pilipili kichaa
JF-Expert Member
- Sep 3, 2013
- 18,406
- 14,643
sheria za kihuni sana hizi na kishetani!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kama bado uko hai ndugu yangu sheria zote zinatungwa kwa ajili ya kumkandamiza mtu wa kawaida kama hujui. Fisadi anaogopwa. Kwa Tanzania fisadi yuko salama kuliko wewe wa kawaida.Kama wewe nifisadi jiandae lakini Kama nimtu wa kawaida uwe na amani mkuu lengo la hii Sheria ni
kuiondoa SERIKALI ILIYO NDANI YA SERIKA
Kwa maoni yangu, hawa watu watajiwekea kinga nyingi sana. Ila pia ni funzo kwetu sisi wapiga kura wao kwamba hayo ndiyo matunda ya kazi tuliyoifanya kipindi cha uchaguzi. Kwa hiyo, kwa upande mwingine tufurahi kwamba hayo ndiyo matunda ya kura zetu. Shida inayokuja kwangu ni kwamba kama hao watu wanatenda haki, kinga zaidi ni ya nini? Au huwa hawatendi haki? Kama hawatendi haki wanastahili wachukuliwe hatua za kisheria. Kuongeza kinga "kwa makosa yanayoweza kutendeka wakati wa utekelezaji wa majukumu..." maana yake ni kuruhusu ukiukwaji wa sheria wakati wa utekelezaji wa sheria. Kama sheria zinafuatwa, hayo makosa yatatendekaje wakati wa utekelezaji wa majukumu? Kuweka kinga kwa maoni yangu kunaongeza mwanya wa kukiuka sheria wakati wa utekelezaji wa majukumu/sheria. Pili, kuongeza kiwango cha adhabu kulingana na uzito wa kosa ili kuendana na mazingira ya sasa hakuna maana yoyote. Kwani mazingira ya sasa ndiyo yanayohitaji kiwango kikubwa cha adhabu? Sheria ingesema law enforcers waongeze ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao. Ufanisi ndio unaotakiwa na wala siyo kinga wala kiwango cha adhabu. Lakini kuongeza kinga kuna maana kuweka mwanya wa kukiuka haki za watu wanaohisiwa kuwa wametenda kosa.Ibara ya 13 (1) imetanabaisha wazi kabisa kuwa kila mtu akifanya kosa anatakiwa ashitakiwe kwa mujibu wa sheria bila ubaguzi.
Leo hii CCM wanaenda kupitisha sheria ambayo itawapa kinga maofisa wa TISS wakifanya makosa . Hii ina maana gani?
View attachment 2640934
Pia soma: Muswada wa Mabadiliko ya Sheria ya Idara ya Usalama wa Taifa unaoifanya iwe chini ya Usimamizi wa Rais watua Bungeni