Kati ya DED na DAS nani bosi wa mwingine?

Kati ya DED na DAS nani bosi wa mwingine?

Una haki ya kuchanganyikiwa mkuu,hata mimi huwa nachanyikiwa,lakini naona kama wako at par,ingawa wakati mwingine naona kwa vile DAS ndiye kiongozi wa watumishi wote Wilayani,basi DED yuko chini ya DAS.Inachanganya kwa kweli.

Mimi huwa nadhani kuna haja ya kufuta mfumo wa kuwa na Halimashauri, ili kuondoa huo mkanganyiko ambao kiukweli unaleta misuguano na mikanganyiko isiyo ya lazima na hivyo kukwamisha utendaji kwa ujumla.Hivi kwa nini tusiwe na DC na DAS tu na chini ya DAS kukawa na idara mbali mbali ambazo zitashuhulikia issues za Willaya?Huu mfumo wa kuwa na Halimashauri unaongeza tu bureaucracy,matumizi ya fedha yasiyo ya lazima,ugumu wa udhibibiti na hivyo kuongeza uwezekano wa upigaji.Kwa ujumla mfumo huu uko inefficient.

Binafsi sioni faida za msingi za Halimashauri,infact naona kama they are just a liability to the government.
Halimashauri zetu zimeshindwa kabisa ku-meet expectations za Watanzania.
DED ni mwajiri kwa ngazi ya halmashauri pia mkumbuke na DAS hawezi kuajiri. Hapa mkubwa ni DED.
 
DC anateuliwa na Rais wa Jamhuri lakini DED anateuliwa na Waziri wa TAMISEMI. DC anakazi zake na DED anakazi zake, hawaingiliani.


Kwenye awamu hii wote wameteuliwa na rais.
Zamani TAMISEMI ilipokuwa ofisi ya waziri mkuu ndio ilikuwa DED anateuliwa na PM.

Siku hizi tamisemi IPO ofisi ya rais.

Zipo wilaya zenye halmashauri zaidi ya moja, DED -2, but DAS mmoja.

Wana majukumu tofauti, at one point DED anareport kwa DAS.
DAS anahudhuria vikao vya CMT kama mshauri, pia anahudhuria vikao vya baraza LA madiwani but hawajibiki kwao.

DAS line yake ya utendaji wa kila Siku iko sana kwa maafisa tarafa na wenyeviti wa vijiji/ vitongoji na mitaa , vyombo vyote vya ulinzi na usalama wilayani. He can surmon all government agencies in the district ( TRA,tanesco na taasisi nyingine zote kutoka wizara mbalimbali zilizo wilayani kwake) wakati DED anadeal zaidi na watumishi wa idara mbalimbali wakiwemo watendaji kata/ vijiji + madiwani. Na mamlaka ya DED yanaishia kwenye taasisi zilizo chini ya tamisemi tu.
Kisiasa imedeatelty juu ya DED yupo mwenyekiti wa halmashauri/ meya wakati kwa DAS yupo DC.

DAS yupo kidola zaidi wakati DED yuko kiutumishi/ umma zaidi.

DED ana nafasi kubwa ya kufa akiwa tajiri wakati DAS ana nafasi kubwa sana ya kufa maskini.
 
Kwenye awamu hii wote wameteuliwa na rais.
Zamani TAMISEMI ilipokuwa ofisi ya waziri mkuu ndio ilikuwa DED anateuliwa na PM.

Siku hizi tamisemi IPO ofisi ya rais.

Zipo wilaya zenye halmashauri zaidi ya moja, DED -2, but DAS mmoja.

Wana majukumu tofauti, at one point DED anareport kwa DAS.
DAS anahudhuria vikao vya CMT kama mshauri, pia anahudhuria vikao vya baraza LA madiwani but hawajibiki kwao.

DAS line yake ya utendaji wa kila Siku iko sana kwa maafisa tarafa na wenyeviti wa vijiji/ vitongoji na mitaa , vyombo vyote vya ulinzi na usalama wilayani. He can surmon all government agencies in the district ( TRA,tanesco na taasisi nyingine zote kutoka wizara mbalimbali zilizo wilayani kwake) wakati DED anadeal zaidi na watumishi wa idara mbalimbali wakiwemo watendaji kata/ vijiji + madiwani. Na mamlaka ya DED yanaishia kwenye taasisi zilizo chini ya tamisemi tu.
Kisiasa imedeatelty juu ya DED yupo mwenyekiti wa halmashauri/ meya wakati kwa DAS yupo DC.

DAS yupo kidola zaidi wakati DED yuko kiutumishi/ umma zaidi.

DED ana nafasi kubwa ya kufa akiwa tajiri wakati DAS ana nafasi kubwa sana ya kufa maskini.
 
DAS anawajibika kwa RAS, hali kadhalika DED. Hivyo hakuna line ya uwajibikaji wa moja kwa moja wa DED kwa DAS. Hata hivyo kiitifaki DAS yupo juu zaidi ya DED.

Niongeze kwamba DAS anauwezo wa kumuita DED ofisini kwake na akamuagiza cha kufanya. Lakini DED hawezi kufanya hivyo kwa DAS.
Hujamalizia mpunga DED anampunga mrefu kwamaana ya mapato na matumizi katika halmashauri lakini DAS hakusanyi na anamtegemea DED amsaidie akikwama
 
Huu nao ni ushahidi kuwa wateule wa rais katika TZ ni ngumu hata kufanya kazi. Kwani wote ni wateule wa mkulu na ni rahisi hata kufitiniana.

Angalia hata DC na DED, ndio maana utasikia wilaya fulani DC na DED hawaelewani na hapo mkuu asipoingilia kwa kusitisha uteuzi wa mmoja au wote basi hata maendeleo mnasubiri miaka hata 10.
Ukiona hawaelewani juwa DC anaingilia kazi za Halmashauri, badala ya kuwasimamia
 
mimi madhani kama nchi tungepiga sana hatua kama katika halmashauri kuwe na mojawapo kati ya aidha wakurugenzi au DAS / RAS cheo kimoja wapo kifutwe

halafu hiki cheo kinacho itwa Sijui mkuu wa wilaya sijui mkoa. vifutiliwe mbali havina maana zaid ya ulaji tu na siasa chafu na za kishamba usimamizi wa ulinzi na usalama libaki kuwa jukumu la MA RPC na OCD
Cheo cha DC ni cha kisiasa zaidi kwa kweli Kimondoa,kwa hiyo ni kweli kinaweza kufutwa!Hata hivyo let us be realistic,katika mfumo wa vyama vingi, sidhani kama chama tawala(hapa simaanishi CCM,ni chama cho chote kile kilichoko madarakani), kinaweza kukubali kufuta cheo hicho, kwa kuwa kinasaidia chama husika kisiasa.
 
DED ni mwajiri kwa ngazi ya halmashauri pia mkumbuke na DAS hawezi kuajiri. Hapa mkubwa ni DED.
Mkuu DED anaajiri sawa, lakini yuko Halimashauri
(TAMISEMI ) na DAS yuko serikali kuu(UTUMISHI) kwa hiyo hawahusiani hawa.Nadhani swala la kuajiri halina tija sana,mfumo ndio unaompa mamlaka DED kuajiri,ila haina maana kwamba yuko juu ya DAS kimadaraka.
 
DC anateuliwa na Rais wa Jamhuri lakini DED anateuliwa na Waziri wa TAMISEMI. DC anakazi zake na DED anakazi zake, hawaingiliani.
Uko sahihi expert member. However, kiuhalisia DC anaweza kukwamishwa na DED kutekeleza majukumu yake. Nina mfano halisi, it's too bad
 
Una haki ya kuchanganyikiwa mkuu,hata mimi huwa nachanyikiwa,lakini naona kama wako at par,ingawa wakati mwingine naona kwa vile DAS ndiye kiongozi wa watumishi wote Wilayani,basi DED yuko chini ya DAS.Inachanganya kwa kweli.

Mimi huwa nadhani kuna haja ya kufuta mfumo wa kuwa na Halimashauri, ili kuondoa huo mkanganyiko ambao kiukweli unaleta misuguano na mikanganyiko isiyo ya lazima na hivyo kukwamisha utendaji kwa ujumla.Hivi kwa nini tusiwe na DC na DAS tu na chini ya DAS kukawa na idara mbali mbali ambazo zitashuhulikia issues za Willaya?Huu mfumo wa kuwa na Halimashauri unaongeza tu bureaucracy,matumizi ya fedha yasiyo ya lazima,ugumu wa udhibibiti na hivyo kuongeza uwezekano wa upigaji.Kwa ujumla mfumo huu uko inefficient.

Binafsi sioni faida za msingi za Halimashauri,infact naona kama they are just a liability to the government.
Halimashauri zetu zimeshindwa kabisa ku-meet expectations za Watanzania.
Or else halmashauri zijitosheleze kimapato sio kutegemea kwingine
 
Watumishi wote wa wilaya wapo chini ya DAS kwa hiyo DED yupo chin ya DAS
 
Or else halmashauri zijitosheleze kimapato sio kutegemea kwingine
Unajua mkuu,local governments ziliundwa upya mwaka 1982 baada ya kufutwa mwaka 1972.Nia ya kuzirudisha ilikuwa ni kupeleka huduma za serikali karibu zaidi na wananchi.Kwa kufanya hivyo ilitegemewa kwamba ingechangia na kuhamasisha zaidi maendeleo ya wananchi kwa haraka. This was never realized.Badala yake Halimashauri zikaendekeza ufujaji wa fedha za wananchi na kudumaza maendeleo yao.

