Karibu kwetu tukuhudumie mkopo usio na riba wala dhamana

Mkuu kuna watu wana ubongo wa mende hata ukimuelewesha vp haelewi ndiyo maana nimemwambia kama anaamini negative aendelee hivyo hivyo.
Poa mkuu, kila kheri ingawa nilikuwa nakuhitaji PM kidogo kama hutojali maana nina shida na mkopo binafsi serious!
 
Ndio yale ya desi au...something smell fishy...mkopo usio na riba? Tatizo lako ume sugarcoat loan info yako...ujanja ujanja tu
 
Mkopo bila riba wala dhamana, ila kwenye maelezo unasema 100,000 riba ni 25,000, usipotoa utakatwa wewe na wadhamini wako watano! Amazing, nimekumbuka ule msemo wa kizungu kwamba vise versa is also true. Kichwa cha habari kingine, maelezo kinyume chake.
 

Maelezo ni mengi sana, lakini kinachotafutwa hapa ni ADA ya maombi ya mkopo. Hii ni kama tatu mzuka au Biko, ungewaeleza watu kwa uwazi tu ili wajue target yako ni kukusanya pesa toka kwao kupitia so mentioned as "Ada". hayo mengine ya kusaidia watanzania ni njia ya kupitia tu,

ingawa najua wapo mazumbukuku watakaojitokeza na kulipa hizo ada kama tu ambavyo wanatumiwa msg za "hiyo hela tuma kwenye namba hii" na kweli wakatuma

Best regards
 
Asiyejua maana usimwambie maana,maana ukimwambia maana ataharibu maana.
 
Usicheke me nataka waje wengi na ushuhuda.....sijawahi kutapeliwa sasa nisije ingia kibra kirahisi ...mkopo nautaka sana na ni mlipaji mzuri coz nshakopa sehem mbalimbali sasa huyu eeeh
Akili za kuambiwa changanya na zako,,, hahah
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…