Kataa ndoa ni zao la mfumuko wa gharama za maisha na wahanga ya wanawake wasiojielewa

Rorscharch

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2013
Posts
878
Reaction score
2,014
Si mara kwa mara huwa napitia Jamii Forums, lakini mara nilipokuja kuvutiwa na mijadala kwenye jukwaa hili, nilikutana na kundi la vijana wanaojiita “Kataa Ndoa.” Vijana hawa wanazua mjadala mkubwa, na maoni juu yao yanatofautiana sana – kuna wale wanaowaona kama wanaokwepa majukumu, wengine wanaelewa mitazamo yao, na wengine wanawachukia kabisa. Nilichagua kuchimba kidogo ili kuelewa mitazamo yao, na kile nilichogundua kinavutia na kinaongeza ufahamu kuhusu maisha ya vijana hawa.

Cha kwanza nilichogundua ni kwamba maamuzi na mitazamo ya vijana hawa yanachochewa sana na mabadiliko ya kiuchumi yaliyotokea ndani ya miongo miwili iliyopita. Ukitazama thamani ya fedha, mfano, Tshs 1,000,000 ya mwaka 2000 ilikuwa na nguvu inayokaribiana na Tshs 5,000,000 ya sasa. Kipato ambacho kilitosha kuendesha familia miaka hiyo, kwa sasa hakifanyi mambo makubwa. Na hali hii inawaathiri sana vijana wanaotarajiwa kuingia katika ndoa au wanaotarajiwa kuanzisha familia.

Tatizo kubwa ni kwamba wengi wa vijana wa leo wanaingia katika mahusiano na matarajio ya mwaka 2000, wakidhani mwanaume ana uwezo wa kifedha wa kumudu kila kitu kama ilivyokuwa awali. Hata hivyo, gharama za maisha zimepanda kwa kasi sana kiasi kwamba wanaume wengi wanabebeshwa mzigo mkubwa wa kifedha, mzigo ambao unawaathiri kiafya, kiakili, na hata kihisia. Mwanaume anaposumbuliwa na changamoto za kila siku za kifedha na mahitaji ya familia, inakuwa vigumu kuendelea katika mazingira hayo, na hatimaye migogoro midogo midogo hujitokeza – migogoro ambayo inashindwa kusuluhishwa na kupelekea ndoa kuvunjika.

Kuweka hili wazi, sio kana kwamba vijana wa leo hawataki kuwa katika mahusiano au kuwa na familia, bali mazingira ya sasa yamewalazimu kuchukua msimamo mkali ili kulinda ustawi wao binafsi. Mwanamke akitegemea sana kipato cha mwanaume, katika hali ya sasa, anakuwa mzigo kwa mwanaume na anamsukuma mwanaume kufikiria kuondoka. Maamuzi haya sio ya kupenda, bali ni ya kuepuka mateso yanayotokana na mahitaji yanayokosa jibu.

Pia, tofauti na wazazi wetu waliowekeza kwa urahisi katika ardhi, nyumba, na vitega uchumi, vijana wa leo wana nafasi finyu sana ya kumiliki mali. Hali ya sasa ya kiuchumi haimruhusu kijana wa miaka 30 kuwa na nyumba au mali nyingine kwa urahisi. Vijana hawa wamekosa nafasi ya kuweka msingi wa kifedha unaoweza kuwawezesha kutimiza majukumu ya familia kama walivyofanya wazee wetu.

Vivyo hivyo, wale wanaowakosoa vijana hawa kwa “kukimbia majukumu” mara nyingi wanatoka katika makundi mawili: kundi la wale walioko kwenye ndoa changa zenye matumaini au wazee wenye uwezo wa kifedha uliojengeka tangu zamani. Watu hawa hawakupata changamoto zile zile wanazopitia vijana wa sasa, na hivyo wanakosa uelewa wa kina juu ya maamuzi na hisia za vijana wa leo.

