Kansa ya matiti inammaliza mke wangu nikiwa nashuhudia, sina la kufanya. Sijui kama naweza kusahau hili

Kansa ya matiti inammaliza mke wangu nikiwa nashuhudia, sina la kufanya. Sijui kama naweza kusahau hili

Pole sana mkuu. Ni mtihani,kaza moyo.

Uliwahi ulizia kuhusu Butaro Cancer Center of Excellence? Ni kituo cha wamarekani,kipo Rwanda. Nimeonapo watu wengi wa nchi mbali mbali za Africa, sikufatilia kujua ila huenda wakawa na advanced technology kupunguza maumivu. Kupona sizungumzii.

Mgonjwa tuliewahi kuwa nae alitoboka shavu, ila mpaka anakufa, maumivu hayakuwa makali.

Labda ujaribu kufatilia uone kama watakuwa na la ziada
Pole sana .
Alikua na kansa ya eneo gani mpaka anatoboka shavu?
 
Ila kuna vitu vingine vinatia aibu. Mbona magonjwa mengi yanatesa tu waafrika,huko kwingine wanafanyaje? Kesi za magonjwa haya huko hata kama zipo,lakini madhara yake huenda si makubwa kihivi. Sasa,viongozi wetu,wanashinda na kulala huko,hawafikilii hata kuwapunguzia changamoto raia wao!!! Ina maana vifaa wanavyotumia wao,nchi kama nchi haiwezi kumudu? Je,ikishindwa,haziwezi kuungana zaidi ya moja zikashirikiana kupata?! Af utasikia polojo za watu wanawasifia weeeeee, kisa wamepata tu pesa ya unga. Hata ikitokea huyo Mungu anayesemwa akawepo,kuna watu hatopokea aise
 
Sawa umepasua ukweli ila mbona hujasema ni mmea upi huo atumie ila aimarike?, badala ya kusema leta kwanza ufumbuzi wa tatizo, akipona ndiyo tutarudi kupasua huo ukweli mkuu
Huwezi kupona kwa KUBUGIA BUGIA TU madawa au TIBA, lazima akili yako isafishwe kwanza.

Kuna mtu yeye anaamini akimeza MADONGE YENYE KEMIKALI anapona, unaona huyu ni CHIZI. Anahitaji msaada wa kiakili kwanza.

Mwingine anaamini kwamba MIMEA ni UCHAWI, huyu ni mpuuzi na goigoi tu wa kawaida, unamchangamsha kwa NAKOZI mbili tatu anazinduka kisha UNAMPA TIBA.
 
Ahsante sana, ila sijaelewa maji lita 10

Maji nusu lita?

Naomba uniandikie vuzur kama hutojali
Maji lita 5, na majani ndoo ya kilo 10
Dawa hii nlimponesha shemeji yangu ambaye alilazwa bugando kwa kansa ya tezi dume alipofikia mwisho wakatuambia tumrudishe hom ja asingemaliza 4 weeks, akarudishwa hospitali ya wilaya. Ndo nikawaambia tujaribu hii tiba and baada ya miez 2 tu mzee alikuwa mzima na hospitali wakamdischarge aliishi 2years alikuja kuugua enimonia ikamwondoa na tulimrudisha bugando walishangaa kumwona ana afya nzuri
 
Pole sana .
Alikua na kansa ya eneo gani mpaka anatoboka shavu?
Kwenye shavu tu mkuu,kakidonda kadogo kalianzia mdomoni kwa ndani.

Japo dunia ya leo imeshaharibika, kwanza upewe maua yako kwa kumjali mkeo na kufanya kila unaloliweza kuona anapata faraja ya moyo.
Si rahisi kusema kwamba tunatafuta tiba,maana wanaodai walipona huu ugonjwa sijui sijawasikia.
Bahati mbaya,mbaya sana,unajikuta matumizi ya pesa ni makubwa sana,na mtu badae anaondoka,anaacha simanzi na hali duni kwa familia. Hayayepukiki,hatuna namna.
Binafsi nakuelewa,ndugu yangu mmoja hivi karibuni nae kafiwa na mke,alikuwa Kenya. Kazaa kitoto,hajakinyonyesha,kikaletwa na kuhudumiwa. Kimefikisha miezi 6,mama anaonekana kapata nafuu,huyo,kaondoka.
Nachojaribu kusema hapa nikiangalia jama alivyobaki,asikwambie mtu. Jitahidi kujenga ukaribu na watu,pamoja na maumivu apate watu wa kuwa nae karibu,asijikatie tamaa. Wewe pia hivyo hivyo. Kuumia kwako(ni lazima kama binadamu usieona hatma ya jambo hilo),ila kumbuka unapomuonyesha kuishiwa nguvu,hili linamuathili kisaikolojia,huenda anakuona hutoweza kukabiliana na changamoto za maisha ikitokea akatangulia. Uwepo wa watu,utakusaidia hata wewe kutotokwa na machozi au kuonyesha huzuni.
Binafsi nawazaga,kama jf watu wanaweza kujadiliana mambo ya maana, wanashea upuuzi,kungekua hata na namna watu kama wewe wafikiwe,kwa nyakati tofauti tofauti,hakika mpaka unaandika hapa,mawazo yamezidi. Mpaka unahitaji msaada wa kimawazo kwa watu usiowaona na usiowajua,mi nakuelewa. Watu wangejua wenzao walipo,miongoni mwa watu 100 hata wakikutembelea 5, mnacheka,mnafurahi,unaona haupo mwenyewe,watu wanakufariji,hakiki hili linaweza kusaidia pia.
 
Najua yote ni mipango ya Mungu, ila sina matumaini kama mke wangu anaweza kupona kwa sasa
Nikupe pole sana kwa kuuguliwa na mkeo... ila ningependa tu kuweka kitu kimoja sawa...
Kwanza kabisa kwa wewe kusema "najua yote ni mipango ya Mungu" Kiukweli si kila jambo ni lakusema mipango ya Mungu sidhani kama Mungu anaroho mbaya kiasi hicho cha kumfanya mkeo ateseke na kupitia magumu na uchungu kiasi hicho...
Watu wengi tumezoea kusema mipango ya Mungu na kujikuta kumsingizia Mungu vitu ambavyo hahusiki na kusahau kua shetani yupo pia na yeye mwenyewe ndio mshitaki wetu na asiependa kuona mtu anaongezeka, kufurahi,kufanikiwa n.k
Ningependa kunukuu tu maneno haya kutoka kitabu cha..
Yohana 10
10 Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele.
Hivyo kwa kusoma tu hapa nadhani utaona kazi ya adui (Shetani/mwivi) kazi zake hapo na kazi ya Mungu.
Nimeandika tu huenda nikawa nje ya mada ila niseme tu....
Mungu ajawai kushindwa... pale fikra zako zinapoishia na kuona hakuna matumaini tena, ndipo Mungu anapoanzia.
Akili za mwanadamu zina mwisho ila yeye hana mipaka wala ukomo, Mtafute Mungu namaanisha Mungu wa kweli bila kuangalia dini yako wala nini
Mtafute mtumishi wa Mungu Bishop Elibariki sumbe Youtube fatilia mafundisho yake na uchukue hatua ya kufika ibadani, Hakika utamwona Mungu akimfungua mkeo. Akuna lililo gumu kwa Mungu.
Mungu akutie nguvu na ujasiri na roho ya kukata tamaa isipate nafasi, Zidi kumwomba Mungu kutie nguvu wewe pamoja na mkeo mzidi kumwamini yeye na kumtumainia yeye.
Barikiwa Kiongozi.
 
Njoo tupeane moyo.

Nimeanza kumuuguza dada yangu cancer kuanzia mwaka 2019,

Tuliambiwa afanye Chemo baadae afanyiwe upasuaji....

Akaanza mizunguko minne akamaliza, ikaongezwa minne akamaliza. Akarudishwa Muhimbili Kwa ajili ya upasuaji, madaktari wakatuambia arudi ocean road uvimbe haujapungua.

Ikaongezwa mizunguko 8 Tena , akapewa transfer Muhimbili awamu hii mgonjwa akagoma kufanyiwa Op. Akakaa nyumbani mwaka bila matibabu ya hospital.

Ziwa likatoboka likawa linamwaga maji pamoja na usaha, tukarudi hospital,wakasema aanze chemo upya ikaenda mizunguko 6 na mionzi 16. Kamaliza mwez wa 10 mwaka huu Kwa Sasa kapewa mapumziko ya miezi mitatu na dawa anatumia.

Eneo la ziwa limefutika na wekundu kama kamwagiwa maji ya moto.

Cancer ni stage 4.


Ushauri wangu
Kama unaweza mpeleka ocean road mpelekee pale.
Pili kidonda kisafishwe Kila siku na maji ya drip wekeni na fragine ya vidonge mnatwanga mnapakaa eneo la kidonda kabla ya kukifunga

Kidonda usikifunge na khanga Wala kitenge funga na bandage.

Ajitahidi kunywa juisi ya stafeli angalau Kila siku glass Moja.
Majani yake pia chemsha anywee.

Mungu atutie nguvu katika Janga hili 🙏🙏🙏🙏🙏
Poleni sana kwa kipindi mnachopitia.
 
Pole Sana Kiongozi..... Nayahisi maumivu unayopitia....

Sina ujuzi kwenye hili ila Naomba Mungu amlinde na kumpa nguvu Mke wako.

Amuondolee kabisa maumivu yanayomsumbua, na kumponya kabisa hiyo saratani Kwa Jina la Yesu Kristo.

Damu ya Yesu imfunike na naalika ufalme wa Mungu utawale Nyumbani kwako.

Pia mpende sana mke wako Kwa moyo wako wote Katika kipindi hiki anachopitia na Mungu wa Mbinguni atawabariki.

Hakuna linaloshindikana mbele zake Kwa Imani.

Amina.
Ameen mkuu
 
Pole sana mkuu, sipendi kuuongea ukweli huu

Ila ni kwa kuwa umetuomba tutoe ushuhuda

Kiukweli hali aliyofikia si rahisi kupona hapo lazima utampoteza mke wako mpendwa.

Pole sana ndugu.

Tunasali Mungu akupe roho ya uvumilivu, usiache kumfariji mke wako mpendwa na kumwonyesha upendo
 
Yapata miaka miwili imepita tangu mke wangu alipogundulika ana saratani ya matiti, tulianza dozi ya CHEMOTHERAPY pale GOOD SAMARITAN CANCER HOSPITAL Ifakara, tulipatiwa jumla ya mizunguko 8 ya CHEMO, hali ilionekana kuwa nzuri ila ndani ya muda mfupi sana uvimbe ulianza tena.

Baada ya kuona uvimbe umeanza upya tulihamia Dodoma BENJAMIN MKAPA napo tulipatiwa chemo 4 kisha ukafanyika upasuaji ili kuondoa titi lililoathirika na saratani, upasuaji amefanya mwezi wa 4 mwaka huu.

Baada ya upasuaji hali ilionekana kama ipo vizuri, ila baada ya miezi ipatayo mi3 mgonjwa ameanza kusumbuliwa tena.

Anasumbuliwa na; MAUMIVU MAKALI SANA MAHALA ALIPOFANYIWA UPASUAJI
KIDONDA KISICHOPONA (kilianza kidogo sana, kama kiji upele, hatimae kikakua. Hakionyeshi dalili ya kupona.

Najua yote ni mipango ya Mungu, ila sina matumaini kama mke wangu anaweza kupona kwa sasa.

KUNA MTU ASHAWAHI KUUGUZA MGONJWA WA SARATANI naomba ushuhuda ambao unaweza nisaidia cha kufanya.

KAMA KUNA DAWA ZA TIBA MBADALA ULITUMIA ZIKASAIDIA, NAOMBA MSAADA PIA.

Kwa sasa mgonjwa yupo tu nyumbani tunasubiri neema ya Mungu

Ushauri wowote pia napokea.
Pole san mkuu
 
Hiyo cancer ipo stage gani? It's so sad mtu anapotea na ndugu mnaona huyu anapotea.
 
Yapata miaka miwili imepita tangu mke wangu alipogundulika ana saratani ya matiti, tulianza dozi ya CHEMOTHERAPY pale GOOD SAMARITAN CANCER HOSPITAL Ifakara, tulipatiwa jumla ya mizunguko 8 ya CHEMO, hali ilionekana kuwa nzuri ila ndani ya muda mfupi sana uvimbe ulianza tena.

Baada ya kuona uvimbe umeanza upya tulihamia Dodoma BENJAMIN MKAPA napo tulipatiwa chemo 4 kisha ukafanyika upasuaji ili kuondoa titi lililoathirika na saratani, upasuaji amefanya mwezi wa 4 mwaka huu.

Baada ya upasuaji hali ilionekana kama ipo vizuri, ila baada ya miezi ipatayo mi3 mgonjwa ameanza kusumbuliwa tena.

Anasumbuliwa na; MAUMIVU MAKALI SANA MAHALA ALIPOFANYIWA UPASUAJI
KIDONDA KISICHOPONA (kilianza kidogo sana, kama kiji upele, hatimae kikakua. Hakionyeshi dalili ya kupona.

Najua yote ni mipango ya Mungu, ila sina matumaini kama mke wangu anaweza kupona kwa sasa.

KUNA MTU ASHAWAHI KUUGUZA MGONJWA WA SARATANI naomba ushuhuda ambao unaweza nisaidia cha kufanya.

KAMA KUNA DAWA ZA TIBA MBADALA ULITUMIA ZIKASAIDIA, NAOMBA MSAADA PIA.

Kwa sasa mgonjwa yupo tu nyumbani tunasubiri neema ya Mungu

Ushauri wowote pia napokea.
Aisee, pole sana mkuu! Mungu akupe moyo mkuu wa uvumilivu! Mungu aweke neema yake!
 
Back
Top Bottom