Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge mbele!

Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge mbele!

(Uamuzi wa kuendelea au kutoendelea ungetegemea Lissu ametoa hoja gani kwenye pingamizi hilo, naamini pamoja na uchache wa wabunge wa upinzani bungeni, wanapotoa hoja ya msingi kwa maslahi ya taifa, na hoja yenyewe ikawa na mashiko, wako wabunge makini wa CCM, kama kina Deo Filikunjombe and the like, lazima wangewaunga mkono upinzani, na kwa vile issue yenyewe ni ya kisheria, naamini wabunge wengi wa ukweli, wangewaunga mkono. Tena kwenye utoaji wa pingamizi hilo, wangebanana na kanuni tuu, Mama Spika angekuwa hana pa kotokea.

Mwisho wa siku, bunge zima sasa ndipo lingepiga kura kuunga mkono, hoja ya pingamizi au laa, kwenye kura sasa, ndipo kama hoja ya Chadema ingekataliwa, hapo sasa, ndipo palipostahili kuwasilishwa kwa hotuba ya kambi rasmi ya upinzani ikifuatiwa na honarable walkout!.)

Mheshimiwa Pasco nawe inabidi ukubali yaisha, umewasema wenzako kuhusu presumption nawe unafanyanini kwenye maelezo haya?
 
Pasco, heshima kwako mkuu!! Nimejitahidi kufuatiria sana mabandiko yote ili nitolewe TONGOTONGO KWA HILI!
Mpaka hapa nimepata mwanga kama sio kuelewa kabisa kinachoendelea!
Ndg Pasco kwa debate hii nakuomba ukubaliane na CDM kuwa walikuwa sahihi!! Ila usikubali tu paspo kuelewa kama bado endelea kuwauliza wadau. HAWANA HIANA!!
 
PASCO huenda uanhoja ambayo hautaki kuiweka wazi. Hebu funguka, kwani kwa matazamo wangu kanuni hiyo ya 86 isingeweza kusaidia kuzuia msawda kusomwa mara ya pili. Pia huenda Lissu asingewasilisha maoni ya kambi rasmi huenda ungekuja na maoni mengine kwamba kwa nini hakusoma maoni yao ndio wapinge. Walichokifanya CHADEMA ninakiona kuwa ni sahihi sana na wameeleza na nimewaelewa kuwa kwanini mchakato mzima utakuwa hovyo na hivyo kunauwezkano mkubwa wa kupata katiba mpya ya hovyo pia
Miradibubu, inapotokea hoja ya msingi inamakosa, kanuni zinatamka kwanza unatoa pingamizi, hoja yangu inabaki na inasimama pale pale, Kwanini Chadema hawakutoa pingamizi?. Kanuni inasema kwanza toa pingamizi, ukishatoa pingamizi, toa sababu, kitendo cha kutoa hotuba ni kumwambia spika hatuna pingamizi, maoni yetu ni haya ... endeleeni, regardless ya content ya maoni hayo, kutungwa kwa sheria ni mchakato, yaani process, unaanzia hapa unapita hapa na hapa na hapa mpaka unafika mwisho, kwanini hawakupinga?.
 
Pasco,Bahati mbaya mpaka sasa hakuna majibu ya maana sijui kwanini tunakwepa swali la msingi ?.

Miradibubu, inapotokea hoja ya msingi inamakosa, kanuni zinatamka kwanza unatoa pingamizi, hoja yangu inabaki na inasimama pale pale, Kwanini Chadema hawakutoa pingamizi?. Kanuni inasema kwanza toa pingamizi, ukishatoa pingamizi, toa sababu, kitendo cha kutoa hotuba ni kumwambia spika hatuna pingamizi, maoni yetu ni haya ... endeleeni, regardless ya content ya maoni hayo, kutungwa kwa sheria ni mchakato, yaani process, unaanzia hapa unapita hapa na hapa na hapa mpaka unafika mwisho, kwanini hawakupinga?.
 
Mwenye macho haambiwi tazama! Unaweza kuwa na macho mazuri yanayokuwezesha kuona mbali na karibu.Unaweza kutazama kitu fulani na watu waliokuzunguka wakaamini pasipo shaka kuwa kitu hicho umekiona lakini kumbe macho yako yametua kwenye kitu hicho kijuujuu pasipo Mashiko.

Katika hali kama hiyo, haina maana kuwa wewe ni kipofu, la hasha! Ikitokea hivyo mambo mawili yanaweza kutokea inawezekana umeangalia(kutazama) kitu hicho kwa haraka ama hukuwa makini na hivyo kukosa muda wa kutafakari vizuri ili kuweza kutafsiri kwa usahihi kile ulichokiona.

Pasco, umejaribu kueleza kwa mtazamo wako jinsi CDM walipokosea. Naomba nikukumbushe kitu kimoja kama ulifatilia mjadala wa mswaada huo baada ya mh.Tundu Lissu kuwasilisha maoni ya kambi ya upinzani waliomba mwongozo wa spika bila kupatiwa fursa hiyo, mpaka wengine wakawa wanasikika wakimtaka chinichini "Hoja ja kupinga mswaada kujadiliwa" Lakini spika hakutaka kuwasikiliza! Sasa ktk hali kama hiyo watamwomba msamaha nani?
clet 8, baada ya muswada kuwasilishwa kuna muda wa kutoa pingamizi, hawakutoa, kanuni hizo zinamlazimisha spika kuzuia hoja zozote, kama nafasi yao ilikuwa ni kutoa pingamizi, hawakutoa, kwenye pingamizi ndipo unaweka sababu zako, ni kweli baasda ya hotuba ya Mhe Lissu, hao waliomba muongozo wa nini wakati there were no room kwa miongozo at that stage, mlaumuni tuu spika kwa udikteta, lakini kanuni ndivyo zinavyoelekeza.
 
Mzee Mwanakijiji, mtu anapotaka kuvuka mto, kina cha maji hakipimwi kwa macho, bali mtu huingiza mguu kidogo kidogo na akifika mahali maji yakamfikia magotini huku hata nusu ya safari hajafika, ndipo hurudi alipotoka kwa kuogopa akiendelea ataweza kuzama.

Mhe. Tundu Lissu hakupaswa kuisoma ile hotuba yake ya kambi ya upinzani, alipaswa kwanza atoe pingamizi, na mano ya kuyasema kwenye pingamizi hilo yameainishwa, baada ya kutoa pingamizi, hatua ya kwanza, muswada ungesitishwa, baada ya hapo Lissu angetakiwa sasa kutoa sababu zake ambazo zingekuwa seconded na wabunge wengine wowote.

Uamuzi wa kuendelea au kutoendelea ungetegemea Lissu ametoa hoja gani kwenye pingamizi hilo, naamini pamoja na uchache wa wabunge wa upinzani bungeni, wanapotoa hoja ya msingi kwa maslahi ya taifa, na hoja yenyewe ikawa na mashiko, wako wabunge makini wa CCM, kama kina Deo Filikunjombe and the like, lazima wangewaunga mkono upinzani, na kwa vile issue yenyewe ni ya kisheria, naamini wabunge wengi wa ukweli, wangewaunga mkono. Tena kwenye utoaji wa pingamizi hilo, wangebanana na kanuni tuu, Mama Spika angekuwa hana pa kotokea.

Mwisho wa siku, bunge zima sasa ndipo lingepiga kura kuunga mkono, hoja ya pingamizi au laa, kwenye kura sasa, ndipo kama hoja ya Chadema ingekataliwa, hapo sasa, ndipo palipostahili kuwasilishwa kwa hotuba ya kambi rasmi ya upinzani ikifuatiwa na honarable walkout!.

Mhe. Lissu baada ya kufika kando ya mto na kuyatazama tuu yale maji, akaamua hapa hatuwezi kuvuka, na kuamua kurudi alikotoka, angepaswa kuingiza kwanza huo mguu na kuona kina cha maji.

Mpaka sasa, hoja yangu ya msingi, haijajibiwa, kwanini Chadema hawakutoa pingamizi kwa muswada ule kwa mujibu wa kanuni?.

Kwanini badala ya kutoa pingamizi, wao ndio kwanza wakatoa go ahead ya majadiliano kuendelea kwa hotuba yao?.

Hivi nikisema kumbe waliotuangusha pale bungeni kwa kuruhusu muswada ule upite kiurahisi vile ndio wenzetu hawa hawa tuliowategemee kupinga kwa kutumia, wao wakapinga kwa kususa?.

Baada ya kusomwa kwa hotuba ya Mhe. Lissu, ndipo wabunge wanasimama kutaka miongozo?, miongozo ya nini tena wakati nafasi ya pingamizi walipewa na hawakuitumia?!. Hata kama spika ningekuwa ndio mimi, ningewazuia ili muswada usonge mbele, na ndicho alichokifanya madam speaker.