Vijana wa “Kataa Ndoa” ni kundi ambalo linataka kuonyesha jinsi mazingira ya sasa ya kiuchumi yanavyoathiri mitazamo ya vijana juu ya mahusiano na ndoa. Wanajua wazi kwamba huenda wana hatari ya kupoteza amani na ustawi wao endapo watajiingiza katika majukumu ambayo kwa sasa ni vigumu kuyamudu.
 
Si mara kwa mara huwa napitia Jamii Forums, lakini mara nilipokuja kuvutiwa na mijadala kwenye jukwaa hili, nilikutana na kundi la vijana wanaojiita “Kataa Ndoa.” Vijana hawa wanazua mjadala mkubwa, na maoni juu yao yanatofautiana sana – kuna wale wanaowaona kama wanaokwepa majukumu, wengine wanaelewa mitazamo yao, na wengine wanawachukia kabisa. Nilichagua kuchimba kidogo ili kuelewa mitazamo yao, na kile nilichogundua kinavutia na kinaongeza ufahamu kuhusu maisha ya vijana hawa.

Cha kwanza nilichogundua ni kwamba maamuzi na mitazamo ya vijana hawa yanachochewa sana na mabadiliko ya kiuchumi yaliyotokea ndani ya miongo miwili iliyopita. Ukitazama thamani ya fedha, mfano, Tshs 1,000,000 ya mwaka 2000 ilikuwa na nguvu inayokaribiana na Tshs 5,000,000 ya sasa. Kipato ambacho kilitosha kuendesha familia miaka hiyo, kwa sasa hakifanyi mambo makubwa. Na hali hii inawaathiri sana vijana wanaotarajiwa kuingia katika ndoa au wanaotarajiwa kuanzisha familia.

Tatizo kubwa ni kwamba wengi wa vijana wa leo wanaingia katika mahusiano na matarajio ya mwaka 2000, wakidhani mwanaume ana uwezo wa kifedha wa kumudu kila kitu kama ilivyokuwa awali. Hata hivyo, gharama za maisha zimepanda kwa kasi sana kiasi kwamba wanaume wengi wanabebeshwa mzigo mkubwa wa kifedha, mzigo ambao unawaathiri kiafya, kiakili, na hata kihisia. Mwanaume anaposumbuliwa na changamoto za kila siku za kifedha na mahitaji ya familia, inakuwa vigumu kuendelea katika mazingira hayo, na hatimaye migogoro midogo midogo hujitokeza – migogoro ambayo inashindwa kusuluhishwa na kupelekea ndoa kuvunjika.

Kuweka hili wazi, sio kana kwamba vijana wa leo hawataki kuwa katika mahusiano au kuwa na familia, bali mazingira ya sasa yamewalazimu kuchukua msimamo mkali ili kulinda ustawi wao binafsi. Mwanamke akitegemea sana kipato cha mwanaume, katika hali ya sasa, anakuwa mzigo kwa mwanaume na anamsukuma mwanaume kufikiria kuondoka. Maamuzi haya sio ya kupenda, bali ni ya kuepuka mateso yanayotokana na mahitaji yanayokosa jibu.

Pia, tofauti na wazazi wetu waliowekeza kwa urahisi katika ardhi, nyumba, na vitega uchumi, vijana wa leo wana nafasi finyu sana ya kumiliki mali. Hali ya sasa ya kiuchumi haimruhusu kijana wa miaka 30 kuwa na nyumba au mali nyingine kwa urahisi. Vijana hawa wamekosa nafasi ya kuweka msingi wa kifedha unaoweza kuwawezesha kutimiza majukumu ya familia kama walivyofanya wazee wetu.

Vivyo hivyo, wale wanaowakosoa vijana hawa kwa “kukimbia majukumu” mara nyingi wanatoka katika makundi mawili: kundi la wale walioko kwenye ndoa changa zenye matumaini au wazee wenye uwezo wa kifedha uliojengeka tangu zamani. Watu hawa hawakupata changamoto zile zile wanazopitia vijana wa sasa, na hivyo wanakosa uelewa wa kina juu ya maamuzi na hisia za vijana wa leo.

