Kashfa nzito: Zitto vs Amina Chifupa

Kashfa nzito: Zitto vs Amina Chifupa

Status
Not open for further replies.
Mumewe Amina hoi!

2007-05-09 16:44:36
Na Badru Kimwaga, Jijini


Siku chache tu baada ya `kumlima` talaka mkewe kwa tuhuma za kutokuwa muaminifu, katika ndoa, mfanyabiashara maarufu nchini, Bwana Mohammed Mpakanjia almaarufu kama `Meddy` imedaiwa kuwa hivi sasa yuko hoi bin taaban kitandani.

Akizungumza na Alasiri kwa njia ya simu mapema leo asubuhi, mfanyabiashara huyo ambaye pia ni mkandarasi wa kutengeneza barabara, amesema hivi sasa yu hoi kitandani kutokana na kusumbuliwa na maradhi ambayo hakuweza kuyafichua.

Meddy ametoa taarifa hizo alipoulizwa juu ya tetesi zilizozagaa mitaani kwamba kumpa kwake talaka mkewe ni kutaka kutikisa kiberiti na kwamba wakati wowote huenda akamrejea mama watoto wake na kuendelea na maisha yao kama kawaida.

Mpakanjia ametengana na mkewe, mbunge wa Viti Maalum-UVCCM, Bi.Amina Chifupa kwa kile kinachodaiwa kuwa bibie huyo alikuwa na mahusiano yasiyo rasmi na mbunge mwenzie toka chama cha upinzani cha CHADEMA, Bw. Zitto Kabwe.

`Iwe natikisa kiberiti...kibatari...ama vyovyote, siwezi kusema kwa sasa, kwa kuwa nimechoshwa kuzungumza na magazeti, pia hapa nazungumza na wewe nikiwa mgonjwa, hivyo niache nipumzike,` Mpakanjia akasema kwa upole.

Hata hivyo pamoja na kutoweza kusema anaugua kitu gani, mfanyabiashara huyo hivi karibuni kabla ya kumpa talaka mkewe alipata ajali ya kuunguliwa na gari na kujeruhiwa sehemu kadhaa za mwili wake.

Ajali hiyo ilimtokea mjini Morogoro wakati wa akielekea Dodoma kwenye shughuli zake za kikandarasi na kupelekea kulazwa hospitali kabla ya kuruhusiwa baadaye.

`Sisi tumeshawazoea wanapeana talaka na kurudiana, na hata hivi sasa pamoja na Meddy kuonekana yupo `siriasi`, lakini ukweli ni kwamba anatikisa kiberiti na wakati wowote atamrejea mkewe kama siku za nyuma,` chanzo chetu cha habari kilisema.

Chanzo hicho kimesema kuwa, wawili hao wanapendana mno na kuachana kwao si rahisi ukizingatia kuwa wana mtoto wanayempenda na kumuona kama `lulu` AbdulRahman `Rahmanino`.

Mtoa habari huyo amesema si mara ya kwanza kwa Meddy na Amina 'kumwagana' na kisha kurejeana mara panapotokea tatizo baina yao.

`Kwani unadhani ni mara ya kwanza kwa Meddy kumuacha Amina na kuapa kutorudiana naye ni kama mara mbili ameshafanya hivyo na hata hii ya safari hii ni geresha tu na ukweli muda si mrefu watarejeana na kuishi kama zamani,` kikasisitiza.

Ndipo Alasiri lilipoamua kumsaka mfanyabiashara huyo kwa njia ya simu na yeye kusema hawezi kusema kama atamrejea mkewe au la kwa vile anaumwa.

Mpaka sasa hakuna uthibitisho rasmi juu ya tuhuma hizo za mauhusiano yasiyo rasmi na haramu baina ya wabunge hao vijana, ingawa juu ya talaka imethibitishwa hata na baba mzazi wa Amina.

