Tetesi: Kampuni ya Indiana Mining imesema haitasita kukamata ndege za Tanzania kama haitalipwa madai yao

Tetesi: Kampuni ya Indiana Mining imesema haitasita kukamata ndege za Tanzania kama haitalipwa madai yao

Hii kesi ni kutokana na uamuzi wa ajabu uliofanywa na awamu ya 5 wa kufuta retention licenses zote na kisha kuwapora wawekezaji huku wakiqa wamekwishatumia mabilioni ya pesa kufanya utafiti.

Lilikuwa ni kosa la wazi kabisa. Sheria ilikuwa inazitambua retention licenses, waliomba wakapewa, halafu mtu akalala na kuamka na kisha kutangaza kuwa kuanzia leo hakuna retention licenses, na wote waliokuwa wanamiliki retention licenses hawana chao!! Ilishangaza sana.


Hii nchi wanaoididimiza ni watawala.
Mabadiliko yoyote ya Sheria huwa na tathmini ya athari na gharama(hasi na chanya) zake kwa taifa.

Inasikitisha sana namna nchi tunavyopata hasara kwa maamuzi yetu wenyewe. Hii sijui ni fidia ya ngapi tutalipa na wanaoumia ni wananchi kutwishwa mzigo mkubwa wa kodi na tozo. Kwa kweli halikubaliki
 
Wewe hujui chochote kwenye hii sekta. Ni aheri ungekaa kimya, usome michango ya wenye kuelewa ili uelimike.

Unatakiwa ufahamu kuwa kila leseni ya madini ina muda wake:

PL ni miaka 4
RL ni miaka 4

Hiyo kampuni ilikuwa na RL. Hii ni leseni ambayo hutolewa kwa kampuni ambayo ilikuwa na PL, halafu kukawa na mazingira ambayo hayaiwezeshi hiyo kampuni kuanza uchimbaji. Hivyo kipindi cha RL huwa hakuna kazi yoyote, labda kipindi hicho kampuni inatafuta mtaji wa kwenda kwenye ML au SML.

Na baada ya miaka 4, RL inakuwa imemaliza muda wake. Na muda ukiisha, mmiliki wa RL haruhusiwi kuongeza muda wa RL wala kurudi tena kwenye PL. Option aliyo nayo ni kwenda kwenye uchimbaji kwa kuomba ML au SML, kwa kutegemea ukubwa wa mtaji.

Kampuni hiyo, wakati RL zinafutwa, ilikuwa imebakiza miezi 8 tu. Kama tungekuwa na kiongozi mwenye busara, angesubiri miezi 8 tu. Hao wangekuwa na option au ya kuomba ML au SML, au kuamua kuachia. Na kama wangeomba ML au SML, ni lazima.ndani ya miezi 36, sheria inawataka waanze kujenga mgodi.

Papara na kukurupuka ndiko kumeliingiza Taifa kwenye hasara ambayo ingeweza kuepukika kiurahisi kabisa.

Baada ya hayo makosa, marehemu alipogundua kpsa walilofanya, waliamua kuwasiliana na wamiliki wote wa RL, na kuwataarifu kuwa maeneo yamerudishwa, wamiliki wa RL waombe ML au SML kwenye maeneo yale yale ambayo yalikuwa na RL, lakini kwa bahati mbaya baadhi ya makampuni, ikiwemo hii ya Indiana, yaligoma kurudi, na kuamua kuendelea na madai yao mahakamani.

Kwa hiyo, marehemu mwenyewe, aligundua kuwa walikuwa wamekurupuka.
Mkuu hao wengine waliogoma wako wangapi, je wemefungua pia kesi za madai?
 
Unazungumza vitu ambavyo huna hata uelewa navyo. Shida ya watanzania kujifanya wajuaji hata kwenye mambo ambayo wanauelewa zero.

Kwanza hao hawakuwahi kuwa na mkataba na Serikali. Waliwekeza kwa kutumia sheria zilizipo.

Ni sawa muwe na sheria leo inayosema kwamba ukitaka kuanzisha kiwanda cha nguo Tanzania unatakiwa ufanye yafuatayo. Wewe ukayafanya yote, ukapewa leseni. Ukaanza kazi.

Halafu akatokea kiongozi mmoja kichaa akasema tusiwe na leseni za viwanda vya nguo, tuwe na leseni moja tu itakayoitwa leseni ya viwanda. Halafu akatangaza kuwa kuanzia leo Tanzania haitakuwa na viwanda vya nguo badala yake kutakywa na keseni moja tu kwa viwanda vyote, itakuwa ni leseni ya viwanda. Vike viwanda vyote vya nguo vinavyofanya kazi, kwa sababu vyenyewe vina leseni ya viwanda vya nguo, na nchi haina leseni tena za viwanda vya nguo, hivyo viwanda vyenye leseni zilizotolewa zamani, leseni za viwanda vya nguo, hazitambuliki tena, na chochote walichofanya, na mitambo yao itakuwa mali ya serikali.

Ndiyo ujinga uliofanywa na awamu ya 5. Unafuta leseni za retention kwenye mfumo wa leseni, na mfumo huo uliweka mwenyewe, mwekezaji aliomba ukampa, halafu baadaye unasema kuwa hakutakywa na leseni za retention, halafu huwaambii wale waliokuwa na retention licenses wafanye nini, huo si wehu kabisa?

Umakini wa watawala nchi hii ni janga kubwa. Ndiyo maana ni muhimu kuwa na katiba mpya. Katiba hii inayotoa mamlaka makubwa kwa Rais, mkiwa na Rais mwenye upeo mdogo na ambaye hatoi nafasi ya kushauriwa, Taifa linaangamia.

Lilikuwa jambo dogo sana kama Rais angekuwa na uelewa na halafu akaamua kutumia hekima. Ilistahiki kuwaambua hao wawekezaji kuwa leseni za mwanzo zimefutwa kwenye mfumo wa sasa, na hivyo wazibadilishe hizo retention licenses kuwa Mining Licenses (ML au SML). Hakungekuwa na kesi wala habari ya kumlipa yeyote.
Hakika nimekuelewa kwa asilimia 100. Tatizo la bwana yule alikuwa jack of all trades, in short baba haambiliki. Mr know all. Sasa kuna wapuuzi watakuja kusema sijui kuna madalali ina maana hao waliopata hasara kwa upuuzi wa bwana yule wasidai pesa zao ? Je wasiweke madalali kufuatilia fidia zao?

The international law on investments ipo wazi sana, if unataka kufanya appropriation ya mali za investor basi lazima ufanye prompt/compensation, failure to which may result into payment of damages and other costs accruing from the same act of appropriation.

Hapa swali la msingi ni kujiuluza kwamba ukiacha huyo aliyetangulia kwenye haki je hawa waliobaki ambao walishauri akina Kabudi na wenzie bado wapo tu? Kwa nini hawawajibishwi kwa kutoa ushauri mbovu namna ile na kuliingiza taifa hasara kubwa namna hii?
 
Back
Top Bottom