Kauli ya Jaji Tiganga kwamba huenda Shahidi Ling'wenya alikuwa anapewa majibu ya maswali aliyoulizwa yawaibua Wadau

Kauli ya Jaji Tiganga kwamba huenda Shahidi Ling'wenya alikuwa anapewa majibu ya maswali aliyoulizwa yawaibua Wadau

hili la bwn Shahidi kuomba hizo documents ni pigo la kustukiza ambalo hakujipanga nalo ndio maana Wakili wa serikali amaamua kutoa hoja kwa maelezo marefu kupoteza muda halafu mwisho anaomba HAIRISHO😄 ili waende kujipanga na kuskilizia maagizo toka muhimili uliojichimbia kwenye mihimili mingine utoe maelekezo kwa jaji akubali pingamizi
Hii imenionyesha namna gani mawakili wa utetezi walivyo smart na kuwa mbele ya muda 😄😄 ngoja tuongeze popcorns zaidi tuendelee kuangalia mwisho unakuaje
Halafu kuna kitu kimoja kimefanyika maksudi, leo ilikuwa mashtaka waje na shahidi, wakabadilikia kizimbani na kutaka utetezi waanze ili kuwashtukiza kwamba wawe hajajipanga, lakini jamaa wako smart, wamepeleka 'faya' hivyohivyo pamoja na kushtukizwa!
 
Halafu kuna kitu kimoja kimefanyika maksudi, leo ilikuwa mashtaka waje na shahidi, wakabadilikia kizimbani na kutaka utetezi waanze ili kuwashtukiza kwamba wawe hajajipanga, lakini jamaa wako smart, wamepeleka 'faya' hivyohivyo pamoja na kushtukizwa!
ukiwa umesimama kwenye ukweli inakua rahisi sana huna haja ya kujipanga maana licha ya kustukiza kwa kufunga ushahidi pia walikuja kwa kuchelewa sana lakini bado wakapigwa na kitu kwenye medula 🤣🤣
 
Hivi Lissu aliwahi kusemaje khs Majaji wa bongo.
2012 au 2013 wakati akitable hotuba ya makadirio ya bajeti kivuli ya Wizara ya katiba na sheria Lissu aliibua mazito juu ya teuzi za majaji na uwezo wao.

Nakumbuka hotuba hiyo mpaka iliibua tetesi za kuwepo kwa jaji mmoja kuwa hakuwa na LLB alikuwa na Diploma. Kuna jaji mwingine alitajwa kuwa toka ateuliwe hakuwahi kuandika wala kusoma hukumu mana hakuwa na uwezo wa kuandika kimombo. Ni madudu mengi yaliibuka juu ya majaji kutokana na hotuba ya Lissu. Nadhani pitia you tube unaweza ipata.

Kwa kifupi CCM imeharibu nchi hii in it's totality. Prof. Assad alikuwa sahihi aliposema 70 percent ya watu wanaoongoza taasisi hawana uwezo. Majaji ni kundi ambalo halijaachwa. Wengi wameteuliwa kwa malengo maalumu na wengi wakiwa hawana uwezo. Tiganga naona anafit kwenye kundi hili.
 
Kabla hamjajifunua, sheria zinasemaje kuhusu kauli ya jaji?

Kama sheria zinakataza, kwanini mawakili wa utetezi walikaa kimya?
walipuuza ndio maana wakili aliyekua anamwongoza akamwambia shahidi amwangalie jaji anapokua anajibu
 
Wewe na mmeo mlikenua sana Sabaya alipofungwa, sheria ni msumeno tulieni dawa iwaingie
Sijawahi kuona mwana ccm mwenye akili timam never, yaani hujitambui kichwa yako imejaa matope tu, kati ya sabaya na Mbowe nani alilalamikiwa toka mwanzo kuwa anafanya mambo ya hovyo? Yaani wewe unastahili matusi ya jumla "mpumbafu wa kutupwa wewe".
 
Kwa mtazamo wangu niliona ni kama aliridhika na namna shahidi wa kweli anavyotoa ushahidi wake, ilikuwa ni kama dhihaka wa mashahidi wa kubumba wa jamuhuri.
Mkuu; wewe umemwelea Jaji sawia! In short ameshangazwa jinsi shahidi aka mshtakiwa alivyonyoosha maelezo!

Dah; mwamba yule kanyoosha maneno hadi raha! Maandiko hayajakosea yanaposema ulimi wa kweli huthibitika milele tofauti na ule wa uongo ambao ni wa kitambo tu!
 
ukiwa umesimama kwenye ukweli inakua rahisi sana huna haja ya kujipanga maana licha ya kustukiza kwa kufunga ushahidi pia walikuja kwa kuchelewa sana lakini bado wakapigwa na kitu kwenye medula 🤣🤣
Ni kweli i see, the truth is always simple, ukweli hauna manjonjo mengi, ni umenyooka tu, wamepelekewa faya mbaya kabisa leo, yaani ni aibu!
 
Nadhani ameshangazwa na umakini wa shahidi mshitakiwa. Kama shahidi mashitakiwa kaamua kusema ukweli anaoujua yeye, ni lazima wenye hila wajiulize kwanini yuko na mtiririko huo!!

Kinachoshangaza kwa sisi maamuma wa sheria ni kama kuna ushahidi usiokuwa na mashaka kuwa mashitaka yatathibishwa - kina haja gani ya mshitaki kuweka pingamizi la kutaka mshitakiwa asijieleze??!!

Ajabu zaidi sababu wanazotumia kupinga upatikanaji wa document ya shahidi wa mashitaka (mpaka ikapelekea kuhoji kama mahakama imewasiliana na mshitaki kinyume cha taratibu) ndio wanazotumumia kuhoji barua anayotaka kuwasilishwa imemfikiaje mahabusu asiyekuwa huru!! Wanasisitiza hata kuhusu chain of custody ni shida, jambo ambalo hawakuonesha ni shida upande wao.

Leo wanasema Kibatala ni wakili wa mshitakiwa wa nne (Mbowe) hivo hakupaswa kuandika barua. Anasahau mawakili hawa hawajiwakilishi bali kampuni zao kama wao wasiviwakilisha isipokuwa serikali! Wanasahau hawajapinga Kibatala kuhoji mashahidi wao ambao walikuwa wanatoa ushahidi kuhusu walivowakata washitakiwa 1-2 na wala sio hata 3.

Mawakili wa serikali wameshindwa hata kutambua kuwa hata wao hawana mawakili dhidi ya mshitakiwa mmoja mmoja. Wamesahau washitakiwa wote wako katika kesi moja 16/2020 na wote wanashitakiwa kwa makosa yanayofanana isipokuwa mmoja kuhusu silaha na risasa!!
Inategemea wakili alijitambulisha anamuwakilisha nani.Ikiwa alijitambulisha kumwakilisha mshitakiwa mmoja na ipo kwenye kumbukumbu wapo sawa.Lakini kama alijitambulisha mwanzo wa kesi kama anawakilisha watuhumiwa wote basi itakuwa ni makosa
 
Rais aache mambo ya kupoteza muda kwa kesi za kihuni na Badala yake afanye mambo yenye tija kwa Taifa
1637855130871.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Leo Jaji kaongea hayo maneno! Je wanasheria kwa uelewa wenu hayo maneno yanaweza kuja kutumika kukatiwa rufaa au kwa sasa hivi kumkataa Jaji?

View attachment 2023472
Huyo ni hakimu wa ngazi ya diploma,anapaswa kuendesha kesi za ugoni,wizi wa mifugo kwenye mahakama ya mwanzo..magu aliwapa ujudge mahakimu wajinga kma hawa ili wamsaidie kutoa hukumu za wapinzani
 
Sheria haina kitu inaitwa kupuuza!

Huoni aligundua kosa lake ndio maana akamlekebisha shahidi!
sawa tuchukue shahidi alikua anapewa majibu.
je yalikua yanatoka wapi na kwa nani
je kwa mazingra ya kotini inawezekana kupewa majibu bila watu wengine kuona aone jaji tu?
 
Mkuu; wewe umemwelea Jaji sawia! In short ameshangazwa jinsi shahidi aka mshtakiwa alivyonyoosha maelezo!

Dah; mwamba yule kanyoosha maneno hadi raha! Maandiko hayajakosea yanaposema ulimi wa kweli huthibitika milele tofauti na ule wa uongo ambao ni wa kitambo tu!
Amina Mkuu
 
Wadau wengi sana wamejitokeza kuhoji uadilifu wa Jaji anayeendesha kesi inayomkabili Mbowe na wenzake watatu , kauli aliyoitoa Mahakamani iliyojaa uongo ya Kwamba Shahidi aliyekuwa anahojiwa na Mawakili wa Utetezi Mbele yake na mbele ya umati wa watu , komando Ling'wenya huenda alipewa majibu ya maswali aliyokuwa anaulizwa , imeleta Taharuki kubwa na imethibitisha mashaka ya siku nyingi kwamba huenda Jaji Tiganga yuko upande wa Jamhuri .

View attachment 2023342
Huyo Jaji Mungu anamwadhibu azidi kufanya vitu vya ajabu bila yeye kujua. Ni ktk njia ya kuiaibisha Jamhuri
 
Impartiality of a judge

It states that impartiality is essential to the proper exercise of the judicial office. Therefore a judge should make sure that his behaviour in court and in his private life maintains and enhances the public´s confidence in the impartiality of the judge and the judiciary. duties of his office.

Sasa Jana Jaji Tiganga amevunja kanuni hiyo kwa kusema kuwa shahidi wa utetezi anapewa majibu! Comment hiyo angelikaa nayo moyoni ingawa kimsingi hata moyoni mwake inabidi asiijenge dhana hiyo ispokuwa atakapokuwa anafanya analysis of evidence with strong reasons to believe so!
 
Ma judge ni watu wanaoheshimiwa sana na hawatakiwi kuwa na mazoea sana na watu wa nje mbali na familia na wafanya kazi wenzao.

Mahakamani huwa kuna canteens zina zinaandaa chakula chao. Kuanzia chai asubuhi, mchana na evening tea. Nyumbani wanakua na housekeepers chef, chauffeured car etc.

Haya yote wanafanyiwa ili watoe hukumu ya haki na wasionekane kirahisi kuweza kupokea rushwa.
 
Back
Top Bottom