SOURCE: Alasiri
 
Kaka mugongomugongo pole sana ndugu yangu. Ulizoe kumuonea Amina katika magazeti yako ya udaku na kujitengenezea mamilioni sasa umegusa pabaya. Zitto sio Amina kaka jiandae kufunga biashara zako. Ile kampeni yako ya "Amina over my dead body" imefikia ukingoni kama yale ya Mzee Chifupa kukukosakosa na risasi haijakuwa somo basi jiandae na hili.
Tanzanianjema
 
Kaka mugongomugongo pole sana ndugu yangu. Ulizoe kumuonea Amina katika magazeti yako ya udaku na kujitengenezea mamilioni sasa umegusa pabaya. Zitto sio Amina kaka jiandae kufunga biashara zako. Ile kampeni yako ya "Amina over my dead body" imefikia ukingoni kama yale ya Mzee Chifupa kukukosakosa na risasi haijakuwa somo basi jiandae na hili.
Tanzanianjema

Mhhh,hapa inaelekea kuna habari ndani ya habari.Tanzanianjema,waweza kutufungua macho katika "tuhuma" hizo dhidi ya Mugongomugongo?
 
Hodi wanabodi! Heshima yenu wakuu! kwa kipindi kirefu mimi nimekuwa msomaji tu makala mbali mbali humu, bila kuchangia chochote, hivyo naheshimu sana mawazo na michango yenu yote, ila katika hili imenibidi nitoe maoni yangu.

Ama kwa hakika suala la ndoa si suala la kuliingilia, kwa maana kwamba, kwangu mimi sitaona ajabu baada ya muda mfupi ujao Bwana MM akaamua kumrudia mkewe Bi AC! Jambo ninalopenda kuwatahadharisha wanabodi n kwamba itakuwa ni aibu kubwa kwa wazee wenye busara kama nyie mkianza 'kusutwa' hadharani mkinukuliwa posts mlizoweka humu.

Jaribuni kulitafakari hili, nadhani Mzee mwkjj, Mkandara na wengineo wachache wamekuwa wajanja katika kutizama pande zote za shilingi bila kuwahukumu hao watuhumiwa moja kwa moja. Hii thread iendelee kujadiliwa ila, muwe makini kuwa huu ni udaku!, na itapofikia wakati wazee wetu mkianza kusutwa, hata maoni yenu mengi tu ya busara yataonekana kama ya udaku udaku tu. Heshima yenu wazee, naomba kutoa hoja!

Shukran.
 
Kaka mugongomugongo pole sana ndugu yangu. Ulizoe kumuonea Amina katika magazeti yako ya udaku na kujitengenezea mamilioni sasa umegusa pabaya. Zitto sio Amina kaka jiandae kufunga biashara zako. Ile kampeni yako ya "Amina over my dead body" imefikia ukingoni kama yale ya Mzee Chifupa kukukosakosa na risasi haijakuwa somo basi jiandae na hili.
Tanzanianjema

Hey! Yamekuwa haya tena! Mugongowa Mugongo una kazi kubwa!, sound people knows u more than urself.
 
  • Thanks
Reactions: amu
Mwandishi Wetu
HabariLeo; Wednesday,May 09, 2007 @00:06



Mbunge wa Viti Maalum (Vijana-CCM), Amina Chifupa akiwa nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma. (Na Mpigapicha Wetu).
BAADHI ya viongozi wa ngazi za juu serikalini na CCM, wanadaiwa kumkataza katika dakika za mwisho, Mbunge wa Viti Maalum Amina Chifupa (CCM) asianike masuala ya familia yake na siasa kwa umma kupitia vyombo vya habari.

Habari za uhakika zinaeleza kuwa Amina alikatazwa kwa nyakati tofauti na viongozi kwa kile kinachodaiwa kingevuruga mambo hata ndani ya CCM.

Juzi Amina alijiandaa kuzungumza na waandishi wa habari katika Idara ya Habari (Maelezo) Dar es Salaam, kuhusu mvurugano uliotokea kwenye ndoa na nia yake ya kuwania nafasi ya ju ya uongozi ndani ya Umoja wa Vijana wa CCM. Hata hivyo, katika mkutano huo hakutokea na badala yake alijitokeza baba yake mzazi Hamis Chifupa, hali ambayo ilifanya masuala nyeti ambayo angeyaibua Amina, kufichwa.

Baba yake Amina katika mkutano huo alionekana hakuweza kujibu maswali ya waandishi wa habari ilivyotakiwa. Vyanzo vya habari vinaeleza kuwa Amina alipanga kuanika ‘madudu’ yote yaliyotengenezwa na wapinzani wake ndani ya CCM baada ya kuhisi anaonyesha nia ya kuwania nafasi ya juu ndani ya UV-CCM.

