Kauli ya kuonja sumu kwa ulimi ni zaidi ya udikteta

Kauli ya kuonja sumu kwa ulimi ni zaidi ya udikteta

Mkuu moja ya silaha wanayoitumia kudhoofisha upinzani miaka yote ni pamoja na kupandikiza mamluki kwenye nyadhifa za juu za uongozi ili kuvuruga mambo hasa pale upinzani unapokuwa tishio..

Mbinu nyingine ya CCM ni kuhakikisha wanaitumia dola kutisha viongozi wa upinzani ikiwa ni pamoja na kukata mianya yao ya kuingiza fedha, kupandikiza kashfa ili kuwachafua kwenye jamii, kubambikiza kesi ili kuwanyima uhuru nk..

Kuwa kiongozi kwenye upinzani unahitaji uwe na uwezo kifedha kulisha familia na ndugu zako, kusomesha watoto wako, unahitajika pia kuwa na Afya njema kukabiliana na mikikimikiki, uwe unaakili za kimjini mjini, uwe mafia kiaina, usiwe mnafiki, usiwe mtu wa kuyumbayumba, uwe na elimu ya wastani, uwe jasiri.. SIASA ZA AFRICA ZINAHITAJI WATU WA HIVYO NA KWA MBOWE SINA SHAKA...

Sina tatizo na utetezi wako maana umeshiba utetezi wenye mashiko, ila mimi sijawahi kuamini kwenye uwezo wa mtu kukaa madarakani zaidi ya miaka 10 madarakani. Hivi akifa leo ndio chama basi? Siamini katika uimara wa mtu, bali naamini katika uimara wa taasisi.
 
Mleta mada uliisikia hiyo kauli ikitolewa na Mbowe au umeichukua mdomoni mwa Sumaye?
Ni vyema ukajiridhisha kuliko kuandika kiushabiki kama unavyofanya? Anyway huenda ndio akili fupi za kiushabiki zinakutuma hivyo!
 
Wanasiasa hawana tofauti sio chadema ,ccm au ACT .. wote ni wachumia tumbo tu..
Kama huna unachogain kwenye siasa ni bora uende kwenye uzi wa kula tunda kimasihara kuliko ushabiki maandazi wa siasa za bongo.
Kabisa, wanajitutumua ni magwiji wa demokrasia kumbe nao ni mzao ule ule wa mama Afrika, nadhani tuwe na mfumo wetu wa kidemokrasia uliozaliwa kwenye mazingira yetu. Afadhali kidooogo ndani ya CCM kuna heshima ya kupokezana kijiti cha uongozi ndani ya chama...CDM sijaona hata chembe ya wanayoitaja ama kuitekeleza inayoitwa demokrasia
 
Kabisa, wanajitutumua ni magwiji wa demokrasia kumbe nao ni mzao ule ule wa mama Afrika, nadhani tuwe na mfumo wetu wa kidemokrasia uliozaliwa kwenye mazingira yetu. Afadhali kidooogo ndani ya CCM kuna heshima ya kupokezana kijiti cha uongozi ndani ya chama...CDM sijaona hata chembe ya wanayoitaja ama kuitekeleza inayoitwa demokrasia
Huu ndio ukweli mchungu ambao wapinzani hawataki kuusikia...
Hata kama jambo la uenyekiti wa chama ni internal affairs..lakini chama kinachojinadi kinafuata demokrasia inabidi kiwe cha mfano...
 
Uwezo wa kupata viti vya kutosha tunao na uhakika huo upo, tena sio viwili tu bali vya kumwaga. Ila huo uchaguzi wa Magufuli ni sawa na kupindua nchi, kiongozi anayeyejisifia kuongoza chama imara ananajisi box la kura ili wagombea wake wapite bila kupigiwa kura zaidi ya 80%, hapo unaweza kusimama na kuongea mbele ya wanaume kwamba wapinzani hawatapata hata viti viwili? Kwenye serikali za kijeshi kina uchaguzi?

Kosa halifutwi kwa kutaja kosa la mwingine; kubali kwanza ugonjwa uliopo ndani ya chama chako;

Listen your opponents' logic to understand not to reply
 
then unakanusha mfano wako wa shetani ulimaanisha ccm... see tricky trucky[emoji1787][emoji1787]
Tafuta popote nilipowahi kutoa utetezi kwamba cdm wakifanya kosa ni sawa kisa ccm pia hufanya kosa kama hilo. Huwa sitoagi utetezi wa kidhaifu hivyo. You are out of context sir.
 
Chadema ni genge la wakora,wakuogopwa kama ugonjwa wa ukoma,RIP Chacha Wangwe
Ninashangaa chama kinachojiita cha ki-demokrasia, kiongozi wao mkuu anatishia wenzake kwamba wasionje sumu kwa ulimi linapokuja suala la kugusa maslahi yake ndani ya chama.

Ghafla maswali machache yanaibuka:

  • Hicho kikao kilikuwa cha maadui ama ndugu zake katika chama? Kama ni wanachama wenzake, lugha yake kwa adui inakuaje?
  • Kama anafikia kusema hayo wakati hana dola vipi akipata usukani wa vyombo vyote vya dola?
  • Kama anatishia yeyote anayesogelea nafasi yake ambayo ni ndogo tu ya uongozi wa chama, vipi akipewa UAMIRI JESHI MKUU WA MAJESHI YOTE NCHINI?
  • hawa sio wale wanaopiga kelele kila siku kwamba chama tawala hakina demokrasia, wao wanaonesha asubuhi ipi kama mfano wa kuigwa? mbona kwao ni usiku linapokuja suala la uhuru wa kuomba nafasi yoyote ndani ya chama?
  • Hawa sio wale tunaosema ni mbadala wa chama tawala, sasa mbona ni dead-brain katika tabia asili za kidemokrasia?

Kuukubali upinzani Tanzania kwa sasa ni janga ambalo sio tu litapelekea kwenye siasa za kikanda na kikabila, bali zitaua kabisa spirit ya umoja na maendeleo kwa Taifa letu.

Heri tubaki na CCM sababu licha ya mapungufu, wana msamiati wa maendeleo, umoja na amani kwenye kutamka na kutekeleza wanayoamini.
 
Bwana Mbowe aliongea katika mkutano wa Chadema wa Kanda ya Kaskazini kuwa haoni mtu wa kumuachia chama kwa kuwa kiti cha uenyekiti wa Chadema Taifa ni sumu, haipaswi kuonjwa. Nimetafakari sana juu ya kauli yake ambayo pia imemtia hofu Sumaye na kuamua kujiondoa Chadema. Najaribu kujiuliza, kama Mbowe anaona uenyekiti wa chama chake tu ni sumu haupaswi kuonjwa, vipi kuhusu Urais wa nchi?
 
Vyama vya upinzani ni kwa ajili ya kuichangamsha ccm isilale

Na sio kuongoza Nchi hiyo haitatokea
 
Bwana Mbowe aliongea katika mkutano wa Chadema wa Kanda ya Kaskazini kuwa haoni mtu wa kumuachia chama kwa kuwa kiti cha uenyekiti wa Chadema Taifa ni sumu, haipaswi kuonjwa. Nimetafakari sana juu ya kauli yake ambayo pia imemtia hofu Sumaye na kuamua kujiondoa Chadema. Najaribu kujiuliza, kama Mbowe anaona uenyekiti wa chama chake tu ni sumu haupaswi kuonjwa, vipi kuhusu Urais wa nchi?
Dalili ni kwamba akiwa rais atajimilikisha kiti
 
Chadema ni kibubu cha kudunduliza pesa za ruzuku na makato ya wabunge kwaajiri ya mbowe anae bisha aje hapa
 
KUNA KILA DALILI NA KUNA KILA AINA YA USHAHIDI KUWA MBOWE ANAHUSIKA KATIKA KUPIGWA RISASI KWA MH TUNDU LISU.SERIKALI KAMATENI MBOWE NA MUANZE KUMSHUGHULIKIA MARA MOJA BILA TASHWISHWI NA BILA KUPEPESA MACHO.
K
 
Sasa mwanaume mzima unaitisha vyombo vya habari unasema umeambiwa sumu hailambwi kisha unajitoa kwenye chama, angeambiwa alambe sumu si angehama nchi? Mngemuuliza Sumaye toka amekwenda cdm amefungua matawi mangapi ya cdm mpaka autake uwenyekiti wa cdm? Mtu anasema hana tamaa ya madaraka lakini ndani ya miaka minne anataka uwenyekiti, kama sio wendawazimu ni nini?

Lile kosa alilolifanya Mbowe la kumpa nafasi yule mzee mwingine tapeli toka ccm, kugombea urais mpaka saa bado tuna hasira nalo, saa hii huu mzigo mwingine nao unataka uwenyekiti, ili iweje kwa mfano? Mnaweza kupiga propaganda mtakavyo lakini hakuna yoyote anayemtaka Sumaye. Sio wote tunamfagilia Mbowe kuendelea kuwa mwenyekiti wa cdm, lakini hatuko tayari kuona takataka yoyote toka ccm inapewa madaraka makubwa ndani ya cdm. Wao warudi ccm wakaunge mkono juhudi za Magufuli.
Suala sio Sumaye, kama jamaa anatema sumu ni hatarr kwa kila mwenye mawazo ya kutaka u'enyekiti
 
Back
Top Bottom