Kataa Ndoa School of Thought, ni upi mtazamo wenu juu ya Masuala haya?

Kataa Ndoa School of Thought, ni upi mtazamo wenu juu ya Masuala haya?

Tatizo ni peace of mind

Ndoa at this moment zimepoteza maana halisi ya ndoa WATU wanaishi ili kulea watoto tu.

If you go broke ,
If ur wife akiumwa ugonjwa wa kutopona mapema you can just see the true color of marriage.


Ushauri
Work hard save ur money
Maintain spiritual Power
Maintain health habit.

In long run , nothing will help you than ur inner efforts towards the happiest life.
 
ajenda hii kataa ndoa iko nyuma ya makundi ya wanaume wafuatao.

wavulana chini ya miaka 20.
wavulana miaka 30 kuendelea ambao hawana ramani yoyote.
walioumizwa na mapenzi kupitiliza wamejikatia tamaa.
ambao wana matatizo ya kutopata uzao,wanatumia kete hiyo kuficha madhaifu yao.
 
Mkuu unaelewa maana ya ndoa kweli.


Ndoa ni taasisi ya kiuchumi iliyoundwa na mwanaume na wa/ mwanamke bikra yenye mrengo wa kumnufaisha mwanamke na kumgandamiza mwanaume siku zote za maisha yake ili kupoteza nguvu kazi ya kiume katika kufikia maendeleo ya kiuchumi ya mwanaume na Taifa kwa ujumla


KATAA NDOA, TUNZA KIBUDA, VIMBA MJINI NA MASHAMBANI ISHI KWA AMANI

nb: watoto tutapata tukitaka
 
Kama yote hayo yanapatikana kwenye ndoa dunia ingekuwa sehemu salama sana kwa binaadamu kuishi. Afrika ingekuwa ni sehemu iliyostaarabika zaidi ulimwenguni
Kataa ndoa wa zamani na wa sasa ndio walio haribu na wanaendelea kuharibu. Familia zinafundisha upendo,huruma na kujali.
Lkn malezi ya mzazi mmoja yana pandikiza chuki miongoni mwa wazazi na watoto.
 
Mkuu unaelewa maana ya ndoa kweli.


Ndoa ni taasisi ya kiuchumi iliyoundwa na mwanaume na wa/ mwanamke bikra yenye mrengo wa kumnufaisha mwanamke na kumgandamiza mwanaume siku zote za maisha yake ili kupoteza nguvu kazi ya kiume katika kufikia maendeleo ya kiuchumi ya mwanaume na Taifa kwa ujumla


KATAA NDOA, TUNZA KIBUDA, VIMBA MJINI NA MASHAMBANI ISHI KWA AMANI

nb: watoto tutapata tukitaka
Mkuu uhalisia mwanamke ameumbwa kupokea, fikiria hata kwenye tendo la ndoa au ngono mwanamke anapokea tunavyo toa sisi wanaume.
Mm nadhani changamoto kubwa ilikuja baada ya dunia kukengeuka kuaza habari za 50/50 hapa ndio shida ilipo zaliwa.
Mwanamke anapaswa amtegemee mmewe ndio amani kubwa inakuwepo.
Kwasasa wanawake wengi ni kama wamefunguliwa kutoka kifungo flani wako huru kufanya chochote kuazia kwa wazazi hadi mtaani
 
Inatambulika dunia kote, toka dunia hii imeanza—haijalishi kwa dhana ya Uumbaji wa Mungu au Evolution ya kisayansi— Baba, Mama na Watoto (Familia), ndio imekua jumuiko la kwanza, kuu na la msingi la wanadamu.

Siku hizi kumeshamiri wimbi [si geni kihistoria] la kupinga Uwepo wa Familia ya Baba, Mama na Watoto—KATAA NDOA.

Wafuasi wa dhana hii, naombeni mnipe mtazamo wenu juu ya masuala haya;

1. Juu ya Malezi na miongozo ya pamoja. Ni kwenye familia ndipo mtoto anafunzwa stadi za Maisha—kupika, kufua, kuosha watoto, kubeba mtoto, miongozo ya elimu ya awali, nidhamu, utiifu mfano namna ya kusalimu watu, kuheshimu watu wote, utunzaji wa mali zake na za familia, upendo, huruma—yote haya yanachangiwa na baba na mama. Nje ya familia haya mtoto atayapata vipi kwa ufanisi?

