Katika Marais wote waliopita Tanzania namkubali Kikwete zaidi

Katika Marais wote waliopita Tanzania namkubali Kikwete zaidi

P h a r a o h

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2024
Posts
785
Reaction score
1,413
Jakaya_Kikwete_2011_(cropped)_(cropped).jpg


sijui ni kwanini Legacy yake haizumgumziwi kabisa,

shule za kata ni moja ya kitu muhimu zaidi alichoifanyia Tanzania, na hakitasahaulika...

Mwana demokrasia na mwana diplomasia ambae hakuna aliyewahi kumfikia Tanzania hii...

Hata chuo kikuu cha UDOM na miradi mingine ameitekeleza yeye mwenyewe akiwa madarakani.

lakini hakuna anaeongelea na kupongeza jitihada
zake.

ni kwasababu ya hulka yake na demokrasia yake ya kuruhusu kila kitu kusemwa hadharani ? l


Legend JK
 
View attachment 3217066

sijui ni kwanini Legacy yake haizumgumziwi kabisa,


shule za kata ni moja ya kitu muhimu zaidi alichoifanyia Tanzania, na hakitasahaulika...


Mwana demokrasia na mwana diplomasia ambae hakuna aliyewahi kumfikia Tz hii...

hata chuo kikuu cha UDOM na miradi mingine ameitekeleza yeye mwenyewe akiwa madarakani.

lakini hakuna anaeongelea na kupongeza jitihada
zake.

ni kwasababu ya hulka yake na demokrasia yake ya kuruhusu kila kitu kusemwa hadharani ? l


Legend JK
Hapo kwenye bold pananiumiza sana..
Taasisi ya urais ni nzito na nyeti kiasi kwamba hakuna atakayepita wala kuja na kusifiwa nayo..
Ndio kusema my president ninaemkubali
 
h
Hapo kwenye bold pananiumiza sana..
Taasisi ya urais ni nzito na nyeti kiasi kwamba hakuna atakayepita wala kuja na kusifiwa nayo..
Ndio kusema my president ninaemkubali

huyu jamaa ni legend na amefanya makubwa mengi tuu ila machawa wankusifia kila kitu hawakwepo

ila kati ya viongozi bora waliotoka chama cha mapinduzi naye yupo

( si support ccm kabisaa )
 
View attachment 3217066

sijui ni kwanini Legacy yake haizumgumziwi kabisa,


shule za kata ni moja ya kitu muhimu zaidi alichoifanyia Tanzania, na hakitasahaulika...


Mwana demokrasia na mwana diplomasia ambae hakuna aliyewahi kumfikia Tz hii...

hata chuo kikuu cha UDOM na miradi mingine ameitekeleza yeye mwenyewe akiwa madarakani.

lakini hakuna anaeongelea na kupongeza jitihada
zake.

ni kwasababu ya hulka yake na demokrasia yake ya kuruhusu kila kitu kusemwa hadharani ? l


Legend JK
Legacy ya huyu Vasco Dagama ni ufujaji wa pesa za wananchi kwenda kubembea marekani na chawa wake na pili kubwa zaidi kuhujumu upatikanaji wa Katiba ya wananchi iliyopendekezwa na Warioba! Bila hujuma ya Kikwete saa hizi nchi ingekuwa imesonga mbele sana kisiasa na kiuchumi
 
Legacy ya huyu Vasco Dagama ni ufujaji wa pesa za wananchi kwenda kubembea marekani na chawa wake na pili kubwa zaidi kuhujumu upatikanaji wa Katiba ya wananchi iliyopendekezwa na Warioba! Bila hujuma ya Kikwete saa hizi nchi ingekuwa imesonga mbele sana kisiasa na kiuchumi
kwanini "Bila hujuma ya Kikwete"

na si wengine wakati yeye ni rais wa nne tu,

kipi kimefanya um highlight yeye na kuwaacha wengine ?
 
shule za kata ni moja ya kitu muhimu zaidi alichoifanyia Tanzania, na hakitasahaulika...
Shule za kata ziliasisiwa wakati wa Mkapa.

Shule hizo zilianza ujenzi wake miaka ya kuanzia 2001.

