Kauli ya Magufuli kuwa Kabudi na Lukuvi hawatagombea Urais haikuwa ya ghafla, ilipangwa siku nyingi na ndio mwanzo wa mgogoro ndani ya CCM

Kauli ya Magufuli kuwa Kabudi na Lukuvi hawatagombea Urais haikuwa ya ghafla, ilipangwa siku nyingi na ndio mwanzo wa mgogoro ndani ya CCM

Kabudi ni Prof. wa Sheria, alipata first class ya LLB pale UDSM, kaenda hadi PhD sheria za kimataifa. Lukuvi "anasema" ana MBA - labda MBA za mtandaoni kama sikosei maana nilisikia sio MBA halisi. Magufuli ana PhD ya chemistry (mambo ya kubangua korosho au kutumia mafuta ya mabangulio ya korosho)

Sasa niambie, yupi kati ya hawa angalau taaluma yake ingempa sifa za kuwa raisi?
Kwa taaluma ya urais (kama ipo) anayekidhi ni Lukuvi, ni mtu anayeweza kusimamia kitu chochote hata kama hajakisomea, alimradi aweze kuzitawala vema rasilimali zilizoko mbele yake kufanikisha malengo yaliyokusudiwa. Hao wa PhD wanaweza kurudi kwenye taaluma za hizo PhDs ndiko wana nafasi ya kung'ara zaidi katika kutengeneza wataalamu wengi wa fani zao.
 
Kwa taaluma ya urais (kama ipo) anayekidhi ni Lukuvi, ni mtu anayeweza kusimamia kitu chochote hata kama hajakisomea, alimradi aweze kuzitawala vema rasilimali zilizoko mbele yake kufanikisha malengo yaliyokusudiwa. Hao wa PhD wanaweza kurudi kwenye taaluma za hizo PhDs ndiko wana nafasi ya kung'ara zaidi katika kutengeneza wataalamu wengi wa fani zao.
Good point. Ila sasa tatizo la Lukuvi ni kwamba hana confidence, na inawezekana ni kutokana na exposure ndogo. Atakuwa mtu wa kukaa ndani tu kama Magufuli.

By the way, katika hizi nchi zetu, kitu kimoja kinachowapa viongozi wetu confidence ya kuwakabili viongozi wa nchi tajiri ni uwezo wa kuongea lugha ya Kiingereza. Upende usipende huo ndio ukweli.

Wewe fikiria, wewe ndio raisi, una wasaidizi wako na Joe Bidden amewatembelea ikulu, kila sentensi Bidden akiongea unamuuliza msaidizi wako jamaa kasema nini? Na kumjibu Bidden unaogopa maana wasaidizi wako wengine wanaongea kiingereza vizuri kukuzidi, unaogopa ku-break mbele yao. Kuomba uongee Kiswahili utafsiriwe unaona aibu maana watu wanajua una PhD kwa hiyo wanategemea lugha ya Malkia ipande. Ni tatizo!

Sasa huyu Lukuvi mzee wa watu kazoea Kihehe kusema tantalizing hawezi anasema tendalizing, pantoni anaita pandoni, tutafika kweli?
 
Most likely ni Hussein Mwinyi.
Jafo atakuwa Waziri Mkuu, na atafaa sana.
CCM wataweka mgombea wa uraisi kutoka visiwani wakijua kwa uhakika kwamba wamekubuhu katika namna mbalimbali za kuiba kura hata washindwe vipi watageuza matokeo. La sivyo siku wanaweka mgombea wa visiwani kuwania uraisi ndio siku upinzani watachukua nchi, maana hata Zanzibar watampigia mpinzani ili akipita avunje muungano
 