2. Juu ya Upatikanaji wa uhakika wa mahitaji ya kimwili.. Ngono ndio hisia na msukumo mkubwa wa Mwanadamu yeyote. Mtu Mzima anahitaji walau kufanya ngono mara tatu kwa wiki, Mke na Mume ndiyo wanatimiziana hayo na kupeana utulivu na hivyo kuweza kutimiza majukumu yao mengine. Bila kuoa, maana yake utakuwa na wanawake tofauti tofauti na kujiweka kwenye risk ya Maradhi, Ushirikina na kuzaa hovyo, mtapanyo holela wa kipato. Kataa ndoa, mna njia ipi mbadala yenye usalama nje ya ndoa?

3. Juu ya mahusiano ya kijamii. Familia ndio networking platform ya kwanza ya mwanadamu. Ndugu wa mke na Mume kwa ujumla wao ndio huwa chimbuko la kupeana fursa mfano Ajira au tender za kibiashara, kusaidiana katika matatizo mf Afrika hatutumii mifumo rasmi ya Bima mf Mazishi au Maradhi, sababu tunamifumo ya kusaidiana wenyewe toka ngazi ya familia. Pia kupitia familia ndipo mwanao anaweza kwenda kufanya kazi sehemu na kufikia kwa ndugu wa Mkeo au mumeo n.k n.k. Hili nyie mnalitazama vipi?

4. Juu ya kuwapa misingi ya Uwajibikaji watoto. Familia inapolea watoto kuwa watiifu na kufuata miiko mbalimbali inawafanya watoto wawe na sense ya uwajibikaji zaidi na hivyo kuwa na jamii bora zaidi, mfano unapolea mtoto usiku ni muda wa kuwa nyumbani, au anayekatazwa udokozi, anayetimiziwa mahitaji yake nafasi ya kuwa na jamii tulivu ni kubwa. Bila familia, nyie mnaona jamii itakuwa na sura gani?

5. Juu ya kujijenga kiuchumi. Mke na Mume hupeana mipango ya maendeleo. Mke humtia moyo mmewe kupambana, mke hupambana kutafutia familia kipato pia, hivyo husaidizana inapotokea kukwama, pia mahitaji ya watoto huwasukuma wazazi kutafuta zaidi. Kubwa zaidi, ukiwa na familia, huwezi zaa hovyo, hivyo hukupa utulivu wa kiuchumi. Je, Nyie hili mnalitazama vipi?

6. Juu ya mafunzo ya kimaadili— Kidini/Kimungu/Kiutu. Mwanadamu yeyote anahitaji dira ya kumuongoza kimaadili—mema na mabaya— maishani (moral compass) ambapo sehemu ya kwanza ni unaipata kwenye familia. Familia ya kiislam, itamlea mtoto kwenye maadili ya kislam na kumpa miongozo ya mema na mabaya, hali kadhalika kwa familia ya kikiristo, au hata ya kipagan ni lazima inayo moral compass yao. Nyie kataa ndoa, mnadhani watoto wanaipata vipi miongozo hiyo ya kimaadili?

Karibuni.
View attachment 2889192
View attachment 2889193
View attachment 2889194
ndoa ni utumwa kwa mwanaume
 
Mkuu uhalisia mwanamke ameumbwa kupokea, fikiria hata kwenye tendo la ndoa au ngono mwanamke anapokea tunavyo toa sisi wanaume.
Mm nadhani changamoto kubwa ilikuja baada ya dunia kukengeuka kuaza habari za 50/50 hapa ndio shida ilipo zaliwa.
Mwanamke anapaswa amtegemee mmewe ndio amani kubwa inakuwepo.
Kwasasa wanawake wengi ni kama wamefunguliwa kutoka kifungo flani wako huru kufanya chochote kuazia kwa wazazi hadi mtaani
Ni kwel mkuu ,je wewe upo tayari kuona mwanao wa kike hapati elimu ,wala kazi ya kumwingizia kipato chochote?
 
