Kashfa nzito: Zitto vs Amina Chifupa

Kashfa nzito: Zitto vs Amina Chifupa

Status
Not open for further replies.
na Mwandishi Wetu

MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zubeir Zitto (CHADEMA) amesema anajiandaa vilivyo kukabiliana kisheria na wimbi la tuhuma zinazoelekezwa kwake zikimhusisha kuwa na uhusiano usiofaa na mbunge mwenzake, Amina Chifupa Mpakanjia (CCM).

Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu kutoka jimboni kwake Kigoma jana, Zitto alisema amesikitishwa kwa kiwango kikubwa na namna vyombo kadhaa vya habari vilivyofikia hatua ya kuandika habari hiyo kwa namna inayoingilia uhuru wake binafsi.

"Nimekuwa mpiganaji siku zote. Ninakuhakikishia nitapambana kutetea haki yangu na nitashinda. Nimeshaanza kujiandaa kuchukua mkondo wa sheria dhidi ya wale wote ambao wamefikia hatua ya kuingilia uhuru wangu binafsi kwa kiwango ambacho hakiwezi kuvimilika tena," alisema Zitto katika hali ya kujiamini kabisa.

Akitoa mfano, mbunge huyo machachari aliyeingia bungeni kwa mara ya kwanza mwaka 2005 alisema ameshtushwa kubaini kuwapo kwa masuala yanayoingizwa katika tuhuma dhidi yake ambayo hayana ukweli hata kidogo.

Mbunge huyo aliliambia gazeti hili kwamba, tayari ameshawasiliana na wakili wake, aliyeko jijini Dar es Salaam ili aanze kuchukua hatua za kisheria dhidi ya vyombo vya habari na wale wote watakaoamua kuingilia uhuru wake katika hali ya kuvuka mipaka.

"Mimi si mtu wa kuacha privacy yangu ikaingiliwa kwa kiwango hicho. Nitapambana na nitashinda. Nimeshawasiliana na wakili wangu ili aanze kulifanyia kazi suala hilo," alisema Zitto.

Mbunge huyo anatoa kauli hiyo baada ya gazeti moja kuahidi kuchapisha ujumbe wa maandishi wa kupitia katika simu ya mkononi unaoonyesha kuwapo kwa mawasiliano yasiyofaa kati yake na Amina Chifupa ambaye sasa ametalikiwa na mumewe.

Aidha, kauli hiyo ya Zitto inakuja siku mbili tu baada ya yeye mwenyewe kulihakikishia gazeti hili kwamba, uhusiano wake na Chifupa umekuwa ni wa kikazi tu na si zaidi ya hapo.

Taarifa nyingine ambazo gazeti hili lilizipata jana zinaeleza kuwa, miongoni mwa masuala yaliyomshtua Zitto ni kuhusishwa kwake na ujumbe mmoja wa maandishi wa kupitia katika simu ya mkononi (SMS) anaodaiwa kuutuma kwa Amina Chifupa.

"Zitto ameshtushwa na ujumbe huo wa SMS anaodaiwa kuwa aliutuma kwa Amina Chifupa ambao mbali ya kuukana ameshaweka bayana kwamba una maneno ambayo si ya mtu wa aina yake," kilisema chanzo chetu cha habari ambacho kiko karibu na Zitto.

Kwa mujibu wa chanzo hicho cha habari, Zitto mwenyewe alipatwa na mshtuko mkubwa alipoonyeshwa ujumbe huo ambao hakumbuki kuwahi kuutuma kwa Amina.

Kwa mara ya kwanza suala hili linalomhusisha Zitto na Amina Chifupa liliandikwa na gazeti moja la kila siku Jumapili iliyopita, ingawa jina la mbunge huyo wa CHADEMA halikutajwa.

Hata hivyo, siku hiyo ya Jumapili, Tanzania Daima ilifanikiwa kuiona barua ya Mohammed Mpakanjia, aliyekuwa mume wa Chifupa aliyoiandika kwenda kwa Spika akilalamika kuhusu kuwapo kwa uhusiano usiofaa kati ya mkewe na mbunge huyo wa CHADEMA.

Tanzania Daima ilipowasiliana na wabunge wote hao wawili kwa nyakati tofauti, walikanusha kuwapo kwa uhusiano huo kati yao na Amina akafikia hatua ya kuhusisha kuachwa kwake na mumewe na ushawishi wa kiongozi mmoja wa juu wa CCM ambaye pia ni Naibu Waziri katika Serikali ya Rais Jakaya Kikwete.

Kutokana na jambo hilo kufikishwa katika vyombo vya habari, Amina Chifupa aliahidi kuitisha mkutano wa waandishi wa habari juzi Jumatatu ambao angetumia kukata mzizi wa fitina kwa kumtaja kiongozi huyo wa CCM ambaye inadaiwa anafanya hivyo ili kumzuia yeye (Chifupa) kugombea nafasi ya uenyekiti wa taifa wa Vijana wa CCM (UV-CCM).

Hata hivyo katika hali isiyotarajiwa, Amina Chifupa (26) alishindwa kutimiza ahadi yake hiyo na badala yake akatokea baba yake mzazi aliyewaeleza waandishi wa habari kuwa, familia ilikuwa imeamua kumzuia mwanawe kuzungumza hadharani masuala yake.

Mzee Chifupa alisema walifikia uamuzi huo wa kumzuia binti yake kuzungumza na waandishi wa habari baada ya kubaini kuwa, masuala yake yangeweza kumalizwa ama ndani ya familia au katika vikao rasmi vya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

"Nimekuja hapa kwa niaba ya Mheshimiwa Amina, kuwaomba radhi kwamba familia imesitisha mkutano na waandishi wa habari… ni kweli amepewa talaka moja.

"Sisi ndio wenye jukumu na mtoto wetu. Watoto ni pensheni zetu sisi wazee, hatutaki kuharibu. Tutashughulikia kichama. Kulinda pensheni ni muhimu," alisema mzee Chifupa mbele ya umati mkubwa wa wanahabari.

Pia alisema iwapo Amina anahitaji kuzungumzia suala hilo, atapaswa kufanya hivyo ndani ya vikao vya vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) na si kuzungumza mbele ya umma.

Tanzania Daima
 
na Absalom Kibanda

HUU ni mwaka wa uchaguzi mkuu sndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kimsingi huu ni msimu wa kuibuka kwa mambo mengi makubwa na madogo yasiyo na kichwa wala miguu.

Waswahili wanao msemo mzuri kabisa unaokwenda sambamba na majira au nyakati. Msemo huu si mwingine bali ule usemao: ‘dalili za mvua ni mawingu.’

Kwa CCM ya zama hizi, limekuwa ni jambo la kawaida kila ukaribiapo msimu kama huu kuanza kusikika na kuonekana kwa matukio ya ajabu ajabu yanayoambatana na vituko vya hapa na pale miongoni mwa wanasiasa wa kada mbalimbali ndani ya nchi hii.

Kwa hakika dalili za msimu mbaya za ‘wanasiasa kuanza kuvuna kile walichopanda na kupanda kile wanachotarajia kukivuna zimeanza kuonekana waziwazi.

Kwa maneno rahisi, kupitia katika vyombo vya habari, huu sasa ni wakati ambapo CCM hujipambanua kuwa chama ambacho wanasiasa wake, wakiwamo wale wanaoonekana kuwa hodari kabisa kuanza kushikana mashati, kushambuliana, kukashifiana na kupeana sifa nzuri na mbaya. Kimsingi hapo ndipo tulipo sasa, tukijiandaa kufika tuendako.

Kwa lugha rahisi, chama tawala kinaingia katika kipindi kigumu kingine kinachotawaliwa na majungu mepesi na mazito ya kisiasa ambayo yanaendelea kuyathibitisha maneno ya Profesa Issa Shivji ya hulka ya siku zote ya wanasiasa kupenda madaraka kuliko kuipenda siasa yenyewe.

Leo hii tunaposoma habari zinazomhusu Amina Chifupa, baadhi yetu tunaishia kuangalia pale alipoangukia mwanasiasa huyo, huku tukisahau kutupa macho yetu kule alikojikwaa.