Kabudi is very very intelligent. Anajua kujishusha ili akwezwe. Hivyo hiyo yote ni strategy. Nimewahi kuwa na Kabudi. He is very calculating. Hivi unaona mtu kama Kabudi kusema yeye ni mtu wa jalalani inaendana na profiling yake ya kuwa presumptuous, flamboyant, cocky na pompous? Anasema hivyo ili kujijenga. Ni strategy ili kumpa confidence Magufuli kuwa ni kitwana wake na pia kuwafanya watu waone ni mneyeyekevu sana. Ndio maana nikasema Kabudi anaweza kujitoa akili na maarifa (wisdom and intelligence) kwa muda mfupi ili kutimiza lengo la muda mrefu.
Kabudi is very very intelligent. Anajua kujishusha ili akwezwe. Hivyo hiyo yote ni strategy. Nimewahi kuwa na Kabudi. He is very calculating. Hivi unaona mtu kama Kabudi kusema yeye ni mtu wa jalalani inaendana na profiling yake ya kuwa presumptuous, flamboyant, cocky na pompous? Anasema hivyo ili kujijenga. Ni strategy ili kumpa confidence Magufuli kuwa ni kitwana wake na pia kuwafanya watu waone ni mneyeyekevu sana. Ndio maana nikasema Kabudi anaweza kujitoa akili na maarifa (wisdom and intelligence) kwa muda mfupi ili kutimiza lengo la muda mrefu.
Kabudi is very very intelligent. Anajua kujishusha ili akwezwe. Hivyo hiyo yote ni strategy. Nimewahi kuwa na Kabudi. He is very calculating. Hivi unaona mtu kama Kabudi kusema yeye ni mtu wa jalalani inaendana na profiling yake ya kuwa presumptuous, flamboyant, cocky na pompous? Anasema hivyo ili kujijenga. Ni strategy ili kumpa confidence Magufuli kuwa ni kitwana wake na pia kuwafanya watu waone ni mneyeyekevu sana. Ndio maana nikasema Kabudi anaweza kujitoa akili na maarifa (wisdom and intelligence) kwa muda mfupi ili kutimiza lengo la muda mrefu.
Kabudi ni useless, ana vimaneno vya kiji.nga utadhani si mwanasheria, mara heshima ambayo sikustahili, mara umenitoa jalalani!none sense!
 
Good point. Ila sasa tatizo la Lukuvi ni kwamba hana confidence, na inawezekana ni kutokana na exposure ndogo. Atakuwa mtu wa kukaa ndani tu kama Magufuli.

By the way, katika hizi nchi zetu, kitu kimoja kinachowapa viongozi wetu confidence ya kuwakabili viongozi wa nchi tajiri ni uwezo wa kuongea lugha ya Kiingereza. Upende usipende huo ndio ukweli.

Wewe fikiria, wewe ndio raisi, una wasaidizi wako na Joe Bidden amewatembelea ikulu, kila sentensi Bidden akiongea unamuuliza msaidizi wako jamaa kasema nini? Na kumjibu Bidden unaogopa maana wasaidizi wako wengine wanaongea kiingereza vizuri kukuzidi, unaogopa ku-break mbele yao. Kuomba uongee Kiswahili utafsiriwe unaona aibu maana watu wanajua una PhD kwa hiyo wanategemea lugha ya Malkia ipande. Ni tatizo!

Sasa huyu Lukuvi mzee wa watu kazoea Kihehe kusema tantalizing hawezi anasema tendalizing, pantoni anaita pandoni, tutafika kweli?
Lukuvi hana PhD lakini anaongea English vizuri. Nilishamsikia mara kadhaa.
 
Siku Magufuli alipotamka hadharani kwamba Kabudi na Lukuvi hawatagombea uraisi kwa sababu ya umri wao mkubwa, wengine walicheka wakiichukulia kama ni kauli ya ghafla. La hasha, hii ilikuwa ni kauli ya kimkakati ambayo Magufuli alikuwa ameitafakari na kupanga kuisema kabla hata ya kuingia uchaguzi Mkuu.

Ni kauli ambayo iliwashangaza sana Kabudi na Lukuvi, kuwashitua, kuwakatisha tamaa na hatimae kuwaudhi sana. Ilibidi tu wajichekeshe mbele za watu.

