Kashfa nzito: Zitto vs Amina Chifupa

Kashfa nzito: Zitto vs Amina Chifupa

Status
Not open for further replies.
Mzee Mwanakijiji uliye ughaibuni. Amina yuko kwao Mikocheni! Infact nasikia kisaikolojia hali yake haitangengamaa...hasa ukizingatia kwamba alikuwa amepania sana kushusha nondo kwenye press conference wakamweka plasta mdomoni.

Naafikiana na wewe kwa kukubali kufunga mjadala wa ngono!hauna tija!

hamna kitu waswahili wakipendacho kama ngono[mtan'samehe]na hadithi zake[kama hii]....we semaaa....kaa mlango wazi...wenzako watapeta!...si unaona shigongo and co. wanavyouza vijarida vyao.....halafu vinavyosomwa kwa wingi...

mawazo yako ni bora....ila hayatekelezeki...bila udikteta...ambao humu haumo!
 
Mnyalu...kama hali yake kisaikolojia siyo nzuri hatakiwi kuwa nyumbani.... apelekwe hospitali... na kwa vile ni mbunge wa Tanzania.. wananchi wanayo haki ya kujua hali ya kiongozi wao kwani wanajali hali yake. So, ni mgonjwa, yuko kifungoni, anaangaliwa asijiue????
 
Mnyalu...kama hali yake kisaikolojia siyo nzuri hatakiwi kuwa nyumbani.... apelekwe hospitali... na kwa vile ni mbunge wa Tanzania.. wananchi wanayo haki ya kujua hali ya kiongozi wao kwani wanajali hali yake. So, ni mgonjwa, yuko kifungoni, anaangaliwa asijiue????

pole mzee wangu wa kijijini....binti ataendelea vizuri tu....kama alivyosema mwenyewe[kwenye hiyo sms]kwamba mchinja huchinjwa...tusubiri...yaonekana ameaga kwao.

ila usiwe na wasi...hiyo hali aliyonayo[kiakili]itapona tu.

pole mzee!
 
Maajabu ya Mussa haya!

Mumewe Amina hoi!

2007-05-09 16:44:36
Na Badru Kimwaga, Jijini

Siku chache tu baada ya `kumlima` talaka mkewe kwa tuhuma za kutokuwa muaminifu, katika ndoa, mfanyabiashara maarufu nchini, Bwana Mohammed Mpakanjia almaarufu kama `Meddy` imedaiwa kuwa hivi sasa yuko hoi bin taaban kitandani.
Akizungumza na Alasiri kwa njia ya simu mapema leo asubuhi, mfanyabiashara huyo ambaye pia ni mkandarasi wa kutengeneza barabara, amesema hivi sasa yu hoi kitandani kutokana na kusumbuliwa na maradhi ambayo hakuweza kuyafichua.
Meddy ametoa taarifa hizo alipoulizwa juu ya tetesi zilizozagaa mitaani kwamba kumpa kwake talaka mkewe ni kutaka kutikisa kiberiti na kwamba wakati wowote huenda akamrejea mama watoto wake na kuendelea na maisha yao kama kawaida.
Mpakanjia ametengana na mkewe, mbunge wa Viti Maalum-UVCCM, Bi.Amina Chifupa kwa kile kinachodaiwa kuwa bibie huyo alikuwa na mahusiano yasiyo rasmi na mbunge mwenzie toka chama cha upinzani cha CHADEMA, Bw. Zitto Kabwe.
`Iwe natikisa kiberiti...kibatari...ama vyovyote, siwezi kusema kwa sasa, kwa kuwa nimechoshwa kuzungumza na magazeti, pia hapa nazungumza na wewe nikiwa mgonjwa, hivyo niache nipumzike,` Mpakanjia akasema kwa upole.
Hata hivyo pamoja na kutoweza kusema anaugua kitu gani, mfanyabiashara huyo hivi karibuni kabla ya kumpa talaka mkewe alipata ajali ya kuunguliwa na gari na kujeruhiwa sehemu kadhaa za mwili wake.
Ajali hiyo ilimtokea mjini Morogoro wakati wa akielekea Dodoma kwenye shughuli zake za kikandarasi na kupelekea kulazwa hospitali kabla ya kuruhusiwa baadaye.
`Sisi tumeshawazoea wanapeana talaka na kurudiana, na hata hivi sasa pamoja na Meddy kuonekana yupo `siriasi`, lakini ukweli ni kwamba anatikisa kiberiti na wakati wowote atamrejea mkewe kama siku za nyuma,` chanzo chetu cha habari kilisema.
Chanzo hicho kimesema kuwa, wawili hao wanapendana mno na kuachana kwao si rahisi ukizingatia kuwa wana mtoto wanayempenda na kumuona kama `lulu` AbdulRahman `Rahmanino`.
Mtoa habari huyo amesema si mara ya kwanza kwa Meddy na Amina 'kumwagana' na kisha kurejeana mara panapotokea tatizo baina yao.
`Kwani unadhani ni mara ya kwanza kwa Meddy kumuacha Amina na kuapa kutorudiana naye ni kama mara mbili ameshafanya hivyo na hata hii ya safari hii ni geresha tu na ukweli muda si mrefu watarejeana na kuishi kama zamani,` kikasisitiza.
Ndipo Alasiri lilipoamua kumsaka mfanyabiashara huyo kwa njia ya simu na yeye kusema hawezi kusema kama atamrejea mkewe au la kwa vile anaumwa.
Mpaka sasa hakuna uthibitisho rasmi juu ya tuhuma hizo za mauhusiano yasiyo rasmi na haramu baina ya wabunge hao vijana, ingawa juu ya talaka imethibitishwa hata na baba mzazi wa Amina.
 