Ilikuwa hivi, kipindi hicho shule zote za kata zilijengwa kwa nguvu za wananchi (kuanzia msingi mpaka kuezeka mpaka finishing).

Kata ambazo walilipokea wazo hilo positively, walichangishana haraka haraka na wakaweza kuanza masomo mapema. Ndiyo maana shule nyingi za kata ambazo kwa sasa ni kongwe kidogo zilianza 2002.

Waliochelewa kidogo walianza 2004, 2005.

Kisha kuna waliokuwa wazembe hao walianza mwaka 2006 miezi ya mwanzoni. Na hao ilibidi waziri mkuu wa enzi hizo Hayati Lowasa awe mkali (nakumbuka hotuba zake sehemu mbalimbali kwa wazembe alivyowawashia moto wakurugenzi kuhakikisha michango inachangwa kwa haraka). Yaani kwa waliochelewa chukulia kama ujenzi wa SGR, uanze wakati wa Magufuli ukamilike wakati wa Samia.

Wakati wa Jakaya, alihakikisha shule zinapata walimu, kwanza kwa kuanzisha ile kitu ilikuwa maarufu kwa jina la walimu wa vodafasta (mwaka 2007, 2008).

Kuanzia mwaka 2011, ndipo walimu walianza kuajiriwa kwa wingi (kila mwaka hadi 2015).

Najaribu kuweka kumbukumbu zangu katika jukwaa kwa kuwa niliona kwa macho yangu namna wazazi walivyokuwa wakijificha kukwepa michango ya kuasisi shule za kata. Na ili wananchi wasiwe na mamichango mengi, kodi ya kichwa (Tsh 4,000/=) ilifutwa rasmi. Katika kata nyingi (hasa za wilaya niliyozaliwa, michango ilikuwa ni Tsh 10,000/= kwa kila darasa. Na kurahisisha kazi, kama kata ilikuwa na vijiji 7, kila kijiji kilipaswa kujenga darasa moja moja kwa kuanzia na baada ya hapo kuendelea na ujenzi wa kuongezea madarasa.

Kama wilaya uliyotoka walichelewa kuanza masomo na wakaanza wakati wa Jakaya, jua kuwa walikuwa na wasimamizi wa wilaya wazembe. Naweza kukutajia shule zote za kata ndani ya wilaya yangu walioanza mwaka 2002, 2003, 2004, 2005 na waliochelewa na kuanza 2006 mwezi wa kwanza, pili au tatu.

Kabla sijamaliza, si unakumbuka MMEM na MMES? Sasa hiyo MMES ndiyo iliyochochea uongezaji wa mashule ya sekondari kwa kuasisi mashule ya kata nchini.
MMEM - mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi.
MMES - Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari.

Katika kuhakikisha shule zinapata walimu wa kutosha, ndipo mpango wa kujenga chuo cha UDOM ukaasisiwa (ndiyo maana wengine hukiita chuo cha kata). Ujenzi ulianza awamu ya Rais Kikwete.

Credit ya shule za sekondari inaangukia kwa awamu ya Kikwete (akiimbwa zaidi Loawasa) kwa kuwa katika wilaya nyingi, wazazi walikuwa wazembe kuchangia na hivyo hawakukamilishi majengo wakati wa awamu ya Mkapa, na ndipo Lowasa akasuma ajenda hiyo kwa nguvu sana kwa wilaya zote zembe zembe.

Shule za kata ujenzi wake ulikuja kupata sapoti ya serikali awamu ya Magufuli, ilikuwa wazazi wanachangishana kuanzia msingi hadi kumaliza boma lote, uezekaji na finishing ikawa inamalizia serikali.

Awamu ya Rais Samia, shule za kata ujenzi wake wa madarasa umekuwa chini ya serikali (kuanzia 2021 disemba chini ya program ya Covid 19).
 
kwanini "Bila hujuma ya Kikwete"

na si wengine wakati yeye ni rais wa nne tu,

kipi kimefanya um highlight yeye na kuwaacha wengine ?
Kikwete amehujumu sana nchi hii kiuchumi enzi ya utawala wake. Yeye ndio alikuwa partner wa Home shopping Centre wakati huo na sasa ili wasijulikane kabla ya Marehemu Magu kuingia madarakani wakabadili jina na kuitwa GSM!!
Hawa walikuwa wanaingiza makontena ya bidhaa kwa ma Elfu bila kulipa ushuru wa bandari miaka yote ya utawala wake. In fact what Home shopping Centre did during Kikwete’s tenure could be characterized as “ STATE CAPTURE “ by Home Shopping Centre!
 