Kwa hakika Amina anapita katika tanuri lenye moto mkali, lililopata kuwakaanga wanasiasa wengi wakongwe katika nchi hii kama kina John Samuel Malecela, Dk. Salim Ahmed Salim, Dk. Abdallah Kigoda, John Pombe Magufuli, Frederick Sumaye, Prof. Mark Mwandosya na wengine wengi wengine.

Amina Chifupa, mwanasiasa mwepesi kiumri na mtu anayeonekana kukosa uangalifu katika mambo yake mengi binafsi, pamoja na kutambua kuwa amekuwa ‘target’, safari hii ametumbukia ndani ya maji ya kina kirefu yaliyopata kuwazoa na kuwamaliza kisiasa kila mmoja kwa kiboko chake wanasiasa hao.

Hakuna shaka kabisa kwamba, watu anaokabiliana nao, wameamua kwa dhati kumvua joho la ufahari wake kisiasa na kimsingi, makosa yake binafsi yanaweza yakagharimu kwa kiwango kikubwa nafasi yake ya kisiasa iwapo hatakuwa makini kukabiliana nao sawasawa.

Amina na wanasiasa wengine wachanga ndani ya CCM wanaojiandaa kwa ajili ya nafasi nyeti za kiuongozi wanapaswa kulifahamu hilo na kutambua kuwa, jitihada za kuwakata miguu ili kuwazuia wapoteze nguvu za kusimama mchuano wakati utakapowadia, ndiyo azma kuu ya wapishi wa fitina hizo.

Ingawa mbele ya macho yetu tunamuona Amina Chifupa, ukweli ni kwamba, katika suala lake la sasa, yeye ni kivuli tu cha mwenendo wa mambo machafu, siasa za kuvutana mashati na falsafa kuu kuu ya majungu na yenye mafanikio makubwa kabisa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

‘Fitina’ mbaya kisiasa anayojaribu kukabiliana nayo leo na ambayo sasa imempotezea mume huku ikijaribu kusonga mbele na kumpokonya ubunge wake na baadaye kumnyima matunda mengine ya kisiasa, inaweza ikamfanya abakie kuwa majeruhi kwa kipindi kingine kirefu kijacho.

Kwa namna yoyote ile, magwiji wa mtandao wanaokabiliana na Chifupa wanaungwa mkono kisirisiri na genge kubwa la maadui wa mwanasiasa huyo wanaomtuhumu yeye kwa kuwahusisha na biashara za dawa za kulevya.

Kwa bahati mbaya sana, miongoni mwa wale ambao wanapinga harakati za kujijenga za mwanasiasa huyo ni wabunge wenzake na wengine ni wanachama wenye madaraka ndani ya CCM, wakiwa ama wabunge au wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho tawala.

Kile ambacho kimekuwa kikionekana kuwa ni jitihada za Amina kujijengea jina na kujipatia umaarufu mkubwa hata kuwashangaza baadhi ya watu waliokuwa wakimdharau wakati alipoingia bungeni kwa ‘mlango wa nyuma’ akizishinda jitihada za viongozi wake kadhaa ndani ya Umoja wa Vijana wa CCM, sasa kinageuka haraka haraka na kuonekana kuwa uchafu usiopaswa kutetewa.

Jitihada ya kumjengea taswira chafu mwanasiasa huyo, inafanana na kile kilichoitwa uziro wa Sumaye, uarabu wa Salim Ahmed Salim, ukabila wa Mwandosya, ukarani wa Mangula, ubadhirifu wa Kigoda na uzee wa Malecela.

Kwetu sisi, watawaliwa, walipakodi, wananchi wa kawaida na umma wa Watanzania tatizo tunalopaswa kuliangalia sasa, si kile kinachoweza kuonekana leo kuwa ni ufuska wa Amina Chifupa unaoweza ukafananishwa na sifa mbaya wanazojaribu kubebeshana wana CCM.