Habari zinasema viogogo waliamua kujitosa kuepusha mvurugano ambao ungeweza kujitokeza ndani ya CCM na Serikali kwa ujumlakama angezungumza na vyombo vya habari. Kuvunjika kwa ndoa ya Amina na Mohammed Mpakanjia kunahusishwa moja kwa moja na masuala ya kinyang’anyiro cha uongozi ndani ya UV- CCM.

Moja ya ujumbe wa maandishi ambao unaonyesha kuwapo kwa mvutano unaotokana na kinyang’anyiro cha uongozi ndani ya CCM ni ule unaodaiwa kutumwa na Amina kwa mmoja wa vigogo wa CCM na kiongozi wa Serikali ambao ulisomeka: “Alichounganisha Mwenyezi Mungu binadamu hawezi kukitenganisha.

Nakuheshimu sana kama kiongozi wangu, Mwenyekiti wangu, Naibu Waziri, M-NEC, M-CC, mkubwa wangu kiumri, mbunge nakadhalika. Nimesikitishwa sana jitihada za kutaka kuvuruga ndoa yangu, nakutakia kila la heri, lakini usisahau malipo ni hapa hapa duniani na kila mwenye kufanyia wenzake mabaya na yeye hulipwa kwa ubaya.

Nampenda sana mume wangu na ntailinda ndoa yangu kwa gharama yoyote cko tayari kumpoteza, mi ni zaidi ya mwanamke. Asante sana, kila la heri na kazi yenye katika kulifanikisha hilo, wizara yako nyeti sana, ina mambo mengi sana. Bye.

Ujumbe huo unadaiwa kusambazwa Mei 3, mwaka huu kwa baadhi ya watu wa karibu wa Amina na kigogo aliyetumiwa ujumbe huo.

Mara nyingi wakati uchaguzi unapoingia ndani ya CCM, huibuka kashfa za kila aina, hali ambayo kuweza hata kuwaharibia sifa watu wanaowania nafasi mbalimbali. CCM imekwisha kuanza kufanya uchaguzi wa viongozi wake katika ngazi mbalimbali kuanzia ngazi ya mashina.
 
Habari ambazo zinazidi kupenyezwa kwa wenu mtiifu... ni kuwa bi. Amina inadaiwa hali yangu ya kiafya ya kiakili si nzuri na licha ya watu wa karibu kutambua hilo hajafikishwa hospitali hadi hivi sasa. Jambo lolote ambalo litamtokea akiwa mikononi mwa hawa jamaa wajiandae kwa hatua kali za kisheria kwa kumshikilia Mbunge wa Jamhuri ya Muungano bila ya ridhaa yake. Kama kweli Bi. Chifupa hali yake ndivyo ilivyo apelekwe hospitali kabla mambo hayajawa mabaya, haitaeleweka!!

Free Amina Now!
 
Kaka mugongomugongo pole sana ndugu yangu. Ulizoe kumuonea Amina katika magazeti yako ya udaku na kujitengenezea mamilioni sasa umegusa pabaya. Zitto sio Amina kaka jiandae kufunga biashara zako. Ile kampeni yako ya "Amina over my dead body" imefikia ukingoni kama yale ya Mzee Chifupa kukukosakosa na risasi haijakuwa somo basi jiandae na hili.
Tanzanianjema

Eh!! Yashakuwa haya tena, ndio maana naipenda JF
 
Mambo yanatiririka kwa haraka kweli.... kuna kila uwezekano wa Amina kujivua Ubunge (kuvuliwa??? kwa kisingizio cha kujiuzulu mwenyewe?) kwani itakuwa vigumu kwa minders wake kumuacha azungumze hadharani. Jitihada za kutaka kuwaambia anachotaka kuzungumzia hadharani zimegonga mwamba.
 
Hawa watu wawili ni watu wazima na akili zao, wana uhuru wa kufanya maamuzi, ya ku 'do' au kuto ku'do' . Kama wamefanya au la! wao ndio wanaojua.Tukianza kuangaliana kwa uchafu hapa nani atapona? sote tunajua hata vigogo wetu walivyo wachafuzi wa mazingira! Nini hii ya Amina na Zitto?Tuyaache ,Ni masuala ya watu binafsi .....Ndugu zetu wa CCm wajanja sana, wameshindwa kuelezea ufujaji wa fedha walioufanya kama Ripoti ya Mkaguzi mkuu inavyoooshesha wanaanza kutudanganyia Zitto na Amina.Na sisi tusiingie kwenye mkumbo huo! Tuhoji mambo yenye maslahi ya Umma! Propaganda za CCM zisitupeleke wanapotaka wao twende!Mandugu nchi yetu yazidi ingia shimoni!
 
