Kampuni ya Maziwa ya unga ya Cowbell Matatani

Kwahiyo ndugu yangu wewe hapo ungepokea mlungula, bila kujali maziwa haya yangeumiza watanzania wenzako!?

Naanza kuamini ni sisi kweli, tuliowauza ndg zetu utumwani...

🙂 Huenda hata Yuda alikuwa Mwenye asili yetu.
Nakubaliana na kauli hii: Kazi ya kuongoza watu ni ngumu sana.
Nakumbuka ilishatokea China maziwa ya watoto kuongezwa vitamins fake. Watoto kadhaa walikufa.
Mmiliki wa kiwanda aliuawa kwa kupigwa risasi. Hujuma iligunduliwa kwa wenzetu wa magharibi. Wale wako serious na afya za watu.
 
Inaonekana soko gumu, walaji wachache. Mimi binafsi sijawahi kuyatumia wala kufikiria kuyatumia.
Unaposema ujawai kuyatumia unamaanisha toka umezaliwa au maana naamini 90% yetu tumewai kuyatumia tulivyokuwa watoto.
 
Kazi zuri sana wakaguzi. Tafadhali kagueni na Karanga za kukaanga pamojana korosho madukani. Nyingi zimeoza. Ole wako ununue mida ya usiku, utaharisha mpaka ukome.
 
Hata ufanye vipi, gari lako haliwezi kuwa perfect the same to premises
 
Kazi zuri sana wakaguzi. Tafadhali kagueni na Karanga za kukaanga pamojana korosho madukani. Nyingi zimeoza. Ole wako ununue mida ya usiku, utaharisha mpaka ukome.
Tena karanga zile za kwenye rollers usipojiangalia utaugua kabisa TB, maana watu wanapuliza kwa mdomo kabla ya kuweka karanga.
 
Hivi viwanda vinauza maziwa bei juu sana wakati maziwa yanaribika mtaani
 
Tume kula sumu sana, ndio maana mara kisukari mara pressure kaaaaa.
 
Halafu Mimi ni mteja mzuri wa haya makitu! Haki nimejisikia vibaya!
 
By the way wafanyabiashara na makampuni mengi yanayoagiza bidhaa za chakula kama chocolate, biscuit , cornflakes, cereals n.k. huo ndio mchezo wao. Wengine wana mpaka machines za ku-repack and labelling.
 
Mkuu wewe hujui chochote au unakwepa kuuona uhalisia. Nambie chanzo cha mapato cha TFDA, NEMC, TBS mpaka wawe na mapato makubwa sana ??
Kale kaofisi ka bodi ya maziwa pale Regents estate kadogo, kachafu , halafu jamaa wana njaa ile mbaya. Bila kamata kamata hakuna pesa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…