Katibu mkuu CWT agoma kurudi Temeke kufundisha

Katibu mkuu CWT agoma kurudi Temeke kufundisha

Akirudi ana kuta barua mezani ya uhamisho kwenda swekeni kama sio tukuyu Au huko nkasi basi mabamba mpakani na burundi 😂😂😂
Ni mabanda
 

CWT kuna hela za bure ambazo ni kama vile hazina mwenyewe, hazina kuhoji!...


Kila mwezi fungu linaingia mabilioni...

Ila alichokosea maganga... ni kudharau mamlaka ya uteuzi(Raisi)Akikuteua ukakataa.. ni dharau... unapaswa uchunguzwe. WHY umekataa!?

Atauona moto wa TAKUKURU!
Huyu jamaa atajutia uamuzi wake wa kukataa UTEUZI.

Pia alishindwa kusoma upepo hata kama alinusa harufu ya kutotendewa haki.

Nina imani alikuwa kashakusanya maokoto angerudi fast kwa mwajiri halafu akaendelee na kazi huku akipanga namna ya kusimika mipango ya kuendeleza maokoto yake.

Ona sasa yupo hatarini kufilisiwa na kukosa kazi kabisa
 
Mbona huyo Dinna waliyegoma naye kwenda kuapishwa yeye haadhibiwi? Hii ni double standard. Nchi ya kipuuzi sana hii inayopenda kulipiza kisasi ndio maana imelaaniwa kwa sababu za kishetani kama hizi.
Dinna aliapishwa na yupo ofisini kama DC kule Kigoma
 
Huyu jamaa atajutia uamuzi wake wa kukataa UTEUZI.

Pia alishindwa kusoma upepo hata kama alinusa harufu ya kutotendewa haki.

Nina imani alikuwa kashakusanya maokoto angerudi fast kwa mwajiri halafu akaendelee na kazi huku akipanga namna ya kusimika mipango ya kuendeleza maokoto yake.

Ona sasa yupo hatarini kufilisiwa na kukosa kazi kabisa
Some people are smart; inawezekana jamaa alishakusanya kimyakimya alichovuna huko CTW saa hii yupo zake Boso anaendeleza maisha yake kwa utulivuuu. Najaribu kuwaza tu
 
Halmashauri ya Manispaa ya Temeke imeanza mchakato wa kufungua shauri la nidhamu dhidi ya Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Japhet Maganga baada ya kutorejea katika kituo chake cha kazi tangu alipotakiwa kufanya hivyo Oktoba Mosi mwaka huu.

Maganga ambaye cheo chake ni Mwalimu Mwandamizi katika Manispaa ya Temeke, aliomba kibali cha kuazimwa kuitumikia CWT Agosti 2017 hadi Septemba 30, 2020, akaomba tena Juni 1, 2020 na kumalizika Septemba 30, 2023, na baadaye aliomba kibali hicho kwa mara ya tatu lakini Katibu Mkuu UTUMISHI hakuridhia maombi hayo na kumtaka kurejea kwenye kituo chake cha kazi cha awali.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke, Elihuruma Mabelya amesema Maganga ni mtumishi wa Temeke na alitakiwa kuripoti kazini kama alivyotakiwa katika tangazo la wito, lakini hadi sasa hajaripoti, hivyo kinachofanyika ni kuchukua hatua za kinidhamu dhidi yake.

"Yule ni mtumishi wa Serikali hapaswi kuigomea Serikali, sisi tunachojua yeye ni mtumishi wetu, kule aliko kibali kimeisha sio tena sehemu yake ya kazi, amesema.

Maganga alichaguliwa Desemba 2022 na Mkutano Mkuu wa CWT kuwa Katibu Mkuu akichukua nafasi ya Deus Seif
ambapo awali alikwa akitumikia nafasi ya Naibu Katibu Mkuu.

