Kampuni za Yasser Provison Store na Zenj General zilizohusishwa kashfa ya Sukari na Waziri Bashe zinamilikiwa na nani

Kampuni za Yasser Provison Store na Zenj General zilizohusishwa kashfa ya Sukari na Waziri Bashe zinamilikiwa na nani

Hivi aliyetunga sheria ya kuwapa wazalishaji wa viwanda vya sukari haki ya kuagiza na kusambaza sukari kutoka nje aliwaza nini? Wapi check and balance? Hawa si watakuwa wanajiamulia kila kitu kwenye sekta ya sukari?
 
Wa-Asia wataimaliza hii nchi
Wanaoimaliza ni viongozi wetu wenyewe wenye tamaa za mali, wasiojali kuhusu tanzania, wasikuwa na uzalendo. Hao wa asia tutawaonea bure, kwani mtu akikuletea jambo la hovyo ambalo litaumiza wananchi kuna ulazima ukubali, kwani waziri alishikiwa bunduki.

Viongozi wengi nchi hii ni wapigaji nao ndio sababu kuu nchi hii kutokusonga mbele, hajali maslahi ya taifa ye muhimu apige tu
 
Issue imetokea ni dharura tusubiri mpaka bunge likae ni lini meanwhile kuna bodi ya sukari na vyombo husika .. Luhanga mpina anatumiwa na wale watu saba ambao wanataka ku control soko la sukari na kuumiza watanzania.. kwa ufupi mnaopinga bashe mna maslahi yenu binafsi na mlitaka sukari ifike hadi elfu 20 kwa kilo. FICHA UJINGA WAKO
Emergency ina procedure zake,hivi umesoma Ushahidi uliotolewa mwanzo mwisho,si upo hapa jukwaani?,
Au unajizimia data?
 
Emergency ina procedure zake,hivi umesoma Ushahidi uliotolewa mwanzo mwisho,si upo hapa jukwaani?,
Au unajizimia data?
Achana na Ile rubbish .. ipo kwa maslahi ya watu Saba tu , nimeuliza swali simple sukari walileta au hawakuleta.. na kama walileta bei ilishuka au haikushuka
 
Zanzibar wasipokuwa develiped country katika hiki kipindi cha Samia. Hawataweza tena
 
Kuna Kashfa kubwa ya Kampuni 4 ambazo zimepewa vibali vya kuagiza sukari huku zikiwa hazina sifa wala uzoefu wa biashara ya Sukari Je ni nani wamiliki wa makampuni haya yenye nguvu kubwa hadi Waziri Bashe akaruhusu wapewe vibali vya kuagiza Tani 410,000 za sukari nje ya nchi?

Kampuni hizo zinazotajwa ni

1. ITEL EAST AFRICA LIMITED ambayo 49% ya hisa zake zinamilikiwa na raia wa India (DAR ES SALAAM)
2. Kampuni ya J SQUARE INVESTMENT GROUP COMPANY LIMITED (DAR ES SALAAM)
3 Kampuni ya Yasser Provision Store (ZANZIBAR)
4 Kampuni ya ZENJ GENERAL MERCHANDISE COMPANY LIMITED(ZANZIBAR)
Mmiliki
 
Mimi bado namshangaa mteule wa Bashe kwa nini bado Bashe anaendelea kuwa Waziri wa Kilimo. Ripoti hii inatisha sana. Kampuni ya stationery, Kampuni ambayo kisheria ya Brela hairuhusiwi kufanya biashara na Serikali, Kampuni toka Zanzibar kuruka kuja Tanzania Bara kupewa vibali. Hii inatisha sana.
Mkuu kuna mambo hapa Bongo mpaka unajiuliza hivi hawa watu hawana hata uchungu na huu umasikini uliokithiri mitaani? Inasikitisha sana
 
3.3.4 Kampuni ya ZENJ GENERAL MERCHANDISE COMPANY LIMITED

Kampuni hii ilipewa kibali No. SR No. 3925349484 cha kuingiza sukari nchini tani 60,000 tarehe 30 Aprili 2024 (Kiambatisho 24)

Baada ya kufanya upekuzi wa BRELA (Kiambatisho Na. 25) tarehe 10 Juni 2024 ilibainika yafuatayo:-

Kampuni hii haijawasilisha BRELA Financial Statements tangu mwaka 2016 hadi 2023 miaka 8 sasa. Kiufupi kampuni hili haliko hai na haliwezi kufanya biashara na Serikali.

Kampuni hii imesajiliwa Zanzibar lakini haijahuisha taarifa zake katika Mfumo wa Online Registration System (ORS) wa BRELA.

Kampuni hii imepewa vibali zaidi ya viwanda vyote 5 vinavyozalisha sukari nchini ambavyo vilipewa tani 10,000 kila kiwanda. Lakini pia uwezo wa kifedha wa kampuni hii ni wa kutilia mashaka kupewa kazi ya zaidi ya Bilioni 160.

Hii kampuni ina mkono ya mbunge wa Mpendae.
 
Kuna Kashfa kubwa ya Kampuni 4 ambazo zimepewa vibali vya kuagiza sukari huku zikiwa hazina sifa wala uzoefu wa biashara ya Sukari Je ni nani wamiliki wa makampuni haya yenye nguvu kubwa hadi Waziri Bashe akaruhusu wapewe vibali vya kuagiza Tani 410,000 za sukari nje ya nchi?

Kampuni hizo zinazotajwa ni

1. ITEL EAST AFRICA LIMITED ambayo 49% ya hisa zake zinamilikiwa na raia wa India (DAR ES SALAAM)
2. Kampuni ya J SQUARE INVESTMENT GROUP COMPANY LIMITED (DAR ES SALAAM)
3 Kampuni ya Yasser Provision Store (ZANZIBAR)
4 Kampuni ya ZENJ GENERAL MERCHANDISE COMPANY LIMITED(ZANZIBAR)
nasikia wamo wabunge na vigogo wengine wakubwa ndani ya chama
 
Back
Top Bottom