Sasa tukisema Halimashauri zijitosheleze kimapato tuna maana gani,kwa kuwa Halimashauri hazina vyanzo vya mapato per se,zinategemea kuwachangisha wananchi.Tatizo kubwa la Halimashauri zetu ni kushindwa kutumia mapato yao kama inavyotegemewa.Mkuu sina sababu yeyote ya kuamini kwamba hata kama serikali ikiruhusu Halimashauri zibaki na mapato yao,hali itakuwa nzuri zaidi,kwa kuwa hata serikali kuamua mapato yapelekwe serikali kuu,halafu Halimashauri zigawiwe, ilikuwa kwa sababu ya upigaji.Hapana,
Halimashauri zimeshindwa kutimiza malengo yaliyo kusudiwa,tuzifute tu,kama tulivyofanya 1972.

NB:Ukitaka kujua historia ya serikali za mitaa Tanzania,google,"The history of local governments in Tanzania."
 
Ndio maana madai ya watumishi wa umma,mishahara ambayo haikulipwa Das ndo anaidhinisha ikishatoka kwa DED mfano,mtumishi akafariki mshahara ukatoka it means huo mshahara haukulipwa,DED ataurudisha kwa Das ambaye ataidhinisha na DAS atarudisha kwa RAS ambaye ataurudisha hazina au kama kuna watumishi wa halmashauri wanadai DED ataandaa madai yataidhinishwa na DAS ndo yaende kwa RAS na RAS ataidhinisha na kupeleka kwa katibu mkuu ndo yapelekwe hazina kwa hivyo kwa mlolongo huo DAS ni boss wa DED
 
Unajua mkuu,local governments ziliundwa upya mwaka 1982 baada ya kufutwa mwaka 1972.Nia ya kuzirudisha ilikuwa ni kupeleka huduma za serikali karibu zaidi na wananchi.Kwa kufanya hivyo ilitegemewa kwamba ingechangia na kuhamasisha zaidi maendeleo ya wananchi kwa haraka. This was never realized.Badala yake Halimashauri zikaendekeza ufujaji wa fedha za wananchi na kudumaza maendeleo yao.

Sasa tukisema Halimashauri zijitosheleze kimapato tuna maana gani,kwa kuwa Halimashauri hazina vyanzo vya mapato per se,zinategemea kuwachangisha wananchi.Tatizo kubwa la Halimashauri zetu ni kushindwa kutumia mapato yao kama inavyotegemewa.Mkuu sina sababu yeyote ya kuamini kwamba hata kama serikali ikiruhusu Halimashauri zibaki na mapato yao,hali itakuwa nzuri zaidi,kwa kuwa hata serikali kuamua mapato yapelekwe serikali kuu,halafu Halimashauri zigawiwe, ilikuwa kwa sababu ya upigaji.Hapana,
Halimashauri zimeshindwa kutimiza malengo yaliyo kusudiwa,tuzifute tu,kama tulivyofanya 1972.

NB:Ukitaka kujua historia ya serikali za mitaa Tanzania,google,"The history of local governments in Tanzania."
Interesting! Tuendelee kujadili inawezekana kuna wenye hoja za kutuelimisha zaidi, ila kiukweli kuna shida. Namkumbuka DC wangu mpendwa ambaye DED wake alimbeza kwangu nikiwa na wageni wa Taifa jingine. I felt so bad.
 
Interesting! Tuendelee kujadili inawezekana kuna wenye hoja za kutuelimisha zaidi, ila kiukweli kuna shida. Namkumbuka DC wangu mpendwa ambaye DED wake alimbeza kwangu nikiwa na wageni wa Taifa jingine. I felt so bad.
Pole sana mkuu.Haya ndiyo kati ya mambo yanayotufanya tuamini kwamba Halimashauri zifutwe.Ni kweli kwamba mafungu DED waliyonayo yanawafanya wajione miungu watu na hivyo kudharau watendaji wengine wa Wilaya na kuwaona si kitu kabisa.Tabia hizi hazikubaliki kabisa mkuu.
 