Vijana wa “Kataa Ndoa” ni kundi ambalo linataka kuonyesha jinsi mazingira ya sasa ya kiuchumi yanavyoathiri mitazamo ya vijana juu ya mahusiano na ndoa. Wanajua wazi kwamba huenda wana hatari ya kupoteza amani na ustawi wao endapo watajiingiza katika majukumu ambayo kwa sasa ni vigumu kuyamudu.
Huu uzi kwanza na subscribe, halafu nitaufuatilia zaidi. Katika standard za JF huu uzi uko na zile standard za JF ninayoijua, ukiachilia mbali nyuzi nyingi zimekuwa za watoto kiasi kwamba mtu kama mimi nakosa uhuru wa kutosha kuchangia. Mkuu umeongea uhalisia zaidi, siwezi kukadiria umri wako Ila Kwa makisio tu utakuwa around 50 au zaidi. Maana umegusa uhalisia kabisa yaani wa jamii ya kitanzania ya wanaoishi miji iliyo changamka kama Dar. Uzi wako umenigusa moja Kwa moja kama vile unaongelea maisha yangu. Mimi nipo around 40 na nina familia na ninawajibika kama baba. Ukweli ndiyo huo, vijana wanataka kuwa na familia Ila mahitaji ya kifamilia yanalemea sana kijana kama hana uwezo wa kifedha na anategemewa. Tena wenye matumaini ni wale wenye ndoa changa ama wazee wenye hali nzuri kiuchumi. Thanks again
 
Huu uzi kwanza na subscribe, halafu nitaufuatilia zaidi. Katika standard za JF huu uzi uko na zile standard za JF ninayoijua, ukiachilia mbali nyuzi nyingi zimekuwa za watoto kiasi kwamba mtu kama mimi nakosa uhuru wa kutosha kuchangia. Mkuu umeongea uhalisia zaidi, siwezi kukadiria umri wako Ila Kwa makisio tu utakuwa around 50 au zaidi. Maana umegusa uhalisia kabisa yaani wa jamii ya kitanzania ya wanaoishi miji iliyo changamka kama Dar. Uzi wako umenigusa moja Kwa moja kama vile unaongelea maisha yangu. Mimi nipo around 40 na nina familia na ninawajibika kama baba. Ukweli ndiyo huo, vijana wanataka kuwa na familia Ila mahitaji ya kifamilia yanalemea sana kijana kama hana uwezo wa kifedha na anategemewa. Tena wenye matumaini ni wale wenye ndoa changa ama wazee wenye hali nzuri kiuchumi. Thanks again
Asante Mkuu, mimi nipo around 30 yrs old, huko 50 mbali sana
Ni mazoea tu ya kutafakari jamii
Kuishi na mwanamke ambaye bado ana mfumo dume wa kulelewa ni changamoto sana (this from personal experience)
 
Si mara kwa mara huwa napitia Jamii Forums, lakini mara nilipokuja kuvutiwa na mijadala kwenye jukwaa hili, nilikutana na kundi la vijana wanaojiita “Kataa Ndoa.” Vijana hawa wanazua mjadala mkubwa, na maoni juu yao yanatofautiana sana – kuna wale wanaowaona kama wanaokwepa majukumu, wengine wanaelewa mitazamo yao, na wengine wanawachukia kabisa. Nilichagua kuchimba kidogo ili kuelewa mitazamo yao, na kile nilichogundua kinavutia na kinaongeza ufahamu kuhusu maisha ya vijana hawa.

