Katiba inakupa uhuru wa kukosoa/kutoa maoni haikupi uhuru wa kutoa lugha za kuudhi na kuchonganisha

Katiba inakupa uhuru wa kukosoa/kutoa maoni haikupi uhuru wa kutoa lugha za kuudhi na kuchonganisha

Wewe kada ngoja nikuulize swali dogo tu kuwa unasema Lissu kuita kauli ya mzee Mwinyi kutaka kipindi cha Rais wetu Magufuli badala ya kuwa cha miaka 10 badala yake awe Life President wetu kuwa ni mawazo ya kijinga unayaita hayo ni matusi na ndiyo yaliyomfanya hadi sasa aendelee kusota rumande kule Keko hadi Leo....

Hivi kama ndiyo hivyo, ni kwanini Mkapa hadi leo bado yuko uraiani anatanua hajakamatwa na Polisi wakati majuzi kule Chato alituita watanzania wote wapumbavu na malofa?

Hivi kati ya mtu aliyeita matamshi ya mzee Mwinyi ni ya kijinga na yule aliyesema watanzania wote ni wapumbavu na malofa, hivi kati ya hayo wawili ni nani hasa aliyetukana?

Naomba unijibu bila kutumbukiza ukada wako....
Kila mtanzania ana uhuru wa kutoa Mawazo.Rais mstaafu Mwinyi alitoa mawazo kama mtanzania mwingine.Rais Mkapa aliwaita wapumbavu wale wasiojua kuwa Tanzania ilisha kombolewa toka mikononi mwa wakoloni.Angalia kamusi ya uone mtu ambae haui kitu na hataki kuelimishwa anaitwa nani?
 
Ivi maana ya kutoa mawazo yako nini maana yake?je usifie tuu hauluhusiwi kukosoa?unajua maana ya uhuru wa mawazo?uhuru wamawazo upo pande mbili kusifia au kukosoa.je katba hairuhusu kukosoa?na je unatambua mtu yeyote akikosoa huonekana anakupinga nakuhisi unatukanwa?hayo nimawazo yake binafsi serikali au mkuu kama ime muuzi alipaswa amjibu tundulisi kipointi sio kumkamata.niishie hapo maana jiwe kamwe haliwez kuwa nazi.tuhangaikeni nahii nchi mpaka vitukuu vyetu ndo vitalikomboa hili taifa.
Kasome kiswahili kwanza...Hauluhusiwi=Hauruhusiwi.
 
N
Kwa mantiki yake hata raisi alivyosema atachomoa mwingine mwenye akili na sio wale VILAZA,,,nayo ni lugha ya kuuzi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Rafiki unaonekana kazi ya kufikiri umemuachia Lisu to an extent kwamba kila anachoongea unapigia makofi,,,Rekebisha kiswahili chako kwanza ndio urudi hapa ''lugha ya kuuzi=lugha ya kuudhi''
 
Lisu kapelekwa chuo kama alivyopelekwa Lema ili awe ana "THINK WIDELY BEFORE SHOUT"
Akitoka Segerea atakuwa ni Great thinker"
 
Lisu kapelekwa chuo kama alivyopelekwa Lema ili awe ana "THINK WIDELY BEFORE SHOUT"
Akitoka Segerea atakuwa ni Great thinker"
Sana tu, waambie akitoka atakuwa kanyooka.Yule muota ndoto haoti tena siku hizi
 
nitaendelea kuchomoa wenye akili, vilaza nawaacha huko huko.....
Naona hii ina lugha ya kufurahisha
 
Na kuwaita watu vilaza siyo lugha ya kuudhi? Au kusema kale "kabunge ka chadema" nayo imekaaje?
 
Nimemsikia mwanasheria wa Lisu akiongea jana baada ya kesi ya Lisu kuahirishwa na yeye(Lisu) kurudishwa rumande.Napenda tu nimkumbushe huyu mama kuwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inampa mtanzania yeyote uhuru wa kutoa maoni na kukosoa.Lakini katiba hii haikupi uhuru wa kutoa maneno yenye kuudhi na kuchonganisha jamii.

Nikirejea kauli ya Lisu ambayo leo imemfikisha Rumande,alisikika akisema yafuatayo:

1. Alisema anawaomba wahisani wasimsaidie Rais kwa fedha,kwanza nimkosoe kitu kimoja wahisani hawamsaidii Rais wanawasaidia watanzania maskini.Hizo pesa za donors zikija hali Rais na familia yake ni kwa ajili ya watanzania wote wakiwemo na Iramba mashariki ambako ndiko jimboni kwake.