Kimsingi tatizo ni CCM. Mfumo wake wa uongozi na staili ya viongozi wa zama hizi wa chama hicho kukubali kuliongoza taifa hili kwa njia haramu kabisa ya kupikiana majungu.

Iwapo Amina Chifupa anastahili kuvuna kile alichopanda kwa sababu ya kukosa kwake uaminifu katika ndoa yake au hata katika chama chake, bado hilo halitoshi kulifanya taifa hili liwe la watu wanaosubiri mabaya ya wengine kama kigezo cha kuanza kuchafuana.

Wenzetu Wamarekani ambao tumenyofoa mambo kadhaa muhimu katika mfumo wa vyama vingi vya siasa wamefikia hatua ya kuwapima viongozi wao kwa kuangalia rekodi zao za utendaji wa kazi za kisiasa kabla hawajaingia katika nafasi ya uongozi.

Ingawa mfumo wetu wa siasa ya vyama vingi bado ni mchanga, binafsi naamini kwa dhati kabisa kwamba, CCM, chama kikongwe kuliko vyote, kilipaswa kujijengea mfumo madhubuti wa kuwapata viongozi wake, ambao ungekuwa na uwezo wa kuwaandaa makada, wasomi katika ngazi mbalimbali.

Hii tabia ya chama hicho tawala kujijengea desturi ya kukusanya wanachama kwa mfano wa kokoro linalovua samaki, pasipo kuangalia rekodi za siku za nyuma kisiasa, kijamii na hata kiuchumi za wanachama wake eti tu kwa sababu ya kuwaonyesha jeuri wapinzani, ni moja ya chachu kuu za kujengeka na kushamiri kwa hulka mbaya za majungu yasiyokoma ndani ya chama hicho.

Kile chama chenye heshima ambacho Baba wa Taifa alijaribu kukijenga chini ya mwamvuli wa kaulimbiu ya ‘huyu ni mwenzetu’ iliyokuja kubadili maana yake halisi ya awali na kuwa kitovu cha kuwakataa baadhi ya watu makini, leo hii inakitafuna polepole chama hicho.

Taifa linalojaribu kujitoa katika tatizo lililoota mizizi la ufisadi, kamwe haliwezi kupata nafasi ya kujinasua katika jinamizi hilo, iwapo nyufa za namna hii zitaendelea kustawi na kuboreshwa.

Leo hii unaposikia taarifa kwamba, viongozi wa juu wa kiserikali, wakijiingiza katika mitandao ya kuwabomoa baadhi ya wanasiasa na wafanyabiashara kwa sababu zisizo na maslahi ya kitaifa, unapata picha halisi ya mahali tulipo Watanzania na pengine mwelekeo wetu wa siku za usoni.

Si rahisi kujua ni vikao vingapi vya CCM au Bunge vitakaa na kulijadili suala hili la Chifupa ambalo kwa namna ambayo si rahisi kuielezea, limepenyezwa kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa njia ya barua ambayo nakala yake anayo Katibu Mkuu wa CCM.

Hivi kweli, viongozi wetu wakuu, wanazo sababu za msingi za kukubali kuingizwa katika mtandao wa majungu ambayo wakati mwingine huwa tunaambiwa huwa yana baraka za viongozi ambao ukiambiwa majina yao na kuangalia nyadhifa tulizowapa unapigwa na butwaa.

Je, baada ya sakata la Reginald Mengi na Mbunge Adam Malima, ambalo chimbuko na hitimisho lake ni majungu lililogharimu takriban sh milioni 100, bado Bunge hilo hilo na chama kile kile tawala vina sababu ya kuendelea kujiingiza katika masuala ya kijinga yasiyo na tija?

Hivi kweli tunamtendea haki spika wetu ambaye hivi sasa yuko katika kipindi kigumu cha kulijengea Bunge heshima kwa kuwa na meno ya kujadili mambo yenye tija kitaifa, kuendelea kumuingiza katika masuala ya ufuska ya wabunge wake?

Je, ni sahihi kwa Yussuf Makamba, kumuingiza katika mjadala mwingine wa ugomvi wa Amina Chifupa na mumewe na akaacha kukiandaa chama chake kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa ndani baadaye mwaka huu, au hata akaweka kando mazungumzo muhimu anayoyaongoza kati ya chama hicho na kile cha CUF.

