Kati ya AZAM na STAR TIMES, ipi itakayowafaa wazee wangu kijijini?

Ujiandae pia na kifurushi kizuri ni 35,000 kwa mwezi...
 
Sijui kama naye ni mfuasi wake ila kuna kijana wake ambaye yuko naye hapo nyumbani, amekuwa akimtaja taja sana Mwamposa, kwa hiyo naye ataenjoy kukiwepo na channel yenye mahubiri ya Mwamposa.
 
Ujiandae pia na kifurushi kizuri ni 35,000 kwa mwezi...
Mkuu, cha 35,000/= cha kazi gani? Kwangu kwenyewe ni mara chache naweka hicho kifurushi. Labda, nitamuwekea mara chache, hasa kwa ajili ya wajukuu wake. Sidhani kama yeye atakuwa na muda wa kukimbizana na machannel ya kule "duniani".
 
Wanatumia kwasababu ni bei rahisi kununua lakin hakuna cha maaana huko startimes, azam kateka soko la ndani
Wanatumia Kwa sababu ya ligi ya bongo.

Tena siku hizi Kwa wale wenye vibanda umiza na bar wanapiga hela kupitia Azam Kwa kuonesha mpira wa bongo.

Mbali na mpira wa bongo, Azam hana cha Maana.

Kuhusu bei, DSTV ndo Bei rahisi lakini Bado kina watumiaji wachache.
 
Angalia chenye gharama nafuu zaidi kuliko kingine sasa hivi Azam Cha Antenna 49,000/- wakati startimes ni 79,000/- kwa hio chagua hapo alafu Azam wametandaza waya Nchi nzima hakuna kukwamakwama sijui ku-scrutch mawimbi kupotea hakuna km ilivyo startimes kuna mda wana-scrutch balaa especially kukiwa na mawingu au mvua ikinyesha
 
Kwahiyo startimes wana kipi cha maana? Ukisema Azam ukitoa ligi ya bongo hawana cha maana inaonekana hujawahi hata kumiliki azam TV, kwa wapenzi wa mpira Azam inaonyesha ligi kibao NBC ya ndani, bundesliga,league 1, mechi 1 ya epl kila jumamosi, inaonyesha Saudi Pl ligi ambayo wapo kina Ronaldo,Neymar, sadio mane,benzema, kwa wapenzi wa movies zipo channel kibao, wapenzi dini zipo channel za dini tofauti, Kwa Tz azam ndo king'amuzi standard ambacho ukiwa nacho unaburudika.

Ukimiliki hiyo startimes unaona nini cha maana?
 
Ukisema mbali na ligi ya bongo hawana cha maana inaonyesha hujawahi kutumia azam TV au labda ni chuki, azam anaonyesha ligi kibao, Epl mechi 1 kila wiki, anaonyesha bundesliga ya german mechi zote, League 1 ya france mechi zote, ligi ya ndani mechi zote, Saudi PL unamuona Ronaldo,mane,benzema,neymar kila wiki, bado kwa wapenzi wa boxing utaona vitasa kwenye movies zipo channel kibao, news channel kibao.

Hiyo startimes inakipi kipya cha kushindana na azam hapa ndani?
 
Mimi sijawahi kuona Azam Tv wakitaja neno Xmass wala Pasaka! Kimsingi wako biased kwenye mambo ya dini, hata hizo channel chache za kikristo wanalazimika tu kuziweka kwa shingo upande. Mimi Azam TV nilikuwa nayo nimeiacha kwa sababu ni mpira wa bongo tu ninaofaidika nao ambao sasa ivi niko DSTV naenjoy mipira
 
Dstv ni rahisi kununua lakin ni expensive kukitumia kwahiyo wanakimbia pia kwasababu hiyo
Inategemea unahitaji channel zip,maana kifurushi cha chini ni elf 10
 

Acha upuuuz mbona Azam zipo za dini karibu zotee mzee
 
Kama unapesa ya kulipia kila mwezi Azam ni kizuri
Lakini kama huna Pesa ya kulipia kila mwezi basi Startime ndio kizuri Kwa sababu ndio king'amuzi Chenye Chanel nyingi nzuri za Bure.

Kam utakuwa na uwezo zaidi nunua vyote viwili kwani havizidi laki tatu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…