Nasema hivi! Nchi yetu imepoteze Trillion 1.3 kwenye madini, imeshindwa kujibu bungeni Bil 7 ambazo hazijulikani zilipo kwenye matumizi ya ziada 2003/2004, imeshindwa kuelezea matumizi ya maduhuli lukuki kwenye ripoti ya mkaguzi, inajenga ofisi mpya ya waziri mkuu(jijini Dar es salaam), imeshindwa kuidai kodi kampuni ya williamson Diamond toka mwaka 1980 mpaka leo( japo mkataba wa mwaka 1994) , uliwataka waanze kuwadai kodi toka 1999? Tunaye Richmond na Dada yake Dowans anayepigwa dana dana Bungeni! Tunaye Tanzania Greens ambaye inasemekana ni pacha wake TIC centre- kwa maana kwamba mwekezeji yeyote akienda TIC anapelekwa kwenye kampuni ya CCM ...nk nk nk...........tuache mambo yasiyo na Tija, tujadili issues.... Tutaachiwa mahandaki!
 
mnyalu pokea 5.
hata mimi naona hii shughuli ya ac na kz ni
changa la macho. si bure ni kwa makusudi watu
wanaelekezwa kwingine ili wasijadili masuala muhimu
ya wakati huu.
 
Mzee Mugongo mugongo, heshima mbele bro kwa kuweza kuongeza heshima ya forum, maana yako sio mawe ila ni kokoto, na keep it up bro!

Mzee TZ njema,

Mugongox2 has nothing to do na any gazeti wala media outlet za bongo, ninamfahamu in the real life ndio maana ninashangaa ninapoona anpachikwa majina na maneno kibao ambayo wala hahusiani nayo, nafikiri tuache tabia ya kusema hapa kwenye forum bila ya kuwa na ukweli kuhusu watu tusiowajua,

I am amazed na jinsi watu wanavyoweza ku-create maneno yasiyokuwa na ukweli kuhusu wengine, na baadhi yetu wakaamini, I mean Mugongo au kwa jina lake maarufu Songombwingo, anahusiana nini na magazeti na Zitto? Pleaseee!


Kuhusu hii ishu ninasema kwamba ni halali kuizungumzia hapa na popote pale Tanzania, maana ni lazima tujue kesho na kesho kutwa, tutawapaje hawa wabunge wa wawili madaraka ya kuamua mambo muhimu ya taifa letu, wakati tayari tunajua kuwa ni wadhaifu, kwa mfano Tanzania tumeamua kumpa ac au Zeeee madaraka ya kutuamulia kama taifa kama tujiunge na EAC au tusijiunge nayo, sasa ni wazi kabisaa kuwa kama Kenya wanaitaka zaidi EAC, watampa ac mwanaume ili aamue kwa kuwapendelea, au kama ni Zeee watampa kimwana aaamue kwa upendeleo wa nchi hiyo, huku sisi tukiumia,

I mean wewe kweli ngono iliyomfanya Mungu amfukuze Bin-Adam na Eva kule Paradise, unasema ni ishu ya binafsi? Then why the creator wa life na dunia hakusema hivyo, kuwa hii ishu ni ya binafsi? Yes, kwa maneno yenu hayo munamuita the creator, yaani God kuwa ni mjinga kwa kuisambaratisha Sodoma na Gomora, si wote tunajua kuwa chanzo chake kilikuwa ni nini kama sio ngono? Kwa nini hakusema hiii ni ishu ya binafsi kwa hiyo Noah tengeneza boti kila mtu aingie, no wale mabingwa wa ngono hawakuingia kwenye ile boti bro! Ninasema hii ishu ni valid na ni yetu as a nation, we are not about ku-create taifa la wazinzi, anayetaka kuendelea na huo uzinzi ni lazima aufanye kwa siri, lakini tukijua na ni kiongozi wetu wa taifa, tutamvua nguo hapa hapa, msituambie kuwa waziri wa Liberia aliyejiuzulu majuzi baada ya picha zake kuwekwa nje alikuwa mjinga, na huyu naibu wa Condoleeeza-Rice, aliyejiuzulu majuzi kwa kutuhumiwa kupewa massage tu naye ni mjinga je angekula kama huyu Zeee ingekuwaje? Rais wa benki ya dunia antaka kuuwekwa nje kwa sababu tu ya kumpandisha cheo kimada wake leo mnasema eti ni ishu binafsi?