Cha kwanza nilichogundua ni kwamba maamuzi na mitazamo ya vijana hawa yanachochewa sana na mabadiliko ya kiuchumi yaliyotokea ndani ya miongo miwili iliyopita. Ukitazama thamani ya fedha, mfano, Tshs 1,000,000 ya mwaka 2000 ilikuwa na nguvu inayokaribiana na Tshs 5,000,000 ya sasa. Kipato ambacho kilitosha kuendesha familia miaka hiyo, kwa sasa hakifanyi mambo makubwa. Na hali hii inawaathiri sana vijana wanaotarajiwa kuingia katika ndoa au wanaotarajiwa kuanzisha familia.

Tatizo kubwa ni kwamba wengi wa vijana wa leo wanaingia katika mahusiano na matarajio ya mwaka 2000, wakidhani mwanaume ana uwezo wa kifedha wa kumudu kila kitu kama ilivyokuwa awali. Hata hivyo, gharama za maisha zimepanda kwa kasi sana kiasi kwamba wanaume wengi wanabebeshwa mzigo mkubwa wa kifedha, mzigo ambao unawaathiri kiafya, kiakili, na hata kihisia. Mwanaume anaposumbuliwa na changamoto za kila siku za kifedha na mahitaji ya familia, inakuwa vigumu kuendelea katika mazingira hayo, na hatimaye migogoro midogo midogo hujitokeza – migogoro ambayo inashindwa kusuluhishwa na kupelekea ndoa kuvunjika.

Kuweka hili wazi, sio kana kwamba vijana wa leo hawataki kuwa katika mahusiano au kuwa na familia, bali mazingira ya sasa yamewalazimu kuchukua msimamo mkali ili kulinda ustawi wao binafsi. Mwanamke akitegemea sana kipato cha mwanaume, katika hali ya sasa, anakuwa mzigo kwa mwanaume na anamsukuma mwanaume kufikiria kuondoka. Maamuzi haya sio ya kupenda, bali ni ya kuepuka mateso yanayotokana na mahitaji yanayokosa jibu.

Pia, tofauti na wazazi wetu waliowekeza kwa urahisi katika ardhi, nyumba, na vitega uchumi, vijana wa leo wana nafasi finyu sana ya kumiliki mali. Hali ya sasa ya kiuchumi haimruhusu kijana wa miaka 30 kuwa na nyumba au mali nyingine kwa urahisi. Vijana hawa wamekosa nafasi ya kuweka msingi wa kifedha unaoweza kuwawezesha kutimiza majukumu ya familia kama walivyofanya wazee wetu.

Vivyo hivyo, wale wanaowakosoa vijana hawa kwa “kukimbia majukumu” mara nyingi wanatoka katika makundi mawili: kundi la wale walioko kwenye ndoa changa zenye matumaini au wazee wenye uwezo wa kifedha uliojengeka tangu zamani. Watu hawa hawakupata changamoto zile zile wanazopitia vijana wa sasa, na hivyo wanakosa uelewa wa kina juu ya maamuzi na hisia za vijana wa leo.

Vijana wa “Kataa Ndoa” ni kundi ambalo linataka kuonyesha jinsi mazingira ya sasa ya kiuchumi yanavyoathiri mitazamo ya vijana juu ya mahusiano na ndoa. Wanajua wazi kwamba huenda wana hatari ya kupoteza amani na ustawi wao endapo watajiingiza katika majukumu ambayo kwa sasa ni vigumu kuyamudu.
Umeongea vema.
Umeongea uhalisia.
Umeongea ukweli.
Umeongea kwa shabaha.

Factor uliyoiongelea ndo tatizo kubwa sana katika kizazi chetu.

Ila nnachojiuliza ni mbona matajili wakubwa ktk kizazi chetu hichihichi, swala la ndoa limekua ni shida sana kwao ingawa fedha na mali kwao sio tatizo kabisa. Mfano: Bilgates, Dangote, Elon, 50 cents, Jef Bezoz, Robeto Carlos, Kaka, na wengine weeeengi sana.

Nahisi tatizo landoa limeenda mbali zaidi yakua tayari tu kiuchumi, yani fedha na mali..
 