Sasa alipitisha karatasi akachukua maoni yetu wananchi kuwa hatutaki wahisani? Rais alichaguliwa na watanzani walio wengi, kwa kauli ile ya Lisu alitumwa na watanzania wa wapi? Maana ninajua watanzania walio wengi wanamuunga mkono Rais,Wanataka barabara,wanataka huduma za maji,Elimu na hospitali.

Hii ni kauli ya kuudhi.Mimi kama mtanzania nieudhika na kauli hii na nina imani wapo wengi kama mimi ambao pia wameudhiwa na hii kauli.Kutoa lugha ya kuudhi ni kosa kisheria

2. Bwana huyu pia alisikika akisema mawazo aliyotoa Rais Mwinyi ni ujinga? Hivi hili sio tusi? Unamuitaje mtu kuwa katoa mawazo ya kijinga kisa anatofautiana na wewe? Una uhakika gani kama hakuna mtanzania mwingine ambae angependa Rais Magufuli atawale miaka zaidi ya 10?

Unadhibitishaje hili bila kupata maoni ya wananchi? And then unapata authority wapi ya kuyaita mawazo ya Binadamu mwenzio ni ya kijinga? Ok fine let me agree with you kuwa ni ya kijinga and then Yenye akili/hekima ni yapi? na una uhakika upi kuwa watanzania walio wengi wana kuunga mkono kwa hayo yako unayo dhani ndio yana hekima? ,,,,,

Hapa napo kuna kosa la kujibia, Huyu bwana aliongea lugha ya kuudhi, kaniudhi mimi na Mtanzania mwenzangu ambao tuna mawazo kama ya mzee Mwinyi kwa kutuita tuna mawazo ya kijinga ,,,hili ni tusi pia.Huwezi kuniita kuwa nina mawazo ya kijinga wakati hakuna reference point inayonipa mawazo sahihi.

Ungeweza kuniita mjinga endapo ningeshindwa kujibu 1+1=2,,Hapo sawa coz kila mtu at some point anaweza kuwa mjinga wa jambo fulani.Lakini kwa hili la kutoa maoni and then UNAYAITA YA KIJINGA NI TUSI MUBASHARA.

Kama ni katiba, katiba sio msahafu kama wananchi wakitaka katiba ibadilishwe ili Rais aendelee kutawala miaka dahari na dahari hawawi wajinga kwa kufanya hivyo bali ni hekima coz hekima ndio inawaongoza kuamua hivyo kwa kuona potential alizo nazo Rais in comparison na other presidential candidates.

3. Halafu Bwana huyu alisikika akisema kuwa Rais kafanya ukabila katika teuzi zake,,,Alitoa tuhuma ambazo sio za kweli.Alitaja viongozi wachache ambao Rais aliwataeua and by coincidence wakawa wanatokea kanda ya ziwa.Lakini kuna teuzi nyingi tu Rais kafanya ambazo hazitoki kanda ya ziwa.

Naweza mtajia Teuzi kadhaa hapa: Waziri mkuu,Mh Mwigulu,Mh Kabudi, Mh Mbarawa,Mh Ummy,Mh Kigwangala etc ,....Actually wewe pia unaweza nisaidia kumalizia hii list na mwishoni utagundua kuwa huyu Bwana (Lisu) hakuwa na lengo jingine zaidi ya kuleta chuki za kikanda na kikabila.

Hili nalo ni kosa la kujibu.

Help us spread patriotism by your like and share.
Visit us at:Dr Magufuli For Better Tanzania

1. Tundu lisu alioposema wahisani wasusie, kwa mwenye akili fupi hawezi kuona usahihi wa Lisu.

Haiwezekani tuendelee kubebeshwa mizigo ya madeni ambayo tutalipa sisi walipa kodi, au kuhesabiwa tumepokea misaada ambayo matumizi yake hayafanyiki kwa mujibu wa vipaumbele na kanuni za taifa.

Nakupa mifano hii hapa chini.
a) Ninaomba useme hapa, ni lini bunge lilipitisha badgeti ya kujenga uwanja wa ndege wa kimataifa chato?
b) Lini bunge lilipitisha budget ya kununua ndege zinazonunuliwa kwa cash huku watu wakifa hosptailni kwa kukosa oxygen?
c) Ni wataalamu gani walifanya maamuzi ya kuweka vipaumbele vya kiuchumi na kjamii katika hayo masuala?
d) Wewe unaona ni halali Tanzania izidi kuingia katika madeni na matumizi ya raslimali yasiyokuwa na tija lakini sisi na watoto wetu waendelee kubeba zigo la kodi kulipa hayo madeni?
Nimtu mwenye ufahamu tu ndiye anaweze kuona upeo wa Lisu.