Huyu ac anapenda sana ujiko, mimi ninamlinganisha na Paris Hilton celebrity for nothing, na pia ni lazima nii-question system ya ccm ya kuwachagua wagombea wake wa ubunge, how in the world unaweza kumpitisha huyu denish ambaye toka aingie imekuwa ni aibu tupu, kwanza akadai kuwa bendi ya academia ni bora kuliko Twanga, mbunge mzima wa taifa, next ikawa wauza unga, halafu mbunge mzima wa taifa haelewi dressing code ya bunge la taifa, sasa ngono na mtu ambaye si mumewe mbunge mzima wa taifa, what the hell is going on na hili taifa?

I mean this en thing, yaani total waste, the guy is a big joke to the point alishafikia mahali akadhani anaweza kuwa Veeep wa ccm, mikono yake imejaa damu kwa ajili ya madaraka, sasa ungetegemea kuwa baaada ya kupewa makali yake na Muuungwana, kwamba atabadilika, kumbe bureee waziri wa nchi anafanya nini na kuwaandikia wananchi talaka kwa wake zao ambao ni wabunge? angekuwa Spika ningeelewa kuwa kwa sababu ni mkuuu wa kazi wa mke, Muuungwaana it is about time ukaanza kuwapumzisha mapema hawa nanga ambao tunajua kuwa unataka kuwatema kabla ya uchaguzi, WHy not now?

Mpakanjia ni mtoto wa kunyumba, lakini damn what is this?
 
Mwanakijiji,

Mbona watuzingua?.... Kinachoendelea ni nini hasa?
AC kazuiwa kutoka nje ama kwenda hospitali na nani, maradhi yake ni yapi hayo na yametokana na kitu gani?
nani anayemzuia kuzungumza na waandishi wa habari na nani anayetaka ajiuzulu...
 
Mkandara, Amina amezuiwa kuzungumza na baadhi ya watu (angalia kwenye post Kuu) na kama nilivyowaripotia mara ya kwanza baada ya kugundua hatatokea hadharani. Sababu kubwa ambayo imetolewa ni kuwa hali yake ya kiakili inatajwa kuwa si nzuri na leo kuna maneno ya kuwa "she is under somekind of suicide watch"... Kuhusu kujiuzulu bado sijasikia source nyingine kuconform lakini inatafutwa njia muafaka ya kuhakikisha kuwa atakapotokea hadharani hatazungumzia sakata hili. Kwa mtu ambaye ni free spirit kama yeye basi inakuwa vigumu kukubaliana na wale wanaomtaka anyamaze wakati ndoa yake iko matatani, hadhi yake imeendelea kuchafuliwa na heshima yake kukanyagwa kanyagwa. Kwa maoni yake njia pekee ni "kuweka wazi mambo yote yaliyosababisha kuvunjika ndoa yake.

Kuna baadhi ya "wazee" wanajaribu kuwarejesha wana ndoa hawa ili mambo haya yamalizwe kiutu uzima.

Maoni yangu:

- Jinsi gani AC atalalamika mbele ya wakubwa wa chama kuhusu "mbaya wake" na jinsi wakubwa hao watashughulikia madai hayo ni kama vita vya panzi mbele ya kunguru!

- Mtego ambao Zitto amewekewa ni mbaya sana na kwa kutokutaka kulikalia kimya jambo hili anazidi kujinasisha. Hata hivyo inaonekana ni mtego wa kujitakia.
 
Mzee ES
Mimi hainishangazi kitu. That is how low CCM has sunk.Mwungwana kwa kuhonga taifa zima ili apate kura sitegemei kuwa atakuwa mstari wa mbele kupambana na uovu huu ulioshamiri nchini. Kama alivyosema Mkapa, wote ndani ya CCM wameshaloa damu ya corruption ndiyo maana kila kukicha hamna nafuu ya Richmond, Dowans,madini na kila kitu wanachogusa. Ninachosubiri sasa ni mpasuko wa ndani ambao utasaidia kulikomboa taifa letu na hawa majambazi waliojipachika madarakani.
 
