[emoji1787][emoji1787]Ujue Nimesoma Sana Huu Uzi Ila Maswali Yako Sijaona Yakijibiwa Hata Moja Alafu Unawapa Vitu Original Kutoka katika kitabu Chao. Yamebaki kurudia rudia tu Porojo Ambazo Hazieleweki..
MAJIBU HAYA HAPA YA MASWALI YAO..[emoji116] SITUMII KITABU CHANGU KWAKUA HAWAKIAMINI.
Mmoja Anasema Muhammad SAW Amefundisha Waislam kupiga Wanawake. Hili Sioni Umuhimu Wa Kulielezea Sana Kwasababu Ni Porojo tu ila Embu Tuangalie Tu Hapa Tanzania Ni Watu Gani Wanaongoza Kupiga Wake Zao Tuangalie Na Matukio Ya Wake Kunyanyasika Ni Watu Gani Wanaongoza.. Kama Waislam Wamefundishwa Hivyo Katika Dini Yao Kwanini Wapo nyuma kuliko Hawa Waliofundishwa Kuwatunza na kutowapiga Hili Ni Jibu Tu Kuwa Ameokota Mafundisho Ambayo Sio Sahihi.. Alafu Mbona Mapenzi Yanasifika Zaidi Pwani Ambapo Asilimia 90 Ni Waislam [emoji12] Ilihali Wanafundishwa Na Kiongozi Wao Kupiga Wake Zao...
Anasema Tena Kuhusu Ndoa Ya Mut'ta Huyu Sijui Ni Mkristo Kweli Msomi au Ni Mjinga Mjinga tu wa kucopy na Kupaste Mtandaoni Okay Nakupa Kingine Copy Ukapaste. Hata Pombe Katika Uislam Ilikuwa Halali Na Watu Walikuwa Waipiga Haswaa...
Ipo Hivi Mwenyezi Mungu Vitu Vyote Ameviweka kwa taratibu maalum Kutokana na alivyomuumba Mwanaadamu. Anapotuma Mtume au nabii Huwa Haji Moja kwa Moja Kuwabadilisha Watu kwa Mara Moja Bali huwapa Somo Taratibu Kama alivyofanya Yesu Kuwa na Wanafunzi Ili Wajifunze nao Wawafunze wengine hii haimaaanishi Mungu alishindwa kuweka uelewa Moja Kwa Moja kwa wanadaamu Bali Ni taratibu ambazo aliweka Mwenyewe kwakua Hapangiwi Bali anafanya anachopenda Yeye.
Mfano Tukija Katika Biblia Kuna agano la kale Na Agano Jipya Katika Biblia hizi yapo mambo Mengi yanapingana Sana Mfano Uharamu wa Nguruwe na Hata Swala La Kuoa Zaidi ya Mke Mmoja nk.. Katika ufafanuzi wake Kwanini imekuwa hivyo Mafundisho yanasema Imekuwa hivyo kwasababu mwanzo Jambo Hilo lilikuwa Halali Kisha baadae MUNGU akalifanya likawa Haram. Na ndivyo pia ilivyo katika Uislam Kuna Mambo yalikuwa Halali mwanzo Kisha baadae yakawa haramu Mfano Swala la Mut'ta na pombe yalikuwa Halali Kisha baadae yakawa Haram. Kama unaona Ni ajabu kuwa hivyo Basi Anza kuona Ajabu katika Biblia Yako Kwanza..
Jambo Jingine Anasema Kuhusu Uislam Unadai Mwanamke Anyonyeshe Mtu Mzima Na Ushahidi Anasema Mama Aisha Alisema Kuwa Umeliwa Na Mbuzi Huu Ni Upotoshaji Wa Makusudi.. Sawa Kama Umeliwa Na Mbuzi Basi kukosekana kwa Ushahidi Ndio kushinda Kesi ukitaka tuendelee na hii mada lete Hizo Aya Hapa au ukitaka tuendelee bila ushahidi Nipe Kwanza injili ya Yuda Kwakua Vipande Vidogo Vilivyookotwa Vimeonyesha kuwa Ndio ilikuwa inazungumzia ujio Wa Mtume Muhammad SAW Au Yuda Hakuwa Katika Wanafunzi Wa Yesu..? Mbona injili yake Haipo...? Ipo Wapi..? Ilipotea Vipi..?