Je, ni haki kwa Watanzania wote kujiingiza katika mtego mwingine wa kuwa washangiliaji wa ugomvi wa Mpakanjia na Amina au ufuska wa Mheshimiwa Kabwe na Amina, hata kusahau masuala mengine mazito na ya msingi tunayokabiliana nayo?

Kwa namna yoyote ile, Watanzania tunapaswa kuachana na hulka ya kuendekeza majungu kama kweli tunataka kujenga mustakabali mwema wa taifa hili wa siku zijazo.

CCM inapaswa sasa kurejea masomo ya maadili kwa viongozi wake ambayo hatimaye yatawarudisha katika mstari wa kusudio la kuasisiwa kwake. Wanahabari tunao wajibu wa kukwepa kuingia katika mtego wa habari za kashfa za ngono kila kukicha wakati nchi hii ikiwa na masuala mengi mengine ya kijamii ya kuyaandikia.

Tanzania Daima
 
Nafikiri swali muhimu hapa ni kwamba katika nchi yenye demokrasia makini au inayojaribu kuwa kama yetu, who sets the political national debates?

na kwa kutumia vigezo gani?
 
Naona hapa wote tumefungwa goli na Nchimbi.

Muhimu ni kuachana na huu upuzi.

Nakubaliana na Mkandara kwamba tunapoteza bure muda wetu. Hii topic ni siasa tupu.
 
kwa nini ili hali ile ni siasa na kaa unavyojua kuwa watu wengi wakija JF wanaingia kwanza kwenye siasa kisha ndo wanatembelea sehemu zinginezo?
 
Samvula unapenda sana udaku .Na uko kwenye Kamati ya Umoja wa Watanzania UK na kwenmye CCM UK basi utawamaliza . Yaani habari za Zitto is not an issue here . Issue kasome alichosema Mtanzania ndiyo Siasa . Udaku ule hata kutoka Bungeni was not supposed to be there . Mtu mmoja alisema wafute ile mada maana ni udaku na siasa chafu . Baadaye CCM wakagundua last minutes kuchemka kwao wakambana koo Amina asiteme Cheche . Walidhani wanataka kummliza Zitto sasa wamejiwashia moto wenyewe . Samvula wewe mtu wa Buguruni sana mada zile nenda kwenye magazeti ya Jpili . Kwenye siasa we have serious issues mzee .
 
Tuwaache washughulikie, kwanini kuna mtu hapa ana ubia na ndoa ya Medi na Chifupa? au ana ubia na maisha ya Zitto? Kama wameboronga bila ya shaka wameboronga, na hilo liwe funzo kwa wingine, hakikisha huachi ushahidi!!

Kwa hiyo kumbe tatizo ni kuacha ushahidi na sio kuzini tena? MKJJ, come on you are compromising a lot of your principles, I am afraid!

Hata hivyo kwa mujibu wa Tanzania Daima, Zitto ameshakataa katukatu kwamba alizini na dada Amina. Kwa hiyo tunaweza kusihia hapo.

Lakini narudia tu ushauri wangu wa bure kwa wahusika, ikitokea kwamba ni kweli kitendo cha zinaa kilifanyika kati ya hawa waheshimiwa wetu, ambao wote walionekana kuwa ni role models kwa vijana, wanawajibika kujitokeza hadharani kukiri na kuomba msamaha kwa kusababisha usumbufu mkubwa kwa familia zao, kwa vyama vyao na kwa taifa. Hawa ni viongozi wa kitaifa, kwa hiyo hatuwezi kulazimishwa kukubali kwamba the issue we are discussing thus far is a trivial one. Hatuwezi kuficha udhaifu wa viongozi wetu kwa kubadilisha mambo makubwa kuwa madogo.

