Madaraka au magari ya escort?
https://www.jamiiforums.com/threads/chadema-jifunzeni-kwenye-ziara-ya-makamu-wa-rais-kahama.2057817/
Mbona tuko wazi mno ndugu?
Hayo ni machukizo kwetu!
Kwa mtu ambae Hana uelewa mkubwa kama ww, lazima utake katiba mpya
Na ukiulizwa ww kama ww binafsi umeadhirika vipi na katiba ya sasa I'm sure hauna majibu
Wanasiasa ndio wanataka katiba mpya na sio Kwa maana ya kuwasaidia wanainchi hapana ni Kwa manufaa yao wenyewe
Sasa ww unafata mkumbo tu
Hamna lolote mnataka kufanya watu wajinga Tu, kwanza mnataka katiba mpya utambue serikali Pacha,
That's means lisu akiwa wa pili ndio awe makamu wa rais eeeh kuna nn hapo kama sio magari ya escort?
Haya mnataka tume iwe huru, eeeh tume ikiwa huru bei za Mchele zinashuka? Bei za mafuta zinashuka?
Au faida ya tume kuwa huru ni nn? Kama sio mambo ya madaraka
Open Ur eyes kijana
Unaelewa maana ya katiba au hata umuhimu wake ewe mwenye kujidhania (unilaratelly) kuwa na uelewa
mkubwa?
"Ama kweli nyani haoni kundule."
Hivi ni binadamu gani wapi hahitaji mustakabala bora zaidi baina yake na wengine maishani mwake?
Ama Kwa hakika ni mlamba asali, mfu au zezeta kweli kweli - mwenye kuamini kuwa mustakabala wa 1977 tulionao unajibu changamoto zote tulizo nazo leo, na tena kwa ufanisi mno.
lete fact, katiba ya mwaka 77 inakuadhiri nn ww personal?
Haya mbona yameongelewa sana ndugu au wewe ndiyo sasa kufika duniani kutokea anga za juu? Hivi unajua kuwa:
View attachment 2500002
Hayo ni nukuu ya 2021 post #28 ya uzi huu:
https://www.jamiiforums.com/threads/katiba-mpya-ni-muhimu-kwa-sekta-zote.1921681/
Angalia pia post #13 ya jun 2021
Tuwatambue wanaohaha kutusambaratisha kama Taifa
Kutofautiana kimawazo katika nchi ni jambo la afya. Haiwezekani sote tukawa na mtizamo mmoja. Hata watoto mapacha hutokea wakati wakatofautiana. Kwa bahati mbaya kuna zama zimepita kwa kutofautiana tu pana watu wamekufa, wamepotezwa, wamejeruhiwa, wamedhulumiwa, na mengi ya namna hiyo...www.jamiiforums.com
Karibu duniani mjomba
Hayo yote uliyosema hapo juu, yanakuadhiri vipi ww kama ww?
And second, kama katiba ya sasa inakataza watu kuiba na still wanaiba Je hiyo katiba mpya itazuia vipi?
Shida mnasahau kwamba hapa ni africa uwa mnaona kama hapa ni ulaya
Hakuna inchi Africa inafata katiba yake 100% hakuna na haitokuwepo
Hayo yote uliyoongea hapo juu hata zije katiba mpya 100000000 still hayo mambo yatakuwa hivyo hivyo
Kwamba:
1. Katiba iliyopo haiwawajibishi baadhi ya watendaji wakuu kwa kuikiuka, na hii ni kwa mujibu wa katiba yenyewe?
2. kwa katiba iliyopo pana watu hata kama wakiiba, wakipora, wakiuwa, wakidhulumu nk hiyo ni halali kwa mujibu wa katiba yenyewe?
3. katiba iliyopo inawapa baadhi ya watu mamlaka ya kujifanyia lolote bila kuhojiwa au hata kuwajibishwa tu?
4. Katiba iliyopo haitoi haki sawa kwa watu wote ndani ya nchi?
5. Kuna mianya mingi katika katiba hii ambayo inaweza kuifanya mihimili mingine hata kupoteza uhuru wake wa kiutendaji kwa mujibu wa katiba yenyewe?
6. Kuna utitiri wa nafasi za uongozi wasio na tija wala ridhaa ya wananchi ambao pia ni mzigo mkubwa kwa mlipa kodi?
7. Kuna rundo kubwa la vigogo wasio na tija na wasiolipa kodi wanaopata uhalali tokea katika katiba yenyewe?
8. Nk, nk.
Bado unadhani kuwa katiba iliyopo hainiathiri?
Lipi hapo juu ambalo halikuathiri wewe katika hali ya sasa? Kwani wewe ni Msoga boy?
"Wewe utakuwa mlamba asali au hujitambui kweli kweli?"
Pole ndugu.
Twende hiyo namba mbili! Kwa katiba ya sasa Nani anaruhusiwa kuua?
Jambo la kheri kuwa bila shaka #1 utakuwa umeielewa vyema.