Mnamo Januari 25, mwaka huu, Maganga, Makamu wa Rais wa CWT, Dinna Mathaman na Rais wa CWT, Leah Ulaya waliteuliwa na Rais Samia Suluhu kuwa Wakuu wa Wilaya lakini Maganga na Mathaman hawakufika kuapa.
Hii inaonekana ni vita
Kwani yeye mwenyewe amesema ana shida na hiyo kazi?
 
Some people are smart; inawezekana jamaa alishakusanya kimyakimya alichovuna huko CTW saa hii yupo zake Boso anaendeleza maisha yake kwa utulivuuu. Najaribu kuwaza tu
Hata kama ni hivyo, amekosea.

Ilitakiwa arudi kwenye kituo chake cha kazi cha mwanzo then baadae angeweza kuacha kazi kwa taratibu zinazoeleweka na asingepata taabu ambayo anaenda kuipata sasa.

Ila humo CWT inaonekana kuna maokoto ya bwerere sana, sio kwa mtifuano huo
 
Aliyekuwa Rais wa CWT ndio nasikia alikubali/alihudhuria kuapishwa/uapisho
Yule anaitwa Leah Ulaya. Waliogoma ni Dinna na Maganga. Kwanini Dinna haguswi anakomaliwa Maganga tu? Ipo namna hapa sio bure. Serikali kuna mahali inajichanganya yenyewe kwenye maamuzi yake kwa sababu uovu wao umeshikwa pabaya.Kwanini serikali inaingiza siasa CWT kila mwaka kutaka kuingiza mamluki ili wachote pesa za walimu? Wamezoea kuchota.pesa kwenye mifuko ya hifadhi ya kamii na NHIF. Kule CWT wamekosa kuingia wanakuwa wakali. Kwani nyie serikali hizo hela ni za kwenu hadi mtake kuzipora? Mungu anawaona!
 
Yule anaitwa Leah Ulaya. Waliogoma ni Dinna na Maganga. Kwanini Dinna haguswi anakomaliwa Maganga tu? Ipo namna hapa sio bure. Serikali kuna mahali inajichanganya yenyewe kwenye maamuzi yake kwa sababu uovu wao umeshikwa pabaya.Kwanini serikali inaingiza siasa CWT kila mwaka kutaka kuingiza mamluki ili wachote pesa za walimu? Wamezoea kuchota.pesa kwenye mifuko ya hifadhi ya kamii na NHIF. Kule CWT wamekosa kuingia wanakuwa wakali. Kwani nyie serikali hizo hela ni za kwenu hadi mtake kuzipora? Mungu anawaona!
Naona bora Maganga aachane nao, kina cha maji ni kirefu asije akapoteze vyote bure
 
Kwani bado alikwenda ofisi za CWT kama Rais/Katibu Mkuu wao.Au nako ameacha kwenda.Ukaguzi maalum ufanyike kuhakiki mali na fedha za wanachama.Ukionq kiongozi haendi likizo au hataki kuachia uongozi,ujuwe kuna makandokando au masilahi binafsi ni makubwa,ukilinganisha na masilahi ya umma
 
Pay ya Maticha imewapa kiburi sana! CWT ni dude fulani dhulmati viongozi wake hujiona kama miungu
 
Yule anaitwa Leah Ulaya. Waliogoma ni Dinna na Maganga. Kwanini Dinna haguswi anakomaliwa Maganga tu? Ipo namna hapa sio bure. Serikali kuna mahali inajichanganya yenyewe kwenye maamuzi yake kwa sababu uovu wao umeshikwa pabaya.Kwanini serikali inaingiza siasa CWT kila mwaka kutaka kuingiza mamluki ili wachote pesa za walimu? Wamezoea kuchota.pesa kwenye mifuko ya hifadhi ya kamii na NHIF. Kule CWT wamekosa kuingia wanakuwa wakali. Kwani nyie serikali hizo hela ni za kwenu hadi mtake kuzipora? Mungu anawaona!
Ametakiwa yeye arudi kituo chake cha kazi, hawezi kujitetea mbona mwenzake hajarudi, atekeleze alichotakiwa kufanya
 
Back
Top Bottom