Haya ni baadhi,Vitu kupanda bei kiholela na serikali kusingizia Vita ya Urusi huku maisha yanakuwa Magumu.
Kula kwa kamba ya urefu wake.
Watu wachache kulamba Asali.
Wizi na ujambazi kurudi kwa kasi. Sasa hivi wenye vibanda vya mpesa na tigo pesa wanakaa kwa wasiwasi sana.
Mauwaji yameongezeka kwa hari ya juu. Watu wanauwana ni dalili ya kukosa uongozi madhubuti.
N. K
Ikumbukwe kuwa ufananisho wa haki Ni Hadi Samia aongoze miaka tano!Kinachoitwa uwekezaji ni kukaribisha wezi kuiba rasilimali zetu.
Hakuna unyama uliofanyika kama kuwaondoa wamasai kwa kutumia majeshi yetu kwenye ardhi yao na kumpa mwekezaji.
Ni jambo la aibu mno kusitisha mradi wa Bwawa la Nyerere na kuanzisha mwingine wa Gesi.
Wizi na ubadhirifu wa fedha za miradi na huduma mbovu ni jambo la kawaida kabisa kwa sasa.
Kuruhusu wafanyabiashara kupandisha bei wanavyojisikia ni kitendo cha kuwaumiza wananchi ambacho serikali imekibariki.
Kwa ufupi ni kwamba awamu hii imejaa uovu mwingi kuwahi kutokea katika historia ya Taifa letu.
Mnadanganywa sana nyie watu. Mnatumia nguvu kubwa kumchafua jpm. Tuseme ushahidi ulishaandaliwa kumshitaki Mbowe, tena mbona awamu hii ikaamua kuendelea nayo hiyo kesi? Si wangeacha tu. Hampendi sana kuambiwa kwamba Mbowe alishitakiwa na Serikali hii iliyopo. Mnaona kama ni doa siyo?
Sent from my TECNO PR651H using JamiiForums mobile app
Kwa sasa karibu wote whni...........................Wafuasi wa Magufuli wanaituhumu serikali ya sasa kuwa ina wahuni, wakiongozwa na yule mtu wao aliyepelekwa Malawi na hashtag yake ya #KataaWahuni
Sasa nataka tuende kwa fact na records, mimi nataka waniambie ni uhuni gani umefanyika serikali ya Samia kushinda uhuni wa Serikali ya Magufuli
Kwa kuanzia tu, Kipindi cha Magufuli ndio mbunge alipigwa risasi katika viwanja vya Bunge na watu waliompiga kung'oa CCTV Camera zilizorekodi tukio
Kipindi cha Magufuli ndio watu walitekwa kwa wingi zaidi kama akina Kinguye, Ben Saanane, azory Gwanda, Mdude Chadema, Roma Mkatoliki, Mo Dewji, Abdul Nondo n.k
Kipindi cha Magufuli ndio mkuu wa mkoa huku akirekodiwa na Camera alivamia kituo cha Tv kuamrisha habari yake isomwe na wala hakuchukuliwa hatua yoyote
Kipindi cha Magufuli ndio tulisikia mkuu wa mkoa akipiga watu marufuku kuja kwenye 'mkoa wake'
Kipindi cha Magufuli ndio mtu kama Sabaya alitamba sana, na kuna matukio kibao kama ya ubakaji, uporaji, kubambikizia kesi n.k
Achilia mbali uhuni wa kuengua asilimia 90 ya wagombea wa upinzani kwenye uchaguzi Serikali za mitaa kwa kigezo kuwa hawajui kusoma wala kuandika
Achilia mbali kulazimisha na kuhonga wapinzani kujiuzulu ubunge na udiwani kisha kugombea tena jimbo hilo hilo ili Magufuli aonekane anapendwa
Ndio kipindi tumedanganywa miradi mikubwa tunajenga kwa fedha za ndani
Achilia mbali kauli za kihuni za Magufuli kama 'Baki na mavi yako nyumbani', 'Mnataka mpanuliwe wapi', na kusifia wake za watu hadharani
Huu ni uhuni mdogo sana kati ya uhuni mwingi aliokuwa akifanya Magufuli
Haya sasa niambieni matukio ya kihuni kwenye serikali ya Samia tulinganishe
Ni kweli kisha wakajidai ku-back date tarehe za faili kuandaliwa eti akisubiriwa kizito wa Bomang'ombe huku aliyepisha kiti na hayupo kujitetea akisingiziwa ndiye aliianzisha..................dunia itawaumbua mpaka basi. Kweli yule jamaa kama alinuia kumweka nyuma ya nondo angekamata wadogo amwache mkubwa? Hapana ni uongo ambao walioshiriki hawakujipanga kitaaluma..kesi ya mbowe ilitengenezwa na Ssh.
..alipoona kesi inakwenda vibaya, polisi, serikali,na mahakama, wanaadhirika, akaona waifute.
..nadhani hata huko nje anakotembelea mabeberu watakuwa wamemnong'oneza asiige ukatili wa waziwazi wa awamu ya 5.
Yaani utazani Ikulu kuna Sanamu.Haya ni baadhi,
Tutazidi kujazia kadri miaka inavyokwenda, hadi atimize mitano Kama Magu!