Kauli ya Lissu ya Rais Mzanzibar ni matokeo ya kufumba masikio Tanganyika kuwa na Serikali yake na viongozi wake watakaoamua mambo yao, asilaumiwe!

ha haa! yaani siku zote nyinyi muwe watawala sisi tuwe watawaliwa, unadhani hiyo ni sawa?
 
Mbona huyo Mwinyi amezikwa Zanzibar, na kijana wake ni Rais huko pia.
Inakuajee hapoo??
si ni CCM (Magu) ndiyo wamemuweka madarakani? Na huyu Mheshimiwa si aliwahi kuwa mbunge wa Mkuranga baadae ndiyo akaondoka na kwenda kupewa jimbo Zanzibar, au umesahau hiyo?

Wacha tunyamaze tu.
 
Huko kwenye ardhi ni mbali sana, hata ateue mtu wa bara akawe DC Unguja tu
 
Yeah,kuna maafisa afya wa kiunguja huku Tanganyika wakati huo afya si swala la muungano
 
Zanzibar imeunga na Tanganyika, katika porojo lako lote hili haukutaja neno Tanganyika hata mara moja. Sijajua unazungumzia muungano gani, laiti ungetumia akili kidogo tu basi ungelijua kutokuwepo Tanganyika hapo ndio shida zote zinaanzia. Mitano tena mama, mpaka waseme. Akili nyingi mbele kiza, Watanganyika tulieni acheni kujazana ujinga.
 
Ukiona hoja nzito kama za Tundu Lissu , tena za Kisheria zinajibiwa na Nape Mnauye .. ujue kitu kimegonga ! Nape Ndio Think Tank ya CCM kujibu hoja nzito za Kisheria ! Zingekuwa ni hoja nyepesi AG angejibu Kwa niaba ya Serikali!
 
Lissu anahitajika kushughulikiwa. Kuchochea ubaguzi haijawahi kuwa uhuru wa kujieleza. Lissu ni kirusi and should be treated as such!
 
kama kuna kitu kinaitwa kero za muungano, ulishawahi kusikia wapi kuna kero ya watanganyika? yaani ni kama mchepuko vile, kero zote ni zao, sisi hakuna hata tunacholalamika, wakati hakuna hata tunachofaidika. wanini sasa hawa?
 
Hii kitu imeniuma sana
Nilikuwa timu Mama sana . Kitendo cha TPA NA WAMASAI, imebidi nirudi nyuma

Watoto Zake na jamaa zake kawaingiza sana kwenye UDC na UDED, anaamini watanganyika hatuoni na kujua
Bahati mbaya historia hiyo ya chifu Hagaya itabaki kwenye kumbukumbu kama historia ya chifu Mangungo.
 
Rais Samia aliisha sema yeye hana kabila bali ni Mzanzibar. Nape unapojibu hoja nenda na context ya mazingira ya sasa kipindi cha siasa za akina Malechela miaka ya 80 imebadilika mno
Kwani kuitwa mzanzibar ni dhambi?
 
Ni Muungano wa kipuuzi kabisa. Rais wa JMT ana mamlaka ya kila kitu kwa Tanganyika, hata yasiyo ya Muungano, ila kwa Zanzibar, Rais wa JMT hana chake, isipokuwa kwa mambo ya muungano tu!!
Tanganyika imevaa koti la muungano na Rais wa muungano ni mzenji poleni sana
 

Kama kweli uzanzibari wake ndio uliomfanya agawe bandari na mbuga kwa waarabu, wakati anafanya hayo
Kwanini Serikali ilimuachia? kuanzia Bunge mawaziri wakurugenzi amabao 95% ni watanganyika?
Kwa nini chama chake cha CCM kilimuachia ambacho zaidi ya 90% ya viongozi wake na wafuasi wake ni watanganyika?
Kwanini JWTZ ilimuachia wakati zaidi ya 90% ni watanganyika?
Na kwanini TISS walimuachia ambao nao zaidi ya 90% ni watanganyika?

Mkuu munachokifanya ni kueneza chuki, nchi nyingi ambazo leo hazikaliki kwa civil wars zilianza na chokochoko kama hizi.
 

Katika orodha ya mambo ya muungano Ardhi ya tanganyika hakuwemo ni nani aliengiza katika muungano? Na kwa nini Alifanya hivo?
 
Shaka Hamduni Shaka
 
Waimbaji wa mapambio hili pambio la Uzanzibar wa mkuu mbona kama hamlipendi vile. Ongezeni sauti, watanganyika wasikie vizuri 🤣🤣😂
 
tumewatawalaje sasa? Rais mnae wa kwenu na serikali yenu, sisi tanganyika hatuna rais pia hatuna tulichonufaika kuungana na nyinyi zaidi ya kero makerere ulalamishi na pia sisi watanganyika kupata hasara kuungana na kainchi masikini kasiko na rasilimali yoyote kenye watu wavivu kufanya kazi wenye kupenda misaada.! Sisi tuna kila kitu kuanzia madini aina zote, tuna maziwa na mito na bahari, tuna misitu na mashamba makubwa kujitosheleza, tunawatu wenye nguvu ya kufanya kazi na pia bado tuna maadili na uvumilivu wa kiimani yani mkiristo muislamu na mpagani wote wanachangamana na hakuna shida, halafu imekua vema nyie kutawala ili tuwajue rangi zenu halisi. Ili akija rais mtanganyika jambo la kwanza n kuvunja muungano na kufukuza kila mzanzibari aliyeko tanganyika ili muishi kwa misaada ya hao warabu wenu. Sasa sijui warabu washindwe kupeleka misaada palestina halafu walete zanzibar inafikirisha sana. Yote kwa yote tumewachoka bandari zetu na wanyama wetu wanatuuma sanaa!
 
Nisha uliza swali,lakini mpaka sasa sijapata jawabu nadhani hapa naweza pata jibu la swali langu.

Ni nani aliye iuza Tanganyika na Mali zake zote kuwa za Muungano ?
 
Mkuu heshima kwako.

Serikali ya Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania haiwezi kuwa serekali ya Tanganyika,kwa sababu Tanganyika haipo.Ndio maana ni ngumu kutetea kitu ambacho hakipo.Zanzibar ni rahisi kutetea maslahi yao sababu serikali ya MP ipo kwa ajili ya Zanzibar.

Mimi napenda kujua ni nani aliye iuza Tanganyika yetu na maslahi yetu ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…