Kanuni Mpya vyama vya Siasa zinazotaka kupenyezwa

Kanuni Mpya vyama vya Siasa zinazotaka kupenyezwa

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Kufanya siasa hapa nchini hakujawahi kupungikiwa vitimbwi.

Haki, usawa na ustaarabu vimemilikishwa chama tawala. Mamlaka ikajikita kuhakikisha wengine hawafurukuti.

Yote haya yakifanikishwa kutokana na mapungufu makubwa ya makusudi kwenye katiba ya nchi isiyokidhi zama tulimo.

Pana sheria zinazo simamia uwepo na shughuli za vyama vya siasa zenye kujitosheleza kwa mujibu wa katiba.

Ajabu na kweli mamlaka imekuwa ikizikiuka sheria hizi kwa miaka yote. Kwa sababu hawawezi tena kuendelea kuzikiuka kama zilivyo, sasa kunakuja zinazoitwa kanuni ili kuhalalisha batili hii kuendelea.

Kufanikisha hili TCD ya Mwami Ruyagwa imekabidhiwa mikoba hiyo.

Katika TCD kuna vyama vya 5 (ACT, CCM, Chadema, CUF na NCCR). CCM na ACT vina agenda zilizo tofauti zaidi na vingine. Hawa ndiyo wanaoonekana kuwa waasisi wa mkakati mpya huu.

Lengo kuu likiwa kufifisha agenda ya madai ya katiba mpya.

Haihitajiki kuwa nabii kutambua kuwa msingi mkuu wa zinazosemekana kanuni za vyama siasa zitakuwa kuhakikisha hakuna katiba mpya hadi angalau baada ya 2025.

Panga pangua kwa mujibu wa kanuni za kina Mwami Ruyagwa na wenzake, kudai katiba mpya kabla ya 2025 itakuwa ni haramu kuliko kulima bange.
 
Wenge la katiba mpya🐒🐒🐒
 
Unafiki huwa haufichiki milele, Zitto ambae amejificha miaka mingi lakini wajuaji tukisema ni kibaraka na ndumilakuwili na sasa ipo wazi!
Kumbukeni CDM walishamstukia miaka mingi na ndio maana walimtimua, huwa anatumika sana kwa ujira.
 
🐒🐒🐒
WYCgC_rl.jpg
 
Hakuna jambo baya kama kuishi kwa mazoea. Miaka mingi sana CCM imekuwa ikitabiriwa kufa lakini bado iliendelea kushika madaraka japo si kwa njia zilizonyooka. Hili limeifanya iwe na mazoea na kujiamini kuwa watapita tu.

Jambo baya la mazoea ni kujenga dharau, kibri na kujiamini kupitiliza. CCM wanasahau kuwa nyakati zinabadilika, utandawazi umekuwa mkubwa kupelekea uelewa mkubwa zaidi. Zile zama za kuwa siasa ni kwa ajili ya wazee tu zimepita.

Hili swala la katiba ndio hasa litakaloleta anguko la CCM, kwa sasa hata mtoto mdogo keshajua kuwa tuna katiba mbovu, hivyo watafanya kiini macho, watapotosha ukweli na hata kutumia nguvu kama kawaida yao lakini mwisho wa siku katiba mpya itabidi ipatikane tu ili mambo yaende sawa.

Ni muda mfupi ujao Katiba mpya haitokuwa ombi tena bali ni amri, Mungu ajaalie tusifike huko maana athari yake haitokuwa ndogo. Amri ya kutaka katiba itaamsha machungu ya hata yale yaliyopita.
 
Hakuna jambo baya kama kuishi kwa mazoea. Miaka mingi sana CCM imekuwa ikitabiriwa kufa lakini bado iliendelea kushika madaraka japo si kwa njia zilizonyooka. Hili limeifanya iwe na mazoea na kujiamini kuwa watapita tu.

Jambo baya la mazoea ni kujenga dharau, kibri na kujiamini kupitiliza. CCM wanasahau kuwa nyakati zinabadilika, utandawazi umekuwa mkubwa kupelekea uelewa mkubwa zaidi. Zile zama za kuwa siasa ni kwa ajili ya wazee tu zimepita.

Hili swala la katiba ndio hasa litakaloleta anguko la CCM, kwa sasa hata mtoto mdogo keshajua kuwa tuna katiba mbovu, hivyo watafanya kiini macho, watapotosha ukweli na hata kutumia nguvu kama kawaida yao lakini mwisho wa siku katiba mpya itabidi ipatikane tu ili mambo yaende sawa.

Ni muda mfupi ujao Katiba mpya haitokuwa ombi tena bali ni amri, Mungu ajaalie tusifike huko maana athari yake haitokuwa ndogo. Amri ya kutaka katiba itaamsha machungu ya hata yale yaliyopita.

Pichani alidhani atakomaa:

IMG_20220326_121150_939.jpg


Kulikoni Ngorongoro, kulikoni hata wafuasi wa Zumaridi? Kumbe mambo hayaendi bila kujitoa zaidi? Kumbe jela si mali kitu?

Wafuasi wa Zumaridi wanapotoa Somo kwa Makamanda
 
Inawezekana Zitto ameshakata tamaa na maisha katika Ulimwengu wa siasa, anatafuta mitaji ya biashara tu au uwekezaji mkubwa.
Hakuna biashara atafanya na kufanikiwa, hawezi kuuza uhai wa wazanzibar kirahisi hivyo, na abaki salama.
Zitto na Samia wataokota makopo, albadiri zinazopigwa hawatapona katu.
Wazanzibar wameamua kuwashitaki kwa Allah mapemaaa.. na ramadhani inayokuja duaaa zote ramadhani yote, ni kuwalaani wapinga katiba mpya. Na INSHAALLAH Mungu atatenda.!
 
Inawezekana Zitto ameshakata tamaa na maisha katika Ulimwengu wa siasa, anatafuta mitaji ya biashara tu au uwekezaji mkubwa.

Huu sasa ndiyo unaoitwa ubinafsi uliopitiliza.

Katika nchi nyingi huu huwa hauna msamaha.
 
Back
Top Bottom