Zanzibar 2020 Kamwe Joni hawezi Kusafiri na Hussein kwenda nae Zanzibar, ila atasafiri na Makame ambaye si tu amemzoea bali pia anammudu sana

Zanzibar 2020 Kamwe Joni hawezi Kusafiri na Hussein kwenda nae Zanzibar, ila atasafiri na Makame ambaye si tu amemzoea bali pia anammudu sana

Makame ni Chaguo sahihi kwa Zanzibar atavunja Usultani na hoja ya " Uunguja " atajenga Mahusiano mapya baina ya hivyo Visiwa viwili.

Hata Mimi natamani sana huyu ndiyo awe Rais wa huko Isles Ndugu, kwani anaonekana kuwa na Faida nyingi za Kiutendaji kuliko kwa Hussein.
 
halafu utamu zaidi hawa wote hawajawahi kuhudumu kabisa kwa ukamilifu katika SMZ

Huyu Makame ndo hata jimbo alishindwa kulipata kule kwao ni Ngangari tupu. Labda akaanzie na uwakilishi kwanza

ila siasa za mwaka 2020 zitakua na mengi mapya kama tuliyoyashuhudia yakitokea miaka hii 5 yote. Yale yasiyowezekana yamewezeshwa kuwezekana. Tunapata new "NORMALS"
Ila makame mbarawa ni mtu makini sana,anafit hata kuwa rais wa jamhuri ya muungano
 
Kwa kura CCM hamufui dafu ila kwa kuiba hakuna anae washinda. Kwa vile ni watu wasiokuwa na haya wala hawaoni vibaya, wataiba kura za wazanzibari wampe mtu karubandike ambae hatakiwi. Yote ni kuua zanzibar isiweze kuwa na maandeleo. Nchi yetu imeuliwa na CCM kiasi kwamba hamna hata cha kuringia ukasema hiki ni cha wazanzibari.
 
Sasa kama Taarab zangu zinakukwaza si uache tu Kuzisikiliza? au kuna Mtu amekushikia Jiwe Kubwa la FATUMA na Kukulazimisha uzisikilize?
Pole sna Nina Iman una hekima nzuri...
 
Kuna Mzee Mmoja ( Jina Kapuni ) japo alishawahi Kuniongoza Kikatiba huko nyuma taratibu sasa naanza kuona jinsi ambavyo huenda Ugonjwa wa Moyo utakavyoanza Kumuathiri na pengine hata Israeli anaweza Kuamua Kuondoka nae mapema tu kwenda katika Mapumziko yake ya Milele.

Sababu kubwa ni kwamba kama kuna Mzee ambaye si tu alikuwa anajikomba bali bado pia anajikomba kwa Joni huku akijiaminisha kabisa kuwa iwe isiwe Mwanae Mpendwa aliyeyazoea Maisha ya kuishi na Wanajeshi kwa miaka mingi atakuja nae Kuirithi Kazi yake huko kwa Waunguja na Wapemba ila kwa upepo unavyoenda sasa Mwanae huyo hiyo Kazi ataisikia tu katika Bomba.

Si tu kwamba Joni hataki Kuongozana na Hussein katika Safari yake ya kwenda Kisiwani Zanzibar ila anaogopa kuwa huenda huko mbeleni akaja Kumsumbua hasa ukizingatia Hussein kaanza kuwa katika Mfumo kabla yake na ana Mtandao mkubwa ulioratibiwa vyema na Baba yake alipokuwa Kazini hivyo anaona bora tu asafiri na Makame ambaye amemzoea na anammudu vilivyo kabisa.

Na kinachosikitisha na hata kutia Huruma kabisa ni kuwa tayari Hussein alishaanza Kuuvaa uhusika wa hiyo Kazi anayoenda Kuikosa na Kuijutia.
Baba na mwana... Chama na mtandao
 
Hiyo April Fool's day was just a coincidence, hizo hoja ni valid na bado namtafuta Polepole.
P

Si yupo pale lumumba mkuu..!? Au kwani ni lazima uende kwake? Mbona wengine hivyo vipeperushi wanavichukulia mashinani au ndio unataka kiki..!??

...lakini ujiandae kushikiwa akili na kuanza kuongozwa na remote!
 
CCM ya sasa haina mazoea... Atakuja mtu hajapatwa kuandikwa popote kwa jina lake...
 
