna platform zinaanzishwa ambapo mtu anakuwa na idea ya biashara au kishaanzisha biashara lakini anataka kuongeza mtaji. Anajiunga katika platform ambayo mtu yoyote anaweza kuchangia chochote alichonacho iwe 100, 200 mpaka mtaji utakapotimia. ulichochangia kinagawanywa kwenye mtaji ili kujua una umiliki wa asilimia ngapi katika kampuni. Kampuni inapopata faida mnagawana faida kutokana na asilimia uliyochangia. Njia hii ni nzuri sababu inajumuisha watu wengu hata wale wasio na uelewa wa biashara au kutotaka kujishughulisha na biashara. Ni njia fulani ya uwekezaji. Nadhani tubadilishe mentality tu na kujituma. Hakuna kinachishindikana.
 
Dah very Sad, shida yetu nini hasa? Sijui tumezaliwa na Tamaa au vipi
yaan sijui nn maana kuna mifano mingi hata katika level ya fãmilia baba anashirikiana na watoto kuendesha kampuni ila watoto wanahujumu!! sasa kama watoto wa baba mmoja mama mmoja hawawezi kufanya kazi pamoja vipi kwa marafiki??
 
USHINDI MM MKUU KUNA MMOJA NILIFANYA NAE PROJECT YA KILIMO TUKAENDA VIZURI SANA KUFIKIA HATUA YA KUVUNA AKAACHIA NJIANI NAKUNIACHA NJIA PANDA HASARA NILIYOIPATA ACHA TU
 
YAANI NDUGU YANGU KUNA MTU ALIKUWA NA MAONO YA KAMPUNI AKATUKUSANYA TUKAKAA TUKAJADILI TUKAANZA KWA KUPLEDGE SASA ALIKOTOKOMEA SIKUJUI AKAWA UKIMPIGIA HAPATIKANI MARA HOOO NASOMA SASA YAANI MPAKA ILE IDEA IKAFA NA WATU WAKAJONYOFOA MMOJAMMOJA
 
Ikiwa wachangiaji wa uzi huu wanawakilisha sehemu (sample) ya watanzania na wote mnaonekana kujua tatizo, sasa je wanaofanya hayo ni akina nani? Ni wakati wa kuacha kuipa kasumba nguvu na kuanza kufanya inavyostahiki.

Wanasema ukijiaminisha wewe ni mwizi basi utakuwa mwizi kwasababu unachokiamini kitapelekea utende hivyo na kudhihirika hivyo.
Muhimu ni je tufanyeje kutoka hapa na kubadili mtazamo na mienendo?
 
Anza na je nifanyeje? Tutumiw nafisi ya kwanza.
 
Nimekuwa na ndoto kubwa za kumiliki kampuni lakini mtaji unakuwa tatizo nikawa naunganisha nguvu kwa kutumia narafiki nikaishia kupoteza pesa nikawaunganisha classmates tukachanga pesa tatizo likajirudia lile lile mpaka nimekata na tamaa
 
Unaongelea venture capitalist mkuu.
Nikitu kizuri ingawa kina changamoto kadha ila ni stage nzuri ya kujifunza uthubutu na uvumilivu kwenye biashara.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…