Magufuli ameitoa kauli hiyo akiwa amesoma wazi nia za Kabudi na Lukuvi kutaka kuwa maraisi wajao. Ukiangalia kwa makini, Kabudi na Lukuvi wamekuwa waaminifu sana kwa Magufuli, wakiwa nyuma yake kwa 100%, wakimpamba kila wanapopata nafasi, na lengo lao ilikuwa kupata kuungwa mkono na Magufuli ili kuwa raisi awamu ifuatayo. Kuna wakati mtu kama Kabudi anajitoa kabisa maarifa na akili (wisdom and intelligence) ili mradi tu ajiweke upande wa Magufuli na Magufuli amuone ndio Waziri anaefaa kuwa raisi ajaye.

Sasa kwa kauli hii Magufuli amefanya kosa kubwa sana. Ametangaza vita na mgogoro ndani ya CCM katika suala la raisi atakaemrithi. Magufuli ameishaanza kumpigia debe "kijana" anaetaka amrithi, kijana ambae Magufuli ataweza kumtawala (kum-influence) kirahisi wakati amemaliza awamu hii. Na watu wanajua ili Magufuli awe na "mrithi" wa kumtawala, lazima awe ni kijana wake mtiifu kabisa kama vile Makonda, au kijana wa kutoka kanda ya ziwa.

Sasa ndani ya CCM kuna watu wameanza kuliona hilo na hawataki kabisa! Kuna watu wanaona Lukuvi au Kabudi ndio mawaziri "wenye hekima na busara" wanaofaa kumrithi Magufuli.

Magufuli amekuwa na haraka mno kuanzisha vita ya wa raisi ajayo, akidhani kuwakatisha tamaa mapema Kabudi na Lukuvi itasaidia kuwaondoa uwanja wa mapambano. Magufuli alipaswa ajifunze toka kwa Kikwete, ambaye alijua kabisa Mwandosya alitaka kuwa kumrithi kiti cha uraisi, na Kikwete akajifanya kumuunga mkono Mwandosya hadi dakika za mwisho kabisa ndio akatoa majina yake mfukoni. Mwandosya akawa amepigwa knock out kwa " sucker punch" hakuamini betrayal ya Kikwete! Sidhani hata kama hata wanasalimiana hadi leo. Kikwete mtoto wa mjini, Magufuli mtu wa kuja, ndio tofauti zao.

Sasa athari za Magufuli kuonyesha karata zake mapema ni kwamba ile support aliyopata toka kwa Kabudi na Lukuvi katika awamu ya kwanza hataipata tena! Hilo ndilo kosa kubwa Magufuli amefanya. Sasa Kabudi na Lukuvi hawatampta tena ile 100% waliyompa huko nyuma. Kibaya sana kinachoweza kutokea ni kwamba wataunda makundi yao ndani ya CCM ya kuwa support, lengo likiwa kupanda mbegu ndani ya watu wa CCM kwamba Magufuli ni kiongozi asie na hekima hata kumuunga mkono juu ya chaguo lake la raisi ajae itakuwa ni kosa kubwa!

Yajayo ndani ya CCM yatafurahisha sana. Mpambano ndio kwanza unaanza!
Kuna memba humu alishaambia akaandika na uzi huu , Mahesabu makali ya Mzee Ally Hassan Mwinyi , mmesahau , alisema wakati wa kikao cha mkutano mkuu kuchagua mgombea urais ccm kuwa rais Magufuri aongeze muda wa miaka mitano , ili mwanae Hussein Mwinyi atimize miaka kumi Zanzibar ili baadaye aje amrithi Magufuri . Haya Sasa mnaiona hii coincidence ?
 
Kabudi is very very intelligent. Anajua kujishusha ili akwezwe. Hivyo hiyo yote ni strategy. Nimewahi kuwa na Kabudi. He is very calculating. Hivi unaona mtu kama Kabudi kusema yeye ni mtu wa jalalani inaendana na profiling yake ya kuwa presumptuous, flamboyant, cocky na pompous? Anasema hivyo ili kujijenga. Ni strategy ili kumpa confidence Magufuli kuwa ni kitwana wake na pia kuwafanya watu waone ni mneyeyekevu sana. Ndio maana nikasema Kabudi anaweza kujitoa akili na maarifa (wisdom and intelligence) kwa muda mfupi ili kutimiza lengo la muda mrefu.

Kabudi hana akili hiyo, labda kama unacheza mind games.
 
