Ameshasahau juzi tu aliwaambia waandamane akiibiwa kura, lakini alivyogeuka nyuma hakuona mtu, Lissu mwenyewe akawaita waoga, ajabu bado analazimisha njia ile ile iliyofeli kwa wafuasi wake wale wale akitegemea outcome tofauti!.Hao hao wajinga unaosema hapa ndio wanaomdanganya mpaka anaamini kuwa yeye sasa ni sikio lililozidi kichwa, kwamba anaamini kuwa yeye sasa yuko juu zaidi ya chama na viongozi wengine wa chama.
Ila ameshindwa kujifunza kupitia kwa kina zito na Dr Slaa ambao wajinga wengine walikuwa wanawaaminisha kuwa ni maraisi wa mioyo yao. Lkn mwisho wa siku wakajikuta wameondoka peke yao na familia zao.
Kumbe umekuwa ukiizimia Chadema na kuionea wivu,ila sio kwa kutangatanga kwenye vyama vyote hivyo🏃🏃Habari zenu wana JF wenzangu,
Kwanza kabla ya kuendelea na mada hii ningependa watu wengi wafahamu kwamba mimi nimeandika mada hii kwa utashi wangu mwenyewe. Sikushawishiwa, sikulazimishwa wala kushikiwa akili na mwanasiasa yoyote iwe wa upinzani, wa CCM au wa kujitegemea. Bali nimeandika hili kutokana na mapenzi ya kweli niliyonayo kwa nchi yangu ya asili ya Tanzania.
Ndugu wana JF wenzangu, mimi nimekuwa mfuatiliaji mkubwa wa siasa zetu za Tanzania toka enzi za uanzishwaji wa mfumo wa vyama vingi, hadi leo hii ninavyoandika mada hii, naweza kusema kwamba nina ujuzi na ufahamu wa kutosha kuhusu siasa zetu za Tanzania. Miaka yote hiyo nakiri kwamba niliwahi kuwa mwanachama wa vyama vikubwa tofauti.
Kwanza mimi na familia yetu mpaka bibi zetu na babu zetu tulianza kuwa upande wa NCCR - Mageuzi chini ya aliekuwa mwanasiasa machachari na hodari wa enzi hizo hayati Augustino L. Mrema. Baadae miaka ya 2000, binafsi nikaamua kuhamia chama cha Wananchi CUF baada ya kuona vyama vingine vya upinzani kama vile NCCR Mageuzi na TLP vinaendeleza migogoro mbali mbali. Kwa upande wa familia yetu wengine walihamia TLP, na wengine wakabaki NCCR Mageuzi.
Mwaka 2009 nikajiunga rasmi Chadema, japo sikuwa mwanachama, lakini nikawa shabiki na kuhakikisha natembeza elimu ya kutosha kwa vijana wenzangu ili na wao wajiunge na chama hicho au hata kama hawakujiunga kwa njia ya uanachama, basi wahakikishe wawe wanakipigia kura chama hicho katika chaguzi mbali mbali.
Kwa vile mimi binafsi niliamini kuwa chama hicho kina viongozi wa kweli na wenye malengo ya kweli ya kutuletea ukombozi haswa baada ya kuisomwa na kuelewa ile list ya mafisadi wa taifa letu kule mwembe yanga.
Pilika pilika za kukiombea kura Chadema nilikuwa nazifanya nikiwa tayari naishi nje ya nchi, kwa kuwahamasisha watanzania wenzangu waendelee kukiamini na kukitegemea Chadema katika maisha yao.
Mwaka 2015, niliamua kuachana na Chadema baada ya mwenyekiti wetu na genge lake kuharibu hali ya hewa chamani, na kupelekea matumaini yetu ya kukichinjia baharini chama tawala kuyayuka kama chumvi ndani ya maji. Kibaya au kizuri zaidi CCM wao wakasimamisha mtu ambae ilikuwa ngumu kwa mtu anaejielewa wakati ule kumnyima kura. Jamaa alipata kura kwa wana CCM na wasiokuwa wana CCM, kwa wanasiasa na wasiokuwa wana siasa. Huku kwa upande wa upinzani wakitumia muda mwingi kupangua kashfa za ufisadi walizomuanzishia wao wenyewe mgombea wao.
