DOKEZO Kasulu: Eneo la NYAKITONTO, Kamchape wanahatarisha usalama wa raia na Polisi wapo kimya!

DOKEZO Kasulu: Eneo la NYAKITONTO, Kamchape wanahatarisha usalama wa raia na Polisi wapo kimya!

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Mchawi hapaswi kuishi,maana anafanya kazi isiyo na faida kwake Wala kwa jamii zaidi ya kuwa mateka wa shetani.
 
Mimi mwenyewe nimeshangaa kwamba kundi lote hili linaaamini uchawi upo. Kweli tuna safari ndefu sana
Inasikitisha Sana kuona Hadi nyakati hizi Kuna watu wanaamini ugumu katika maisha Yao sababu ni ndumba.
 
Subiri hao unaowatetea wakikuulia mwana family yako ksa wivu wa maendeleo ndo akili itakukaa sawa.
 
Wachawi ni adui wa maendeleo na hawa KAMCHAPE nasikia iliasisiwa na rais baada ya kufanyiwa mazingara alivotembelea Kigoma, ndo akawapa mamlaka ya kuwakomesha wachawi. Sasa hawa wanaowapinga KAMCHAPE itakuwa ndo wachawi wenyewe wanaogopa kuachishwa uchawi wao
 
Ni muda sasa kumekuwepo na hili wimbi la watu wanaojiita kamchape kiboko ya kutoa uchawi katika wilaya ya kasulu.

Mwanzoni Serikali kupitia jeshi la polisi walitoa maonyo kuhusu hawa watu lakini wananchi wengi waliyapuuza.

Kinachotokea sasa wanadhalilisha watu, wanatengeneza chuki dhidi ya wanajamii kupitia ramli yao chonganishi, Wanadhulumu watu pesa zao kidogo kwa ahadi watawasafishia nyumba zao zisiwe na uchawi, wanasambaza magonjwa ya zinaa ikiwemo kaswende na gono.

Kinachotokea katika kata ya Nyakitonto
Watu wanadhalilishwa, wanaibiwa pesa zao ,ndoa zinavunjika, maelewano katika familia yanapotea, raia wasio na hatia wanapigwa, watu wanavunjiwa nyumba zao.

Askari polisi kama walinzi wa usalama wako kimya kuhusu hali hii. Juzi kuna raia asiye na hatia kutokea Kitema kapigwa manusura ya kufa, jana mwananchi asiye na hatia kidogo avunjiwe nyumba yake.

Jeshi la Polisi liko wapi kupinga dhulma hii na uonevu huu au na wenyewe ni sehemu ya kamchape?

Waziri wa Mambo ya Ndani, sikiliza kilio cha hawa wanachi wasio na hatia. Kinachopaliliwa sasa hivi ipo siku kitatoa matunda na matunda hayo itakua ngumu kuyateketekeza.

RPC Kigoma angalia suala hili ni jipu linaloiva litakua kidonda ndugu siku moja. OCD Kasulu umewatelekeza raia wema ambao kila siku wanakupa ushirikiano kudhibiti uhalifu
Wachawi mpigwe tu
 
Ni muda sasa kumekuwepo na hili wimbi la watu wanaojiita kamchape kiboko ya kutoa uchawi katika wilaya ya kasulu.

Mwanzoni Serikali kupitia jeshi la polisi walitoa maonyo kuhusu hawa watu lakini wananchi wengi waliyapuuza.

Kinachotokea sasa wanadhalilisha watu, wanatengeneza chuki dhidi ya wanajamii kupitia ramli yao chonganishi, Wanadhulumu watu pesa zao kidogo kwa ahadi watawasafishia nyumba zao zisiwe na uchawi, wanasambaza magonjwa ya zinaa ikiwemo kaswende na gono.

Kinachotokea katika kata ya Nyakitonto
Watu wanadhalilishwa, wanaibiwa pesa zao ,ndoa zinavunjika, maelewano katika familia yanapotea, raia wasio na hatia wanapigwa, watu wanavunjiwa nyumba zao.

Askari polisi kama walinzi wa usalama wako kimya kuhusu hali hii. Juzi kuna raia asiye na hatia kutokea Kitema kapigwa manusura ya kufa, jana mwananchi asiye na hatia kidogo avunjiwe nyumba yake.

Jeshi la Polisi liko wapi kupinga dhulma hii na uonevu huu au na wenyewe ni sehemu ya kamchape?

Waziri wa Mambo ya Ndani, sikiliza kilio cha hawa wanachi wasio na hatia. Kinachopaliliwa sasa hivi ipo siku kitatoa matunda na matunda hayo itakua ngumu kuyateketekeza.

RPC Kigoma angalia suala hili ni jipu linaloiva litakua kidonda ndugu siku moja. OCD Kasulu umewatelekeza raia wema ambao kila siku wanakupa ushirikiano kudhibiti uhalifu
Wanasambazaje magonjwa ya zinaa mkuu?
 
Unauaje chanzo ambacho hakipo?
Acha ubishi wenzetu walitutangulia kwenye kuregulate sheria na kanuni kwenye kila jambo ila sisi tulikuwa tunapuuzia baadhi ya mambo na kujifanya kama jambo halipo na leo hii inatugharimu.
Achilia mbali ulaya hata Dubai kuna sheria kali kuhusu uchawi,ukishikwa na hirizi,tunguli au kitu chochote kinachotumika kwenye mambo ya uchawi au ushirikina unakamatwa na kupelekwa jela
 
Ngoja Atoe Ufafanuzi
Jibu lake ni jepesi sana.
Ufanyazi wao wa kazi wanafanana na wataalamu wa Computer science.
Kuna wanaofanya cyber attack na kuna wengine wanafanya cyber security ila wote wamesomea computer science.
Na waganga vs wachawi pia ni hivyo hivyo mchawi ni mtu wa kuharibu na mganga ni mtu wa kuweka kinga usiharibiwe na wachawi ila wote wanajua hiyo taaluma
 
Acha ubishi wenzetu walitutangulia kwenye kuregulate sheria na kanuni kwenye kila jambo ila sisi tulikuwa tunapuuzia baadhi ya mambo na kujifanya kama jambo halipo na leo hii inatugharimu.
Achilia mbali ulaya hata Dubai kuna sheria kali kuhusu uchawi,ukishikwa na hirizi,tunguli au kitu chochote kinachotumika kwenye mambo ya uchawi au ushirikina unakamatwa na kupelekwa jela
Acha kuleta humu stori za vijiweni? Ulaya gani wanafunga wenye tunguli!!?
 
Back
Top Bottom