Juu ya Malezi na miongozo ya pamoja. Ni kwenye familia ndipo mtoto anafunzwa stadi za Maisha—kupika, kufua, kuosha watoto, kubeba mtoto, miongozo ya elimu ya awali, nidhamu, utiifu mfano namna ya kusalimu watu, kuheshimu watu wote, utunzaji wa mali zake na za familia, upendo, huruma—yote haya yanachangiwa na baba na mama. Nje ya familia haya mtoto atayapata vipi kwa ufanisi?
Atapata kwa wazazi, ni kwamba hawaishi pamoja, sio kwamba wametengana, na hata kama wametengana, atalelewa na mzazi mmoja ama ndugu wa wazazi
2. Juu ya Upatikanaji wa uhakika wa mahitaji ya kimwili.. Ngono ndio hisia na msukumo mkubwa wa Mwanadamu yeyote. Mtu Mzima anahitaji walau kufanya ngono mara tatu kwa wiki, Mke na Mume ndiyo wanatimiziana hayo na kupeana utulivu na hivyo kuweza kutimiza majukumu yao mengine. Bila kuoa, maana yake utakuwa na wanawake tofauti tofauti na kujiweka kwenye risk ya Maradhi, Ushirikina na kuzaa hovyo, mtapanyo holela wa kipato. Kataa ndoa, mna njia ipi mbadala yenye usalama nje ya ndoa?
Maradhi, watoto, kuna njia za kuzuia
3. Juu ya mahusiano ya kijamii. Familia ndio networking platform ya kwanza ya mwanadamu. Ndugu wa mke na Mume kwa ujumla wao ndio huwa chimbuko la kupeana fursa mfano Ajira au tender za kibiashara, kusaidiana katika matatizo mf Afrika hatutumii mifumo rasmi ya Bima mf Mazishi au Maradhi, sababu tunamifumo ya kusaidiana wenyewe toka ngazi ya familia. Pia kupitia familia ndipo mwanao anaweza kwenda kufanya kazi sehemu na kufikia kwa ndugu wa Mkeo au mumeo n.k n.k. Hili nyie mnalitazama vipi?
Poa tu hamna kizuizi
4. Juu ya kuwapa misingi ya Uwajibikaji watoto. Familia inapolea watoto kuwa watiifu na kufuata miiko mbalimbali inawafanya watoto wawe na sense ya uwajibikaji zaidi na hivyo kuwa na jamii bora zaidi, mfano unapolea mtoto usiku ni muda wa kuwa nyumbani, au anayekatazwa udokozi, anayetimiziwa mahitaji yake nafasi ya kuwa na jamii tulivu ni kubwa. Bila familia, nyie mnaona jamii itakuwa na sura gani?
rejea hoja no.1
5. Juu ya kujijenga kiuchumi. Mke na Mume hupeana mipango ya maendeleo. Mke humtia moyo mmewe kupambana, mke hupambana kutafutia familia kipato pia, hivyo husaidizana inapotokea kukwama, pia mahitaji ya watoto huwasukuma wazazi kutafuta zaidi. Kubwa zaidi, ukiwa na familia, huwezi zaa hovyo, hivyo hukupa utulivu wa kiuchumi. Je, Nyie hili mnalitazama vipi?
sio lazima kupeana mipango ya kimaendeleo, kuzaa ovyo ni maamuzi ya mtu, wapo wenye familia na wanazaa ovyo
Juu ya mafunzo ya kimaadili— Kidini/Kimungu/Kiutu. Mwanadamu yeyote anahitaji dira ya kumuongoza kimaadili—mema na mabaya— maishani (moral compass) ambapo sehemu ya kwanza ni unaipata kwenye familia. Familia ya kiislam, itamlea mtoto kwenye maadili ya kislam na kumpa miongozo ya mema na mabaya, hali kadhalika kwa familia ya kikiristo, au hata ya kipagan ni lazima inayo moral compass yao. Nyie kataa ndoa, mnadhani watoto wanaipata vipi miongozo hiyo ya kimaadili?
kwa wanaomlea
 
Hii vita siku mkiimaliza mtuambie. Kuna jamaa yangu ka umri kalienda kidogo, maneno yakawa mengi sana. Mwaka jana akapata kazi TRA, hivi ninavyoandika nafuatilia mbuzi kwa ajili ya ka sherehe ka engagement yake na soon ni ndoa.

Msichokijua wengi ni kwamba maisha yamebadirika sana, kama ulibahatika kuzaliwa kwenye chochote kuna wenzio wanajitafuta ili wapate chochote ndio waoe lengo ni kutoitesa familia.

Kijana mwenye akili timamu hawezi kuoa eti mke huja na riziki zake huo ni ukuda sana. Acha nifuatilie mbuzi kijana afanye yake, mnawasema watu hadi wanakosa raha. Kwenye vifua vya vijana wengi kuna maumivu ya kusemwa juu ya haya mambo na chanzo ni uchumi mbovu wa vijana wengi
 
Back
Top Bottom