Mzee Bob,

Duh! hii article kali sana bro, naona yetu sasa yatakuwa macho huku tukimsubirir Mzee Zeee, nasikia jamaa wa cccm wanajitayarisha kutoa picha za huo mchezo, wamesubirir tu Zeee aseme halafu waachie kama zile za wazirir wa Liberia,

Eeeh bwana patakuwa patamu sana hapo!
 
Padri asababisha kifo akimtoa mimba binti




na Ramadhani Siwayombe, Manyara



PADRI mmoja wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mbulu (jina linahifadhiwa), anatuhumiwa kumpa ujauzito mwanafunzi wa kidato cha pili wa Shule ya Sekondari ya Dongobesh wilayani Mbulu.
Kama hiyo haitoshi, inadaiwa kuwa baada ya kubaini kuwa binti huyo ni mjamzito, padri huyo alimtorosha na kwenda naye mjini Babati kwa lengo la kuitoa mimba hiyo lakini kwa bahati mbaya binti huyo alifariki dunia wakati wa zoezi hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari juzi, shangazi wa binti huyo, ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini kwa kuhofia usalama wake, alimtaja mwanafunzi huyo kuwa ni Veneranda Anthony Yessaya, ambaye alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na padri huyo kwa muda mrefu.

Shangazi huyo alisema kuwa padri huyo alifanikiwa kumrubuni binti huyo kwa njia ya kujifanya mfadhili wake, ambaye atamgharimia masomo.

Alisema padri huyo alijitokeza wakati marehemu Veneranda akijiunga na kidato cha kwanza mwaka 2006 katika Shule ya Sekondari ya Gidhim, iliyopo wilayani Mbulu.

Alibainisha kuwa, padri huyo aliamua kumhamisha na kumpeleka Shule ya Sekondari ya Endaraftal, iliyopo wilayani Karatu.

Alisema baada ya muda, walishangaa padri huyo akimhamisha tena binti huyo na kumpeleka Dongobesh Sekondari, ambako aliendelea kuwa na mahusiano naye kimapenzi.

Akisimulia zaidi, shangazi huyo alisema walianza kuhisi uhusiano usiofaa baina ya binti yao na mfadhili wake Aprili 20, mwaka huu, baada ya padri huyo, ambaye alihamishiwa Kiru akitokea Dongobesh, kufika kijijini Dongobesh na kuonekana akiwa na binti huyo.

Na baada ya kuulizwa, padri huyo alidai amefika hapo kumchukua ili akamnunulie vitu muhimu vya shuleni.

Aprili 26, binti huyo aliomba ruhusa kwa uongozi wa shule, kwa madai kuwa alikuwa anakwenda nyumbani kwa wazazi wake, ambapo baba yake ni mwalimu katika Shule ya Msingi ya Dumanangw na alipofika nyumbani alipewa fedha na wazazi wake na kuaga kuwa anarejea shuleni.

Shangazi yake huyo alisema hata hivyo, binti huyo hakufika shuleni tena na badala yake alikwenda Babati, ambako inadaiwa alikutana na padri huyo na walikwenda katika moja ya nyumba ya kulala wageni mjini hapo.

Ilielezwa kwamba baada ya siku kama mbili, padri huyo alimfikisha binti huyo katika hospitali moja (jina tunalo), iliyopo mjini Babati, akiwa mahututi. Baadaye, padri alimpigia simu mama mzazi wa binti huyo, ambaye kwa wakati huo alikuwa mjini Arusha.

"Baada ya kuona hali ya binti huyo ni mbaya, kabla hata ya wazazi wa binti huyo kufika, padri huyo alitoroka na kumwacha binti huyo katika hospitali hiyo na baadaye alifika mama yake na baba yake ambao walilazimika kumchukua na kumpeleka Hospitali ya Rufaa ya KCMC iliyopo mjini Moshi," alisimulia shangazi huyo.

Uchunguzi uliofanywa na daktari katika Hospitali ya KCMC ulibaini kuwa binti huyo alikuwa ametolewa mimba lakini kitendo hicho hakikufanywa ipasavyo kwani kulikuwa na uchafu uliokuwa umebaki tumboni na kufanya sehemu za mwili wake zianze kuoza.

Akisimulia mkasa huo kijijini kwake Dongobesh juzi, baba mzazi wa marehemu, Mwalimu Anthony, alisema: "Uchunguzi wa madaktari wa Hospitali ya KCMC umegundua kuwa utumbo pamoja mfuko wa uzazi navyo vilianza kuoza."


Mwalimu Anthony alisema kutokana na hali hiyo, familia yake imeamua kufungua kesi Polisi dhidi ya padri huyo. Hata hivyo, alidai kuwa uongozi wa kanisa jimboni Mbulu unamkingia kifua padri huyo ambaye amejificha.

Mmoja wa madaktari walioufanyia uchunguzi mwili wa binti huyo, ambaye alikataa kutajwa kwa vile si msemaji wa hospitali hiyo, alisema binti huyo aliyekuwa na ujauzito wa miezi mitano, alikuwa ametolewa mimba kwa vifaa vichafu.
 
Sifikiri kama Zitto atasema lolote kabla ya Amina kusema kwanza.. sasa hapo watu watakinga mikono kungojea mvua jangwani!
 
Tunafahamu kuwa ufuska ni jambo la kawaida kwa wanasiasa wa Tanzania. Taarifa zinazowahusiha viongozi wakuu wa serikali kufanya ngono na wake za watu ni nyingi sana hadi wengine wakavunjiwa ndoa zao na wengine kupewe UDC kutokana na ngono za viongozi wa serikali. Hawa ZK na AC wanasakamwa kwa sababu za kisiasa tu siyo kwa sababu za kimaadilia kama wanavyotaka tuamini. Kwa vile hakuna differential power baina yao, ni wazi kabisa kuwa waliafikiana kufanyana vile kwa hiari zao kabisa. Ingawa kuna kosa la kimaadili katika maamuzi yao hayo, lakini hilo siyo swala la kupelekwa kwa spika au kamati kuu au organ nyingine yoyote kwa vile hakuna aliyetumia madaraka yake vibaya ili kuweza kumfaidi mwenzie kati yao.


Kama kweli viongozi mafuska wote na wale wanaotumia vibaya madaraka yao wakijiuzulu, Tanzania tutabaki hatuna serikali kabisa. Itabidi tuitishe uchaguzi mkuu mara moja

Ninaamini kabisa kuwa Bwana Medi ndiye bomu kwa vile alikurupuka sana alivyoambiwa mambo hayo bila hata kuyatafakari. Alitumiwa kusudi kutimiza haja ya kisiasa ya maadui wa AC na ZK na akatumika. nadhani baada ya kutafakri sasa hivi anajutia na ndiyo maana taarifa zake za hivi karibuni zimekuwa zinaonyesha kuwa anajutia hatua aliyochukua.
 
Kitendo cha kumteka nyara huyu binti baada ya skendo lile kinaonyesha kuwa skendo lenyewe lilikuwa la kupikwa tu, na alivyotishia kuwa atatoa siri zao wakaogopa kwa kufanya vile. Huenda sasa hivi wanamshawishi kwa vitisho kuwa ukitoa siri utavuliwa uanachama na kupoteza ubunge. Sijui ukweli wenyewe ni nini ila hizi ni siasa za kupumbavu kweli kweli kumnyamazisha mtu kwa nguvu kusudi ukweli wake usieleweke.

