Katika nchi 35 zilizokataa kupiga kura suala la Urusi kuvamia Ukraine 50% ni za Afrika, ikiwemo Tanzania

Katika nchi 35 zilizokataa kupiga kura suala la Urusi kuvamia Ukraine 50% ni za Afrika, ikiwemo Tanzania

Nasikitika sana. Halafu utakuna hawa wanaojiita viongozi wetu kwa unafiki kabisa wanasema tukumbuke leo siku ya kumuenzi Nyerere. Wanamuenzi kitu gani, kila alichosimamia wamegeuka?
Kwa hiyo wewe unaamini Nyerere alikuwa sahihi kwa kila alichosimamia? Kumbuka alikuwa binadamu, hivyo kukosea si ajabu. Hivyo inawezekana kabisa kuna baadhi ya misimamo yake haikua sahihi, au huenda ilikuwa sahihi kwa nyakati zile, lakini kwa sasa ikawa kinyume chake.
 
Kwa hiyo wewe unaamini Nyerere alikuwa sahihi kwa kila alichosimamia? Kumbuka alikuwa binadamu, hivyo kukosea si ajabu. Hivyo inawezekana kabisa kuna baadhi ya misimamo yake haikua sahihi, au huenda ilikuwa sahihi kwa nyakati zile, lakini kwa sasa ikawa kinyume chake.
Sio kwa jambo kama hili. Lina ugumu gani? Ni halali kuvamia nchi nyingine kwa kuwa eti unaona kuna watu wa lugha yako wanaonewa? Siku Wamakonde wa Msumbiji wakisema wanaonewa na serikali ya Msumbiji tupeleke majeshi Mtwara kusogeza mpaka kuingia ndani ya Msumbiji ili tukawakomboe Wamakonde wenzetu?
 
1. Rwanda ina jitambua katika nini ?

2. Mkuu una mkubali Kagame na Rwanda yake ?
Rwanda wanajitambua katika hili suala la Russia na Ukraine, huko kwingine unakotaka twende mie sijaongelea kwenye hii thread
 
Unamtukuza Nyerere lkn hujui philosophy zake. Nyerere ndo mwanzilishi na muumini wa "siasa za kutofungamana na uoande wowote" na huo ndo msingi wa Tanzania. Ulitaka Samia aende kinyume na misingi yenu alafu muanze kumnanga?!
Sikiliza video clip. Usitafsiri mambo kinyume cha maumbile. Labda tukufafanunulie maana ya kutofungamana na upande wowote katika siasa. Unavyoelewa wewe ni kwamba ukikuta mkeo anamtukana dada yako utakaa kimya kwa sababu hutaki kuonyesha unafungamana na upande wowote. Sasa huo ni ujinga sio kutofungamana
 
Hizo zote shobo.Mambo yao waachie wenyewe.

Badala ya kutumia fursa ya matajiri kuwa katika migogoro wenyewe kwa wenyewe ili nchi masikini ziamke kujitafuta, ndiyo kwanza tunazidi kufa njaa eti kisa matajiri wanapigana.

Ukishakuwa masikini uwezekano wa kuwa mpumbavu ni 90%.

Nipo busy na kutafuta ugali wangu sio kuingilia migogoro isiyonihusu.
Akili za mwafrika bhana, anyway hayakuhusu ila usije kulialia hapa kuhusu tozo na mafuta kupanda
 
Mimi nadhani kafanya vzr, sisi hatuegamii upande wowote,ndio Sera yetu kitambo.

Bado hatuna misuri katika nyanja nyingi mpaka tuwe na jeuri kuchagua upande.
Kifupi sisi ni omba omba so tunaogopa kuchagua upande maana tunataka kuomba kote.
 
Niliweka thread humu JF kwamba suala la Urusi na Ukraine ni dogo sana kwa mtu asie na ukahaba wa kisiasa wa kufuata bwana atakaekupa maslahi bila kujali utu wa mtu huyo.

Nilisema wazi, leo hii wakati tunamkumbuka Nyerere tutafakari angesimamia wapi katika suala la Urusi na Ukraine. Nyerere alisema siku zote mipaka ya nchi zetu inayotambulika kimataifa tunaweza tusiipende, lakini sio sababu za kuvamia nchi nyingine.

Hilo moja, pili ni kwamba, hatupaswi kuwa watumwa wa nchi fulani kwa sababu ya misaada yake, kwamba kwa kuwa tunasaidiwa au tulisaidiwa na nchi fulani, basi hiyo nchi inapofanya mambo kinyume cha maumbile tutakuwa upande wake. Huo ni umalaya wa kisiasa. Dhambi ni dhambi, ifanywe na rafiki au adui.