Wale ambao wameamua kufunika kombe mwana haramu apite, siamini kwa kufanya hivyo mnawasaidia Zitto, Amina, vyama vyao wala taifa letu. Mimi siku zote nimeamini kwamba katika forum hii tutasimamia principle kwa kiasi cha kutosha na kwamba ushabiki wetu kwa vyama na wanasiasa tunaowapenda hautatuburuza kushindwa kuona ukweli wa mambo.

Hakuna shaka kwamba swala la uzinzi wengi linatushinda. Lakini hii haina maana kwamba jambo hili ni jema na kwamba likitokea tulifumbie tu macho, hasa pale linapohusu viongozi wetu. Sisi tuliobahatika kusoma na wale ambao ni viongozi wetu wa kisiasa ni vioo vya jamii yetu. Sisi na viongozi wetu ndio tunaopaswa kuongoza kila kitu yakiwemo mapambano dhidi ya ukimwi. Tutapata wapi basi nguvu za kuwahamasisha wananchi kubadili mienendo ya tabia zao za kingono ili waepuke ukimwi kama sisi wenyewe tunasema kuvuana nguo ovyo ovyo hakuna ubaya?
 
NNA OMBI MOJA KWA ADMIN

HUU UKUMBI UBADILISHWE JINA KUTOKA BUNGENI NA UWE YANAYOHUSU BUNGE NA WABUNGE

sababu moja ni kuwa hili suala halikutoka bungeni na kusema kutoka bungeni utakuwa hujatenda haki na haliendani, juast mtazamo

nnaomba kuwasilisha
 
iitwe "Ya Bunge na Wabunge" (nimefupisha tu). Binafsi naacha kuchangia jambo hili kwa wakati huu nasubiri nisikie vikao vya CCM vitafanya nini.. na kuliacha hili jambo liendelee kushughulikiwa katika familia.. n.k Mwanasiasa... uko serious sana.. that was supposed to be a joke!
 
iitwe "Ya Bunge na Wabunge" (nimefupisha tu). Binafsi naacha kuchangia jambo hili kwa wakati huu nasubiri nisikie vikao vya CCM vitafanya nini.. na kuliacha hili jambo liendelee kushughulikiwa katika familia.. n.k Mwanasiasa... uko serious sana.. that was supposed to be a joke!

Wakati wewe unasubiri vikao vya CCM viseme nini (but I thought CCM SG kwenye magazeti ya leo amesema wao hawajadili masuala binafsi ya watu), mimi nasubiri vikao vya CHADEMA viseme nini. So far, they are busy preventing news media from printing more details (i.e. evidence) (you must have noted Zitto's threat to sue anybody anayeingilia "privacy" yake). Ngoja tuone kama vyombo vina uhuru kweli. Otherwise, JF will always be the avenue.

This story inatia kichefuchefu but unfortunately it is with us and it will be with us for quite some time, depending on what Zitto will do.
 
Mugongo2
Sijakuona unatapika. In fact the impression I get is you are relishing the story.
 
NNA OMBI MOJA KWA ADMIN

HUU UKUMBI UBADILISHWE JINA KUTOKA BUNGENI NA UWE YANAYOHUSU BUNGE NA WABUNGE

sababu moja ni kuwa hili suala halikutoka bungeni na kusema kutoka bungeni utakuwa hujatenda haki na haliendani, juast mtazamo

nnaomba kuwasilisha


Fine, observed and changes to follow...

Hope wengine wanaafiki. Lakini nitaandika... Bunge na wabunge wetu au italeta maana nyingine?
 
Siko hapa kuhukumu kama "wamegandamijana" tulitegemea hayo. hebu twende mbele na nyuma, nani anajua ni sifa zipi zilimbeba AC kuingia Bungeni? Nasema tena tulitegemea hayo si AC wala MM aliye salama hivi mke haya haki ya kutoa talaka? kama ni hivyo AC alingoja nini?

Pole nyote waungana kwa hili, lakini CV ya mwanadada huyu ilikuwa inasomeka vizuri na haikuwa taabu kupata kiti cha bunge tukufu. Walijua chakula inakuja, bahati mbaya baadaye sahani ikawa mbali yao.

Ni mavuno ya rushwa ya ngono, vinginevyo hakusitahili kuwa na hadhi ya Mh.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom