Katika hili mimi nasimama na Mbowe, hakika jamaa kakomaa kisiasa na anaijua vizuri siasa

Katika hili mimi nasimama na Mbowe, hakika jamaa kakomaa kisiasa na anaijua vizuri siasa

Mwaka haujaisha kwenye nini Boss?
Mwaka haujaisha toka serikali chini ya CCM iingie katika maridhiano na wapinzani.
Kwahiyo hakuna sababu ya kuanza kulalamika na wakati maswala yao yanafanyiwa kazi.

Ikifika mwaka au zaidi hapo ndo itakuwa ruhusa makamu huyo kuanza kukilaumu chama chake na viongozi wake kuhusu maridhiano hayo.
 
Usipende kuwaamini sana wanasiasa, maana kuna siku watakwambia ukinichagua mimi nitahakikisha unaishi maisha yako yote bila kufa. Na wakati kiuhalisia hakuna mwanadamu anaeweza kuishi bila kufa akiwemo yeye mwenyewe mwanasiasa husika.
Siwaamini wanasiasa nauamini ukweli
 
Wewe mwana CCM una Maslahi yepi na Mbowe Hadi umwone Lissu Hana ADABU?

Pambana na RUSHWA ndani ya chama chako kwanza.
Mimi ni mtanzania na Chadema ni ya watanzania.
Pia chama hicho wakiwepo viongozi wao wanapokea ruzuku ambayo ndani yake kuna kodi yangu, so hakuna mtu wa kunizuia kuhoji.

Wewe anzisha chama chako ambacho utakiendesha kwa hela zako uone kama mimi nitakuja kuhoji kuhusu uendeshaji wako.
 
Kwa taarifa yako huko CDM tuko kwa kufuata misimamo yake na sio mtu, ndio maana akina Slaa na Zito walitoka kama wao. Hata huyo Mbowe akianza kwenda kinyume na misimamo ya chama atabaki huko chamani na anaokubaliana nao. Pressure ya Lisu kwenye hayo maridhiano itasababisha maridhiano yasiwe na hila, ila kila mmoja akikaa kimya kutaingizwa maridhiano yenye hila ndani yake. Anachofanya Lisu kitasaidia sana haya maridhiano yasiwe ya kuburuzana.
Hapa nimekuelewa kwa namna fulani.
 
SUK itufunze kuwa CCMM hawana jadi ya kuheshimu maridhiano na makubaliano.

Uchaguzi wa marudio majuzi wameendelea kupora uchaguzi bila kuheshimu terms za SUK.

Tupambanie Tume huru ya Uchaguzi na KATIBA mpya na tuhakikishe uchaguzi haufanyiki bila mambo hayo muhimu kupatikana.
Ok lets wait to see kile kitachofanyika.
 
Usipende kuwaamini sana wanasiasa, maana kuna siku watakwambia ukinichagua mimi nitahakikisha unaishi maisha yako yote bila kufa. Na wakati kiuhalisia hakuna mwanadamu anaeweza kuishi bila kufa akiwemo yeye mwenyewe mwanasiasa husika.
Kumbuka na hii ya dikteta uchwara akiyapokea kwa heshima zote za chama majizi yaliyokimbilia Chadema
FB_IMG_1581491063368.jpg
 
Mimi ni mtanzania na Chadema ni ya watanzania.
Pia chama hicho wakiwepo viongozi wao wanapokea ruzuku ambayo ndani yake kuna kodi yangu, so hakuna mtu wa kunizuia kuhoji.

Wewe anzisha chama chako ambacho utakiendesha kwa hela zako uone kama mimi nitakuja kuhoji kuhusu uendeshaji wako.
Kwann umeficha identity Yako ya CCM?

Ungedeclare interest ungeeleweka vizuri zaidi.
 
Lisu huwa anapenda aonekane kuwa yeye ndio mwenye mawazo chanya chamani, na kwamba viongozi wengine wote hawana uwezo au ujanja wa kuona yale anayoyaona yeye.

Swala la katiba mpya na mengineyo yapo katika mchakato. Na tayari tumeshasikia kwamba raisi kaagiza viongozi wanaohusika na swala hilo la katiba waanza kufanyia kazi yale yanayohitajika. Hiyo ni hatua nzuri ambayo kwa muda wa miaka zaidi ya 7 hatukuishuhudia, wala kufikiria kuishuhudia.
Sasa sijui Lisu anataka raisi afanyaje?

Lakini pia kuna taratibu za kichama ambazo mtu unatakiwa kuzifuata ili kuufikisha ujumbe wako na kufanyiwa kazi na viongozi husika. Sasa yeye hizo taratibu hakupenda kuzifuata na badala yake kaanza kuandaa mikutano ili apate namna ya kuongelea mabaya ya viongozi wenzake kwamba wamefanya maamuzi ya kijinga na kwamba yeye ndio mjanja asiekubaliana na maamuzi yale.