Wadungu naomba nami nichangie mada hii ambayo wengi wanaona kama uhusiano wa DED na DAS ki-protokali unachanganya. Mchango wangu utazingatia sheria, kanuni na taratibu za nchi.
1. Mkuu wa Wilaya (DC)
Mkuu wa Wilaya anateuliwa na Raisi kwa mujibu wa kifungu cha 13 (2) cha sheria ya Tawala za Mikoa (The Regional Adminstration Act, 1997). Majukumu yake ni pamoja na kuwa mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya. Kwa mantiki hiyo anakuwa muwakilishi wa Raisi katika kusimamia ulinzi, usalama na shughuli za maendeleo kwa ujumla. Akishateuliwa mkuu wa Wilaya anaapishwa na kusimamiwa kiutendaji na mkuu wa Mkoa (kifungu 13 kifungu kidogo cha 3).

2. Katibu Tawala wa Wilaya (DAS)
Kifungu cha 16 (2) cha sheria ya Tawala za Mikoa kinamtambua DAS kama principal adviser (yaani mshauri mkuu) wa DC. Kifungu hiki pia kinasema DAS anateuliwa kwamujibu wa sheria ya Utumishi wa Umma. Bahati mbaya sina hiyo sheria hapa na nimetafuta mtandaoni sijaweza kuipakua. Ila natoa hoja yangu hapa kwa kuzingatia uteuzi wa Ma-DAS uliofanywa tarehe 5.8.2018 na Waziri mwenye dhamana ya Utumishi wa Umma. Katika tangazo lake kifungu cha 1.2 Waziri alisema, "Leo nimewaita kuzungumza nanyi kuhusu Uteuzi na Uhamisho wa baadhi ya Makatibu Tawala wa Wilaya. Kwa mamlaka niliyokasimiwa kwa mujibu wa Sheria nimefanya uteuzi wa Makatibu Tawala wa Wilaya ili kujaza nafasi wazi kumi nane (18) zilizopo katika wilaya za Kinondoni, Mpwapwa, Dodoma, Iringa, Bukoba, Kigoma, Siha, Mtwara, Newala, Misungwi, Njombe, Kondoa, Manyoni, Kilindi, Chunya, Pangani, Bagamoyo na Handeni".
Hivyo, kwamujibu wa tangazo la Waziri mwenye dhamana ya Utumishi wa Umma ambalo nimenukuu hapa, uteuzi wa DAS upo chini yake kisheria.

3. Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya (DED)
Kwa mujibu wa kifungu cha 22 (2) cha Sheria ya Utumishi wa Serikali za Mitaa ( The Local Government Service Act, 1982), DED anateuliwa na Raisi. Majukumu kiutendaji DED anakuwa Chief Executive wa Halmashauri na anaripoti kwa Katibu Tawala wa Mkoa (RAS).

Hitimisho
Kwangu mimi sioni mkanganyiko wowote wa kisheria kati ya DED na DAS, maana DED anateuliwa na Raisi na DAS anateuliwa na Waziri wa Utumishi wa Umma. Sema DAS anaweza kuonekana katika mazingira flani kuwa boss wa DED pale ambapo anatekeleza kazi anazotumwa na DC. Pia, nimewahi kuona mahala DAS anaudhuria vikao vya Council Management (CMT) ambavyo DED ndio mwenyekiti. DC ni mkuu kiitifiki kwa DED ingawa wote wanateuliwa na Rais, utofauti wao unatokana na majukumu. DC anapolinda amani, usalama na maendeleo ni pamoja na kazi anazofanya DED na wakuu wengine wa vyombo vya Ulinzi na Usalama kwenye ngazi ya Wilaya.
Huu ni uelewa wangu kwa kadri nilivyoelewa sheria husika, kama kuna mahala nimekosea niko tayari kukosoloewa maana mimi si mwanasheria kitaaluma. Asanteni

Nimeshawishika na namna nzuri uliyoitumia kueleza hoja yako. Hongera sana mkuu. Kwa hoja ya nani anateuliwa na nani (kama ulivyoeleza ni kweli) basi huenda kweli DED yuko juu kiitifaki kuliko DAS, swali langu hapa ni je, ni lazima mtendaji aliyeteuliwa na Mamlaka ya juu awe juu kiitifaki kuliko yule aliyeteuliwa na mamlaka ya chini ?
 
Kwa dhana ya "Wilaya" dhidi ya "halmashauri," mimi nadhani DAS yuko juu kiitifaki kuliko DED kwa mchanganuo ufuatao:-

DAS ni mtumishi wa wilaya. (Wilaya moja, DAS mmoja).

DED ni mtumishi wa halmashauri (kwenye Wilaya moja kunaweza kuwa na halmashauri zaidi ya moja).

Kwa maana hiyo tunaweza kusema kwamba "Wilaya moja, DAS mmoja".

Na pia tunaweza kusema, "Wilaya moja halmashauri moja au mbili na hivyo DED mmoja au wawili"

Katika mazingira haya simuoni DED akiwa juu ya DAS.
 
Back
Top Bottom