Kama kweli wana picha za video kuthibitisha kuwa ZK na AC walikuwa wauvunja mambo si waitoe na wamwache naye atoe stori zake? Tanzania ni nchi huru jamani, au hatujui maana ya uhuru wetu?
 
Kichuguu, inasikitisha watu wanafikiri tunazungumzia mambo ya ngono hapa. Tunachozungumzia ni jambo zito sana. Mbunge wa Jamhuri ya Muungano anataka kuzungumza na waandishi akikimbilia haki yake ya kutoa maoni na mawazo ili kusema alichonacho halafu analazimishwa na watu wachache na kunyang'anywa simu, na kila analofanya kuwa na watu wanaomuangalia. Dereva wake amebakia kushangaa kwani hawezi kumsikiliza bosi wake na kwenda naye anakotaka kwenda... Kulifumbia macho jambo hili ni ukosefu mkubwa wa maadili kwa kuruhusu ukandamizaji mbele ya macho yetu!!

Je, hebu jiulizeni hivi Amina atapata nafasi yoyote tena ya kusimama hadharani na kusema lolote kwa uhuru wake? Je akitokea na kusema "nimebadili mawazo" huku kazungukwa na wanafamilia, mtaamini maneno yake? Je kuanzia sasa atakuwa huru tena kwenda mahali popote, kukutana na mtu yeyote, na wakati wowote bila kuwa na mtu wa karibu "kumsimamia"? Je Amina anaweza kuitisha mkutano wa waandishi wa habari akitaka kuzungumzia mambo mengine ya kijamii bila kufanya "wakubwa" waumwematumbo?

Kuna njia mbili kubwa za kumnyamazisha na ya kwanza imeshaanza kuwekewa msingi:

a. Madai ya kuwa ni mgonjwa wa kiakili/saikokojia.
Kumbukeni kuwa kwa mujibu wa sheria zetu "akili timamu" ni mojawapo ya sifa zinazomwezesha mtu kuwa Mbunge. Je, Amina bado ana "akili timamu"?

b. Ya pili ni kumrudisha kwa mumewe.

c. La tatu nitawaacha mlifikirie....

FAN FAN FAN
 
1251.jpg


1250.jpg
 
*Baadhi wahofia siri za chama hicho kuvujia CCM
*Wapo waliosubiri kitoe tamko kuhusiana na hilo

Na Waandishi Wetu

BAADHI ya viongozi, makada na washabiki wa CHADEMA wameelezea kufadhaishwa na madai dhidi ya Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Bw. Zitto Kabwe, kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mke wa mtu hadi kuvunja ndoa yake.

Wamesema uhusiano wake na Mbunge wa Viti Maalumu (Vijana) kupitia Bibi Amina Chifupa (CCM), umekiweka njia panda chama hicho.
Wakizungumza kwa wnyakati tofauti na gazeti hili jana Dar es Salaam, wengi walieleza kuwa na wasiwasi kwamba baadhi ya mambo muhimu yanayohusu CHADEMA pamoja na mikakati yake yatakuwa yamevujishwa kwa CCM kupitia kwa Bi. Chifupa.

Baadhi yao walielezea wasiwasi mkubwa kwamba huenda chanzo cha uhusiano huo kilikuwa ni mpango wa CCM kumtumia Bi. Chifupa kumshawishi Bw. Kabwe kuhamia CCM.

Bw. Kabwe amekuwa mmoja wa viongozi wa vyama vya upinzani ambaye amekuwa akitafutwa kwa muda mrefu na CCM kuhamia chama hicho.

Wengine walielezea kusikitishwa kwao na Bw. Kabwe ambaye amewaangusha kwa kiasi kikubwa baada ya wanachama na mashabiki wa CHADEMA kuweka matumaini makubwa kwa mbunge huyo, kwamba ni kiongozi makini na mwadilifu.

"Siku zote tumekuwa tukijua kwamba kuna ufuska wakati wa vikao vya Bunge. Lakini sikuwahi kufikiria kabisa, kwamba Bw. Kabwe angekuwa mmoja kati ya watu wanaofanya vitendo hivyo. Kwa kweli ametuangusha sana," alikaririwa Bw. Pendael Macha ambaye lijitambulisha kuwa mmoja wa washabiki wa CHADEMA aliyekutwa akisubiri basi eneo la Mchikichini, Ilala.

