Kauli ya Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma ni vema ikajadiliwa' ni kuhusu Mitandao ya Kijamii

Kauli ya Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma ni vema ikajadiliwa' ni kuhusu Mitandao ya Kijamii

MwanaHalisi Digital imemnukuu Jaji Mkuu wa Tanzania akikemea vikali tabia ya baadhi ya watu wakiwemo wanasheria ya kumkosoa Jaji au mwanasheria wa upande mwingine kiasi cha kumtaja kwa jina na picha yake , na wakati mwingine kutaja hadi mahali anakokaa .

Amekwenda mbali hadi kufikia kusema , wote wanaofanya hivyo wanafahamika na kwamba siku zao zimekwisha .


View attachment 2039314




Hii ni kauli kali mno kutolewa na Jaji Mkuu , ambayo bila shaka imechagizwa na jazba , mimi nilidhani Mh Jaji Mkuu angejaribu kuangalia kufuatilia kisa cha majaji kushutumiwa mitandaoni badala ya kuwapiga mikwara watoa shutuma
Kwani jaji yeye ni nani mpaka asisemwe vibaya mitandaoni?

Mbona majaji walipokuwa wakisemwa vizuri mitandaoni hakuja kukemea hiyo hali?

Ni lini kumtaja jaji jina mitandaoni, kuonyesha picha yake au kutaja mahali anapoishi kulikuwa ni kosa?

Kwani maisha ya majaji ni siri zisizopaswa kusemwa hadharani?

Wanasheria wa upande wa pili ni wakina nani hao, maana kikawaida mahakamani kuna wanasheria wa pande mbili zinazokinzana, sasa ukimtaja mwanasheria yoyote maana yake umetaja upande upi?
 
Huyu mzee anatakiwa afungwe kabisa

Ana ulinzi wa uhakika kwa sasa kwakuwa anasimamia uovu kwa maagizo ya watawala. Hivyo anatoa vitisho kwa wataka haki ili udhaifu wa Muhimili anaousimamia usiendelee kupuuzwa. Hapo alipo ana hukumu ya rais dhidi ya Mbowe, hivyo anaweka vitisho ili watu waogope siku hukumu ya kihuni ikitoka.
 
Wananchi na binadamu kwa ujumla hujua haki ilipo kwa asilimia kubwa bila hata kusoma sheria.
Majaji au mahakimu wakitoa haki hawashambuliwi. Mashabulizi huanza pale ambapo Imani ya haki inapokosekana.
Majaji wanatakiwa wasisitize kuwa watatoa haki na ionekane kuwa imetendeka.
 
Ana ulinzi wa uhakika kwa sasa kwakuwa anasimamia uovu kwa maagizo vya watawala. Hivyo anatoa vitisho kwa wataka haki ili udhaifu wa Muhimili anaousimamia usiendelee kupuuzwa. Hapo alipo ana hukumu ya rais dhidi ya Mbowe, hivyo anaweka vitisho ili watu waogope siku hukumu ya kihuni ikitoka.
Tutamalizana naye hata kwa waganga wa kienyeji
 
MwanaHalisi Digital imemnukuu Jaji Mkuu wa Tanzania akikemea vikali tabia ya baadhi ya watu wakiwemo wanasheria ya kumkosoa Jaji au mwanasheria wa upande mwingine kiasi cha kumtaja kwa jina na picha yake, na wakati mwingine kutaja hadi mahali anakokaa.
Kwa hii kauli ya jaji hivi punde mtaanza kusikia tena watu wasiojulikana
 
J

Jaji Mkuu yuko SAWA, hao WANAWASHAMBULIA hivyo na yeye anayo haki ya KUWASHAMBULIA kwa mkwara mzito na hata ikibidi KWA VITENDO. Kama wana hoja waende huko kwenye mfumo wao wa Mahakama waitafute haki yao. Siyo kufanya mambo kama watu ambao hawakusoma.
Kwani huyo Jaji Mkuu wapi yeye kama yeye kaonyesha kasoma na sisi raia tukaona Taaluma kwenye matendo yake??? Asiwatishe watu wazima kama yeye kama vile school's Kids.
 
Yaap nimeona nchi ya jirani hapo kwa uhuru nyeusi inaitwa nyeusi nadhani jaji anapaswa kuwanyoshea vidole hao majaji wake kwanza bahati nzuri hii kesi ya mchongo inawaaibisha mno
Una uhakika hawanyooshei kwa utaratibu rasmi? Hiyo ni mahakama mzee, hakuna kukosoana kwa style za Mtaka na Ummy hadi umma usikie. Unaweza kumkosoa mtu bila kumdhalilisha.
 
Kulingana na maadili ya uwakili hutakiwi kwenda kumshambulia Jaji kwenye mitandao au sehemu yoyote ile. Kama ametoa uamuzi ambao hujaupenda au amekufanyia kitu chochote ambacho hakipo sawa kuna sehemu za kupeleka malalamiko yako na siyo kwenye mitandao.

Kiukweli naona Jaji mkuu wetu yupo sahihi kabisa kuhusu mambo yanayofanywa na baadhi ya Mawakili. Naomba tu Jaji mkuu aendelee kuwashughulikia mawakili wote wanaoenda kinyume na maadili yao.
 
MwanaHalisi Digital imemnukuu Jaji Mkuu wa Tanzania akikemea vikali tabia ya baadhi ya watu wakiwemo wanasheria ya kumkosoa Jaji au mwanasheria wa upande mwingine kiasi cha kumtaja kwa jina na picha yake, na wakati mwingine kutaja hadi mahali anakokaa.

Amekwenda mbali hadi kufikia kusema , wote wanaofanya hivyo wanafahamika na kwamba siku zao zimekwisha.

Hii ni kauli kali mno kutolewa na Jaji Mkuu, ambayo bila shaka imechagizwa na jazba, mimi nilidhani Mh Jaji Mkuu angejaribu kuangalia kufuatilia kisa cha majaji kushutumiwa mitandaoni badala ya kuwapiga mikwara watoa shutuma

View attachment 2039314
Anaposema siku zao zimekwisha ana maana watawapiga risasi kama walivyofanya kwa Tundu Lissu?

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom