Kampuni ya Australia iliyofutiwa leseni yatishia kukamata ndege ya Tanzania

Kampuni ya Australia iliyofutiwa leseni yatishia kukamata ndege ya Tanzania

Wenye akili waliliona hili mapeeeeeema Sana !! Wapumbavu hawajielewi!! Mliambiwa huwezi vunja mikataba halali uliokwisha sainiwa!?! Wakasema wapinzani wanapinga Kila kitu !!;haya Sasa twende kaziiiiii
Hao walio sign ndo majizi yenyewe
 
hopeless and stress, The Sun always heat the surface. believe me... there is something called Miracle.
 
Huo ni mchongo wa watu sampuli ya Nimrod Mkono, yanauza kesi na kula 10% kwenye fidia.., hii nchi hatujawahi kushinda kesi
 
Eti ‘Tanzania took my asset’ , kwani ukipewa leseni na ukakiuka masharti ya leseni kinachofuata ni nini kama sio kunyang’anywa?? Kwanini hata wasimpeleke Kibatala kwenye hizo kesi?
 
we kweli ni poyoyo huyo unayeamini alikuwa strong ndiyo amesababisha hayo madhila yote. Strong ktkt nini, kufokafoka? Mama ndiyo strong anaheshimu sheria siyo yule mfu wenu ametuachia haya madhila. Kwa mfano huyo unayeamini ni strong angefanya nini ndege imekamatwa nje ya nchi? Tumia akili kufikiri.
angepeleka wanasheria kwenda kushindana kwa hoja na hatimaye ndege yetu kukombolewa kama alivyofanya kipindi hicho.lakini huyu wa sasa kwa kuwa ni dhaifu atakimbilia kulipa wakati mkataba wenyewe haukuwa na faida kwa nchi ispokuwa kwa mabeberu.
 
Inaelekea uelewa wako wa Biashara za kimataifa na uwekezaji, na mikataba ya kimataifa ya uwekezaji kati ya Nchi na Nchi au baina ya makundi ya Nchi ni mdogo sana! Lakini si kosa lako, maana inawezekana hujaenda shule kiasi Cha kutosha kuelewa Haya mambo.

Si rahisi kukusomesha hapa nafasi na muda havitoshi; ila kama unaweza Google, jaribu kusoma Bileteral and Multilateral Investment Treaties. Majadiliani ya biashara na uwekezaji Duniani Huwa ni magumu sana na huwa yanachukua muda mrefu sana. (Mfano angalia Uruguay Round of negotiations au angalia ya hapa kwetu 'EU-EAC free trade and investments negotiations' ambayo kwa miaka takriban 10 hakuna makubaliano. Ni kwasababu Haya mambo yanahusu uwekezaji na Kodi baina ya Nchi na Makampuni binafsi. Yanahusu Mali!!

Na hii mikataba inayoingiwa ni kwasababu Duniani Kuna hatari nyingi za kupoteza Mali (Wealth, not only Money)Miaka ya baada ya Vita ya pili ya Dunia, hasa miaka ya 1950-1980 kuliibuka mapinduzi na Madikteta wengi Duniani; hatari ya Dikteta mmoja kuamka asubuhi na kusema 'kuanzia Leo nimetaifisha hiki au kile' iliongezeka! Nchi ilibidi ziunde makubaliano ya kimataifa ya kisheria ya kulinda uwekezaji dhidi ya hatari ya Madikteta, au Vita, au Machafuko ya kisiasa. Uruguay round ni maarufu sana kwenye hili eneo. Ndio maana Kuna WTO, UNCTAD, IATA, nk. Mengine ni ya Nchi na Mengine ni ya Industry! Na Nchi zilijiunga kwa hiyari, bila kulazimishwa, kwasababu ilikuwa ndio njia ya kuaminiwa na Nchi nyingine, na Makampuni ya kimataifa: kwamba wote tutafuata tulichokubaliana, hatutakuwa wakurupukaji na kufanya mambo ya ajabu yasiyo ya kistaarabu! Makampuni yakienda kukopa Mabilioni mabenki makubwa Duniani wanaangalia: Hawa wanenda kuwekeza North Korea au Sweden? Kama North Korea wanakutolea nje; kwani Dikteta wa North Korea anaweza kufanya ujuha siku yoyote pesa zikapotea zote!

Kwa hiyo hakuna mchawi wala wahuni, ni mambo yetu tuu! Nafasi haitoshi, lakini tafuta kitabu kinaitwa 'Introduction to International Trade and Investments' na kingine kinaitwa "Introduction to International Business'. Tahadhari: vitabu hivi vina kurasa karibu 500 Kila kimoja, kwa hiyo usiwe mvivu kusoma. Hata Mwaka wa kwanza chuo Kikuu hawakisomi chote, wanapewa chapters zile muhimu zaidi. Hata hivyo, hakikisha unasoma Chapter ya kwanza 'Introduction' kwasababu itakupa muongozo.mzuri wa kuelewa mambo kabla hujachagua chapters nyingine unazozipenda zaidi, hasa zile zinazoongelea mikataba ya kimataifa ya uwekezaji.
Karibu!
Umetoa somo zuri sana Kwa wale wachangiaji wenye mihemko na hawajui lolote kuhusu biashara na mikataba. Jifunzeni mambo na siyo unachangia mada Kwa kujaza punda. Hongera sana Kwa maelezo Yako.
 
