Katiba Mpya: Ukweli Usiosemeka

Katiba Mpya: Ukweli Usiosemeka

Mazingira yanaoizunguka katiba mpya ni muhimu yakajulikana yote wazi wazi.

Inafahamika kuwa CCM walio wanufaika wa katiba iliyopo, hawana sababu yoyote ya kujitia kitanzini kwa kuridhia ujio wa katiba mpya kirahisi.

Kutokupatikana kwa katiba mpya kutaifanya CCM kuwa imefanikiwa katika malengo yake. CCM inategemea itafanikiwa malengo yake kwa kuamini:

1. Wadai katiba ni wastaarabu wasiotaka kutumia nguvu au makabiliano yoyote ya kuhusisha nguvu.

2. Wadai katiba wako tayari kususia chaguzi zote bila ya kuwa na tume huru au katiba mpya.

Sababu mbili hizi zinapendwa sana na CCM kwani:

1. Kwa kukomaa tu, wadai katiba kistaarabu watapisha makabiliano. Hivyo CCM wataendelea kwa raha zao.

2. Kwa kukomaa tu, wapinzani watasusa chaguzi na CCM wataendelea kwa raha zao.

Inatakikana jitihada kubwa ya makusudi ya kuukata mnyororo huu wa matukio.
Katiba mpya haikwepeki ila lazima kuwepo kifungu kuwa yeyote atakayeshughulika na katiba asigombee nafasi yeyote ya uongozi kwa miaka 20 ijayo. Hapo tutapata katiba iliyo bora. Ili kusiwepo na mgongano wa kimaslahi
 
Sasa mwenyekiti wa kudumu aanze kuibadili ya chama then aachie madarka kwa wengine hapa lazima tuwaunge mkono kurekebisha hii ya nchi.
Watu hapa mlitaka kumuongezea Maghufuli mpaka Mungu akaona isiwe noma. Mbowe yuko muhula wa tatu na sasa keishasema hagombei tena. Tena Bora Mbowe kuliko walioutaka uenyekiti CDM na kuishia kuunga juhudi mkono e.g . Mwambe , Lowassa & co. Bora Mbowe pamoja na kufirisiwa na Jiwe ,lakini ana msimamo wa kusonga mbele.
 
Kwa nini watu wanadai KATIBA mpya? Majibu mengi: Kwa ajili ya uchaguzi na wanaongeza na sababu hii bila KATIBA mpya hatushiriki Uchaguzi. Hapo naona vyama vya upinzani ni WASAKA TONGE. Wangedai katiba mpya kuboresha kilimo cha nchi badala yake katiba mpya kwa ajili ya UCHAGUZI tuu hapo kuna shida. Katiba mpya kwa ajili ya madaraka BIG NO. KATIBA yetu ni nzuri na kazi iendelee.

Sababu za kudai katiba ni mbalimbali kwa kila mwananchi na ndiyo maana makundi yote hushirikishwa.

Hapa chini ni baadhi ya mapungufu ya wazi ya katiba iliyopo, ambayo yanaweka umuhimu na dharura ya katiba mpya hasa kwa mtanzania yule wa kawaida:

1. Katiba iliyopo haiwawajibishi baadhi ya watendaji wakuu kwa kuikiuka, na hii ni kwa mujibu wa katiba yenyewe.
2. kwa katiba iliyopo pana watu hata kama wakiiba, wakipora, wakiuwa, wakidhulumu nk hiyo ni halali kwa mujibu wa katiba yenyewe.
3. katiba iliyopo inawapa baadhi ya watu mamlaka ya kujifanyia lolote bila kuhojiwa au hata kuwajibishwa tu.
4. Katiba iliyopo haitoi haki sawa kwa watu wote ndani ya nchi.
5. Kuna mianya mingi katika katiba hii ambayo inaweza kuifanya mihimili mingine hata kupoteza uhuru wake wa kiutendaji kwa mujibu wa katiba yenyewe.
6. Kuna utitiri wa nafasi za uongozi wasio na tija wala ridhaa ya wananchi ambao pia ni mzigo mkubwa kwa mlipa kodi.
7. Kuna utitiri wa vigogo wenye mapato yasiyoakisi tija, wala kuwa na ridhaa ya wananchi na wasiolipa kodi wanaopata uhalali kwenye katiba hii.
8. Kwa katiba hii polisi wanaweza mshikilia mtu kwa kumbambikizia kesi hata kwa miaka kadhaa. Mhanga akaja kuachiliwa bila ya wahusika kuwajibika kwa lolote. Hili likihalalishwa na katiba hii.
9. Nk.Nk.

Yako mengi, kwenye mazingira haya hudhani kuwa mwananchi wa kawaida anaihitaji zaidi katiba mpya kuliko hata hao wanasiasa?

Kwamba, hudhani kuwa anayedhani hahitaji katiba mpya ni kwa sababu tu ya ujinga wake au kukosa elimu au kuwa na uelewa mdogo tu?

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Watu hapa mlitaka kumuongezea Maghufuli mpaka Mungu akaona isiwe noma. Mbowe yuko muhula wa tatu na sasa keishasema hagombei tena. Tena Bora Mbowe kuliko walioutaka uenyekiti CDM na kuishia kuunga juhudi mkono e.g . Mwambe , Lowassa & co. Bora Mbowe pamoja na kufirisiwa na Jiwe ,lakini ana msimamo wa kusonga mbele.
Lowasa si matokeo ya gear ya angani.. umesahau zile harakati za kuzungusha mikono.
 
Kwa incentive ipi?
Bila machafuko sioni katiba mpya kupatikana. Uzoefu unaonyesha machafuko hupelekea kupatikana katiba iliyonyooka wangalau kwa 70%+. Kitendo cha kuingia kwenye katiba mpya na ccm kukiwa na amani, ni kuwaruhusu ccm kuteka mchakato wasiouamini.
 
Sababu za kudai katiba ni mbalimbali kwa kila mwananchi na ndiyo maana makundi yote hushirikishwa.

Hapa chini ni baadhi ya mapungufu ya wazi ya katiba iliyopo, ambayo yanaweka umuhimu na dharura ya katiba mpya hasa kwa mtanzania yule wa kawaida:

1. Katiba iliyopo haiwawajibishi baadhi ya watendaji wakuu kwa kuikiuka, na hii ni kwa mujibu wa katiba yenyewe.
2. kwa katiba iliyopo pana watu hata kama wakiiba, wakipora, wakiuwa, wakidhulumu nk hiyo ni halali kwa mujibu wa katiba yenyewe.
3. katiba iliyopo inawapa baadhi ya watu mamlaka ya kujifanyia lolote bila kuhojiwa au hata kuwajibishwa tu.
4. Katiba iliyopo haitoi haki sawa kwa watu wote ndani ya nchi.
5. Kuna mianya mingi katika katiba hii ambayo inaweza kuifanya mihimili mingine hata kupoteza uhuru wake wa kiutendaji kwa mujibu wa katiba yenyewe.
6. Kuna utitiri wa nafasi za uongozi wasio na tija wala ridhaa ya wananchi ambao pia ni mzigo mkubwa kwa mlipa kodi.
7. Kuna utitiri wa vigogo wenye mapato yasiyoakisi tija, wala kuwa na ridhaa ya wananchi na wasiolipa kodi wanaopata uhalali kwenye katiba hii.
8. Kwa katiba hii polisi wanaweza mshikilia mtu kwa kumbambikizia kesi hata kwa miaka kadhaa. Mhanga akaja kuachiliwa bila ya wahusika kuwajibika kwa lolote. Hili likihalalishwa na katiba hii.
9. Nk.Nk.

Yako mengi, kwenye mazingira haya hudhani kuwa mwananchi wa kawaida anaihitaji zaidi katiba mpya kuliko hata hao wanasiasa?

Kwamba, hudhani kuwa anayedhani hahitaji katiba mpya ni kwa sababu tu ya ujinga wake au kukosa elimu au kuwa na uelewa mdogo tu?

Au nasema uongo ndugu zangu?
Mwenyekiti wa kudumu aachie ngazi apishe wengine waongoze chama.
 
Sasa kama katiba ya wananchi sasa kwanini mwenyekiti wa kudumu anatuongelea utafikiri tulikaa na akakusanya maoni yetu?

Atuoneshe kwa vitendo aachie na wengine waongoze.

Maoni yetu wananchi yapo kwenye rasimu ya Warioba. Una lingine tukusaidie?
 
Sasa kama katiba ya wananchi sasa kwanini mwenyekiti wa kudumu anatuongelea utafikiri tulikaa na akakusanya maoni yetu?

Atuoneshe kwa vitendo aachie na wengine waongoze.

Kwenye wananchi wamo watanzania wote wenye vyama na wasio na vyama. Katiba inahusisha wote wenye vyama na wasio na vyama. Kila Mwananchi mwenye chama au asiye na chama anayo haki ya kudai katiba bora zaidi katika wakati wowote.

Kwani wewe ni nani unayekuja na masharti yoyote kwenye jitihada zozote za yeyote kudai katiba kwa mujibu wa sheria?
 
Kwenye wananchi wamo watanzania wote wenye vyama na wasio na vyama. Katiba inahusisha wote wenye vyama na wasio na vyama. Kila Mwananchi mwenye chama au asiye na chama anayo haki ya kudai katiba bora zaidi katika wakati wowote.

Kwani wewe ni nani unayekuja na masharti yoyote kwenye jitihada zozote za yeyote kudai katiba kwa mujibu wa sheria?
Mwenyekiti wa kudumu ajisahihishe kwanza
 
Kama Mwenyekiti wa kudumu hataki kuachia hatamu je ataheshimu katiba kwa kutoka madarakani endapo akiwa Rais wa nchi?

Chama kinachodai katiba kina kasoro za kikatiba katika chama chao.
Katiba yao inasemaje kuhusu uenyekiti mamii?
 
Back
Top Bottom