Very sad. Wamekosa sifa gani? Kwani katiba inasema anayezidi umri gani ndio asigombee urais?
Inasikitisha sana rais wa nchi badala ya kuchaguliwa na wananchi, tunachaguliwa na Mwenyekiti wa CCM

Magufuli ni mtu wa ajabu sana.

Anahimiza watu kwamba uchaguzi umekwisha, tuchape kazi sasa.

Halafu hapo hapo anaanzisha habari za nani atakuwa rais wa kumrithi na nani hawezi kuwa rais, kimsingi anaanza kampeni za urais tena hata kabla ya kufanya kazi ya urais kwa mwezi tu!

CCM huwa wana tabia ya kuanzisha vigezo ambavyo havipo katika katiba ili kumkata mtu fulani.

Kwa mfano, walipotaka kumkata marehemu Samwel Sitta kwenye Uspika wa Bunge, walileta kigezo ambacho hakipo kwenye katiba yoyote, kwamba wanataka Spika mwanamke.

Walipotaka kumkata Lowassa, walileta kigezo cha umri.

Na sasa Magufuli anaendeleza tu kigezo hiki cha umri ambacho hakipo katika katiba yoyote.

Mimi si mtetezi wa Kabudi wala Lukuvi, lakini, nchi hii marais hawachagui rais ajaye.

Ndiyo maana Nyerere hakumpata rais aliyemtaka, Salim Ahmed Salim.

Ndiyo maana Mkapa hakumpata Dr. Omar Ali Juma wala Abdallah Kigoda.

Ndiyo maana Kikwete hakumpata Membe.

Na zaidi, Magufuli akijifanya kuanza kumtangaza mgombea anayemtaka na kulazimisha awe rais ajaye, kama watu hawamtaki, watu wanaweza kumfanyia kitu mbaya kama alivyofanyiwa Dr. Omar Ali Juma.

Nakumbuka nilikaa na mtoto mmoja wa familia ya Mkapa, aliniambia "huyu Dr. Omar ndiye rais anayefuatia wa Tanzania". Hizo habari zilikuwa za kutoka nyumbani kwa Mkapa kabisa.

Kilichofuatia ni historia.
 
Exactly! Kama ambavyo Kikwete alijua wazi Mwandosya akimrithi uraisi hatakaa amsikilize kamwe, ndivyo Magufuli anajua kamba Kabudi au Lukuvi wakimrithi uraisi hawatakaa wamsikilize kamwe! Kwa hiyo kama vile Kikwete alijua Membe ndie atamwezesha ku-prolong enzi yake, ndivyo ambavyo Magufuli anatafuta kijana wa ku-prolong enzi zake, ila jina bado kaliweka mfukoni.
Singida labda?.
 
Kumbe kabudi pia nae ni chizi ,kwa kulopoka na kutuchonganisha na wahisani wetu

wadau wa maendeleo wakisusa wawekezaji , watalii na wafadhili wa miradi ya jamii watatoka wapi kama si do haohao anaowatukana

Jeuri zitamtokea puani mwendawazimu huyu
 
Hotuba ya Kabudi aliyotoa kwa wafanya kazi wa mambo ya ndani ina kila namna ya viashiria kwamba ameanza kujitofautisha ili watu waone anaweza kuwa raisi wa namna gani
 
Kumbe kabudi pia nae ni chizi ,kwa kulopoka na kutuchonganisha na wahisani wetu

wadau wa maendeleo wakisusa wawekezaji , watalii na wafadhili wa miradi ya jamii watatoka wapi kama si do haohao anaowatukana

Jeuri zitamtokea puani mwendawazimu huyu
Kama unaongelea aliyosema kwa wafanya kazi wake wa wizara ya mambo ya ndani, lengo lilikuwa ni mbali zaidi. Amejionyesha wazi jinsi gani yeye ni kiongozi bora zaidi hasa katika kushughulika na mambo ya kimataifa, kuifanya Tanzania iheshime nk. Huyu sio yule mtu anaesema nimeokotwa jalalani, ndio maana nikasema huwa anaamua kujishusha ili akwezwe
 
Back
Top Bottom