Katika Kanda 10 za CHADEMA, Lissu anaweza kuambulia kura kutoka maeneo gani?

Katika Kanda 10 za CHADEMA, Lissu anaweza kuambulia kura kutoka maeneo gani?

BaDo sijaona unafiki hapo. Mwulize Wenje ndiye mhusika wa hayo ambaye mnamtuma kufanya hujuma kwa kiongozi mwenzake
mtu anaropoka ati fulani amepewa au kupokea rushwa,

anaulizwa atoe ushahidi, ana mbwelambwela tu,

unafiki ulioambatana na tamaa na usaliti ni kitu cha hovyo sana aise dah!:pedroP:
 
Kimsingi, CHADEMA kama chama cha siasa nchini, kina kanda 10 za kiutawala.

Na kanda zote 10 zina viongozi waandamizi ambao wamechaguliwa awamu hii katika uchaguzi ambao ulianza mapema 2023 na utahitishwa rasmi na uchaguzi ngazi ya Taifa Jan.22,2025.

Viongozi karibu wa kanda zote 10 waliochaguliwa hivi karibuni na viongozi mikoa na wilaya kadhaa nchini, waliweka wazi misimamo yao dhidi ya nani ambaye wanamuunga mkono kwenye nafasi ya Uenyekiti wa CHADEMA Taifa2025-2030.

Kama mdau wa siasa na demokrasia, na kwa kutumia hisabati ya siasa, unadhani Tundu Antipas Lissu anaweza kupata kuungwa mkono kutoka kwa wajumbe wa mktano mkuu wa CHADEMA Taifa, kutoka katika kanda zipi? Mikoa na wilaya zipi haswa hata awe Mwenyekiti wa chadema Taifa?

Na vipi kuhusu Freeman Aikaeli Mbowe, kwa kutumia sayansi ya siasa, anaweza kujizolea kura nyingi zaidi za kishindo kutoka kanda zipi za kiutawala, mikoa ipi na wilaya zipi humu nchini?

Mungu Ibariki Tanzania
Katika mkoa wa Singida anaotoka Lissu,Mbowe anakura za uhakika zisizopungua 19.Hata katibu wake jimbo la Singida mashariki,anamuunga mkono Mbowe.
 
Lissu kanda ya kati anakura chache sana, sababu kubwa ni ubahili na kudhani kutoa misaada kwa Wajumbe ni rushwa.
kwahiyo ni mgombea mwenye dhana potofu dhidi ya matumizi ya pesa, right? :pedroP:
 
naona umefafanua kijumla vizuri sana katika aya ya kwanza, kwamba nafasi ya muungwana kushinda ni finyu mno, ni kama vile ngamia kupita katika tundu la sindano,

hata hivyo,
ufafanuzi wa ziada ulioutoa ni wa kinadharia zaidi, na pengine kinabii au kiroho zaidi, amboa kwa wasio amini Mungu wataona hauna athari zozote za moja kwa moja kisiasa kwenye uchaguzi huo na kwa Taifa kwa ujumla :pulpTRAVOLTA:
Wakati Fulani kwenye Sayansi ya Siasa ...utabiri,Unabii na masuala Unayoita ya kiroho ni halisi na yanafanya kazi!
 
mtu anaropoka ati fulani amepewa au kupokea rushwa,

anaulizwa atoe ushahidi, ana mbwelambwela tu,

unafiki ulioambatana na tamaa na usaliti ni kitu cha hovyo sana aise dah!:pedroP:
Leo ya chadema yanaakuuma sana?
 
Unaweweseka, wapiga kura tupo.
We unafahamu mi ni mjumbe kutoka kanda ipi?
Atasema, ah..
20250109_125729.jpg
 
Mbowe alishajaza watu wake lisu amekuja kushtuka kumekucha tayar kanda ya kat anawaza akaambulia kitu
 
Wakati Fulani kwenye Sayansi ya Siasa ...utabiri,Unabii na masuala Unayoita ya kiroho ni halisi na yanafanya kazi!
Imani ya kwamba utashinda na hutafuti kura na wala huna kura ni sawa na ushirikina tu gentleman,

kura ni ya kutafuta kabisa gentleman na sio story za pata potea mitandaoni.🐒

Na sio kwamba umuache Mungu
 
Mbowe alishajaza watu wake lisu amekuja kushtuka kumekucha tayar kanda ya kat anawaza akaambulia kitu
siasa ni kuhipanga aise,
saa zingine hii maneno ya kuzingatia upepo tu bila kufanya jitihada za makusudi, mtu anaweza kuambulia patupu hadi home areas 🐒
 
Back
Top Bottom