Katiba mpya tunaitaka, lakini sio kuliko maji, chakula na afya

Katiba mpya tunaitaka, lakini sio kuliko maji, chakula na afya

Wewe unadhani ni demokrasia gani ya kukufaa: ya kukupa kila kitu na ya kusifia tu, ukisema jambo fulani siyo zuri linaweza kufanyika kwa namna bora zaidi unakuwa umekosea? Hiyo ndiyo demokrasia unayoitaka? Hata hiyo unayoitaka ulizaliwa nayo au nayo utakuwa umeletewa na hao wanaoitekeleza? Elimu umeletewa, mbona huipingi? Afya umeletewa, mbona huipingi? Aina ya ujenzi wa miundombinu ya kisasa, usafiri wa magari, ndege etc na hata uvaaji wa nguo, viatu, matumizi ya TV, kompyuta, simu etc - vyote hivi umeletewa...Kwa hiyo, unasemaje, tufanyeje? Tuvirudishe huko vilikotoka?
Tujitahidi Subira yavuta Heri 🙏🙏
 
Vyama vya upinzani UKAWA ndio waliokwamisha upatikanaji wa Katiba kwa kulazimisha serikali 3 badala ya 1 au 2. Hii Ina maana kuwa mchAkato utakwamia palepale tena pa muundo wa serikali kama watu watakuwa na misimamo Yao juu ya muundo wa serikali.
Ngoja Tusubiri tuone !
 
😍
Ni kweli kabisa hatuwezi kurudi tulipotoka ni lazima twende mbele!
Swali fikirishi ni kwamba je wakubwa wetu wana utashi wa dhati wa kutupeleka mbele kiuchumi na kisiasa ??!
Bara la Africa lina rasilmali nyingi sana lakini ndio Bara masikini kuliko mabara yote Duniani !

Bara la Afrika ndiko ambako huwa tunawaza na kupanga mikakati ya kushinda uchaguzi by any means !!
Je bado unaamini hii demokrasia tuliyoletewa inatufaa na sisi huku Africa ???!
Je ni wapi katika Afrika ulisikia the Incumbent head of state ameshindwa kwenye uchaguzi mkuu na akakubali kuachia madaraka ??!
Ndipo huwa najiuliza je hii demokrasia tuliyonayo inaweza kweli kutuvusha ??!
Bara la Afrika ni masikini lote kabisa bila kubagua kanda. Wenye nafuu ni waarabu tu walioko Afrika kimakosa. Hii ni kusema kuwa shida yetu iko nje Katiba zetu. Wizi wa viongozi wetu, demokrasia ya kulazimishwa na magharibi, mifumo ya dunia ya uchumizi kandamizi ndio sababu halisi ya hiki kinachotokea Afrika. Mtu anadai katiba mpya lakini kipaumbele chake ni tume huru ya uchaguzi sawa na kima wapya kwenye msitu uleule.
 
Bara la Afrika ni masikini lote kabisa bila kubagua kanda. Wenye nafuu ni waarabu tu walioko Afrika kimakosa. Hii ni kusema kuwa shida yetu iko nje Katiba zetu. Wizi wa viongozi wetu, demokrasia ya kulazimishwa na magharibi, mifumo ya dunia ya uchumizi kandamizi ndio sababu halisi ya hiki kinachotokea Afrika. Mtu anadai katiba mpya lakini kipaumbele chake ni tume huru ya uchaguzi sawa na kima wapya kwenye msitu uleule.
Yaani Nimecheka sana 😅😅😅 🙏
 
Yaani Nimecheka sana 😅😅😅 🙏
Wanaouongoza upinzani lazima wajue kuwa hizi shule za kata zilizotapakaa nchi nzima sio za kubeza, watanzania wengi sasa hivi angalau wanafika Form 4, hata kama wanaishia hapohapo lakini angalau kuna mwanga wanaupata kuhusu nchi yao. Wamekuwa wakiwachagua wagombea wa vyama vya upinzani lakini mwisho wake wanaishia kurudi tena CCM bila maelezo wala chama chao kuwaomba msamaha wapiga kura wao. Wamefanya hivyo tangu enzi za akina Lamwai, Lyatonga, Marando, Lipumba, Dr, Slaa, Sumaye, Lowassa, Mgwila, Kafulila na wengine wengi bila vyama kutoa maelezo wala kuomba samahani kwa wapiga kura waliopiga kura, kuhesabu na kulinda kura zao. Huwezi kuwadanganya watu wote siku zote kwa wakati mmoja. Sasa hivi ukiwasikiliza kwa makini hoja zao ni zilezile tena za kutaka kwenda Ikulu kwa kutumia hadaa ya Bandari na Katiba Mpya. Hawaelezi kama wakishinda wataenda kufanya nini Ikulu tofauti na CCM ya miaka 60 madarakani. Wanachotaka ni Ikulu, ubunge, udiwani baaasi mambo mengi tutayajua hukohuko wakifika Ikulu.

Wananchi wanazidi kuelimika kila siku na kila mwaka. Ni kwa maslahi yao tu.
 
Tuzungumzie katiba bora badala ya mpya tu.
Kweli kabisa. Wako watu wanaotaka katiba inayoweza TU kuwafikisha Ikulu na inayovunja muungano baaasi, na hapo ndipo tunapokwimia na patakapotukwamisha kupata Katiba Bora.
 
Kuna inch AFRICA HAINA SHIDA ZA MAJI NA UMEME NA AFYA HAKUNA ZOTE SHIDA ZINAFANANA KWA SABABU VIONGOZ WAKE WOTE WANFANAN AKILI ZAO
 
Kwahii inchi swala la katiba ni kizungumkuti...sana sizan kama litakuja kufanyia kazi...maana 75% is for Ruling Party only...,,,Ila serikali wanatakiwa iliweke kama somo mashuleni wanafunzi wajifunze ili unapokuja kukosoa uwe na evidence za kutosha...tatizo watu tunaongea sana bila fact...
 
Kwahii inchi swala la katiba ni kizungumkuti...sana sizan kama litakuja kufanyia kazi...maana 75% is for Ruling Party only...,,,Ila serikali wanatakiwa iliweke kama somo mashuleni wanafunzi wajifunze ili unapokuja kukosoa uwe na evidence za kutosha...tatizo watu tunaongea sana bila fact...
Hata kama katiba mpya itanza kuandikwa itakwamia pale pale ilikokwamia wakati ule, muundo wa muungano kama Kuna watakaong'ng'ania serikali 3 au muungano wa mkataba.
 
Back
Top Bottom