2. Ujinga ni kukosa ufahamu, maarifa ama taarifa sahihi. No one is informed in everything. Mwinyi aliposema alionyesha kukosa ufahamu.

Mtu mjinga anaondolewa ujinga kupewa taarifa sahihi na si kwa kutokuambiwa kwamba hajui.

Huwezi kulazimisha watu wote wasikie mtu anafurunda halafu eti waseme hayo ndiyo maarifa haswa na kupiga makofi. Unaweze kupongeza ujinga ukiwa mjinga na wewe ama mnafiki. Lakini waache wenye uelewa na wasio wanafiki wamsahihishe ili aondokane na ujinga. Tatizo liko kwapi?

a) Tunaposema adui wa Tanzania ni umaskini, maradhi, rushwa na ujinga, huwa tunawatukana Watanzania? Naomba uwe serious .

b) Lisu amesema Mwniy amenena ujinga. Nani mlalamikaji katika hilo shauri la mwingi kuambiwa kanena ujinga?

Wasaidie wasiotaka kuambiwa wamenena ujinga wasinene ujinga.

Ni yupi anayetahili kukamatwa kwa uahrifu wa maneno kati ya mtu anayesema "MTU ANAYETETEA UAHRIFU NI MJINGA", na ule anayesema " WATU WANAOTETEA SHERIA, HAKI NA UHURU WA BINADAMU, DEMOKSRASIA , RASLIMALI NA MAENDELEO YA TAIFA NI MALOFA NA MPAUMBAVU"????

3. Kwa hiyo wewe unataka watu wawe na uhuru wa kukosoa kikatiba lakini hutaki raisi akosolewe?

Anapoambiwa aangalie tribalism na nepotism zinaligawa taifa anakuwa anatukanwa?

Nyerere alipoambiwa anapendelea watu wa Kazkazini aliwatukana na kuwakamata walalamikaji na kuwatia ndani?

Unapashwa kuelewa kwamba "image analysis", ni strength kwa kila kiongozi makini?

Ukituhumiwa, angalia hilo eneo na ama alitolee ufafanuzi ama arekebishe. Kuwatia watu pingu kwa kuwa wamekukosoa tena kwa nji aza amani ni dalili ya tatizo kubwa kuliko lililoko mezani kwa saas.

Kushabikia suppression za feelings za watu na kuendesha mambo kwa ubabe mkitegemea bunduki, zinaweza kuleta machafuko makubwa sana hapa nchini.

MATUMIZI YA BUNDUKI HAJAWAHI KUJENGA MTANGAMANO WA KIJAMII NA WALA HAYAJAWAHI KUWA SIASA SAFI WALA UONGOZI BORA.
 
Waloitwa itwa wapumbavu ni wale ambao hawajui kuwa Tanzania ilisha kombolewa toka kwa wakoloni,,,,soma kamusi ya kiswahili uone mtu ambae hajui kitu na hataki kuelimishwa anaitwaje?
Wapumbavu ni nyinyi mliovalishwa miwani ya mbao na ccm

In God we trust
 
Kila mtanzania ana uhuru wa kutoa Mawazo.Rais mstaafu Mwinyi alitoa mawazo kama mtanzania mwingine.Rais Mkapa aliwaita wapumbavu wale wasiojua kuwa Tanzania ilisha kombolewa toka mikononi mwa wakoloni.Angalia kamusi ya uone mtu ambae haui kitu na hataki kuelimishwa anaitwa nani?
Kama mnalijua hilo kwanini mnawakamata wapinzani kwa kutoa mawazo yao?

In God we trust
 
Nimemsikia mwanasheria wa Lisu akiongea jana baada ya kesi ya Lisu kuahirishwa na yeye(Lisu) kurudishwa rumande.Napenda tu nimkumbushe huyu mama kuwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inampa mtanzania yeyote uhuru wa kutoa maoni na kukosoa.Lakini katiba hii haikupi uhuru wa kutoa maneno yenye kuudhi na kuchonganisha jamii.

