Tetesi: Kampuni ya Indiana Mining imesema haitasita kukamata ndege za Tanzania kama haitalipwa madai yao

 
Mwisho ni Bora Serikali ikaenda Bungeni na kueleza Umma kesi zote za Nje inazodaiwa, inazodai na inazoendelea na mashauri Ili Watanzania wajue maana Sasa imekuwa too much..[emoji1752][emoji1548][emoji817][emoji818]
 
Wameshaaona tz ni mteremko na aina ya Raisi tuliyenaye
 
Hii ndio kazi ya Tundu Lissu huko ughaibuni siku zote.
 
Hii kesi ni kutokana na uamuzi wa ajabu uliofanywa na awamu ya 5 wa kufuta retention licenses zote na kisha kuwapora wawekezaji huku wakiqa wamekwishatumia mabilioni ya pesa kufanya utafiti.

Lilikuwa ni kosa la wazi kabisa. Sheria ilikuwa inazitambua retention licenses, waliomba wakapewa, halafu mtu akalala na kuamka na kisha kutangaza kuwa kuanzia leo hakuna retention licenses, na wote waliokuwa wanamiliki retention licenses hawana chao!! Ilishangaza sana.


Hii nchi wanaoididimiza ni watawala.
 
Well Noted Mkuu.....
 

Hamna cha kuwalipa hao mabeberu kanzu, maana wakati mkataba umeamdikwa hao wachukuwe 97% na Tanzania [emoji1241] ipate 3% only walifurahi na kujiona wajanja wa gololi kwa almasi, hahaha [emoji2957] imekula kwao sasa, haki ni ya Mwenye Enzi Mungu walahi
Ndege zenyewe hatuja maliza mkopo kwa hiyo bado hazijakuwa za kwetu, uwiii watalamba mchanga kwa kweli!
 
Unazungumza vitu ambavyo huna hata uelewa navyo. Shida ya watanzania kujifanya wajuaji hata kwenye mambo ambayo wanauelewa zero.

Kwanza hao hawakuwahi kuwa na mkataba na Serikali. Waliwekeza kwa kutumia sheria zilizipo.

Ni sawa muwe na sheria leo inayosema kwamba ukitaka kuanzisha kiwanda cha nguo Tanzania unatakiwa ufanye yafuatayo. Wewe ukayafanya yote, ukapewa leseni. Ukaanza kazi.

Halafu akatokea kiongozi mmoja kichaa akasema tusiwe na leseni za viwanda vya nguo, tuwe na leseni moja tu itakayoitwa leseni ya viwanda. Halafu akatangaza kuwa kuanzia leo Tanzania haitakuwa na viwanda vya nguo badala yake kutakywa na keseni moja tu kwa viwanda vyote, itakuwa ni leseni ya viwanda. Vike viwanda vyote vya nguo vinavyofanya kazi, kwa sababu vyenyewe vina leseni ya viwanda vya nguo, na nchi haina leseni tena za viwanda vya nguo, hivyo viwanda vyenye leseni zilizotolewa zamani, leseni za viwanda vya nguo, hazitambuliki tena, na chochote walichofanya, na mitambo yao itakuwa mali ya serikali.

Ndiyo ujinga uliofanywa na awamu ya 5. Unafuta leseni za retention kwenye mfumo wa leseni, na mfumo huo uliweka mwenyewe, mwekezaji aliomba ukampa, halafu baadaye unasema kuwa hakutakywa na leseni za retention, halafu huwaambii wale waliokuwa na retention licenses wafanye nini, huo si wehu kabisa?

Umakini wa watawala nchi hii ni janga kubwa. Ndiyo maana ni muhimu kuwa na katiba mpya. Katiba hii inayotoa mamlaka makubwa kwa Rais, mkiwa na Rais mwenye upeo mdogo na ambaye hatoi nafasi ya kushauriwa, Taifa linaangamia.

Lilikuwa jambo dogo sana kama Rais angekuwa na uelewa na halafu akaamua kutumia hekima. Ilistahiki kuwaambua hao wawekezaji kuwa leseni za mwanzo zimefutwa kwenye mfumo wa sasa, na hivyo wazibadilishe hizo retention licenses kuwa Mining Licenses (ML au SML). Hakungekuwa na kesi wala habari ya kumlipa yeyote.
 
Hii nchi si tuliaminishwa kwamba sisi matajiri sasa haya madeni deni tena nduguzangu yanatoka wapi? au ni njama za hao mabeberu?
 
Kweli ng’ombe wa maskini hazai.
 
Yote haya yanatokana na kuwa na serikali dhaifu ya awamu hii.vitajitokeza vikampuni uchwara kuiyumbisha serikali.Na kwa kuwa machawa wa mama wamejikita kuelekeza lawama kwa magufuli na syo weledi,vikampuni hivi vitatupiga sana.
 
Hivi hii nchi haina snipers! Maadui wote hawa wanaofungua kesi za kuidhulumu nchi maskini walitakiwa wawe wamepelekwa 'resting room'...
Kama watu wasipoishi kwa kukupenda, inabidi waishi kwa kukuogopa.
Hii principle imemsaidia sana North Korea..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…