Kauli ya CDF mstaafu kuhusu waliotaka kupindisha katiba ili Rais Samia asiapishwe inanipa picha halisi ya kwanini Bashiru na wenzake walitenguliwa

Kauli ya CDF mstaafu kuhusu waliotaka kupindisha katiba ili Rais Samia asiapishwe inanipa picha halisi ya kwanini Bashiru na wenzake walitenguliwa

Bashiru huyu aliyerudisha mali za CCM zilizowashinda vigogo wa chama asingekubali kutoa bure rasilimali za nchi. Wala Bashiru sio kilaza, hata kama humpendi utakubaliana na hilo.

Bashiru sio mtu wa kulalamika na kukosa maamuzi au asijue la kufanya. Wala asingesuasua kuendeleza miradi kama bwawa lingekuwa linazalisha umeme muda.

Hata Majaliwa angekuwa nafuu ya sasa. Yani mkuu wa usalama, PM, KM hawakukosea kwa pamoja kuwa na wasiwasi na huyu "kwa kudra za mwenyezi Mungu"
#Weak points,
Katiba ndio Muongozo wetu,mlipo mchagua Mama awe makamu wa Raisi hamkuwa na wasiwasi hawezi, yaliyo tokea yametokea Uraisi ni Taasisi , hizo kenge zilizo taka kupindisha Katiba ningekuwa mshauri wa mama wote kwenye system wangekuwa nje wanacheza na vijukuu nyumbani,Tuheshimu Katiba yetu hayo hawezi au ana weza mkenjipanga kabla ya kumpa Umakamo wa Raisi.
 
Mim naona lawama apewe magufuli tu maana yeye ndio alimchagua awe mgombea mwenza.
 
Mabeyo kwenye hii ishu alitumika tu sidhani kama he saw what was coming, Mabeyo ni pro Magufuli na ndio maana baada ya mwaka tu alipoona mambo yanaanza kuenda mrama, akatangaza kustaafu bila sababu za msingi

Ni wazi pro Magufulis kina Bashiru and co hawakumtaka Mama, maana since day one alishaonesha dalili kuwa ni pandikizi la Godfather ndio maana walitaka kupindisha katiba, ila Godfather akaingilia kati akaamua kumtumia Mabeyo hapo

Akamuambia kwamba waambie hao kina Bashiru and co kuwa tumeshitukia mchezo wao, hivyo waambie wamuapishe huyo Mama haraka iwezekanavyo, kwahiyo ni kama Godfather alitumia advantage ya katiba kwa maslahi yake na genge lake
Mabeyo alitangaza tu kustaafu bila sababu za msingi? Seriously? Are you that ignorant?

Hujui kuwa jeshini ma CDF hustaafu kwa mujibu wa sheria muda wao ukifika?

Kwani Davis Mwamunyange na Robert Mbona walistaafu kwa sababu gani za msingi? By the way, hao nao walikuwa ma CDF.

Goodness gracious 🤣.
 
Mabeyo alitangaza tu kustaafu bila sababu za msingi? Seriously? Are you that ignorant?

Hujui kuwa jeshini ma CDF hustaafu kwa mujibu wa sheria muda wao ukifika?

Kwani Davis Mwamunyange na Robert Mbona walistaafu kwa sababu gani za msingi? By the way, hao nao walikuwa ma CDF.

Goodness gracious [emoji1787].

Nawafahamu CDFs wote mkuu ila kustaafu kwa Mabeyo kuliibua maswali kadhaa kwa waliokuwa wanajua kinachoendelea, ila mwisho wa siku Jibu likawa tu "amestaafu kwa mujibu wa sheria", na wengi kama wewe waliamini kuwa kweli Mabeyo alistaafu kwa mujibu wa sheria, hivyo nilitegemea comment kama hii wala sishangai, ila acha ibaki hivyo hivyo mkuu
 
..Mabeyo anastahili lawama.

..Kwanini MAKAMU WA RAIS hakuwa mtu wa kwanza kupewa taarifa kuwa Rais amefariki?

..Nimemsikia Mabeyo akisema eti kulikuwa na mjadala wa nani atangaze kifo cha Rais.

..Hivi Mabeyo na usomi wake, kutumikia jeshini kwa miongo kadhaa, na kutembelea nchi mbalimbali, hajui nani ana mamlaka ya kutangaza kifo cha Raisi? Kwamba walihitaji majadiliano?
Yale mahojiano pengine yamefanywa kwa wema ila yameniacha na maswali mengi sana juu ya uongozi wa nchi yetu na hatma ya Katiba yetu.

Ina maana wakati wote wa ugonjwa hadi rais hawezi tena kuongea, nani alikuwa anaongoza nchi?
 
Ni ajabu sana kwamba siku za mwisho hadi Pombe anazidiwa kiasi hicho, VP alifichwa sinema nzima. Ningetegemea awe na taarifa kuhusu maendeleo ya matibabu ya boss wake. Kwa nini wamfiche mtu ambae kikatiba alitakiwa kuchukua madaraka baada ya Pombe kuzima?
Wataka kusema Sa100 alikwenda Tanga na kukaa kule bila kufahamu kinoendelea?
 
Yale mahojiano pengine yamefanywa kwa wema ila yameniacha na maswali mengi sana juu ya uongozi wa nchi yetu na hatma ya Katiba yetu.