Baadhi yao walielezea kusikitishwa kwao na kitendo cha mbunge huyo kujitetea kwa kusema kwamba atavifikisha mahakamani vyombo vya habari au watu wanaoingilia maisha yake binafsi.

"Mimi sijawahi kusikia kiongozi wa umma ana maisha binafsi. Wewe ukiwa mbunge, basi kila unalofanya linatazamwa kwa kina na linaongelewa na jamii. Cha msingi hapa ni kwa mwenzetu huyu kuja na kusema ukweli wake wa ndani na kama ni kuomba radhi, kwa familia ya Mpakanjia, kwa wana CHADEMA na umma kwa ujumla, basi tutamsikiliza," aliongeza.

Hata hivyo, wengine walilihusisha sakata hilo zima na siasa chafu zinazoendelea kuhusu nafasi ya uenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Taifa wa CCM ambapo inasemekana Bi. Chifupa alionesha nia ya kugombea mwakani.

Hata hivyo, wengine walibainisha kwamba suala la msingi ni maadili binafsi ya wabunge hawa vijana wawili. "Hapa suala si siasa. Kama Amina angeheshimu ndoa yake na kama Zitto angemheshimu Amina kama mke wa mtu, yote haya yasingetokea".

Baadhi ya wananchi waliohojiwa, walishangazwa na ukimya wa CHADEMA katika suala hili, wakieleza kwamba CHADEMA ni chama ambacho hutoa matamko ya haraka haraka, mara linapotokea jambo lenye mjadala katika jamii.

Walisema hii ni dalili, kwamba mambo si shwari ndani ya chama hicho baada ya Bw. Kabwe kuwaweka njia panda wenzake na kuamua kukimbilia Kigoma, badala ya kubaki Dar es Salaam na kutafuta namna ya kukabiliana nalo.

Baadhi yao waliohojiwa kwa masharti ya kutotajwa majina, walitilia shaka zaidi kwamba huenda Bw. Kabwe alikuwa akivujisha siri za CHADEMA kwa Bi. Chifupa ambaye yeye na baba yake ni makada wa CCM.

"Kama kulikuwa na kupeana habari katika uhusiano huu, basi wenzetu wa CCM watakuwa ndio walionufaika. Kabwe ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA na ni mtu aliye karibu sana na uongozi wa juu wa CHADEMA na anayejua mambo mengi sana ya chama chetu.

"Kwa upande wa Amina, yeye si kiongozi wa juu ndani ya chama na wala si mjumbe wa vikao vyovyote nyeti vya CCM," alisikitika kiongozi mmoja wa CHADEMA ambaye hakutaja jina lake litajwe kwa madai kwamba si msemaji wa chama.

Source: Majira, Ijumaa Mei 11, 2007; http://www.majira.co.tz/kurasa.php?soma=tanzania&habariNamba=2869
 
Aisee mkjj hii kitu inavutia sana inabidi watumiwe wabunge wa CCM na baadhi ya wazito wa umoja wa vijana!!
 
Mkjj
JJ

Nimekuvulia kofia. Nitume clipp ya hayo ma-Tshirt kwenye email yangu. Nadhani ni vyema ukafanya email circulation.

Teh teh teh

Jj
 
Sio kila anachosema Mzee Mwanakijiji ni gospel. Hakuna mwenye authority na accuracy ya information za Amina zaidi ya Mzee Chifupa (na Zitto labda). Kama Amina hapatikani kwa simu, Mzee Mwanakijiji kajuaje kwamba kashikiliwa kinyume cha matakwa yake na kwamba amechanganyikiwa.

Mzee Chifupa katuambia pale Maelezo kwamba Amina ndio pensheni yake kwahiyo hawezi kumruhusu kuropoka mambo na lazima am-guide na kwamba jambo hili watalimaliza kifamilia. Kwahiyo Mzee Chifupa ni mwehu kuhatarisha maisha ya mwanae?

In any case, I am impressed by your devotion to this issue to a point of spending time kwenye photoshop kutengeneza fulana. Duh, kweli kuna watu wana mapenzi na nchi!
 
wamemshikilia kwa sababau wanaogopa vivuli vyao.

Huuu !!! Baba Paroko weka alama ya kuuliza!!-???-

Jamani sio vizuri...Muachiaeni huru!! Mbona ni kiongozi mzuri!!
Mna mshambulia na mapezi ya kizamani...
sababu Ya hofu yake Mna mbaka!!...

Huuuuuuuuuuuuuuu!!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom