Inside10
JF-Expert Member
- May 20, 2011
- 29,909
- 32,414
KANTE AMTAFUTE HAKIMI. EMMANUEL EBOUE AWE CASE STUDY.
Ngolo Kante, nyota wa zamani wa Chelsea na mshindi wa kombe la dunia akiwa na timu ya taifa ya Ufaransa amemuoa mwana mama raia wa Uingereza anayeitwa Jude Littler (pichani). Jude ni mfabiashara na mtangazaji wa television ya ITV Wales and S4C.
Jude Littler alikuwa ni mke wa zamani wa Djibrin Cisse, mchezaji wa zamani wa Liverpool na timu ya taifa ya Ufaransa. Cisse na Littler alioana mwaka 2005, ilipofika mwaka 2012; Cisse na Littler walitalakiana na Littler alichukua sehemu kubwa ya utajiri wake.
Miaka miwili baadae 2014, Ngolo Kante alikutana na Jude Littler kwenye klabu ya usiku na walioana miezi michache baadae. Jude Littler ana umri wa miaka 48 huku Ngolo Kante akiwa na umri wa miaka 33, Jude anamzidi umri kwa miaka 15.
Cha kufurahisha zaidi ni kwamba wakati Kante anamuoa Jude alimkuta na watoto 3 kwa mumewe wa zamani Djibrin Cisse ambaye Ngolo Kante sasa anawalea kama watoto wake. Kante na mke wake Jude hawana mtoto wa kumzaa.
*****
Huu ni mtego wa kiungo wa boli, Ngolo Kante. Huu mtego aliusanukia Hakimi ila ulimnasa Emmanuel Eboue na akaachwa bila kitu. Mwamba anakaba sana uwanjani ila huku amekabwa aiseee! 😂
Source @mdemupolycarp X