johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 97,869
- 171,716
Catholic church ni wauaji kama alivyo Jiwe. Kukaa kimya kwa haya yanayotendeka ni kushiriki mauaji. Ni wauaji kama aidd Amin, Lukashenko and other tyrants and dictators!Baba askofu Ruwaich wa Kanisa Katoliki jimbo la DSM anawaalika wananchi wote wenye mapenzi mema kushiriki uchaguzi mkuu kwa amani tukizingatia ukomavu wetu, Upendo wetu na nidhamu ya hali ya juu.
Naye Katibu wa baraza la maaskofu Dr Kitima amewaomba wananchi kutumia haki yao ya kikatiba ya kuchagua na kuchaguliwa kwa amani.
Dr Kitima amewataka watu wote wenye mapenzi mema kusoma Waraka wa Paulo mtume kwa Warumi kujua wajibu na umuhimu wa kuchagua viongozi kama Mungu anavyotubariki.
Source: ITV habari
Maendeleo hayana vyama!
forgiveness not only for the offenses of the church herself, but also for crimes committed against the native peoples during the so-called conquest of America.
Kanisa lisijifanye halisikii malalamiko ya wananchi kuwa tume haiko kwa ajili ya uchaguzi wa haki, tume tayari inalojina la mshindi.Baba askofu Ruwaich wa Kanisa Katoliki jimbo la DSM anawaalika wananchi wote wenye mapenzi mema kushiriki uchaguzi mkuu kwa amani tukizingatia ukomavu wetu, Upendo wetu na nidhamu ya hali ya juu.
Naye Katibu wa baraza la maaskofu Dr Kitima amewaomba wananchi kutumia haki yao ya kikatiba ya kuchagua na kuchaguliwa kwa amani.
Dr Kitima amewataka watu wote wenye mapenzi mema kusoma Waraka wa Paulo mtume kwa Warumi kujua wajibu na umuhimu wa kuchagua viongozi kama Mungu anavyotubariki.
Source: ITV habari
Maendeleo hayana vyama!
Ulitaka lifanyeje?Kanisa lisijifanye halisikii malalamiko ya wananchi kuwa tume haiko kwa ajili ya uchaguzi wa haki, tume tayari inalojina la mshindi.
"Kanisa lisijifanye halisikii malalamiko ya wananchi kuwa tume haiko..."Kanisa lisijifanye halisikii malalamiko ya wananchi kuwa tume haiko kwa ajili ya uchaguzi wa haki, tume tayari inalojina la mshindi.
Hauwezi kumpata kiongozi wa haki kama kura yako siyo haki yako, Tume inamtangaza inayoamriwa imtangaze na hakuna kuhoji."Kanisa lisijifanye halisikii malalamiko ya wananchi kuwa tume haiko..."
Nadhani ujumbe uliotolewa na kanisa ni somo zuri sana kwa wananchi..., wajitokeze kwa wingi sana wakapige kura ili kumchagua wanayemtaka awe kiongozi wao.
Kwa hiyo ni wajibu wa wananchi kutimiza hilo. Kuhusu tume kutimiza kazi yao itakiwavyo, hilo bado halijulikani; hakuna ushahidi kwa sasa hivi, kwa hiyo kanisa haliwezi kulisemea hilo hadi baada ya tukio la kupiga kura.
Wananchi wakipiga kura nyingi kwa wanayemtaka, halafu tume imkatae, na kanisas likabaki kimya, hapo litastahiri kulaumiwa.
Ndiyo, inajulikana kuwa tume sio huru kwa mambo mbalimbali iliyoyafanya hadi sasa kabla ya uchaguzi; lakini hii ndio sababu kubwa inayopelekea wananchi kuhimizwa wakapige kura kwa wingi wao, ili kama ushahidi utakuwepo wa kura zao kuharibiwa, basi iwe bayana, kuliko wapiga kura wachache tu wakijitokeza na kura zao ziwe rahisi kuvurugwa.
Binafsi sioni tatizo na tamko lililotolewa na kanisa.
Ni wapi iliposemwa "kura yako sio haki yako" mkuu 'elvischirwa'?Hauwezi kumpata kiongozi wa haki kama kura yako siyo haki yako, Tume inamtangaza inayoamriwa imtangaze na hakuna kuhoji.