Umeongea vema.
Umeongea uhalisia.
Umeongea ukweli.
Umeongea kwa shabaha.

Factor uliyoiongelea ndo tatizo kubwa sana katika kizazi chetu.

Ila nnachojiuliza ni mbona matajili wakubwa ktk kizazi chetu hichihichi, swala la ndoa limekua ni shida sana kwao ingawa fedha na mali kwao sio tatizo kabisa. Mfano: Bilgates, Dangote, Elon, 50 cents, Jef Bezoz, Robeto Carlos, Kaka, na wengine weeeengi sana.

Nahisi tatizo landoa limeenda mbali zaidi yakua tayari tu kiuchumi, yani fedha na mali..
Hapo kuna tatizo jingine, ukiona mtu ana pesa na ndoa kwake bado ni changamoto basi hapo most likely linakuwa tatizo la malezi (unajua mika kama jando na unyago zilikuwa na nafasi yake pia )
 
Hali hiyo imechochewa kwa kiasi kikubwa zaidi na miongoni mwao kuzongwa na ugumu wa maisha kutokana na ukosefu wa ajira, kukata tamaa, uvivu na kutokua na uhakika wa kesho yao mfukoni, kesho yao tumboni, kesho yao kwenye makazi yao, kesho yao kwenye mahusiano yao na hata kesho yao kwenye maisha yao ya kila siku. Hii ni kumaanisha, members wengi zaidi wa movement hii hawana ajira au uhakika wa kipato. Wale wenye ajira za uhakika ambao ni members wa movement hii, ujue wameathirika pakubwa mno na suala la afya ya uzazi.

Hali hii imewafanya wawe wanyonge zaidi na wenye msongo wa mawazo wa kiwango kibaya zaidi, kiasi kwamba hakuna kazi au jukumu la kutumia nguvu wanaloweza kulitekeleza, ikiwa ni pamoja na tendo la kugegeda mbususu halisi. Sabuni zimewamaliza kabisa nyoro zao kwa mujibu wa shuhuda za baadhi ya members wao walio surrender movement hii isiyo na tija, faida wala maana yoyote.

Wengi wao wana hofu na stress za kiwango cha juu sana, hata wameanza kuiona fainali ya uzeeni mapema zaidi kabla ya wakati wao. Wengi wanaonekana wazee, lakini ukweli ni vijana, wamekomazwa mno na ugumu wa maisha. Na faraja yao siku hizi imekua ni visungura kuliko deto.

Na kuna hatari ya miongoni mwa members wa movement hii, kutumbukia kwenye dimbwi la ufirauni, kitu ambacho ni fedheha na hasara kubwa sana kwao wenyewe binafsi, kwa familia zao na Taifa kwa ujumla.

Nashauri vijana wote waliomo kwenye movement hii potofu na ya kihalifu, kujiengua mara moja na hatimae kujibrand na kujifomat upya kisaikojia na hatimae kua viumbe vipya, ya kale yamepita tazama yamekua mapya.

Heshimisheni familia zenu na sio kujifedhehesha kwa aibu ya uzee bila ndoa au mtoto 🐒

Mungu Ibariki Tanzania
 
Ilo linajulikana long sana. Huwezi kua mwanaume halisi uwe na shaka na hitaji kuu la kibaolojia.
 
Hali hiyo imechochewa kwa kiasi kikubwa zaidi na miongoni mwao kuzongwa na ugumu wa maisha kutokana na ukosefu wa ajira, kukata tamaa, uvivu na kutokua na uhakika wa kesho yao mfukoni, kesho yao tumboni, kesho yao kwenye makazi yao, kesho yao kwenye mahusiano yao na hata kesho yao kwenye maisha yao ya kila siku. Hii ni kumaanisha, members wengi zaidi wa movement hii hawana ajira au uhakika wa kipato. Wale wenye ajira za uhakika ambao ni members wa movement hii, ujue wameathirika pakubwa mno na suala la afya ya uzazi.

