Karibu tena JF member "National Anthem", natumai wewe na familia yako mtapona haraka katika hili

Karibu tena JF member "National Anthem", natumai wewe na familia yako mtapona haraka katika hili

Mkuu Mimi sijali Kama Ni mawazo yako au ndugu zako. Ila just know sisi Ni team kubwa. Na familia kiujumla[emoji120][emoji120]
Sawa nyie ni familia kubwa lakini kwanini mambo mengine ( hasa jambo zito kama ili likachukua mda kidogo then ndo mkaja kublast mitandaoni?))
 
Sa

Sa hapa unamlaumu mfiwa au mleta uzi?
Je unafikiri mleta uzi ametumwa au kaleta uzi kwa mapenzi yake mwenyewe?

Ukifiwa huwezi kufungua jf au insta au hata wasap ambazo zote ni mitandao ya kijamii?

Kuingia jf kutakuondolea kumcha Mungu?

Nisamehe tu ni maswali nimejiuliza tu.
Huyo mfiwa si yuko kwenye majonzi? si juzi tu hapa kafiwa? Huyo mleta uzi angempa mda kidogo wa relief then akaja na hii sympathy [emoji848]

Sasa mtu kafiwa uzi hakujapoa mara paap uzi mwingine tena wa mfiwa duuh
 
Nilikuwa sikujibu wewe!

Unfortunately huwa sijibishani na mtu ambaye siongei naye...

Umeleta liuzi hapa...

Mawazo mbadala yatakuwepo tu utake usitake!

Kwa hivyo usikomae sana na kutaka ku-control mawazo ya watu hapa.

After all, you must be grieving.

Please respect yourself and let the little angels rest in peace!
Duuh[emoji119][emoji119][emoji419][emoji419][emoji419]
 
KAtika jumuia flani..
Tuliwahi kuwa na mtu akipinga sana
Kutembelewa watu wenyeshida na
Kupelekewa chochote alisema ni upotevu wa muda na pesa.

Lskini ilifika zamu yake alipatwa na tatizo flani...
Tulijipanga kwenda kumtembelea na tulinunua vitu vya thamani na kabahasha kadogo chenye pesa kidogo.

Tulimtembelea J2 jioni na kufanya sala na maneno machache ya faraja.

Huyo jamaa alilia sana na kutushukuru sana na alisema hivi;

Wanaume wenzangu naomba radhi...sijawahi kujua umuhimu wa watu kupoteza muda wao kumjali mwingine...nimejisikia kufarijika mnoo na kuanzia sasa nitakuwa mstari wa mbele kuwafariji wengine.

Kwako bwana Thomas Edson
Ukiwa umeshiba hutamewlewa mwenye njaa.
Ukiwa umepewa vingi huwezi kumwelewa muhitaji.

Ukiwa na amani huwezi kumwelewa mwenye huzuni.

Marafiki hupatikana popote hivyo alivyofanya Intelligent businessman
Sioni ubaya ndg
Sasa kama ni kufariji si angemfariji hata kwa simu?

Au mtandaoni ndo vinanogaa?
 
Mi nashauri wanaoleta Uzi wakitegemea positive comments only waende FB , JF utakula nyundo tuu za negative hlo halipingiki... Kama Yesu mwenyewe alipingwa hadharani sembuse wewe mleta Uzi unayekunya Kwa kulenga
Hahaha...anakunya kwa?

Lazima mtu upokee posi+tive na nega-tive kwenye uzi wako!

Usitarajie shangwe tu, kila mtu na maoni , mtazamo tofauti
 
Kama utoto si unaachana nao,unapita zako tu Mkuu
Si lazima ukazingatia kila uzi.
Tuna perceptions tofauti, wewe utasema hiki, mi ntapinga, usitarajie kupata agreement kila kona...free mind
 
Mnapata faida gani kuanika maisha yenu mitandaoni humu? Is this real necessary? Do you think people genuinely care?

1. Kaoa (Uzi)
2. Kapata watoto mapacha (Uzi)
3. Mapacha wamefariki (Uzi)
4. Karudi tena mitandaoni (Uzi)
5. Mke kapata mimba tena (Uzi)
6. Mke kajifungua mapacha tena (Uzi)

Seeking attention/sympathy? From who? At what cost? Kama kuna mabinti ambao pengine alishawaahidi kuwaoa humu akaishia kuwachezea na kuwatosa unafikiri walifurahi waliposikia kuwa kapata watoto mapacha? Unafikiri machozi yao waliyolia waliposikia kaoa yalikwenda bure?

Mambo mengine mnafanya ni utoto tu wallahi!

Anyway pole sana kwa mfiwa japo nilitegemea pengine achukue angalau kama mwezi hivi ili kuliflect na kumuomba Mungu; na kupata msaada wa kichungaji/kisaikolojia kabla ya kukimbilia kurudi tena kutamba mitandaoni humu hata wiki moja haijaisha. Labda masikini bado yuko kwenye denial!

Mungu Ambariki na kuwapoza wafiwa wote na hasa mkewe ambaye naamini kama mama bado atakuwa na wakati mgumu sana japo tayari mumewe kesharudi mitandaoni humu kusaka sympathy na attention!

Note: Haya ni mawazo yangu tu huru na hayana nia ya kumkwaza mtu wala kudogosha tukio la kusikitisha lililotokea. Let the innocent little ones peacefully rest in Jesus' endless blessings.

[emoji419][emoji419][emoji419]Tuwe na faragha kidogo wapendwa - humu mitandaoni na kwingineko. Inasaidia sana hasa katika jamii zetu hizi za Kiafrika![emoji419][emoji419][emoji419]
Mleta thd yupo tu kwa shemeji yake juu ya kochi, kutwa kuanzisha thd za wazazi utafikiri kapata kazi wodi ya wazazi.
 
Back
Top Bottom