Ina maana wakati wote wa ugonjwa hadi rais hawezi tena kuongea, nani alikuwa anaongoza nchi?
Sikiliza tena alokisema Mabeyo ametumia misamiati kadhaa kukujulisha ni nani walikuwa wasimamizi wa shughuli nzima.

Yeye alibaki kama mtazamaji au tuseme mwamuzi wa mpira au VAR.
 
Nawafahamu CDFs wote mkuu ila kustaafu kwa Mabeyo kuliibua maswali kadhaa kwa waliokuwa wanajua kinachoendelea, ila mwisho wa siku jibu likawa tu "amestaafu kwa mujibu wa sheria", na wengi kama wewe waliamini kuwa kweli Mabeyo alistaafu kwa mujibu wa sheria, hivyo nilitegemea comment kama hii wala sishangai, ila acha ibaki hivyo hivyo tu mkuu
Umesema alistaafu bila sababu za msingi. Sawa….sababu za msingi za CDF kustaafu ni zipi?

David Musuguri, Ernest Kiaro, Robert Mboma, George Waitara, na Davis Mwamunyange walistaafu kwa ‘sababu’ gani ‘za msingi’ zilizo tofauti na sababu za Mabeyo kustaafu?

Nataka tu kujua hizo sababu za msingi kwa lengo la kujifunza. Nitashukuru ukinifahamisha maana yawezekana mimi sizijui. Napenda kujifunza mambo mapya.
 
Kama nchi, tujitafakari sana namna ya kupata Makamu wa Rais.
Nimewahi kusema tena humu, kwasababu ya ubinafsi wa watu wanaoteuliwa kugombea urais hasa ndani ya CCM, huwa wamekuwa na utaratibu wa kuteua wagombea wenza wenye ushawishi mdogo ndani ya chama na hata kwa wananchi.

Kwa lugha nyepesi ni kwamba, marais wamekuwa wakipenda makamu wa rais ambao hawawezi kuwafunika. Si unaona hata Rais wa sasa alimteua mtu gani kuwa makamu wake?

Upatikanaji wa makamu wa rais unapaswa kuzingatia kwamba, huyu mtu muda wowote anaweza kuwa Rais wa nchi!
 
#Weak points,
Katiba ndio Muongozo wetu,mlipo mchagua Mama awe makamu wa Raisi hamkuwa na wasiwasi hawezi, yaliyo tokea yametokea Uraisi ni Taasisi , hizo kenge zilizo taka kupindisha Katiba ningekuwa mshauri wa mama wote kwenye system wangekuwa nje wanacheza na vijukuu nyumbani,Tuheshimu Katiba yetu hayo hawezi au ana weza mkenjipanga kabla ya kumpa Umakamo wa Raisi.
Ww ndio umetoa most weak point
 
Nimewahi kusema tena humu, kwasababu ya ubinafsi wa watu wanaoteuliwa kugombea urais hasa ndani ya CCM, huwa wamekuwa na utaratibu wa kuteua wagombea wenza wenye ushawishi mdogo ndani ya chama na hata kwa wananchi.

Kwa lugha nyepesi ni kwamba, marais wamekuwa wakipenda makamu wa rais ambao hawawezi kuwafunika. Si unaona hata Rais wa sasa alimteua mtu gani kuwa makamu wake?

Upatikanaji wa makamu wa rais unapaswa kuzingatia kwamba, huyu mtu muda wowote anaweza kuwa Rais wa nchi!
Lakini umesahau JPM alisema yeye alimtaka nani awe makamu ( na sio Sa100) wake na alisema hiyo ilikuwa ni siri ila msukuma akaisema hadharani.
 
Sikiliza tena alokisema Mabeyo ametumia misamiati kadhaa kukujulisha ni nani walikuwa wasimamizi wa shughuli nzima.

Yeye alibaki kama mtazamaji au tuseme mwamuzi wa mpira au VAR.
Mkuu, nimefuatilia labda kama kuna kipanda nimekosa unisaidie kufafanua.

Kama tunafuata Katiba, Makamu wa rais ni mtu wa pili kimamlaka katika nchi yetu. Rais anapokuwa mgonjwa, usukani anatakiwa kuwa nao makamu wa rais mpaka rais akae sawa na aweze kutekeleza majukumu yake. Wakati wote wa matibabu, wanaomtibu Rais wanapaswa kutoa taarifa na maendeleo ya afya yake kwa Makamu wa rais kama mtu wa pili kimamlaka katika nchi.

Itoshe tu kusema, simulizi yote ya Rtd CDF wetu imenijuza nisichojua mimi Mfugaji wa huku kijijini kando kando ya Tanzania!
 
..swali langu ni kwanini Mabeyo hakuwa akimpa taarifa Makamu wa Raisi / Kaimu Raisi.

..kwanini aliwataarifu Waziri Mkuu na Katibu Mkuu kiongozi kabla ya Makamu wa Rais ambaye kwa hali ya kiafya ya Rais alikuwa / alipaswa kuwa KAIMU RAISI?

..Suala la maradhi na kuugua kwa Raisi Magufuli ilikuwa ni jambo linalotakiwa kusimamiwa na Makamu wake.
Mkuu kama labda hujawahi kufanya kazi kwenye taasisi yeyote..!!lakini katika watu 3 viongozi lazima wawili watajikata na kuwa wasiri na kumtenga 1...na ndo ilivyokuwa kwa jpm...MAMA hakuwahi kuaminiwa hata siku moja
 
Back
Top Bottom