Siamini km SERIKALI za wenzetu walioendelea walifanya zeleheba wakafikia hapo walipo kwa mtindo huo. Wanakua wakali kwenye jambo lao na hatua zinachukuliwa papo hapo, hapa ilipaswa hicho kituo kifungwe haraka sana na hatua nyingine kali za kisheria zifuate ndiyo ingeleta impact ya maana. Hicho alichokifanya huyo kiongozi kwa mazingira km hayo ni kulea uzembe. Wakati mwingine tunamlaumu JPM kwa kuchukua hatua za papo kwa papo lkn hiyo imesaidia sana kuliko hii ya kutoa ultimatum ambayo haina mwendelezo mahsusi wa ufatiliaji. Kumbuka hapa tunashughulika na haki za watoto wetu ambazo zinavunjwa maksudi na watu ambao tumewalipa ili wazilinde.