Angalia kura zilivyopigwa Umoja wa Mataifa juu ya suala la Urusi na Ukraine, na angalia Tanzania ilisimamia wapi. Aibu tupu kwa nchi iliyojiita nchi ya mstari wa mbele kwenye ukombozi wa nchi nyingine. Nasema wazi, tulichofanya hapa ni umalaya wa siasa za kimataifa

Katika hotuba ya mwisho ya Nyerere Umoja wa Mataifa, alisema hiki anachofanya Samia leo hatutafanya hata siku moja! Lakini ndio hivyo tena. Tunafanya. Samia ame-surrender our freedom and dignity. Angalia video hapo chini.

Nchi kama Zambia, Kenya, Rwanda nk wanajitambua sana

View attachment 2387354

Msimamo wa nchi za Afrika juu ya suala la Urusi na Ukraine ni jambo dogo sana linalopaswa kuongozwa na kanuni, sio maslahi ya nchi zetu

Marekani ni mbaya sana!! Naipongeza nchi yangu kutokuunga mkono azimio hilo!!
 
Ebu watuache Waafrika tuendelee na umaskini wetu!
Wamemuuwa Sekou Toure, Lumumba na kusaidia hata kuuwawa Sankara. Waafrika kimya!
NATO na washirika wake wakavamia Libya. Waafrika kimya. Wanahakikisha kufa na kupona DRC hakuna amani. Tupo kimya!
Hao binadamu ni katili akili za kinyama na ulafi na roho mbaya kuliko binadamu wote duniani.
Wacheni wauane....
 
Angalia kura zilivyopigwa Umoja wa Mataifa juu ya suala la Urusi na Ukraine, na angalia Tanzania ilisimamia wapi. Aibu tupu kwa nchi iliyojiita nchi ya mstari wa mbele kwenye ukombozi wa nchi nyingine. Nasema wazi, tulichofanya hapa ni umalaya wa siasa za kimataifa
Mkuu 'Synthesizer', unaweka tafsiri yako na kufanya hiyo tafsiri iwe ndiyo angesimamia Mwalimu Nyerere katika swala hili unalozungumzia hapa.

Hilo ndilo kosa kubwa unalofanya hapa.
 
Mkuu umesema kitu ambacho watu wengi hawajui. Warusi ni wabaguzi wabaya wa watu weusi hata kaburu hafai? Hebu google racist killings of blacks in Russia utaona wasivyo watu hawa!
Alaa, kumbe umeanzisha mada ukiwa tayari na upande unaolalia, na siyo kwa sababu ya maswala ya msimamo wa nchi?
Sasa unataka Tanzania kama nchi nayo ifuate hisia binafsi katika maswala ya kitaifa?
 
Mimi nazipongeza sana hizo nchi ambazo hazikupiga kura kuunga mkono au kupinga hiyo motion ya suala la vita vya Urusi vs Ukraine, pamoja na zilizopinga. Nazipongeza kwa sababu zimeonyesha ukakamavu mkubwa wa kuwaambia hao wababe wa dunia kwamba sisi siyo vikaragosi wao wa kuunga mkono kila uchafu wao.
Ingekuwa ni kuonyesha unafiki mkubwa wa kujali haki za binadamu kama Tanzania, na hizo nchi, zingepiga kura kuunga mkono hoja ya marekani na rafiki zake kuhusu Ukraine, wakati hao hao wamarekani wanaikalia Syria kinyume na matakwa yake. Hao wanaodai haki itendeke kwa Ukraine, walivamia Libya na kumuua Gaddafi bila kujali uhuru wa nchi na wananchi wake kujiamulia mambo yao.
Hao hao walivamia Iraq kwa kutumia sababu za UONGO wa wazi, bila kujari uhuru wa hiyo nchi!
Kama wanatambua uhuru wa nchi kuwepo na territorial integrity, basi walete motion za kukiri kuwa walikosea kwa waliyotenda huko Iraq, Libya, na wanayofanya sasa huko Syria. Watubu kuwa walikosea na walipe fidia kwa madhira waliyowatendea wananchi wa nchi hizo.
Haya mambo ya kunya anye kuku akinya bata kaharisha hayana nafasi ktk dunia ya leo. Enzi zile za ukoloni na ukoloni mamboleo yaliwezekana, lakini sasa hivi ktk dunia ya utandawazi hayana nafasi.
Hongera sana Tanzania kwa kusimia misingi halisi ya haki za binadamu, bila kujali kuwa wenye motion wanatupa misaada kiasi gani. Huo msimamo imara uliasisiwa na Baba wa taifa mwl Nyerere uendelee 💪🏽
 
Niliweka thread humu JF kwamba suala la Urusi na Ukraine ni dogo sana kwa mtu asie na ukahaba wa kisiasa wa kufuata bwana atakaekupa maslahi bila kujali utu wa mtu huyo.

