3.3.4 Kampuni ya ZENJ GENERAL MERCHANDISE COMPANY LIMITED
Kampuni hii ilipewa kibali No. SR No. 3925349484 cha kuingiza sukari nchini tani 60,000 tarehe 30 Aprili 2024 (Kiambatisho 24)
Baada ya kufanya upekuzi wa BRELA (Kiambatisho Na. 25) tarehe 10 Juni 2024 ilibainika yafuatayo:-
Kampuni hii haijawasilisha BRELA Financial Statements tangu mwaka 2016 hadi 2023 miaka 8 sasa. Kiufupi kampuni hili haliko hai na haliwezi kufanya biashara na Serikali.
Kampuni hii imesajiliwa Zanzibar lakini haijahuisha taarifa zake katika Mfumo wa Online Registration System (ORS) wa BRELA.
Kampuni hii imepewa vibali zaidi ya viwanda vyote 5 vinavyozalisha sukari nchini ambavyo vilipewa tani 10,000 kila kiwanda. Lakini pia uwezo wa kifedha wa kampuni hii ni wa kutilia mashaka kupewa kazi ya zaidi ya Bilioni 160.