Kanisa jipya la Anglikana laanzishwa Tanzania, Kuzinduliwa Septemba 15

Kanisa jipya la Anglikana laanzishwa Tanzania, Kuzinduliwa Septemba 15

Inside10

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2011
Posts
29,909
Reaction score
32,414
Kanisa jipya la Anglikana lijulikanalo kama Episcopal Anglican Province Tanzania linatarajiwa kuzinduliwa Septemba 15 jijini Wilaya ya Kongwa jijini Dodoma.

Kuzinduliwa kwa kanisa hilo kunatajwa kuwapa chaguo waumini wote wa Anglikana kuamua waabudu kanisa lipi kati ya hili jipya na lililopo nchini.

Kuanzishwa kwa kanisa hili kunatajwa kurejesha na kusimamia misingi ya Kanisa la Anglikana kama ilivyokuwa miaka 60 kabla kwa mujibu wao.

Akizungumza na wanahabari, Askofu wa kanisa hilo, Elibariki Kutta amesema kuanzishwa kwa jimbo hilo jipya hakumaanishi kuwa kanisa la Anglikana limemeguka, bali inatanua wigo kwa waumini kuamua wasimame na imani ipi.

“Anglikana haijameguka. Ni moja, ila uhuru wa wewe unataka kuwa na mtazamo gani au njia ipi katika maono yako,” amesema Kutta.

Amesema kuanzishwa kwa kanisa hilo haimaanishi kuwa wameondoka Anglikana lakini wanajaribu kusimama katika misingi ya kanisa mama la Kianglikana.

Snapinsta.app_458391491_506118422012879_1233298691445610533_n_1080.jpg
 
Hao ndo wale ukijachanganya unaweza dhani na Wakatoliki....
Wakatoliki siku hizi bado tu padri anasamehe dhambi? Na bado Yesu ni Mungu hadi leo?nilikuwa navutiwa sana unapoenda kwa padri huku umeweka mikono kifuani unaanza "Namuungamia Mungu wangu nawe padri wangu tangu majuma sita sijaungama na dhambi zangu ni hizi niliba nazi,nilitukana,nilitapeli simu nk mwishoni padri anaongea kwa mamlaka Mwenyezi Mungu amekusamehe dhambi zako zote nenda kasali baba yetu mara 4 na salamu maria 6
 
Wakatoliki siku hizi bado tu padri anasamehe dhambi? Na bado Yesu ni Mungu hadi leo?nilikuwa navutiwa sana unapoenda kwa padri huku umeweka mikono kifuani unaanza "Namuungamia Mungu wangu nawe padri wangu tangu majuma sita sijaungama na dhambi zangu ni hizi niliba nazi,nilitukana,nilitapeli simu nk mwishoni padri anaongea kwa mamlaka Mwenyezi Mungu amekusamehe dhambi zako zote nenda kasali baba yetu mara 4 na salamu maria 6
Kuna siku nikiwa mdogo nilienda kuungama kwa Padre nikamwambia kwa kauli ya kudogosha "niliiba kaembe kadogo, nilichukua chenji ndogo ya 200". Padre akanikaripia kama kaembe kalikuwa kadogo uliiba kwanini, si usingeiba.
 
Back
Top Bottom