Hali hii imewafanya wawe wanyonge zaidi na wenye msongo wa mawazo wa kiwango kibaya zaidi, kiasi kwamba hakuna kazi au jukumu la kutumia nguvu wanaloweza kulitekeleza, ikiwa ni pamoja na tendo la kugegeda mbususu halisi. Sabuni zimewamaliza kabisa nyoro zao kwa mujibu wa shuhuda za baadhi ya members wao walio surrender movement hii isiyo na tija, faida wala maana yoyote.

Wengi wao wana hofu na stress za kiwango cha juu sana, hata wameanza kuiona fainali ya uzeeni mapema zaidi kabla ya wakati wao. Wengi wanaonekana wazee, lakini ukweli ni vijana, wamekomazwa mno na ugumu wa maisha. Na faraja yao siku hizi imekua ni visungura kuliko deto.

Na kuna hatari ya miongoni mwa members wa movement hii, kutumbukia kwenye dimbwi la ufirauni, kitu ambacho ni fedheha na hasara kubwa sana kwao wenyewe binafsi, kwa familia zao na Taifa kwa ujumla.

Nashauri vijana wote waliomo kwenye movement hii potofu na ya kihalifu, kujiengua mara moja na hatimae kujibrand na kujifomat upya kisaikojia na hatimae kua viumbe vipya, ya kale yamepita tazama yamekua mapya.

Heshimisheni familia zenu na sio kujifedhehesha kwa aibu ya uzee bila ndoa au mtoto 🐒

Mungu Ibariki Tanzania
Fala kwel
 
Hali hiyo imechochewa kwa kiasi kikubwa zaidi na miongoni mwao kuzongwa na ugumu wa maisha kutokana na ukosefu wa ajira, kukata tamaa, uvivu na kutokua na uhakika wa kesho yao mfukoni, kesho yao tumboni, kesho yao kwenye makazi yao, kesho yao kwenye mahusiano yao na hata kesho yao kwenye maisha yao ya kila siku. Hii ni kumaanisha, members wengi zaidi wa movement hii hawana ajira au uhakika wa kipato. Wale wenye ajira za uhakika ambao ni members wa movement hii, ujue wameathirika pakubwa mno na suala la afya ya uzazi.

Hali hii imewafanya wawe wanyonge zaidi na wenye msongo wa mawazo wa kiwango kibaya zaidi, kiasi kwamba hakuna kazi au jukumu la kutumia nguvu wanaloweza kulitekeleza, ikiwa ni pamoja na tendo la kugegeda mbususu halisi. Sabuni zimewamaliza kabisa nyoro zao kwa mujibu wa shuhuda za baadhi ya members wao walio surrender movement hii isiyo na tija, faida wala maana yoyote.

Wengi wao wana hofu na stress za kiwango cha juu sana, hata wameanza kuiona fainali ya uzeeni mapema zaidi kabla ya wakati wao. Wengi wanaonekana wazee, lakini ukweli ni vijana, wamekomazwa mno na ugumu wa maisha. Na faraja yao siku hizi imekua ni visungura kuliko deto.

Na kuna hatari ya miongoni mwa members wa movement hii, kutumbukia kwenye dimbwi la ufirauni, kitu ambacho ni fedheha na hasara kubwa sana kwao wenyewe binafsi, kwa familia zao na Taifa kwa ujumla.

Nashauri vijana wote waliomo kwenye movement hii potofu na ya kihalifu, kujiengua mara moja na hatimae kujibrand na kujifomat upya kisaikojia na hatimae kua viumbe vipya, ya kale yamepita tazama yamekua mapya.

Heshimisheni familia zenu na sio kujifedhehesha kwa aibu ya uzee bila ndoa au mtoto 🐒

Mungu Ibariki Tanzania
Mkuu nimecheck sana pm naona kimya kidogo kiongozi
 
Umeongea vema.
Umeongea uhalisia.
Umeongea ukweli.
Umeongea kwa shabaha.