Hii ni sawa na mwanaume uwambie wazazi wako kwamba unataka kumpa talaka mkeo baada ya kumkuta na mwanaume ndani ya chumba chako wakigegedana. Afu baadae uje uwambie kwamba umeahirisha kumpa talaka baada ya kugundua kwamba mkeo na huyo kijana hawakuwa wakigegedana bali walikuwa wakitafuta panya chumbani kwako. Imagine kwa utetezi huo wazazi watakuelewaje??
Zile zilikuwa ni siasa uchwara ambazo wengi hatupendi zirudie.
Anyway pamoja na pilika pilika zilizotokea miaka 7 iliyopita kati ya CCM na Wapinzani. Sasa chama hicho tawala kimeamua kukaachini na wapinzani ili kumaliza tofauti zao zilizokuwepo huko nyuma, kwa kuanzisha maridhiano ambayo yatapunguza kelele kwa pande zote mbili. Yani upinzani na serikali ambayo ndio CCM yenyewe. Katika hili watu wengi tuliwasifu wapinzani na watawala kwa kukaa chini na kupanga namna ya kuitengeneza upya Tanzania yenye amani, upendo na mshikamano kupitia vyama vya siasa na asasi mbali mbali.
Tuliwapongeza pia wenyeviti wa vyama hivyo ambao ndio waliouwezesha mchakato huo wa maridhiano kama vile mwenyekiti wa CCM mh raisi Samia S. Hassani, mwenyekiti wa Chadema mh Mbowe, mwenyekiti wa CUF mh Lipumba, kiongozi wa ACT Wazalendo mh Zito Kabwe, mzee wa ubwabwa nk.
Naweza kusema kwamba viongozi hao japo wana akili zao, madaraka yao na maamuzi yao, lkn inaonesha kuwa hawafanyi haya kwa mawazo yao, bali kwa kufuata miongozo thabiti ya vyama vyao.
Sasa anapokuja mtu kutoka ughaibuni ghafla na kuanza kupinga hadharani kile kinachofanywa na kiongozi wake au chama chake, huyo anakuwa ni mtovu wa nidhamu kwa chama chake na viongozi wake. Kwa sababu kama mtu haupendi au haukubaliani na kile kinachofanywa na chama chako au kiongozi wako, kwanini usipeleke madai yako katika chama yakajadiliwa na kutatuliwa kichama, badala ya kuja kuliongelea katika public kwa lengo la kumchafua na kumfanya yule kiongozi anaesimamia swala hilo (mwenyekiti) aonekane hana uelewa wowote juu ya swala hilo analolisimamia?
Inamaana mwenyekiti hufanya haya bila kuwashirikisha viongozi wa chama, na kama huwa anawashirikisha ni kwanini makamu huyo asimwambie kwamba hafurahishwi na maridhiano yao, ili wakae chini wayamalize kuliko kuja kulalamikia kwenye mikutano ya hadhara. Matokeo yake mwenyekiti atachoshwa na vijembe na yeye aamue kujibu na kupelekea mtifuano ambao utaharibu mchakato mzima wa hayo maridhiano yaliopo.
Mbona hatujasikia kelele hizi kutoka katika vyama vingine? Yani ni kilekile tu ambacho watu wengi ndio wanakiangalia!
Anyway katika hili mimi nasimama na Mbowe maana watanzania wengi tushachoshwa na siasa za majitaka, kuchafuana, kuingia barabarani kupambana na vyombo vya dola afu mwisho wa siku alieshawishi watu waingie barabarani akimbilie tena ulaya akaendelee ku claim ukimbizi kupitia mgongo wa fujo alizoziratibu mwenyewe nchini kwetu.
Haya yanafanywa sana na viongozi wa nchi za fujo na za vita kama Congo au Nigeria kwa kuendelea kuwadhamini waasi wapigane ili wao waendelee kupewa ukimbizi huko ughaibuni.
Mbowe asitishwe na kelele za chura, yeye aendelee kusimamia kile anachoona kina manufaa kwa taifa na chama chake. Afu huyo mleta kelele akiona hasikilizwi basi aanze chama chake mwenyewe, mbona Zito alipoona haeleweki akaanzisha cha kwake, Lisu anangoja nini?.
Sio kwa vile anaona uchaguzi wa chama unakaribia ndo ajaribu ku take advantage kupitia swala hili ili alitumie kama fimbo katika vikao vya chama kumuangusha mwenyekiti.