Mwingine akasema kuhusu Mussa Kudhalilishwa Na ALLAH kwakua alitembea Uchi. Kwani Mungu wa tatu Mkuu Wa Biblia akipomtuma mwanae wa pekee Kisha akamuacha akalia kumuomba Msaada mpaka machozi ya Damu yakatoka na hakumsaidia kisha akapigwa mpaka kuuliwa pamoja na kuwekwa msalabani sehemu ambayo walikuwa wanawekwa watu waovu kabisa Tena akiwa na nguo ambayo sio ya kumsitiri Ivi huku sio kumdhalilisha..? Ukipata Jibu La hiyo Basi Utapata jibu la Mussa Usituchoshe..
Mmoja pia Amesema ALLAH amebariki Dhambi tofauti na Mungu wa Biblia Ambae Ametoa Adhabu. Okay Sawa Tusiende Mbali Tuanze Kwako Wewe Unamtukuza Mungu Wa Biblia asietaka Dhambi katika post zako Nimesoma matusi makubwa makubwa umeandika mengine hata kuyasoma naishia nusu. Naamini Wewe Ni Mwalim Mzuri wa Biblia naamini maisha yako yanaishi kwa nguzo za Biblia na hapa unatufundisha Biblia so hayo bila shaka ndio Mafundisho ya Biblia thanks you Tumejifunza Biblia[emoji7][emoji7]..
Kuna Mmoja Amesema Yesu Kwa Kiarabu Anaitwa Yoshua akasema Nenda YouTube kasearch Arabic Gospel.. Vizuri kwa kujua Hilo. Ila Huyu jamaa katika Comments Zake amekuwa akitukana Sana jina ALLAH Ila Anampenda MUNGU na JEHOVA Sasa Mbona hujatuambia kuwa Biblia za kiarabu zimeandikwa ALLAH Sehemu Zote Za Mungu Au Jehova..? Au Hilo hujui..? Basi Nenda kafatilia baada ya kusikiliza Arabic Gospel. Sawa Dogo [emoji12] Usipende Tu Kukata Mauno..
Mwingine Kasema Muhammad SAW Ametoa Visa Katika Biblia [emoji1787][emoji1787] Hii Atasema Kichaa Tu Yani Hii Biblia Unaijua Kweli Historia Yake au umekurupuka Tu. Hii Biblia ya juzi Muhammad SAW atoe visa Humo[emoji15][emoji23] Kasome Kwanza Uijue Biblia ndio Tuendelee na hiyo Mada..
Akasema Qur'an Ni Mashairi Yasiyojitosheleza. Mfano Akatoa Kuhusu Jua kuzama katika matope. [emoji848] Bahati Mbaya ameona Hiyo Tu Labda Nikuambie pia huu Mfumo wa Uliosoma Shule Historia ya Mtoto kukua Tumboni kwa miezi Tisa wote upo katika Qur'an Miaka zaidi ya Elfu moja iliyopita na leo unathibitishwa kwa vyombo Vya kisayansi Tena inaonyesha vile vile bila makosa Fatilia Hilo Utajifunza kitu kuhusu hii Qur'an [emoji120].. Alafu Nipe Kitu Kimoja Tu Katika Biblia mfano wa hicho Tukiacha Ile Aibu kuhusu Sungura kucheua.. Nenda Alafu Uje Hapa..
Anyway Mimi Siwaiti Makafiri Ila Kiukweli Mpo na Ukafiri Mwingi kwakua mnapinga kitu huku mnajua Ukweli.. Alafu Huyo Ni Mtu Mmoja Tu Anatumia ID Mbili ajitekenya na kucheka Mwenyewe kwakua hakuna wa kumsapoti upuuzi Wake Huo..
Sent from my TECNO CC6 using
JamiiForums mobile app