View attachment 3217066

sijui ni kwanini Legacy yake haizumgumziwi kabisa,

shule za kata ni moja ya kitu muhimu zaidi alichoifanyia Tanzania, na hakitasahaulika...

Mwana demokrasia na mwana diplomasia ambae hakuna aliyewahi kumfikia Tanzania hii...

Hata chuo kikuu cha UDOM na miradi mingine ameitekeleza yeye mwenyewe akiwa madarakani.

lakini hakuna anaeongelea na kupongeza jitihada
zake.

ni kwasababu ya hulka yake na demokrasia yake ya kuruhusu kila kitu kusemwa hadharani ? l


Legend JK
Hii nchi ina wapumbavuh wengi mpaka naona aibu hata kurudi Kuja Ishi Tanzania. Ngoja niendelee kubaki ishi huku ughaibuni. Wewe utakuwa ni Division 5 kilaza wa vyeti fake.
 
Hii nchi ina wapumbavuh wengi mpaka naona aibu hata kurudi Kuja Ishi Tanzania. Ngoja niendelee kubaki ishi huku ughaibuni. Wewe utakuwa ni Division 5 kilaza wa vyeti fake.
JK Kuna malafa flani km huyu ambao wanamchukia na hawataki kusema ukweli lkn Kuna mengi amefanya (sijasema Hana madhaifu.......hayo Kila mtu anayo). Kuna kitu flani wakati wa JPM walilishwa wanyonge na ghafla wakaibuka na chuki kubwa dhidi yake. Matokeo yakawa Kila alichokifanya basi anapewa JPM. Nitatoa mifano michache;
-Wanyonge wanaamini mwendo Kasi ni JPM (ukweli ni jk ndiye aliyeasisi na kuanza kushughulikia)
-Flyovers wanyonge wanaamini ni JPM (ukweli ni uasiso wa jk)
-wanyonge wanaamini jk hajajenga barabara Bali ni JPM. Ukweli hakuna aliyejenga mtandao mrefu wa barabara kumzidi jk.
Na mengine meeeengi, hayo ni kwa uchache tu.

Jk analipwa chuki, wengi tukiwa hata hatujui kwanini tunamchukia Bali tunafuata tu tulichoambiwa.

Ila jamaa ni mwamba kweli kweli, Hana hoyana na mtu. Anawaonyesha tu tabasamu na Mungu anamjaalia mambo yake yanaenda vizuri sana.....no stress. Wanamchukia na kujaribu kumharibia wanachemka wao Huku wakimuacha vilevile. Kina Bashe na Makonda wamejaribu sana kumfuatafuata lakini kawakaushia na wanajikuta wanahangaika wao peke yao.
 
Legacy ya huyu Vasco Dagama ni ufujaji wa pesa za wananchi kwenda kubembea marekani na chawa wake na pili kubwa zaidi kuhujumu upatikanaji wa Katiba ya wananchi iliyopendekezwa na Warioba! Bila hujuma ya Kikwete saa hizi nchi ingekuwa imesonga mbele sana kisiasa na kiuchumi
Umeandika upumbavu. Ya Warioba ilikuwa rasimu ya katiba na sio katiba pendekezwa. Na kwa mujibu wa sheria ilikuwa lazima rasimu ijadiliwe na bunge maalum. Ila nyie wapumbavu mlitaka sheria isifuatwe ili rasimu ya Warioba ipite kama ilivyo.
 
Kipindi chake Upinzani uli enjoy!
Alikubali kusemwa,Kukosolewa na kuwa tayari kutekeleza yale aliyoona yana maslahi mapana kwa nchi yetu.
Sema tu aliiweka rehani Nchi yetu kwa Mafisadi.
Mapungufu yake ndiyo yale ambayo JPM aliyafanyia Reform!
 
Back
Top Bottom