Lakini vile vile huenda jamaa amepewa mission na wabeberu ili aje ayumbishe maridhiano kwa lengo la kutengeneza migogoro itakayozaa vita, na vita ikiingia yanakuwa yale ya Congo. Wao wanaingia kujichotea tu bila mtu yoyote kuwa control. Maana wabeleji sio watu wazuri, wanachokifanya Congo na wajomba zao wamarekani kila mtu anakiona.
Hapa wenye upeo unaogusa mbingu ndo wataelewa.
Huo mkutano ndio ambao pia Lissu amezungumzia habari za nusu mkate na mengine.....kuna mkutano Lissu ameshutumu Ccm kwa kuweka mabango nchi nzima kwamba kuna " upatanisho " wakati wahanga mbalimbali hawajapewa haki yao.
..Lissu amem-challenge Mama kuwa upatanisho huendana na kutoa HAKI kwa walioumizwa, na uombaji radhi wa walioumiza wenzao mambo ambayo hayajafanyika bado.
..Jambo lingine Lissu ameonya kuhusu hila wanazotaka kufanya CCM za kuwaahidi Chadema nafasi kadhaa za ubunge ili wasikazie madai ya Katiba Mpya na Tume Huru.
..Again, tatizo ni mbinu chafu za CCM na sio manung'uniko anayoyatoa Tundu Lissu.
Huo mkutano ndio ambao pia Lissu amezungumzia habari za nusu mkate na mengine...
Hoja hapa, hayo anayozungumza ameshawaambia wenzake chamani wakagoma kumsikiliza mpaka aende kuropoka barabarani?
Au tunakubaliana Chadema hakuna taratibu zozote, kila mwenye jambo lake anaruhusiwa kusema popote atapoamua?
Hii tabia ya kila kiongozi kujiamulia kuongea anachotaka popote ikiota mizizi itasababisha wale wanaosema Chadema ni kama kambale baba ndevu..watoto ndevu.. wapate hoja, lazima ikemewe mapema.
Aisee....Ccm wana utaratibu wa kukabidhi akili zao kwa Mwenyekiti.
..Chadema kila mwanachama ni "kambale" na ana ruhusa ya kutoa mawazo na msimamo wake.
Aisee..
Kumbe Chadema hakuna kufuata taratibu, ni kuropoka tu!.
Lazima ujue kutofautisha kati ya kiongozi na mwanachama wa kawaida, hawa usiwachanganye utaharibu kila kitu.
Mwanachama wa kawaida anaweza kusema au kuandika chochote kama tufanyavyo huku JF, lakini kwa kiongozi, hatakiwi hata mara moja kuwa "kambale" wale wana vikao vyao chamani wakayazungumzie huko watoke na msimamo mmoja ili kuepuka kuwachanganya wanachama wao.
Uhuru usio na mipaka ni chanzo cha vurugu...wewe unaona anaropoka.
..wengine wanaona anatoa mawazo yake kwa uhuru.
Kuhoji sio tatizo lkn sasa jamaa ni kama vile anabeza wenzake kukubali maridhiano.Hata Lema akiwa nje ya nchi Naye amekuwa akihoji maridhiano na kusema huo ni msimamo wake binafsi.
Hata Msigwa pia ilikuwa hivyo ktk suala la Loriondo.
CDM IPO democracy, hivyo ni kawaida.
1. Swali la kwanza nilieleza huko juu kwamba niliyumba yumba au kuhama hama sababu ya migogoro (ya kimasilahi) iliyokuwepo katika vyama hivyo kati ya viongozi kwa viongozi.Makala ndefu hizi huchosha kusoma, lakini nimekusoma vya kutosha hadi ulipoanza kujitambulisha sababu zinazokufanya umshabikie Mbowe.
Kwanza nikusifu kwa uandishi mzuri, na umejieleza vyema toka mwanzo historia yako ilivyo kuhusu maswala ya siasa.
Kwa wakati huu ngoja nisiandike mengi sana, lakini inatosha kusema yafuatayo:
1. Umejiunga na vyama tele, lakini hujaeleza hasa sababu zako za kuyumbayumba kote huko. Hii ni dalili mbaya, na wengi watakuhukumu kwa msimamo wako huu wa sasa kutokana na yumbayumba yako hiyo
2. Umemsifu Mbowe kwa uhadari wake wa uongozi hadi hapo alipoingia yule jamaa 2015. Sasa swali kwako ni hilo hilo, unajuaje wakati huu na Samia Mbowe huyo huyo hakukengeuka kama alivyokwishaonekana kuwa huko nyuma, au kwa vile tu wakati huu ni Samia na siyo Ngoyayi?
Hapana, usinielewe vibaya, sina maana mbaya kwa Samia, lakini huyo huyo ndiye Mwenyekiti wa Chama ambacho katika uhai wa maisha yako yote hukueleza kuwa uliwahi kuwa mwanachama au mpenzi wa chama hicho. Hapa unahitaji kutoa maelezo juu yake. Huu ni upungufu mkubwa kwa upande wako
3. Hivi vyama vya siasa havianzishwi kwa sababu ya kutafuta maslahi ya viongozi wao. Katika maelezo yako mengi hujaeleza kwa nini wakati huu unaona Mbowe anacheza vizuri na uongozi wake wa chama kiasi cha kustahili sifa unazommiminia.
Hakuna mtu hata mmoja anayekata maridhiano, kama kuna maridhiano juu ya jambo lolote, lakini hiyo siyo sababu ya kubadili mwelekeo wa chama katika malengo yake.
Ngoja niishie hapa kwa sasa, isije ikawa gazeti jingine.
Nimetoa hukumu kivipi mkuu?Makala yako imeanzia hapa kuwa mbovu, kwa sababu ulionyesha waziwazi rangi zako zilivyo. Umeshutumu na kutoa hukumu palepale.
Dunia ina mengi hii, kama haujui inavyokwenda hauwezi kuelewa.Aiseee!
Nilikuwa sijakusoma hadi huku chini.
Ukianzia pale ulipoanza kumsema "mtu wa ugaibuni, hadi huku mwisho; mada yako umeinyonga kabisa. 'Objectivity'
ukaitupa jalalani moja kwa moja!
Pole yako.
Uko sahihi...Lissu hapingi maridhiano.
..Lissu anatetea maridhiano yenye tija.
..Hoja za Lissu ndizo zitakazompa nguvu Mbowe anapojadiliana na CCM.
SahihiUhuru usio na mipaka ni chanzo cha vurugu.
CCM ndio serikali. Kwahiyo wanataka amani na mshikamano kupitia hayo maridhiano, maana kuna mda ilifikia watu wa familia moja wanagombania maiti kisa upande wa baba ni CCM na upande wa mama ni Chadema au ACT Wazalendo. Kwahiyo hali inapofikia hapo wa kulaumiwa ni serikali ambayo ipo chini ya chama cha mapinduzi (CCM)..CCM wanataka nini kwenye maridhiano?
..Why are they in maridhiano? What are they trying to achieve?
..Lingine, CCM wana maoni gani kuhusu Katiba Mpya?
..Mwenyekiti wao ameruhusu mchakato wa Katiba Mpya lakini sijasikia makada wa CCM wakiweka hoja zao mezani kuhusu Katiba Mpya.
Tofauti ya Mbowe na Lisu ni kwamba Mbowe anatumia akili zaidi kuliko nguvu na mdomo, Lisu anatumia nguvu na mdomo zaidi kuliko akili na maarifa.Ameshasahau juzi tu aliwaambia waandamane akiibiwa kura, lakini alivyogeuka nyuma hakuona mtu, Lissu mwenyewe akawaita waoga, ajabu bado analazimisha njia ile ile iliyofeli kwa wafuasi wake wale wale akitegemea outcome tofauti!.
Ila wewe, kwa sababu unazozijua mwenyewe, huwezi kamwe kufikiri kwamba Rais huyo huyo unayemsifu hapa anatumia mbinu tofauti tu na yule wa mwanzo kuendeleza jitihada za kuwamaliza CHADEMA!Sasa ameingia raisi mungine ambae ameamua kurudisha uelekeo wa kisiasa uliokuwepo miaka yote kwa kuruhusu mikutano ya kisiasa, uhuru wa kutoa maoni na kufanya maridhiano yatakayosaidia kupatikana suluhu ya matatizo ya kisiasa yaliokuwepo na yaliopo nchini.
Sijui haya ya "amani" yanatoka wapi?Hii ni hatua nzuri ambayo inahitajika kupongezwa na watu wanaopenda amani na siasa zenye muelekeo wa kujenga taifa bila kujali ilikadi za vyama vyao. Anapokuja mtu na kuanza vijembe mikutanoni ili mwisho wa siku alete mgawanyiko ndani ya chama wa wanaosapoti maridhiano na wasiosapoti hadi kupelekeo mchakato mzima wa maridhiano kuvunjika inakuwa haileti picha nzuri.