Nilisema wazi, leo hii wakati tunamkumbuka Nyerere tutafakari angesimamia wapi katika suala la Urusi na Ukraine. Nyerere alisema siku zote mipaka ya nchi zetu inayotambulika kimataifa tunaweza tusiipende, lakini sio sababu za kuvamia nchi nyingine.

Hilo moja, pili ni kwamba, hatupaswi kuwa watumwa wa nchi fulani kwa sababu ya misaada yake, kwamba kwa kuwa tunasaidiwa au tulisaidiwa na nchi fulani, basi hiyo nchi inapofanya mambo kinyume cha maumbile tutakuwa upande wake. Huo ni umalaya wa kisiasa. Dhambi ni dhambi, ifanywe na rafiki au adui.

Angalia kura zilivyopigwa Umoja wa Mataifa juu ya suala la Urusi na Ukraine, na angalia Tanzania ilisimamia wapi. Aibu tupu kwa nchi iliyojiita nchi ya mstari wa mbele kwenye ukombozi wa nchi nyingine. Nasema wazi, tulichofanya hapa ni umalaya wa siasa za kimataifa

Katika hotuba ya mwisho ya Nyerere Umoja wa Mataifa, alisema hiki anachofanya Samia leo hatutafanya hata siku moja! Lakini ndio hivyo tena. Tunafanya. Samia ame-surrender our freedom and dignity. Angalia video hapo chini.

Nchi kama Zambia, Kenya, Rwanda nk wanajitambua sana

View attachment 2387354

Msimamo wa nchi za Afrika juu ya suala la Urusi na Ukraine ni jambo dogo sana linalopaswa kuongozwa na kanuni, sio maslahi ya nchi zetu


Kwanini nchi za kiafrika ziwe na umuhimu kama jambo linawafaidi tu wazungu na siyo vinginevyo?

UN haina nia njema na Afrika and it remains a tool for America and its allies to control other countries.

Of all the organisations, UN is the most bogus institution which must be either restructured or disbanded like yesterday.
 
Unamtukuza Nyerere lkn hujui philosophy zake. Nyerere ndo mwanzilishi na muumini wa "siasa za kutofungamana na uoande wowote" na huo ndo msingi wa Tanzania. Ulitaka Samia aende kinyume na misingi yenu alafu muanze kumnanga?!
Asante kwa kumsaidia. Maana Kuna watu wanakinbilua kuleta nyuzi humu wakati hawana ufahamu na wanacho andika
 
Niliweka thread humu JF kwamba suala la Urusi na Ukraine ni dogo sana kwa mtu asie na ukahaba wa kisiasa wa kufuata bwana atakaekupa maslahi bila kujali utu wa mtu huyo.

Nilisema wazi, leo hii wakati tunamkumbuka Nyerere tutafakari angesimamia wapi katika suala la Urusi na Ukraine. Nyerere alisema siku zote mipaka ya nchi zetu inayotambulika kimataifa tunaweza tusiipende, lakini sio sababu za kuvamia nchi nyingine.

Hilo moja, pili ni kwamba, hatupaswi kuwa watumwa wa nchi fulani kwa sababu ya misaada yake, kwamba kwa kuwa tunasaidiwa au tulisaidiwa na nchi fulani, basi hiyo nchi inapofanya mambo kinyume cha maumbile tutakuwa upande wake. Huo ni umalaya wa kisiasa. Dhambi ni dhambi, ifanywe na rafiki au adui.

Angalia kura zilivyopigwa Umoja wa Mataifa juu ya suala la Urusi na Ukraine, na angalia Tanzania ilisimamia wapi. Aibu tupu kwa nchi iliyojiita nchi ya mstari wa mbele kwenye ukombozi wa nchi nyingine. Nasema wazi, tulichofanya hapa ni umalaya wa siasa za kimataifa

Katika hotuba ya mwisho ya Nyerere Umoja wa Mataifa, alisema hiki anachofanya Samia leo hatutafanya hata siku moja! Lakini ndio hivyo tena. Tunafanya. Samia ame-surrender our freedom and dignity. Angalia video hapo chini.