Factor uliyoiongelea ndo tatizo kubwa sana katika kizazi chetu.

Ila nnachojiuliza ni mbona matajili wakubwa ktk kizazi chetu hichihichi, swala la ndoa limekua ni shida sana kwao ingawa fedha na mali kwao sio tatizo kabisa. Mfano: Bilgates, Dangote, Elon, 50 cents, Jef Bezoz, Robeto Carlos, Kaka, na wengine weeeengi sana.

Nahisi tatizo landoa limeenda mbali zaidi yakua tayari tu kiuchumi, yani fedha na mali..
Kuna masuala ya feminism na loopholes za kisheria ambazo zinasababisha ndoa iwe risk sana kwa mwanaume. Hizo ndizo changamoto kwa watu ambao wamejipata.
 
Hali hiyo imechochewa kwa kiasi kikubwa zaidi na miongoni mwao kuzongwa na ugumu wa maisha kutokana na ukosefu wa ajira, kukata tamaa, uvivu na kutokua na uhakika wa kesho yao mfukoni, kesho yao tumboni, kesho yao kwenye makazi yao, kesho yao kwenye mahusiano yao na hata kesho yao kwenye maisha yao ya kila siku. Hii ni kumaanisha, members wengi zaidi wa movement hii hawana ajira au uhakika wa kipato. Wale wenye ajira za uhakika ambao ni members wa movement hii, ujue wameathirika pakubwa mno na suala la afya ya uzazi.

Hali hii imewafanya wawe wanyonge zaidi na wenye msongo wa mawazo wa kiwango kibaya zaidi, kiasi kwamba hakuna kazi au jukumu la kutumia nguvu wanaloweza kulitekeleza, ikiwa ni pamoja na tendo la kugegeda mbususu halisi. Sabuni zimewamaliza kabisa nyoro zao kwa mujibu wa shuhuda za baadhi ya members wao walio surrender movement hii isiyo na tija, faida wala maana yoyote.

Wengi wao wana hofu na stress za kiwango cha juu sana, hata wameanza kuiona fainali ya uzeeni mapema zaidi kabla ya wakati wao. Wengi wanaonekana wazee, lakini ukweli ni vijana, wamekomazwa mno na ugumu wa maisha. Na faraja yao siku hizi imekua ni visungura kuliko deto.

Na kuna hatari ya miongoni mwa members wa movement hii, kutumbukia kwenye dimbwi la ufirauni, kitu ambacho ni fedheha na hasara kubwa sana kwao wenyewe binafsi, kwa familia zao na Taifa kwa ujumla.

Nashauri vijana wote waliomo kwenye movement hii potofu na ya kihalifu, kujiengua mara moja na hatimae kujibrand na kujifomat upya kisaikojia na hatimae kua viumbe vipya, ya kale yamepita tazama yamekua mapya.

Heshimisheni familia zenu na sio kujifedhehesha kwa aibu ya uzee bila ndoa au mtoto 🐒

Mungu Ibariki Tanzania
Kianzia aya ya pili umeandika upumbavu
 
Maelezo yapo vema sana kuongezea tu kuna hili wimbi la upungufu wa nguvu za kiume ambapo kuna ugomvi mkubwa kwenye baadhi ya ndoa wanawake wakiwatuhumu wenzi wao kuwa wanachepuka kumbe siyo, pia wapo wanaume wenye matatizo ya moyo ambao wamekufa kwa sababu ya kutaka kuwaridhisha wake zao kitandani. Kataa ndoa kwa afya yako
 
Kataa ndoa 🤣
Ndoa ni ubabaishaji
 
Hali hiyo imechochewa kwa kiasi kikubwa zaidi na miongoni mwao kuzongwa na ugumu wa maisha kutokana na ukosefu wa ajira, kukata tamaa, uvivu na kutokua na uhakika wa kesho yao mfukoni, kesho yao tumboni, kesho yao kwenye makazi yao, kesho yao kwenye mahusiano yao na hata kesho yao kwenye maisha yao ya kila siku. Hii ni kumaanisha, members wengi zaidi wa movement hii hawana ajira au uhakika wa kipato. Wale wenye ajira za uhakika ambao ni members wa movement hii, ujue wameathirika pakubwa mno na suala la afya ya uzazi.