Eti ‘Tanzania took my asset’ , kwani ukipewa leseni na ukakiuka masharti ya leseni kinachofuata ni nini kama sio kunyang’anywa?? Kwanini hata wasimpeleke Kibatala kwenye hizo kesi?
Sio umahiri wa mwanasheria; swala ni je, taratibu zilizopo kwenye mikataba zilifuatwa! ? Yaani wengi hapa wangejua Haya makampuni yanavyohangaika huko kwao kupata mtaji, na jinsi wanavyohangaika huku kwetu kwenda porini kufanya utafiti na kutafuta madini(exploration) wasinge comment kirahisi hivi!

Hii kampuni wapo huko porini Nachingwea tangu mwaka 2007. Wametoboa mashimo kwa mamia ardhini wakitafuta madini. Sampo wamehangaika Nazo mpaka wamefika mahali wameona madini. Haya mambo yote yana taratibu zake na deadline zake zilizowekwa na Serikali. Ghafla tu Mwaka 2017 Serikali hiyo hiyo inawanyang'anya bila kufuata mikataba iliyopo. Bila kujali kuwa wametumia zaidi ya Bil 120 miaka yoote hiyo!! Wakishtaki kwenye koti za kimataifa ambazo tumejiunga kama Nchi Ili kuvutia uwekezaji, tunaanza kuongea hovyo: ooh mabeberu, wahuni, wasaliti!!! Hata waTanzania wenzetu wakionya, wakitahadharisha, wakitoa maoni Yao tunawaona ni wasaliti wanaowasaidia mabeberu!!!
 
Sio umahiri wa mwanasheria; swala ni je, taratibu zilizopo kwenye mikataba zilifuatwa! ? Yaani wengi hapa wangejua Haya makampuni yanavyohangaika huko kwao kupata mtaji, na jinsi wanavyohangaika huku kwetu kwenda porini kufanya utafiti na kutafuta madini(exploration) wasinge comment kirahisi hivi!

Hii kampuni wapo huko porini Nachingwea tangu mwaka 2007. Wametoboa mashimo kwa mamia ardhini wakitafuta madini. Sampo wamehangaika Nazo mpaka wamefika mahali wameona madini. Haya mambo yote yana taratibu zake na deadline zake zilizowekwa na Serikali. Ghafla tu Mwaka 2017 Serikali hiyo hiyo inawanyang'anya bila kufuata mikataba iliyopo. Bila kujali kuwa wametumia zaidi ya Bil 120 miaka yoote hiyo!! Wakishtaki kwenye koti za kimataifa ambazo tumejiunga kama Nchi Ili kuvutia uwekezaji, tunaanza kuongea hovyo: ooh mabeberu, wahuni, wasaliti!!! Hata waTanzania wenzetu wakionya, wakitahadharisha, wakitoa maoni Yao tunawaona ni wasaliti wanaowasaidia mabeberu!!!
Jiulize, hicho kitalu cha madini nani anakimiliki kwa sasa? Serikali? Kama ni serikali kwanini hawamrudishii na JPM keshaondoka..., tafakari kwanza
 
Zimeibuka lini? Usijitoe ufahamu mzee walikamata south na Canada huko enzi za Magu
Tena kama ameshahu, wakati wa Magu lilikamatwa mpaka jengo la Tanzania huko Washington, wakawahi kulipa deni kinya kimya. Yakaisha.

Dawa ya madeni ni kulipa tu.
 
Serikali ilivirudisha vitalu vyote na kuvitangaza upya kwa wawekezaji wapya!!
Huyo mwekezaji mpya ni nani?, fuatilia, utakuta ni huyo huyo anaetushtaki ila kwa kutumia jina jipya, hii ni michezo tu tunachezewa.., wewe unaweza kwenda kupora gari halafu umpe tu mtu mwingine, hivi hivi tu? For no reason?!
 
Wakili ni lazima aajiriwe kuifanya hiyo kazi, hajiamulii tu kisa ni wakili. Atamuwakilisha nani? Serikali iliyofujwa haishughuliki, wananchi hawajitambui.
Kaka serikali haina wanasheria wake?
 
Kaka serikali haina wanasheria wake?
Inao chini ya mwanasheria mkuu wa Serikali. Ila wataingia pua wakati wanajua hawashindi. Nina imani wanajadiliana chini kwa chini, kwani ni aibu!
 
Huyo mwekezaji mpya ni nani?, fuatilia, utakuta ni huyo huyo anaetushtaki ila kwa kutumia jina jipya, hii ni michezo tu tunachezewa.., wewe unaweza kwenda kupora gari halafu umpe tu mtu mwingine, hivi hivi tu? For no reason?!
Surprise surprise!
 
Back
Top Bottom