Katika nchi 35 zilizokataa kupiga kura suala la Urusi kuvamia Ukraine 50% ni za Afrika, ikiwemo Tanzania

Cha kuchekesha utakuta hao hao tunarud na kuwaomba misaada Kama unataka uwe huku na huku kuwa tajir Kama China nazan bora wasingeenda kwenye hilo azimio
Wanatoa misaada maana wao wanachukua vingi sana kutoka kwetu !! There’s no free lunch !! Makampuni yao yanabeba madini kila kukicha !!
 
Wanatoa misaada maana wao wanachukua vingi sana kutoka kwetu !! There’s no free lunch !! Makampuni yao yanabeba madini kila kukicha !!
Na kuwa na msimamo haina maana watakunyima misaada. Nyerere alikuwa akiwatukana sana Marekani kwa matendo yao dhidi ya Kina Patrice Lumumba, Kwame Nkuruma nk, lakini haina maana Tanzania tulikuwa adui wa USA. Infact Nyerere na Kennedy walikuwa marafiki sana, japo walipingana katika mambo mengi, pamoja na suala la Afrika Kusini ya Makaburu.

Kwa hiyo kumwambia Putin unakosea kuivamia Ukraine hata kama hupendi wanachofanya sioni kwa nini liwe tatizo. Hivi kwa nini watu wanaona huwezi kumshauri rafiki yako anapompiga mkewe kila siku, au kuitelekeza familia yake? Watu wajue huo sio urafiki, ni unafiki, labda kwa kuwa kuna ofa za bia kila jioni.
 
Mkuu umesema kitu ambacho watu wengi hawajui. Warusi ni wabaguzi wabaya wa watu weusi hata kaburu hafai? Hebu google racist killings of blacks in Russia utaona wasivyo watu hawa!
Sasa mkuu, unapigania "rangi" au humanity? Mbona unayumba sasa!!! Hao blacks wanaouwawa Russia ni msimamo wa serikali ya huko au ni mauaji kama yale ya Marekani?
 
Sasa mkuu, unapigania "rangi" au humanity? Mbona unayumba sasa!!! Hao blacks wanaouwawa Russia ni msimamo wa serikali ya huko au ni mauaji kama yale ya Marekani?
Hujanielewa Mkuu. Nilisema hivi kwa watu wanaodhani Tanzania isipinge Urusi kuvamia Ukraine kwa kuwa Warusi ni rafiki zetu wakati Marekani ni wabaguzi wanaua weusi. Ndio nikasema kama hiyo ndio sababu wanayotumia then wajue Warusi ni wabaguzi dhidi ya weusi kuliko hata Marekani. Kuna mtu alisema humu ukiwa mweusi na uraia wa Urusi, hata kama unacheza soka zaidi ya Pele hawatakuweka timu ya Taifa. Hawataki ngozi nyeusi timu zao za taifa
 
Hatuna ubaya wowote na Russia ,kifupi hatutaki kuuziwa Adui,Adui wa wazungu hatakiwi kuwa Adui wa Kila Mtu,
After all Russia ni boss wetu wa zamani kabla Soviet union haijaharibika ,
Pia Russia hata historia yoyote ya kulitawala bara la Africa ,hatuna Sababu yoyote yenye mashiko

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Nyerere alikuwa hamuogopi mtu yeyote kumwambia ukweli!!
 
Nibora tukibaki non aligned!!
 
Watanzania wengi ni vilaza wa kutupwa panapo Geopolitics
 
Kama hii statement ni kweli basi mhhh hatari sana
 
Unaona unavyojichanganya? hatupigi kura kwa sababu hatutaki kuuziwa adui. Kura haikuwa juu ya kuwa adui au rafiki wa Urusi. Kura ilikuwa ni kwa ajili ya "border integrity", kwamba, kitendo cha Urusi kuvamia ndani ya mipaka ya Ukraine na kumega sehemu ya Ukraine ni sahihi au sio sahihi kufanywa na Urusi?

Sasa ukikaa kimya ni kwamba huna akili ya kuamua jambo ndogo kama hilo, au unaogopa kumuudhi bwana wako. Ndio maana nikaita umalaya wa kisiasa
 
Na unadhani hilo ndio lingetufanya tuwapinge Urusi? Bado tungekuwa wapumbavu kama tungetumia hilo kuwa sababu
 
Watanzania wengi ni vilaza wa kutupwa panapo Geopolitics
Yaani hawajui politics kiujumla, hata local politics tu, 80% ni mbumbumbu kwenye hayo masuala

Ukisoma facebook huko watu walivyoamini zile propaganda za jiwe ndio utajua
Labda mpira wa miguu ndio utawakuta wamekariri hadi pasi alizopiga Messi PSG
 
Shida si akili ,ni kura ambayo Haina manufaa yoyote ,upige usipige Attitude ya mzungu kuhusu wewe haibadiliki,

Yaani Kwa kifupi si jambo la manufaa kuonekana una akili Kwa mzungu , Kuna mambo ya msingi ya kushughulika nayo siyo hizo petition za kipuuzi

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Nasimama na nchi yangu katika hili. Ukraine anajizima data! Kazi ya mjinga ni kuumia.
 
Angalau wewe ndiye niliyekuelewa.
 
Nimeuliza hapo juu, wewe unaweza kuwa na alignment kati ya dada zako wawili?

Sasa ukikuta mmoja wao anampiga mwenzie na kumuumiza akidai kamkosea kwa kufanya urafiki na adui yake, utakaa kimya kwa kuwa huna alignment?
Lazima useme ukweli kwamba wewe fulani umekosea sana kufanya uliyoyafanya !!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…