Katiba mbovu, sheria mbovu, mikataba mibovu. Leo tumetozwa zaidi ya Tsh. Bilioni 260. Kufanywa kichwa cha Mwendawazimu hadi lini?

Hapo kwenye Mikataba na hizo firms za nje utapigwa tena tu, mimi nafikiri hebu tukae chini kama mataifa tuone wapi tulipo kosea, tuunde katiba mpya.
 
Hapo kwenye Mikataba na hizo firms za nje utapigwa tena tu, mimi nafikiri hebu tukae chini kama mataifa tuone wapi tulipo kosea, tuunde katiba mpya.
Hata hiyo katiba mpya watainajisi tu

Hata sasa tuna Katiba ila inasiginwa na kukanyagwa na wote wameichezea sana

Majizi hayataisha mpaka wakifungwa 100 maisha bila kujali nani wala nani maadam katulisha hasara au kaiba au kafilisi mradi weka ndani

Ila kuna tatizo moja, nani wa kumfunga mwenzie wakati wote wwnakula meza moja?
 
Hapa tunazidi kucheka na nyani! Na tutavuna mabua mengi sana. Hivi ukifungua kampuni ukamuajiri manager na akawa anakusababishia hasara Kila mwezi huoni faida zaidi ni madeni,utamuacha akae hadi ufilisike!? Tuamkeni Toka usingizini watanzania,nchi inaisha na itabaki makapi.
 
Wamejiwekea kinga Ili wasishtakiwe ndio maana wanatuletea upumbav walikuwa kabisa hatuna cha kuwafanya na wao wakiendelea kijinufaisha na familia zao. Ujinga kabisa huu!
 
Mmeshauriwa muunde kampuni ndiyo ziwe zinaingia mikataba na hayo makampuni kwa niaba ya serikali.

Sijui kisheria hii imekaaje ikitokea mtifuano,naona wenyewe wameshupaza shingo.
 
Katiba mbovu! Sheria mbovu! Mikataba mibovu!

Ongezea na "Wanasheria wabovu!"
 
Mimi kinachonishangaza ni hii ya kuona jinsi mikataba inavyoligharimu taifa kwa kulipa fidia kwa watu ambao pengine uwekezaji waliofanya haulingani,lakini Bado viongozi wetu wenye dhamana wanaingia tena mikataba kama hiyohiyo.Wako tayari kuumiza raia wanaotoa maoni tofauti au kupinga mikataba hiyo ili mradi tu mikataba iendelee.Mfano ni huu wa Dp world.Kwamba serikali haioni hayati ilipo mbele?
 
Tattizo kubwa ni viongozi wakurupukaji, kama yule Raisi wa malaika kama sio malaria.
 
Mbombo ipo, middle class huyu wa kitanzania loooo, mkuu huoni athari zozote real?inakatisha tamaa nchi hii ,na wanaofikiri hivi ni wengi tu, ngoja nisogee kwenye vitindi vya ulanzi, nikapige mbeta zangu
 
We Upendo wewe..!!!
 
Masikini TANGANYIKA CCM inawatia UMASIKINI WA MILELE
 
Ilani ya CCM ndio iliyoshinda, kwani 2020 kulikuwa na uchaguzi au maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…