Nikirejea kauli ya Lisu ambayo leo imemfikisha Rumande,alisikika akisema yafuatayo:

1. Alisema anawaomba wahisani wasimsaidie Rais kwa fedha,kwanza nimkosoe kitu kimoja wahisani hawamsaidii Rais wanawasaidia watanzania maskini.Hizo pesa za donors zikija hali Rais na familia yake ni kwa ajili ya watanzania wote wakiwemo na Iramba mashariki ambako ndiko jimboni kwake.

Sasa alipitisha karatasi akachukua maoni yetu wananchi kuwa hatutaki wahisani? Rais alichaguliwa na watanzani walio wengi, kwa kauli ile ya Lisu alitumwa na watanzania wa wapi? Maana ninajua watanzania walio wengi wanamuunga mkono Rais,Wanataka barabara,wanataka huduma za maji,Elimu na hospitali.

Hii ni kauli ya kuudhi.Mimi kama mtanzania nieudhika na kauli hii na nina imani wapo wengi kama mimi ambao pia wameudhiwa na hii kauli.Kutoa lugha ya kuudhi ni kosa kisheria

2. Bwana huyu pia alisikika akisema mawazo aliyotoa Rais Mwinyi ni ujinga? Hivi hili sio tusi? Unamuitaje mtu kuwa katoa mawazo ya kijinga kisa anatofautiana na wewe? Una uhakika gani kama hakuna mtanzania mwingine ambae angependa Rais Magufuli atawale miaka zaidi ya 10?

Unadhibitishaje hili bila kupata maoni ya wananchi? And then unapata authority wapi ya kuyaita mawazo ya Binadamu mwenzio ni ya kijinga? Ok fine let me agree with you kuwa ni ya kijinga and then Yenye akili/hekima ni yapi? na una uhakika upi kuwa watanzania walio wengi wana kuunga mkono kwa hayo yako unayo dhani ndio yana hekima? ,,,,,

Hapa napo kuna kosa la kujibia, Huyu bwana aliongea lugha ya kuudhi, kaniudhi mimi na Mtanzania mwenzangu ambao tuna mawazo kama ya mzee Mwinyi kwa kutuita tuna mawazo ya kijinga ,,,hili ni tusi pia.Huwezi kuniita kuwa nina mawazo ya kijinga wakati hakuna reference point inayonipa mawazo sahihi.

Ungeweza kuniita mjinga endapo ningeshindwa kujibu 1+1=2,,Hapo sawa coz kila mtu at some point anaweza kuwa mjinga wa jambo fulani.Lakini kwa hili la kutoa maoni and then UNAYAITA YA KIJINGA NI TUSI MUBASHARA.

Kama ni katiba, katiba sio msahafu kama wananchi wakitaka katiba ibadilishwe ili Rais aendelee kutawala miaka dahari na dahari hawawi wajinga kwa kufanya hivyo bali ni hekima coz hekima ndio inawaongoza kuamua hivyo kwa kuona potential alizo nazo Rais in comparison na other presidential candidates.

3. Halafu Bwana huyu alisikika akisema kuwa Rais kafanya ukabila katika teuzi zake,,,Alitoa tuhuma ambazo sio za kweli.Alitaja viongozi wachache ambao Rais aliwataeua and by coincidence wakawa wanatokea kanda ya ziwa.Lakini kuna teuzi nyingi tu Rais kafanya ambazo hazitoki kanda ya ziwa.

Naweza mtajia Teuzi kadhaa hapa: Waziri mkuu,Mh Mwigulu,Mh Kabudi, Mh Mbarawa,Mh Ummy,Mh Kigwangala etc ,....Actually wewe pia unaweza nisaidia kumalizia hii list na mwishoni utagundua kuwa huyu Bwana (Lisu) hakuwa na lengo jingine zaidi ya kuleta chuki za kikanda na kikabila.

Hili nalo ni kosa la kujibu.

Help us spread patriotism by your like and share.
Visit us at:Dr Magufuli For Better Tanzania
Ni sawa kabisa ndio maana misamiati ifuatayo si lugha za kuudhi "MALOFA WAPUMBAVU... VILAZA... MATUMBILI... WAKALALIE NA WAKE ZAO... NK."
Au Katiba inaangalia upande mmoja TUVUMILIANE TU MAANA WATANZANIA HATUPIGANI KWA MAKONDE BALI MANENO!!
 
N

Rafiki unaonekana kazi ya kufikiri umemuachia Lisu to an extent kwamba kila anachoongea unapigia makofi,,,Rekebisha kiswahili chako kwanza ndio urudi hapa ''lugha ya kuuzi=lugha ya kuudhi''
Umesha laaniwa

In God we trust
 
Back
Top Bottom