Hali hii imewafanya wawe wanyonge zaidi na wenye msongo wa mawazo wa kiwango kibaya zaidi, kiasi kwamba hakuna kazi au jukumu la kutumia nguvu wanaloweza kulitekeleza, ikiwa ni pamoja na tendo la kugegeda mbususu halisi. Sabuni zimewamaliza kabisa nyoro zao kwa mujibu wa shuhuda za baadhi ya members wao walio surrender movement hii isiyo na tija, faida wala maana yoyote.

Wengi wao wana hofu na stress za kiwango cha juu sana, hata wameanza kuiona fainali ya uzeeni mapema zaidi kabla ya wakati wao. Wengi wanaonekana wazee, lakini ukweli ni vijana, wamekomazwa mno na ugumu wa maisha. Na faraja yao siku hizi imekua ni visungura kuliko deto.

Na kuna hatari ya miongoni mwa members wa movement hii, kutumbukia kwenye dimbwi la ufirauni, kitu ambacho ni fedheha na hasara kubwa sana kwao wenyewe binafsi, kwa familia zao na Taifa kwa ujumla.

Nashauri vijana wote waliomo kwenye movement hii potofu na ya kihalifu, kujiengua mara moja na hatimae kujibrand na kujifomat upya kisaikojia na hatimae kua viumbe vipya, ya kale yamepita tazama yamekua mapya.

Heshimisheni familia zenu na sio kujifedhehesha kwa aibu ya uzee bila ndoa au mtoto 🐒

Mungu Ibariki Tanzania
Maelezo yapo vema sana kuongezea tu kuna hili wimbi la upungufu wa nguvu za kiume ambapo kuna ugomvi mkubwa kwenye baadhi ya ndoa wanawake wakiwatuhumu wenzi wao kuwa wanachepuka kumbe siyo, pia wapo wanaume wenye matatizo ya moyo ambao wamekufa kwa sababu ya kutaka kuwaridhisha wake zao kitandani. Kataa ndoa kwa afya yako
Naona bado mzigo mkubwa anatwishwa kijana wa kiume bado na yale yote niliyowasilisha katika Uzi hapo juu bado yanapuuziwa
 
Naona bado mzigo mkubwa anatwishwa kijana wa kiume bado na yale yote niliyowasilisha katika Uzi hapo juu bado yanapuuziwa
kwa mwanaume ndoa ni kujiongezea majukumu kwaiyo lazima mzigo umuelemee. Tafauti ya zamani ma sisi ipo hapo kwenye kipato hii inakwamisha vijana kuoa.

Vilevile mentality ya wanawake imebadilika kidogo. Wakati wanawake wa zamani walikua wanaona sacrifices za mwanaume ni kujali hivyo kuyathamini mahusiano, hawa wa sasa wanaona sacrifices za mwanaume ni ufala hivyo wanawapa wanaume hao majina ya dhihaka mfano danga, na pale mwanaume uyo atakapoyumba na kushindwa ku-provide basi na mapenzi yanaishia hapo.

Tupo kwenye kizazi ambacho mahusiano yamefanywa kuwa biashara kitu ambacho hata wenye uwezo nao wanasita kuoa. Kwanini nipitie mchakato mrefu wa kuwa na mwanamke ilihali hakuna guaranteed return ya uwekezaji wangu wakati naweza kupata sex kwa cheap and fast? hapa ndipo kijana anaona bora anunue dadapoa tu au ajiweke kwenye mahusiano mguu ndani mguu nje.
 
Back
Top Bottom