Kwa wale wote wanaomshutumu speaker kwa ubabe, hebu someni kanuni, kuna wakati kanuni inamuelekeza speaker asikubali kusikiliza hoja yoyote na anachofanya ni kufuata tuu kanuni.

Nadhani, tufike mahali, tukubaliane kutokubaliana, mimi nikisisitiza Chadema were wrong, they failed us na sasa sheria imeshapitishwa, ikishasainiwa, kuipinga ni criminal offence, na at this jancture, nakuhakikishia Mzee Mwanakijiji na wapenzi wote wa Chadema, there is nothing Chadema can do, wala hao wanaharakati!.

Ndipo hapa ule ushauri wangu unaporudi tena, Chadema wakubali, makosa, sio lazima watubu hadharani, hata kimoyo moyo kama walivyosema hadharani hawamtambui rais, lakini kwa vile ana exist, umtambue usimtambue, yeye anabaki kuwa ni rais!.
..pasco jaribu kuelewa bwn, kanuni unayoisema isingebadilisha kitu walichopanga ccm, mbn unauliza katikati wakati spika amekandamiza na kunyima fursa za kuteleza maazimio ya bunge wakati muswada ulipokataliwa na bunge mezi wa nne? ina maana hulijui hilo? kwa nn kupoteza muda kutaka kutumia kanuni ilihali zipo dalili za conspiracy? labda tusaidie ni lini wabunge wa ccm walisupport maoni ya chadema bungeni..? usitutajie mbunge mmoja, unakwa kama kukaa kwako dodoma kusikiliza vikao vya bunge ni sawa na sifuri tu, kama hadi leo unashindwa kuwajua wabunge wa ccm wako kwa faida ya nani!
 
Sijui kwa nini Pasco unang'ang'ania hiki kifungu cha 86 kama ndio silver bullet bila kuangalia kwa ujumla wake. Umeshambiwwa ndani ya hicho kifungu kuna kipengele cha 4 na kinatumika kutoa hukumu ya hoja/pingamizi. Na kimetumika kuzima hoja huko nyuma. Na tayari nimekupa mfano ni jinsi gani kimetumika kupindisha sheria za nchi. Mfano huo ni bunge lililopita ambapo Lissu alitoa hoja ya kutoruhusu mhimili mmoja wa dola kuingilia mhimili mwingine, lakini Spika akatumia hicho kipengele cha 4 na pingamizi la Lissu likatupwa. Mifano iko mingi sana, sasa kama Spika amekuwa anatumia hicho kipengele una uhakika gani kwamba kwenye huu muswada asingetumia?

Lakini kubwa ambalo sijui kwa nini husemi ni kwanini Spika alikataa kumruhusu Mnyika kuongea? Pasco kifungu cha 86 kingekuwa na maana tu kwa nchi au nisema bunge linafuata sheria na taratibu zilizowekwa. Lakini sio hili bunge la Makinda. In fact kama Makinda angekuwa anaaongoza bunge kwa kufuata sheria na taratibu zake huu muswada usingesomwa kabisa kwa mara ya pili kabla maoni maoni ya wananchi hayajachukuliwa. Rejea hansard ya bunge usikie alisema nini Makinda wakati anawaambia wakerebishe muswada mwezi March.

Mkuu mimi naungana na wadau waliosema huyu jamaa anapenda ligi.

Kwanza kataka kutupeleka chaka kataja kifungu tu na akaambiwa akiweke hakufanya hivyo.
MM Mwanakijiji (Mungu ambariki) katuwekea kifungu chote na vipengele vyake.

Ufafanuzi umetolewa tumeona ni wapi ccm wangepatumia kuzima hoja bado huyu jamaa hataki kuelewa.

Kaambiwa aeleze basi je kifungu kingetumika mjadala usingepita?hataki kueleza au hata kutoa mfano mmoja tu lini kilitumika na kikaleta mafanikio.

Tumeona mpaka mifano ya bunge lilopita jinsi kifungu hicho hicho anachong'ang'ania Pasco jinsi kilivyotumika kupitisha muswada wa kidhalimu.
Lakini bado jamaa hataki kukubali.
 