#2. Wako wapi kina Ben, Azory, Lijenje, Mawazo au nini ililikuwa kiwapate kina Lissu?
Hukuwasikia watu wa kwenye viroba?
Kwani wasiojulikana hawajulikani?
Hatua gani zilichukuliwa dhidi yao au hata nani aliwajibishwa tu, kuwahusu wao?
Kwani kweli wewe huyajui haya?
Au tuseme ndiyo kwanza umewasili duniani kutokea kusikojulikana?
Uliiona #3 kwenye mafyongo ya katiba hii?Hao uliowataja wameuliwa na nani? Unamjua aliewaua au unahisia Tu?
Ukiambiwa Leo utoe ushahidi kuwa hawa watu wameuliwa na watu flan utaweza?
Niambie katiba mpya itazuia vipi watu kuwekwa kwenye viloba? Na niambie kifungu gani cha katiba ya sasa ambacho kinaruhusu?
Uliiona #3 kwenye mafyongo ya katiba hii?
"Katiba iliyopo inawapa baadhi ya watu mamlaka ya kujifanyia lolote bila kuhojiwa au hata kuwajibishwa tu?"
Huwajui majina yao waliojiwekea kinga batili hizo Kwa mujibu wa katiba?
Hujui kuwa kuna wenye kuwajibika moja kwa moja kwenye usalama wa raia?
Kwani kwenye kadhia hizo nani hata aliwajibishwa?
Wewe hukupata hata kusikia kwala ya mwisho nani walikuwa Lijenje au Ben?
Kwani mwenye macho haambiwi tazama? Ila tambua our lives matter. Tunataka katiba itakayotuweka sote sawa mbele ya sheria.
Zingatia pia #4.
Bado unaongea mambo ya kusadikika mambo ya vijiweni, hauna fact
Sasa kama hauna fact basi hata kutetea inchi ije na katiba mpya haina haja
Hayo madaraka Kwa watu yatakuwepo Tu, hata katiba mpya still itakuwa na watu wa kusimamia na wanaweza kuvurunda tu
Mpaka sasa Huna hoja
Ofcourse lazima wananchi waoneshe uhitajiAnasema kelele zipigwe sana, hizo ndizo zitawezesha kupatilana Katiba Mpya.
Naona hiyo ni njia nzuri, kwani mpaka sasa bado sijasikia lolote toka kwa Samia aliyetuahidi kuanzisha mchakato wa Katiba Mpya.
Inaonekana anatakiwa kuamshwa kwa kelele nyingi za Katiba Mpya.
Usiyekuwa na hoja ni wewe. Kwa taarifa yako dhidi mamlaka kuna kesi hii mahakamani:
https://www.jamiiforums.com/threads...du-lissu-azory-gwanda-na-ben-saanane.2056272/
Huna lolote mjomba. Wewe na ukae kwa kutulia tu.
Kwenye madai yetu haya ya haki, kwa hakika hatuhitaji mchango wowote kutoka kwa watu kama wewe.
Habari ndiyo hiyo.
Mahakamani ndio sehemu ya haki,
Sasa ww upande wako ukishindwa ndio unaona hakuna haki
Hao watu unasema wameuliwa but hata ww ujui Nani kawaua au wapo hai
Na ww sio mwanafamilia ya hao marehemu ni shabiki Tu so hakuna kitu unajua
Ndiyo ulipo msingi wa hoja #5 uwepo wa uhuru wa mihimili ya utawala ili ule uliojichimbia zaidi ukome kutoa maelekezo yake ya nini kifanyike mahakamani au bungeni.
Nani walikuwa na Ben na pia Lijenje mwisho, mara zote ndipo huwa pa kuanzia. Hao wanafahamika lakini kuwawajibisha ni kesi ya nyani kala mahindi kupeleka Kwa hakimu ngedere.
Nani anawajibika na usalama wa raia aliwajibika kujua au hata kuwajibishwa kama hajali.
La mwisho hili liwezekane vipi katikati ya ngome waliojiwekea wahusika pale #4?
Kwa hakika katiba mpya ni lazima ili kuachana na visingizio vyote uchwara kamq vyako hivi vyenye lengo la kukwepa uwajibikaji ili kuwapora watu haki zao.
Katiba mpya ni sasa!
Ushaenda police kuulizia hao watu? Ukaambiwa nn?
Ushaenda kwenye family ya hao watu? Ukajibiwa nn?
Unataarifa gani mpya ya uchunguzi wa kupotea hao watu?
Hatimaye sasa kesi Iko mahakama kuu Kwa ajili ya kumbukumbu sahihi.
Kwani wewe una taarifa gani kutoka polisi, angalau tu hata za kuwajibishwa mtu?
Au watu wale kwako au kwenu walikuwa sawa na kuku tu?
Ww unataka nani awajibishwe? Watu kupotea au kufa dunian kote hizo mambo zipo
Kwanini yy ndio unamuona maalumu Sana Jambo lake kushikiwa kidete?
Sasa kama kapotezwa na watu ambao hawajulikani unataka kumwajibisha Nani?