Kauli ya Chongolo ni ufedhuli kwa wasomi wa vyuo vikuu. Ipingwe!

Kauli ya Chongolo ni ufedhuli kwa wasomi wa vyuo vikuu. Ipingwe!

Ukiondoa madokta, manesi na walimu.. Mliobaki wote inabidi muende veta kilazim
Wale waliopewa boom la Serikali ndio walazimishwe na wakienda VETA muwape tena boom lingine, sisi wengine tumelipiwa na wazazi wetu hatujagusa hata Senti ya boom la Serikali, tusipangiane
 
Aseme wazi hakuna haja ya vijana kwenda vyuo vikuu kwanza baada ya kumaliza sekondari. Yani wakimaliza tu kidato cha nne wote waende VETA kwanza au pia badala ya kwenda kuruka kwata JKT wale vijana wa kidato cha sita waende VETA ndipo wajiunge na vyuo vikuu.
VETA iko poa sana, wahitimu wengi wa vyuo vikuu hawana maarifa, Ukimuintavyu mtu wa chuo kikuu unaweza kulia. Wengi hawajui hata wamesoma fani fulani ili iweje..
 
Wewe mpika vitumbua uliyehitimu veta usijpe faraja kwa kauli ya Chongolo.

Masomo ya vyuo vikuu hayakupswa kutolewa kama mahubiri ya Mwamposa. Yalipswa kuambatana na vitendo kwa wingi. CCM imefanya siasa ktk elimu ya juu badala kufanya uwekezaji mkubwa utakaowezesha wanafunzi kusoma kwa vitendo
Mimi mpika vitumbua niliyehitimu veta sijipi faraja kwa kauli ya chongolo, nina mbinu zangu nyingine za kujipa faraja.

Tunatoa ushauri kwa manufaa yenu nyie wahitimu wa vyuo vikuu, maana nyie hata kupika vitumbua kama mimi hamuwezi, mnaishia kulalama tu mkiwa hamjui cha kufanya.
 
Punguza uongo, huko VETA wanafundishwa na walimu waliotoka vyuo vikuu, nani Bora hapo, acheni kudhalilisha vyuo vikuu kwa kuvilinganisha na VETA.
Tunalinganisha wanafunzi wa VETA na wale wa vyuo vikuu, siyo walimu!
 
Mimi ningeshauri serikali kwa vile vyuo vyetu vingi havina sehemu za kufanyia tafiti (research centers) basi watu waliokaa kwenye kazi (field) kwa muda mrefu sana ndo warusishwe vyuoni wakafundishe siyo mtu amebakishwa tutorial..within 5years tayari ni lecture kisa amechukua masters na phd tayari. mfano. Akina Kibatara and likes wakatoe elimu ya sheria huko chuo kikuu..

Wale wataalam wanaotengeneza mitambo ya gesi pale kinyerezi na waotengeneza and the likes wakafundishe chuo kikuu.

Wale wahasibu wabobezi warudi wakafundishe.
Wale wataalam wa mabarabara na ujenzi walioko kwenye field muda mrefu wakafundishe.

Wale miners wabobezi kule GGM na Nyamongo warudishwe wakafundishe...

Tuachaneni na Hao wahadhiri ambao vichwa vyao vimeota kutu na hawafanyi vitu kwa vitendo kwasababu hawaoni vitu katika uhalisia...tuchukue watu waliopo kwenye field. Haiwezekani mwanafunzi amemaliza chuo lakini akipewa mtihani kwa vitendo anaonekana kichekesho..
Hivi wewe hilo apingwe umelikariri ee, Chongolo amewaweza team porn stars, Vyuo vikuu tabu sana na bado!!

Mengi mabaya nimejifunzia chuoni, chuo kilifundisha kuwa katili ila mvivu kwenye kazi
 
Tukubali chongolo kaongea ujinga, mtu amalize engineering umwambie arudi VETA. Hao wa VETA wanafundishwa na walimu ambao ni graduates wa chuo kikuu.
Ukitaka ujue kwamba hujui, wape kazi, kijana wa veta na wa chuo kikuu halafu ukae pembeni uangalie, nakwambia utastaajabu ya kenge kuota mapembe!
 
Tofautisha quality ya mwanafunzi na qualification ya lecturer. Huwezi kuwa lecturer bila vigezo vya TCU. Lakini quality ya wanafunzi inaanzia mbali.
Hata lecturers wetu nao quality zao ni hizo hizo za mashaka. Kuna mahali nimeandika kuwa miaka ya nyuma ya 80 lecturers and profs at UDSM sikuwahi kuwaona wanakuja na karata lecture Hall! Walikuwa na knowledge kichwani, wanajua wanavyopashwa kujua.
 
Hatari na nusu basi vyuo vifungwe watu waende veta wakimaliza la 7
Veta haiwezi kuwa na ufanisi wakati sheria zimekaa hovyohovyo, wenzetu hata kuchinja kuku mpaka uwe umesomea na una kibali, sisi kujenga unamxhukua kijana yoyote pasipokujua alisomea wapi na jengo linasimama.
 
Huyo Chongolo angesema hivyo wazi, sio kusubiria watu wamemaliza vyuo vikuu wakiwa kwenye madeni makubwa ya mkopo halafu anasema hatuwezi kuwapa ajira wa vyuo vikuu badala yake warudi kusoma VETA.
Hakukuwa na haja ya mlolongo mrefu wa kidato cha sita na chuo kikuu na gharama za fedha baada ya kumaliza kidato cha nne wakati mpango mzima na suluhu la matatizo ni VETA.
Yuko sahihi, zimpo nchi mtoto anapomaliza form six anaingia college miaka 2 baada ya hapo ndo anaingia university lkn wetu anatoka six anaingia uni
 
Tuandamane na kumtaka aachie vyeo anavyoshikiria mana inaoneka hafai kwa kutaka kuhalalisha haramu kuwa halali
 
Ni wakati Sasa wa kuunda chama Cha siasa chenye sera nzuri kwa vijana na ajira , CCM mpaka Sasa wamefeli, Chadema nao ni dust , ACT ni wafuata upepo,
 
Law school ni post graduate diploma.
Does it make any difference in your opinion? Yaani ni kosa kuwa na degree ya political science halafu ukaenda VETA ukapata certificate ya plumbing?
 
Back
Top Bottom