Pasco,
Unazunguka tu hujajibu swali la MMK. UNAAMINI KWA KUTUMIA KIFUNGU 86.3b TL pingamizi lake lingepita?
Thesi, bunge haliendeshwi kwa imani, linaendeshwa kwa kanuni, kama kanuni mlimtaka TL alete pingamizi, ili angalau hilo pingamizi lisikilizwe, yeye akaenda straight kwenye hotuba ambayo ndio go ahead ya majadiliano yaendelee.

Nichozungumza mimi ni kuwa Chadema hawakuupinga muswada ule. Kwanini?. Sasa kama pingamizi lao lingekubaliwa au lingekataliwa, hayo sasa ni mengine, lakini kwanza pingamizi, mengine yote yangefuatia!.
 
Pasco,
Hii hoja jana ilijibiwa vizuri na Tundu Lisu. Sijasoma maelezo ya wachangiaji wengine wote lakini nasema hivi; Chadema walikuwa sahihi kabisa, hiyo kanuni ya 86 unayoisema mh. Lisu allitumia na akaungwa mkono na wabunge wenzake kwa kusimama kama utaratibu unavyotaka.
Mheshimiwa spika akakaidi kufuata utaratibu wa kuwahoji wabunge. Pamoja na jitihada za baadhi ya wabunge kama Machali na Myika kutaka kuomba mwongozo wa spika lakini walinyimwa nafasi hiyo, spika alikataa kata kata kutoa nafasi hiyo na kuamurui mjadala uendelee, kwahiyo unataka kutuambia kwamba wewe hukumuona spika alivyobananga hicho kifungu?
Ukiwa kama mwanasheria jaribu kujiridhisha na namna spika anavyokiuka sheria na kanuni za bunge kwa favour ya chama chake.

Katika hili wewe ndiye umekosea na unatakiwa kuwaomba radhi chadema pamoja na sisi wanaJF kwa kutaka kutupotosha! Na hii imekuwa ni tabia yako kupotosha mambo mengi yanayofanywa na chadema na ushahidi upo hapa hapa JF.
 
Mkuu Pasco hii ni mara ya pili CDM inachemka.Rejea sakata la meya wa Arusha walikuwa na siku 30 kumfungulia kesi badala yake wakaamua maandamano nilipojaribu kuwauliza kwanini hawafungui kesi nilipata majibu ya aina hii.

Thesi, bunge haliendeshwi kwa imani, linaendeshwa kwa kanuni, kama kanuni mlimtaka TL alete pingamizi, ili angalau hilo pingamizi lisikilizwe, yeye akaenda straight kwenye hotuba ambayo ndio go ahead ya majadiliano yaendelee.

Nichozungumza mimi ni kuwa Chadema hawakuupinga muswada ule. Kwanini?. Sasa kama pingamizi lao lingekubaliwa au lingekataliwa, hayo sasa ni mengine, lakini kwanza pingamizi, mengine yote yangefuatia!.
 
Thesi, bunge haliendeshwi kwa imani, linaendeshwa kwa kanuni, kama kanuni mlimtaka TL alete pingamizi, ili angalau hilo pingamizi lisikilizwe, yeye akaenda straight kwenye hotuba ambayo ndio go ahead ya majadiliano yaendelee.

Nichozungumza mimi ni kuwa Chadema hawakuupinga muswada ule. Kwanini?. Sasa kama pingamizi lao lingekubaliwa au lingekataliwa, hayo sasa ni mengine, lakini kwanza pingamizi, mengine yote yangefuatia!.

Pasco:hapo kwenye redi ndio jibu hilo.hata kama CDM wangeweka hilo pingamizi bado madam spika angekataa tu.Ungesikia tu walio sema ndio wameshinda,mjadala ungeendelea kama kawaida.
 
Mkuu mimi naungana na wadau waliosema huyu jamaa anapenda ligi.

Kwanza kataka kutupeleka chaka kataja kifungu tu na akaambiwa akiweke hakufanya hivyo.
MM Mwanakijiji (Mungu ambariki) katuwekea kifungu chote na vipengele vyake.

Ufafanuzi umetolewa tumeona ni wapi ccm wangepatumia kuzima hoja bado huyu jamaa hataki kuelewa.

Kaambiwa aeleze basi je kifungu kingetumika mjadala usingepita?hataki kueleza au hata kutoa mfano mmoja tu lini kilitumika na kikaleta mafanikio.