Mwisho wa siku Mbowe, Mnyika au Lema uvumilivu utawashinda na wao waanze kumjibu majukwaani au mitandaoni. Chama kigawanyike kuhusu maridhiano hayo na maridhiano yafe na nchi irudi kule kule kwenye siasa za uhasama, mikutano ifungiwe tena na nchi irudi katika mfumo uliyokuwepo miaka iliyopita.
Naamini hao viongozi wengine uliowataja wana hekima, hawawezi kujitia uchizi alionao Lissu waanze kumjibu, wanajua wakifanya hivyo ndio watakuwa wanazidi kukivua nguo chama chao, muhimu Lissu aachwe aropoke tu akichoka atanyamaza.

Ajabu ni pale ambapo huu ujinga anaofanya, lipo kundi linampongeza, wanamuona jasiri muongoza njia, kumbe ni muhuni muongoza njia, wanataka Chadema iondoke kwenye kufuata sheria na taratibu walizojiwekea, sasa kiwe chama cha kila mwenye mdomo na aseme popote alipo!.

Hawa wajinga ni wakuhurumia tu, mahaba yao kwa Lissu yamewafunga upeo wao kifikra hawaoni tena athari za kile Lissu anachofanya kwa sasa, kwao Lissu ni kama malaika aliyeshuka kutoka mbinguni!.
 
SUK itufunze kuwa CCMM hawana jadi ya kuheshimu maridhiano na makubaliano.

Uchaguzi wa marudio majuzi wameendelea kupora uchaguzi bila kuheshimu terms za SUK.

Tupambanie Tume huru ya Uchaguzi na KATIBA mpya na tuhakikishe uchaguzi haufanyiki bila mambo hayo muhimu kupatikana.

Kabisa, haya maridhiano ni wapinzani wanaletwa ili wagaeuzwe makondoo, kisha ikifika uchaguzi wanafanyiwa uhuni, halafu yanatokea maridhiano tena. Kuamini maridhiano kwa watu ambao ikifika muda wa kuheshimu maridhiano wanayakiuka, halafu baadae wajifanye wanaleta maridhiano ni ujuha wa wazi.
 
..CCM ndio kikwazo cha kukamilika kwa maridhiano.

..tutawalaumu Mbowe na Lissu lakini tunajua tatizo liko CCM.
Kama hivi ndivyo kwanini Lissu anahangaika kuwalaumu wenzake chamani? anawachorea ramani waonekane kama wepesi waliokubali kutongozeka mbele ya Samia..

Kama tatizo liko CCM, apeleke shutuma zake huko kwa 100% but not otherwise.
 
Mwaka haujaisha toka serikali chini ya CCM iingie katika maridhiano na wapinzani.
Kwahiyo hakuna sababu ya kuanza kulalamika na wakati maswala yao yanafanyiwa kazi.

Ikifika mwaka au zaidi hapo ndo itakuwa ruhusa makamu huyo kuanza kukilaumu chama chake na viongozi wake kuhusu maridhiano hayo.

Kuna mtu amekuuliza kuhusu maridhiano ya 2010 huko Zanzibar baada ya machafuko ya uchaguzi wa 2001 huko Zanzibar. Je ni kilifanyika kwenye uchaguzi wa 2015 kukiwa na serikali ya umoja wa kitaifa na katiba ya Zanzibar? Naona hutoi majibu bali unaleta porojo tu. Lisu hana haja ya kuamini kwenye maridhiano ya watu wasioaminika.
 
Mwaka haujaisha toka serikali chini ya CCM iingie katika maridhiano na wapinzani.
Kwahiyo hakuna sababu ya kuanza kulalamika na wakati maswala yao yanafanyiwa kazi.

Ikifika mwaka au zaidi hapo ndo itakuwa ruhusa makamu huyo kuanza kukilaumu chama chake na viongozi wake kuhusu maridhiano hayo.

Kuna mtu amekuuliza kuhusu maridhiano ya 2010 huko Zanzibar baada ya machafuko ya uchaguzi wa 2001 huko Zanzibar. Je ni kilifanyika kwenye uchaguzi wa 2015 kukiwa na serikali ya umoja wa kitaifa na katiba ya Zanzibar? Naona hutoi majibu bali unaleta porojo tu. Lisu hana haja ya kuamini kwenye maridhiano ya watu wasioaminika.
 
Wachache mno tena wenye uelewa mpana wa maswala ya kisiasa ndo wataelewa kile ulichoandika.