Jifunze Kuheshimu Mawazo na hata Uwasilishaji wa Members wengine hapa Mtandaoni JamiiForums na acha Kujifanya kuwa Wewe ndiye Einstein au Brainiac wa Jamvi hili zima wakati Kiuhalisia Ukweli siyo huo na hauko hivyo na huenda pia hutobahatika kuwa hivyo. Unaposema Bandiko hili limejaa Hoja za Uwongo Wewe zako ziko wapi na Wewe ni nani mpaka uwe na uwezo wa Kuzithibitsha?

Acha kutaka Kuaminisha na Kuwaaminisha Watu ( Members ) hapa kuwa kile ambacho Wewe huwa unakiwakilisha hapa basi ndiyo Genuine katika katika Facts zake na kwamba Watu wengine wote hawana uwezo wa ama Kukuzidi au kwenda an extra mile na Mtazamo wako. Sijaanza Kukusoma leo japo huwa sishawishiki Kuchangia katika Mada zako kwakuwa huwa sioni kipya zaidi ya blah blah zako na Kujikweza Kwako Kwingi.

Mwisho kabisa hukuwa na haja ya Kuchangia halafu kuniwekea Mada zako na sijui ni kwanini umekuwa na hii tabia ambayo sioni haya ( aibu ) kuiita ya Kishamba. Kama unapenda Mada zako ziwe zinasomwa na uwe unasomwa sana ili Umaarufu wako unaoutaka hapa JamiiForums uzidi nakushauri omba kwa Uongozi wa JamiiForums uwe na Jukwaa lako liitwalo JF Pascal Mayalla Threads Only ili uridhike kwani Unaboa mno tu.

Nimemaliza.
Duh!
 
Mkuu Freddie, huyu kilaza aliyeleta bandiko hili with no facts, hawezi kuupenda mchango wako huu full of facts!.
Anajenga hoja kwa uongo na uzushi, eti Joni ni muoga na anawaogopa watu?, hadi amuogope mtu fulani ambaye yeye ndie amemteua na kumtegemea kumpitisha kwenye vikao vya maamuzi!. Tangu lini Joni ni muoga labda awe ameanza leo!.

P
Mkuu Paskali,
Kuna watu hawamkumbuki Joni akiwa askari wa mwamvuli enzi za BWM. Either hawakuwepo kwenye ulimwengu wa siasa hivyo hawajui na wamekuwa wavivu kusoma historia au kuuliza kwa "waliokuwepo" walau kuwadodosa.

So, far Joni bana, ni mtu mwingine. Sijawahi sikia balozi/kaimu balozi wa taifa kubwa anaitwa kujieleza katoa wapi taarifa za "ugaidi" au hali ya afya kwenye nchi hii.
Uthubutu wa kukataa kuzungumza na ACACIA na kuitaka kampuni mama Barrick kuja kujieleza; ikabidi Prof. Joni L. Thornton akwee pipa na kumwomba balozi wa Canada amshike mkono ili aweze kuonana na Joni magogoni; ni ajabu kusema Joni ni mwoga.

Joni kasimama pekee na kuonesha mwelekeo kama kiongozi namna ya ku-handle issue ya Covid19; Wengine wakiwa wamehamaki, wanapigiana simu kwa zoom. Joni kwa ujasiri aliamua kuongoza vile anaona kuwa inafaa.

Huyu mtoa hoja, nadhani amekurupuka.
 
Duh...!.
Hoja za bandiko hili ni hoja za uongo mkubwa na za kubaini!.
1. Joni sio mtu muoga na asiejiamini kama unavyomuelezea hapa kumuonyeshea ni mtu muoga, hana confidence na anasumbuliwa na tatizo la insecurity ya kuogopa watu kitu ambacho sii kweli!.
2. Hussein hana mtandao wowote, ni mtu simple, humble and down to earth, anasimama mwenyewe with his own merits, hategemei mbeleko ya yeyote!
3. Kitu pekee ulichopatia kwenye bandiko hili ni Makame kwa sababu ni presidential material kama nilivyo muelezea hapa
Prof. Mbarawa ni Presidential material! Tuwaspot na kuwagroom Presidential materials au tumwache tu yeyote awe?
P

Nakukubali sana mkuu
 
Kwa maana hiyo wewe uko sawa na unataka uaminike kwa kila unachoamini kipokelewe kuwa kweli na wengine mitazamo yao ni uongo! Who are you!!
 
Back
Top Bottom