Tumeona mpaka mifano ya bunge lilopita jinsi kifungu hicho hicho anachong'ang'ania Pasco jinsi kilivyotumika kupitisha muswada wa kidhalimu.
Lakini bado jamaa hataki kukubali.
Mpatanishi, sio kweli napenda ligi, nimetoa hoja tatu za msingi, naona mnang'ang'ania moja. Nimesema Chadema walikosea, nikashauri kwanza wakubali makosa, kukubali makosa ni sawa na kuomba radhi, na mwisho nikashauri, wakubali yaishe, wawaambie wanachama na wapenzi wao wasonge mbele!.

Sheria imepitishwa, sasa kwa kususa, walichokipata ni kipi?, sheria ikishainiwa hii ni habari nyingine, hakuna tena chochote mnachoweza kufanya, sio Chadema, si wanaharakati!

Tatizo la baadhi ya manazi wa Chadema, wanaamini Chama chao ni chama kitakatifu na viongozi wake ni watakatifu hawawezi kufanya makosa!.

Mimi kama mwana jf nisiiegemea upande wowote, naelewa fika ukosoaji wa Chadema humu jamvini jinsi unavyoshukiwa.

Mimi naendelea kusimama na ukweli ninauamini, kama utaita ligi, ita tuu, watakaosema nimetumwa na waseme tuu, ila mwisha wa siku, wale wenye kuubali ukweli mchungu, mtanielewa baada ya 2015, tutakapo kuja tena humu humu tunalia lia!.
 
Thesi, bunge haliendeshwi kwa imani, linaendeshwa kwa kanuni, kama kanuni mlimtaka TL alete pingamizi, ili angalau hilo pingamizi lisikilizwe, yeye akaenda straight kwenye hotuba ambayo ndio go ahead ya majadiliano yaendelee.

Nichozungumza mimi ni kuwa Chadema hawakuupinga muswada ule. Kwanini?. Sasa kama pingamizi lao lingekubaliwa au lingekataliwa, hayo sasa ni mengine, lakini kwanza pingamizi, mengine yote yangefuatia!.

Pasco,
Unapopinga kitu sio suala la kusema tu kwamba unapinga na kukaa chini. Unaweza kutoa maelezo ya awali kuonyesha sababu za kupionga kisha unataja kifungu cha kanuni husika na kutoa hoja. Na hilo ndilo alifanya TL sasa hapo huelewi kitu gani?

Kilichotokea ni kitu ambacho ccm na spika hawakukitegemea. Spika ilibidi akiuke kanuni kwakuwa ccm hawakuwa wamelijadili namna ya kulikabili hilo, kwahiyo hakujua msimamo wa wabunge wa ccm vinginevyo angekubali na kuwahoji wabunge na ccm+cuf wangepinga hoja.
 
Pasco:hapo kwenye redi ndio jibu hilo.hata kama CDM wangeweka hilo pingamizi bado madam spika angekataa tu.Ungesikia tu walio sema ndio wameshinda,mjadala ungeendelea kama kawaida.
sulphadoxine, ili mjadala huu uishe, lazima tutafika mahali tukubaliane kutokubaliana, mimi nasema Chadema walikosea, they did a wrong move and they lost the game. Nimewashauri wakubali makosa, wasiangalie walipoangukia bali wageuke nyuma kutazama walipojikwaa, wasimame na kusonga mbele. Sheria ikishasainiwa nakuhakikishieni, there is nothing Chadema can do!.

Dawa ni kukubali walikosea, the sooner, the better hivyo wapenzi na wanachama wao, waingie kwenye mchakato!.
 
Pasco,
Unapopinga kitu sio suala la kusema tu kwamba unapinga na kukaa chini. Unaweza kutoa maelezo ya awali kuonyesha sababu za kupionga kisha unataja kifungu cha kanuni husika na kutoa hoja. Na hilo ndilo alifanya TL sasa hapo huelewi kitu gani?

Kilichotokea ni kitu ambacho ccm na spika hawakukitegemea. Spika ilibidi akiuke kanuni kwakuwa ccm hawakuwa wamelijadili namna ya kulikabili hilo, kwahiyo hakujua msimamo wa wabunge wa ccm vinginevyo angekubali na kuwahoji wabunge na ccm+cuf wangepinga hoja.
Mwita Maranya, ubishani wetu mkubwa humu ni jee TL alifanya alichopaswa kufanya kwa mujibu wa kanuni?.
Hoja yangu nimewaambia alikosea, kanuni inayo sehemu ya kutoa pingamizi na kutoa sababu ambayo TL hakuitumia, na badala yake, akatoa hotuba yake kukamilisha process!.