Ila kwa wale wenzangu na mie walioanza kujifunza siasa mwaka 2010 na kuendelea kwa kweli itakuwa ngumu sana kuona kile ulichoandika.
Hawa jamaa hawajui hii michezo yao ya kufunika moto kwa shuka imeanza siku nyingi sana, malumbano mengi Chadema mwanzo wake mpaka mwisho wake niliyaona, mfano lile la Zitto.

Mambo huanza hivi hivi, mtu anafanya ujinga huko nje then kina Mrema wanakuja na hoja nyepesi za utetezi, matokeo yake mambo yanazidi kuharibika ndani kwa ndani, mwishowe ugonjwa unakuwa mkubwa na kutoka nje, wanakosa cha kujitetea.

Muhimu waache hii style ya kupuliza kama panya, wahakikishe wanakaa huko ndani na huyo msumbufu wamuweke sawa, wakishindwa kufanya hivyo atazidi kuropoka nje mpaka ifike stage ya beyond repair, hapo kitachofuata ni kuagana tu.

Huyu Lissu inawezekana pia akawa na agenda yake nyingine ya siri, ndio anaitafutia sababu kwa hizi kelele zake za sasa...

Let us keep our eyes and brain wide open.
 
Kama hivi ndivyo kwanini Lissu anahangaika kuwalaumu wenzake chamani? anawachorea ramani waonekane kama wepesi waliokubali kutongozeka mbele ya Samia..

Kama tatizo liko CCM, apeleke shutuma zake huko kwa 100% but not otherwise.

..kuna mkutano Lissu ameshutumu Ccm kwa kuweka mabango nchi nzima kwamba kuna " upatanisho " wakati wahanga mbalimbali hawajapewa haki yao.

..Lissu amem-challenge Mama kuwa upatanisho huendana na kutoa HAKI kwa walioumizwa, na uombaji radhi wa walioumiza wenzao mambo ambayo hayajafanyika bado.

..Jambo lingine Lissu ameonya kuhusu hila wanazotaka kufanya CCM za kuwaahidi Chadema nafasi kadhaa za ubunge ili wasikazie madai ya Katiba Mpya na Tume Huru.

..Again, tatizo ni mbinu chafu za CCM na sio manung'uniko anayoyatoa Tundu Lissu.
 
Lissu hapingi maridhiano.

..Lissu anatetea maridhiano yenye tija.

Tuna imani na Lisu na sio hayo maridhiano ya kitapeli ya Mbowe

..Lissu angejikalia nyumbani kwake usingesikia makelele haya dhidi yake.

Leo Lissu yuko barabarani yameibuka makundi ya kila aina kumshambulia.

Sasa kwanini hakukaa na viongozi wenzake wakajadiliana kuhusu mambo hayo, badala ya kuanza kuzunguka nchi nzima kuyananga maridhiano hayo.

kuanza kulaumu maridhiano ambayo bado yapo kwenye hatua ya kufanyiwa kazi

Hakuna haja ya kuendekeza maridhiano ya kupotezeana muda. Lisu anaweka msisitizo kuwa hayo maridhiano yana walakini,

Lisu hakutumia njia nyingine za kichama kuelezea madai yake,

Umejuaje kuwa hayo maridhiano ni makubaliano ya chama?

sisi wafuasi wengine tutasimama na anayesimamia tunachotaka sio porojo za maridhiano

Anayozungumza Lissu yana baraka zote za chama.

CDM hakuna mgogoro, Lissu anajaribu kuwakumbusha Sugu na wenzie kuwa KATIBA mpya ndo kipaumbele, ubunge ndo ufuate.

Ukimsikiliza Lissu anavyoongea unamuona kabisa ametawakiwa na ujuaji, mihemko,

Usipende kuwaamini sana wanasiasa, maana kuna siku watakwambia ukinichagua mimi nitahakikisha unaishi maisha yako yote bila kufa.

tutawalaumu Mbowe na Lissu
 
Hata ikitokea maridhiano yamevunjika Leo, Bado wananchi wataendelea kuiamini CDM Kwa misimamo ya Lissu, Heche na Wenje.

Siasa zetu zinachukua episode ingine.

Tusubiri.
 
Kumbuka na hii ya dikteta uchwara akiyapokea kwa heshima zote za chama majizi yaliyokimbilia ChademaView attachment 2617000
Majizi kupokelewa kwenye chama cha siasa sio tatizo, tatizo ni kuyaweka katika serikali.
Ni mfano leo mwizi au au mzinzi hawezi kuzuiliwa au kukataliwa kuingia msikitini au kanisani. Sema litakuwa kosa kubwa kama mwizi huyo atachaguliwa kuwa kiongozi mwandamizi au mkuu wa kanisa au msikiti huo.
 
Back
Top Bottom