Mlalahoi.. hiyo ndiyo sauti inayotakiwa kusikika. Hata kama hawezi kuzungumza hadharani, basi aonekane hadharani kuwa ni mzima wa afya. Kama ni mgonjwa apelekwe hospitali na siyo kushikiliwa "ili atulie". Mnyezi Mungu ananjia nyingi za kuwaumbua watu!! Jambo likimtokea binti huyu kuna watu itapasa waseme. Kama amefanya kosa la kimaadili, hilo ni jambo moja la kumuangalia binadamu mwenzako kama "pensheni" na hivyo kufanya lolote lile ili "pensheni" isikatike ni kosa kubwa zaidi kwani wanamuangalia binadamu mwenzao kama kitu kinachoweza kutumiwa!

Katiba yetu iko wazi kuhusu hili (msisitizo wote wangu):

Ibara 16:1

Kila mtu anastahili kuheshimiwa na kupata hifadhi
kwa nafsi yake, maisha yake binafsi na familia yake na
unyumba wake, na pia heshima na hifadhi ya maskani yake na
mawasiliano yake ya binafsi.


Hivyo, kama Amina anatakiwa kuwasiliana na mtu yeyote basi waliomchukulia simu yake WANAVUNJA KATIBA

Ibara 17:1

Kila raia (hata kama ni Mbunge! M.M.) wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya
kwenda kokote katika Jamhuri ya Muungano na kuishi katika
sehemu yoyote, kutoka nje ya nchi na kuingia, na pia haki ya
kutoshurutishwa kuhama au kufukuzwa
kutoka katika Jamhuri
ya Muungano.


Wale ambao wanamlazimisha Amina kuwa mahali fulani wakati yeye anataka kuwa mahali kwingine WANAVUNJA KATIBA!

Ibara 18:1

Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru
kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake
, na kutafuta,
kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo
chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa
mawasiliano yake kutoingiliwa kati.


Amina alitaka kutoa mawazo na maoni yake kama mtu huru. Kuna watu wametangaza hadharani ati wamemzuia! Kama Amina angekuwa mtoto wa miaka 18 wazazi wake kweli wangeweza kumsemea. Lakini akiwa mtu mzima tena Mbunge wa Bunge takatifu la Enzi la Jamhuri yetu Tukufu ya Muungano! anayo haki ya kutoa maoni yake bila "Mawasiliano yake kutoingiliwa kati". Waliokiri kufanya hivyo WANAVUNJA KATIBA!

Hivyo basi:

- Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mhe. Amina Chifupa Mpaka nje, apewe uhuru wake wa kusema, kuwaza, kwenda, kufanya atakalo bila kuingiliwa na mtu yeyote, kulazimishwa na mtu yeyote au kukwaza na mtu yeyote hata kama mtu huyu ni ndugu wa damu.

- Familia wanaweza kumshauri mtoto wao na ndugu yao kufanya lolote au kutofanya lolote, lakini kama amewaambia anataka kufanya jambo fulani na wao wanamng'ang'aniza asifanye wakati yeye akiwa na akili timamu na mtu huru anataka kufanya vinginevyo watu hao watishiwe kuchukuliwa hatua za kisheria wasipobadili vitendo vyao mara moja.

- Bi. Amina aachiliwe huru mara moja bila ya masharti yoyote na kama hataki kuzungumzia mambo ya ndoa yake hadharani huo ni uhuru wake na asilazimishwe na mtu yeyote kufanya hivyo. Na kama anataka kuzungumza hadharani basi asinyamazishwe na mtu yeyote hata kama mtu huyo ana malengo mazuri na nia nzuri!

Wenye kuchapisha tisheti chapesheni na picha yake muiweke hadharani hadi huyo binti aonekane hadharani mzima wa afya akiwa mtu huru!!! Uhuru katika nchi yetu siyo hisani ya wazazi wetu kwani Katiba inasema hivi:

Ibara 12:1

Binadamu wote huzaliwa huru, na wote ni sawa.

Miongoni mwa binadamu hao ni Mhe. Amina wa Mpakanjia!!!!
hivyo basi,

FREE AMINA NOW!! FREE AMINA NOW! FREE AMINA NOW

chapisheni tsheti n.k!! ili liwe somo kwa watanzania kuwa nchi yetu bado huru na itaendelea kuwa huru!!!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom