Karia ni mbaguzi wa wadau wa mpira

Karia ni mbaguzi wa wadau wa mpira

Kuweni makini sana, unaweza jikuta unamsapoti mjinga bila kujua, malalamiko kuhusu Karia yote ni ujinga mtupu.
Hebu niambie Mimi na wengine humu, Manara ameivunja kanuni gani ya TFF inayotoa adhabu ya vile? Yaani ukichunguza adhabu Ile ni cumulative. Imekusanya vionjo viingi ambavyo vimewekwa pamoja na kufunikwa shuka moja TU la Manara kazozana na Karia.

Adhabu Ile imelipia na wengine kama Barbara, mo, coastal Union na hata Simba yenyewe. Lakini Karia na Manara ni watu wadogo sana kuliko mpira wetu na Tanzania. Watanzania wanataka mpira wao uchezwe wafurahi na wengine wapate kipato. Utani wa Simba na Yanga ndio mpira wenyewe wa Tanzania, hivyo yeyote atakaeikosea kwa makusudi au kwa bahati mbaya Simba na Yanga atakuwa amekusudia kuukosea mpira wa Tanzania. Atakuwa ameonheza maadui zake kila Kona hata uvunguni mwa kitanda chake.
 
Tulisha ambiwa kuwa, Mwana Yanga, hata awe na akili kwa kiasi gani, awe msomi na mweledi kwa kiasi gani, linapokuja suala la YANGA YAKE, wote hao wanakuwa HAMNAZO! Toka yule jamaa aseme hayo, nimekuwa nikipima yasemwayo na hawa ndugu zetu, yule jamaa, yupo sahihi100%.
Hata hapa JF, wapo watu ambao huwa tunawakubali kwa michango yao ithibitishayo kuwa ni ma - GT, lakini likija suala lihusulo YANGA YAO, unashikwa na mshangao!

Na huu ndiyo ukweli wenyewe.
 
Halafu unatakiwa utofautishe kati ya neno rais na Rais. Wallace Karia ni rais!! Na siyo Rais. Halafu umshauri pia na yeye ajitahidi kujiheshimu, aachane na mihemko ya kijinga, na piaa Aachane na ushabiki maandazi.
Mfano kwenye ile mechi ya fainali angekuja kama rais wa TFF, ule mzozo na mjinga mwenzake Haji Manara usingetokea!

Badala yake aliingia uwanajani kama shabiki wa simba, na pia kama mwananchama wa Coastal Union. Hapa ndipo kwenye chanzo cha malumbano yao.

Hivi nikuulize kitu; angekuwa rais wa TFF ni Leodgar Tenga, ungetegemea kutokea tukio la kutupiana maneno kati ya Haji Manara na Leodgar Chilla Tenga? Mwisho wa siku kama umenielewa, basi utakubaliana na mimi ya kwamba Wallace Karia na Haji Manara, kwa pamoja hawana busara.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] utakufa kwa pressure wallah, vimbaaa hadi upasukeeee, Karia bado yupo sanaaaaa.
 
Simba haihitaji kutafutiwa wadhamini feki mbona nyinyi mnagoma kuvaa logo za mdhamini kama rangi ni nyekundu au Kuna TFF mbili tofauti zinazoendesha ligi
Kukataa kuvaa rangi ya logo sio sawa na kukataa udhamini wa TFF. Rangi ya logo inaweza kubadilishwa hata Ulaya wanafanya hivyo, lakini kukataa udhamini ambao TFF ameutafuta, kuukubaki na kufunga mkataba ni kosa la kikanuni ambalo Lina adhabu kubwa ambayo hata hivyo haikutolewa Wala kujadiliwa na TFF. Hii
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] utakufa kwa pressure wallah, vimbaaa hadi upasukeeee, Karia bado yupo sanaaaaa.
Karia waziwazi kasema alikuwa na hasira na viongozi wa TFF waliomtangulia kabla yake, hivyo analipa kisasi.
 
Kukataa kuvaa rangi ya logo sio sawa na kukataa udhamini wa TFF. Rangi ya logo inaweza kubadilishwa hata Ulaya wanafanya hivyo, lakini kukataa udhamini ambao TFF ameutafuta, kuukubaki na kufunga mkataba ni kosa la kikanuni ambalo Lina adhabu kubwa ambayo hata hivyo haikutolewa Wala kujadiliwa na TFF. Hii
Nitajie nchi moja ya ulaya iliyofanya hivyi
 
Karia waziwazi kasema alikuwa na hasira na viongozi wa TFF waliomtangulia kabla yake, hivyo analipa kisasi.
Mtajua nyie huko huko, halituhusu sie. [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Nikikumbuka kipindi Cha malinzi Simba walivokua wanadalilishwa na kuminywa live[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]leo Yanga wa kulalamika hivi kweliii!
Kuimba kupokezana ndugu zetu,mtumie hvyo hvyoo

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Nilikua sijui kumbe hata humu kuna wapuuzi wengi tu waliojaa utoto mwingi na kuto kujaji mambo kulingana na uhalisia wake.

Hivi kwa mwenye akili kosa la manara ni la kumkingia kifua kweli!!!?

acheni uzombi wakuda nyie.

JF skuiz imekua kama facebook tuu. Watoto wengi bora shule zifungue tuu.

Jifunzeni kuwatii wenye mamlaka maanina zenu
Umeandika ukiwa umevimbiwa makande
 
TFF ndiye mwenye haki ya kutafuta wadhamini wa ligi lakini kwa Simba wameufyata,
Taratibu hazikufuatwa na ndiyo Maana kwa simba Tff huwa wanaufyata . Simba ina wanasheria mahiri , Yanga ni mapoyoyo wanafanya mambo kipoyoyo bila kujua SHERIA ,TARATIBU na KANUNI (STK) zinatakaje.

Rejea kesi zote za utopolo ziwe kwa Tff au Cas hakuna kesi ambayo walishawahi kuishinda.
Itoshe tu kusema Yanga ni mazuzu hayajui kitu tofauti na uroporopo

Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
 
Yaani utopolo buana, kwa hiyo sababu manara kafungiwa ndo woootee hamumpendi Karia?

Karia aendelee kupiga spana, hayo mambo ya kusema sijui kiongozi hatakiwi kuwajibu watu ni ujinga, kariaaa piga spanaa mpaka mwiko kule nyuma uwatoke.
 
Nikikumbuka kipindi Cha malinzi Simba walivokua wanadalilishwa na kuminywa live[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]leo Yanga wa kulalamika hivi kweliii!
Kuimba kupokezana ndugu zetu,mtumie hvyo hvyoo

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Mpira unazo njia zake sio visasi.
 
Yaani utopolo buana, kwa hiyo sababu manara kafungiwa ndo woootee hamumpendi Karia?

Karia aendelee kupiga spana, hayo mambo ya kusema sijui kiongozi hatakiwi kuwajibu watu ni ujinga, kariaaa piga spanaa mpaka mwiko kule nyuma uwatoke.
Manara awepo au asiwepo Yanga itakuwepo TU, tunachotetea hapa ni kupinga matumizi mabaya ya office na double standards.
 
Back
Top Bottom