Kama na wewe umo kwa ile ile ya viongozi wetu ni watakatifu, tangu mwanzo nimewaambia, kama mambo yenyewe ndio haya, msije humu kutulilia, 2015 sio mbali!
 
Mkuu Pasco hii ni mara ya pili CDM inachemka.Rejea sakata la meya wa Arusha walikuwa na siku 30 kumfungulia kesi badala yake wakaamua maandamano nilipojaribu kuwauliza kwanini hawafungui kesi nilipata majibu ya aina hii.

Ngongo,
Siasa za chadema kwako na Pasco ni kina kirefu,hamuwezi kuziogelea na mkijaribu tu lazima mzame. Na hapa pasco ameshazama sasa amebaki anatapa tapa.
Chadema ilipowatimua madiwani wasaliti alikuja na hoja kama hii na wewe ukamuunga mkono kama kawaida lakini sasa kiko wapi? Ni kweli chadema si malaika lakini katika hili pasco amechemka tena vibaya.
 
mkuu PASCO!
kuna mahali uli'comment kuwa ulishawahi kuonana na RA na akakueleza wazi kuwa yeye ndo alimuweka SS na ndiye aliyemtoa na kumuweka Anna makinda kuwa spika, kwa mazingira hayo hayo sioni ni kwanini unaamini unaamini kifungu cha kanuni ya 86 kingefuatwa kihalali (nasema kihalali maana inawezekana kikafuatwa isivyo kihalali) na hivyo mswada kutosomwa mara ya pili, iweje leo mtu aliyewekwa kwenye uspika na fisadi aache kufuata kanuni na masharti ya fisadi huyo? (note: RA na CCM ndo mafisadi)


anapenda kujifagilia kweli....hahaha..full fix.....msukuma mbishi huyu ajabu....yaani yeye na hiyo kanuni ya 86 anzani ndo ulikuwa mwarobaini waibana ccm...
 
Pasco,
Hii hoja jana ilijibiwa vizuri na Tundu Lisu. Sijasoma maelezo ya wachangiaji wengine wote lakini nasema hivi; Chadema walikuwa sahihi kabisa, hiyo kanuni ya 86 unayoisema mh. Lisu allitumia na akaungwa mkono na wabunge wenzake kwa kusimama kama utaratibu unavyotaka.
Mheshimiwa spika akakaidi kufuata utaratibu wa kuwahoji wabunge. Pamoja na jitihada za baadhi ya wabunge kama Machali na Myika kutaka kuomba mwongozo wa spika lakini walinyimwa nafasi hiyo, spika alikataa kata kata kutoa nafasi hiyo na kuamurui mjadala uendelee, kwahiyo unataka kutuambia kwamba wewe hukumuona spika alivyobananga hicho kifungu?
Ukiwa kama mwanasheria jaribu kujiridhisha na namna spika anavyokiuka sheria na kanuni za bunge kwa favour ya chama chake.

Katika hili wewe ndiye umekosea na unatakiwa kuwaomba radhi chadema pamoja na sisi wanaJF kwa kutaka kutupotosha! Na hii imekuwa ni tabia yako kupotosha mambo mengi yanayofanywa na chadema na ushahidi upo hapa hapa JF.

Mwita Maranya, TL hakuweka pingamizi, na ni hotuba yake ilitoa go ahead, majadiliano yaendelee.
Mimi ninapokosea ni mwepesi kuomba msamaha, ila manazi wa Chadema humu wanaamini viongozi wao ni malaika, wengi wanadhani mimi ni mpotoshaji simply kwa sababu niko nje ya box, wengi wenu mko ndani ya box la Chadema, mnbaendelea na safari mkifurahia, ni sisi tulio nje ya Chadema ndio tunaweza kuwaambie huku mnakopelekwa siko!.

Muswada hamkuupinga, halafu mnasusa jumla, sasa sheria imepitishwa bila maoni yenu, nimewashauri baada ya hapo, viongozi wenu wasiwadanganye eti kuna kitu wanaweza kufanya, nothing, nawashauri waipe tuu ushirikiano tume itakayoundwa kukusanya maoni. Kama watawashauri msuse, hili litakuwa kosa jingine!, two wrongs, don't make a right!

Kama na wewe Mwita Maranya, unadhani mimi ni CCM, kaitafute post yangu ya CCM Imechokwa!. Niliwaambia Chadema hamjajipanga, na mpaka sasa hamjajipanga, kama mnadhani 2015 ni mbali, teuendeleeni na mwendo huu huu, tusije tuu kulia baada ya kutangazwa kwa matokeo!.
 
Mwita Maranya, ubishani wetu mkubwa humu ni jee TL alifanya alichopaswa kufanya kwa mujibu wa kanuni?.
Hoja yangu nimewaambia alikosea, kanuni inayo sehemu ya kutoa pingamizi na kutoa sababu ambayo TL hakuitumia, na badala yake, akatoa hotuba yake kukamilisha process!.

Kama na wewe umo kwa ile ile ya viongozi wetu ni watakatifu, tangu mwanzo nimewaambia, kama mambo yenyewe ndio haya, msije humu kutulilia, 2015 sio mbali!

Pasco,
Sitaki kuamini kwamba umetumwa na mtu ama chama fulani, naamini kwamba hii ni hoja yako mwenyewe kwa mtazamo wako mwenyewe.


Je umefanikiwa kuisoma hotuba ya TL? NA UMEONA KWAMBA HAKUTOA HOJA KWA KANUNI HIYO UNAYOISEMA? Je ulitazama bunge siku hiyo? Je uliwaona wabunge wa chadema wakisimama kuunga hoja mkono? Je uliwasikia wabunge wakijaribu kuomba mwongozo wa spika lakini akakataa? Hebu nijibu hayo maswali ili twende pamoja.
 
.....Mhe. Tundu Lissu hakupaswa kuisoma ile hotuba yake ya kambi ya upinzani, alipaswa kwanza atoe pingamizi, na mano ya kuyasema kwenye pingamizi hilo yameainishwa, baada ya kutoa pingamizi, hatua ya kwanza, muswada ungesitishwa, baada ya hapo Lissu angetakiwa sasa kutoa sababu zake ambazo zingekuwa seconded na wabunge wengine wowote.
.

Pengine hapa nimeipata hoja yako kwamba which strategy ambayo TL alitakiwa kutumia! Well and good ukitaka kwenda mlimani city na upo maeneo ya post kuna njia nyingi unaweza tumia waza tumia morogoro rd, bagamoyo rd sijui ndo alhasan mwinyi lakini utlimately utafika mlimani city. Whether TL angepaswa toa kwanza pingamizi (kama unavyo suggest) ama alivyofanya mwisho wa siku muswada ungepita tu. Ungepita tu kutokana na sababu milion nyingi zilizokwisha tolewa na Wakuu hapo awali. So ultimately mswada ungepita tu sema tu ile njiya wewe unayoitaka ipitiwe haikupitiwa lakini hata ingepitiwa isinge badilisha maudhui ama lengo.

Uamuzi wa kuendelea au kutoendelea ungetegemea Lissu ametoa hoja gani kwenye pingamizi hilo, naamini pamoja na uchache wa wabunge wa upinzani bungeni, wanapotoa hoja ya msingi kwa maslahi ya taifa, na hoja yenyewe ikawa na mashiko, wako wabunge makini wa CCM, kama kina Deo Filikunjombe and the like, lazima wangewaunga mkono upinzani, na kwa vile issue yenyewe ni ya kisheria, naamini wabunge wengi wa ukweli, wangewaunga mkono.

Hapana hapana hapana Pasco. Kwa jinsi hali ilivyokuwa bungeni na kwa jinsi CCM walivyokuwa wamejiandaa, na kwa jinsi vugu vugu kabla ya bunge kuanza (including jukwaa la katiba), na kwajinsi tayari walishaumbuka mara ya kwanza, na kwa jinsi kadhalika kadhali kadhalika....hata kama TL angekuwa na hoja gani iliyosimama vipi...there is no way CCM wangeunga nkono hoja ya upinzani. Hapa Pasco hapana, kama uliangalia mchakato mzima hapa hapana. Kama utaweza ona hapa ni hapana angalia JK alipoongea na wazee nini alikiongea uone kama kulikuwa na hiyo possibility. Naona tukubali tu kwamba what Kambi ya upinzani did (na hapa naomba tujuae ni kambi ya upinzani na sio TL ama CDM pekee) was the best they could do na nadhani watanzania tumewaelewa sana.
 
Back
Top Bottom