Nchi kama Zambia, Kenya, Rwanda nk wanajitambua sana

View attachment 2387354

Msimamo wa nchi za Afrika juu ya suala la Urusi na Ukraine ni jambo dogo sana linalopaswa kuongozwa na kanuni, sio maslahi ya nchi zetu

Kama jambo hili ni dogo sana kama unavyoandika, kwa nini unalileta hapa. Si ulipotezee tu.
Tanzania bado ni nchi isiyofungamana na upande wowote, si lazima tufanye kama wao, wote ni wetu.
 
Kwanini nchi za kiafrika ziwe na umuhimu kama jambo linawafaidi tu wazungu na siyo vinginevyo?

UN haina nia njema na Afrika and it remains a tool for America and its allies to control other countries.

Of all the organisations, UN is the most bogus institution which must be either restructured or disbanded like yesterday.
Nazipongeza nchi ambnazo hazikwenda kabisa katika katika jumuiya hii ya Kimafya.
 
Hizo zote shobo.Mambo yao waachie wenyewe.

Badala ya kutumia fursa ya matajiri kuwa katika migogoro wenyewe kwa wenyewe ili nchi masikini ziamke kujitafuta, ndiyo kwanza tunazidi kufa njaa eti kisa matajiri wanapigana.

Ukishakuwa masikini uwezekano wa kuwa mpumbavu ni 90%.

Nipo busy na kutafuta ugali wangu sio kuingilia migogoro isiyonihusu.
Isiyo kuhusu???wakati ungumu wa maisha viongozi wako wanasingizia hivyo vita..au mafuta ya kupanda bei ni kwasababu ya wapinzani wa nchi hii..pathetic.

#MaendeleoHayanaChama
 
Mimi nazipongeza sana hizo nchi ambazo hazikupiga kura kuunga mkono au kupinga hiyo motion ya suala la vita vya Urusi vs Ukraine, pamoja na zilizopinga. Nazipongeza kwa sababu zimeonyesha ukakamavu mkubwa wa kuwaambia hao wababe wa dunia kwamba sisi siyo vikaragosi wao wa kuunga mkono kila uchafu wao.
Ingekuwa ni kuonyesha unafiki mkubwa wa kujali haki za binadamu kama Tanzania, na hizo nchi, zingepiga kura kuunga mkono hoja ya marekani na rafiki zake kuhusu Ukraine, wakati hao hao wamarekani wanaikalia Syria kinyume na matakwa yake. Hao wanaodai haki itendeke kwa Ukraine, walivamia Libya na kumuua Gaddafi bila kujali uhuru wa nchi na wananchi wake kujiamulia mambo yao.
Hao hao walivamia Iraq kwa kutumia sababu za UONGO wa wazi, bila kujari uhuru wa hiyo nchi!
Kama wanatambua uhuru wa nchi kuwepo na territorial integrity, basi walete motion za kukiri kuwa walikosea kwa waliyotenda huko Iraq, Libya, na wanayofanya sasa huko Syria. Watubu kuwa walikosea na walipe fidia kwa madhira waliyowatendea wananchi wa nchi hizo.
Haya mambo ya kunya anye kuku akinya bata kaharisha hayana nafasi ktk dunia ya leo. Enzi zile za ukoloni na ukoloni mamboleo yaliwezekana, lakini sasa hivi ktk dunia ya utandawazi hayana nafasi.
Hongera sana Tanzania kwa kusimia misingi halisi ya haki za binadamu, bila kujali kuwa wenye motion wanatupa misaada kiasi gani. Huo msimamo imara uliasisiwa na Baba wa taifa mwl Nyerere uendelee [emoji1434]
Sijui umeandika pumba gani..nam ni moja ya misimamo ya hovyo na ya kijinga.

Nikumbushe huyo jkn aliiunga mkono palestina zidi ya uvamizi wa Israel.

Pia huyo huyo jkn ndiye aliyekuwa mstari wa mbele kukomboa nchi zingize zidi ya ukoloni.

Kumbuka pia uvamizi wa libya etc tulikenua meno hiyo siyo nam ni unafiki na uoga kwasababu ya umasikini na ujinga waviongozi.

#MaendeleoHayanaChama
 
Kwanini nchi za kiafrika ziwe na umuhimu kama jambo linawafaidi tu wazungu na siyo vinginevyo?

UN haina nia njema na Afrika and it remains a tool for America and its allies to control other countries.

Of all the organisations, UN is the most bogus institution which must be either restructured or disbanded like yesterday.
Hiyo ni dua ya kuku.

#MaendeleoHayanaChama
 
Back
Top Bottom