Kauli ya Magufuli kuwa Kabudi na Lukuvi hawatagombea Urais haikuwa ya ghafla, ilipangwa siku nyingi na ndio mwanzo wa mgogoro ndani ya CCM

Kauli ya Magufuli kuwa Kabudi na Lukuvi hawatagombea Urais haikuwa ya ghafla, ilipangwa siku nyingi na ndio mwanzo wa mgogoro ndani ya CCM

'Fair enough' Mkuu Synthesizer lakini Rais Magufuli hakuangukiwa na ngekewa kama wengi wanavyoamini('at least' yeye ana amini hivyo) lakini aliandaliwa.. Ijapokuwa anaweza asijue moja kwa moja..
Kwa kifupi jaribu kuangalia sheria zilizopitishwa haraka haraka kabla ya uchaguzi wa Rais wa 2015..'statistics act 2013' ,'The Access to Information Act, 2015','Cyber crime act 2015','The media Services Act,2015 etc..
Hapana Mkuu. Hata Mkapa ambaye alikuwa ni rafiki mKubwa wa Magufuli, labda aliona mapungufu fulani ndani ya Magufuli hivyo hakumpa support yote ili kwenye mio za uraisi. Labda pia Mkapa hakutaka kugombana na Kikwete. Ndio maana Magufuli alisema wazi siku zote - hakuna anaemdai katika kuwa kwake raisi, ni juhudi zake peke yake.

Na labda kwa hasira ya Mkapa kutokuwa nae kwenye harakati a kumrithi Kikwete, Magufuli alipokuwa rahisi alikuwa hasikilizi chochote Mkapa alichomshauri. Na wala alikuwa ham-consult. Watu walianza kumlaumu Mkapa kuwa mtu wako Magufuli haambiliki, uwe unamshauri. Mkapa aliweka bayana kwamba hata yeye Magufuli hataki kabisa kumsikiliza, japo ni kweli yeye ndio aliyemfanya afike alipofika.

Ilifikia wakati Mkapa alikasirika akawa hahudhurii function yeyote ya kitaifa.Aliamua kukaa kando kabisa na mambo ya serikali, kama amesusa. Watu wenye busara wakamwambia Magufuli kwamba umeenda mbali sana na Mkapa, mwombe msamaha, huwezi kusahau mlikotoka. Nadhani katika maisha yake Magufuli ya uraisi, ni ushauri huo tu aliowahi kupokea, maana ni kweli alimalizana na Mkapa na Mkapa akawa anashiriki dhifa za kitaifa baada ya hapo.
 
Safu ya CCM 2025
1st preference =Majaliwa
2nd = Jafo
3rd= none
4th= none
Ni zamu ya Rais Muislamu.
Mkuu uraisi wa Tanzania sio uimamu au uaskofu. Sio jambo la zamu kwa mkristo au mwislamu. Tukianza hivyo hatutaishia hapo, tutasema ni zamu ya mwanamke, au Kanda ya Nyanda za juu, au Mchaga, au mwanasheria, nk
 
Swali aliandaliwa na nani?

Sent from my Infinix X653 using JamiiForums mobile app
Mkuu Matola katika kuandaliwa kuna yafuatayo:
Kwanza kunaandaliwa mazingira ya kisheria na kitaasisi ya mtu anayetarajiwa.. haya yalifanyika kabla ya uchaguzi wa 2015
Pili ni sarakasi na minyukano ya ndani ya chama ambaya yalifuatia - kumbuka idadi kubwa ya wagombea wa Urais 2015.
Tatu ni mazingira yaliyoandaliwa kumwangukia aliyeamuliwa..
Kuhusu nani alimwandaa.. jiulize maswali yafuatayo?
Nani walikuwa vyanzo vya haya mazingira? kisheria,kitaasisi.. 'definitely' siyo Rais aliyeko madarakani.. yeye alipewa tu sababu za kawaida za kuwepo kwa sheria zenyewe.. lakini 'central theme'.. asingeijua..
 
Kwa jinsi navyoona kuna uwezekano mkubwa Rais ajaye akawa ni Mwanamama. La hasha Rais atatokea Zanzibar, iwapo rais atatokea CCM.

Kuhusu Rais kutokea Zanzibar, ni suala la Legacy. Ukiangalia mfumo wa uongozi na utawala anaotumia Magufuli unaendana na maono ya mzee Nyerere.

Wakati Nyerere anang'atuka alituachia Mzee Mwinyi wa Zanzibar. Hivyo bila shaka na huyu mtawala atatuachia Mzanzibar Mwengine.

Ikishindikana na kukawa na vita kali kati ya vijana wafuatao CCM, Makamba, Jafo, Mwigulu, Kigwangala, Bashe, na Ndugai. Basi maajabu ya mwanamama kupitishwa na mkutano mkuu wa CCM kwa shinikizo la Mwenyekiti wao.

Above all, Tunaweza kuwa na Rais ambaye hatokani na Baraza la mawaziri kwa mara ya kwanza. Mheshimiwa anaweza kuamka na kuleta jina la mfukoni. Hapa tunaweza kuletewa Mkuu wa mkoa au Katibu wa wizara kama mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM.

Kama hujanielewa. Ki ufupi namaanisha Magufuli hasomeki.
 
Unatakiwa uwe realistic. Angalia historia ya uraisi wa nchi hii kwamba ni Mkapa tu ndie ilipangwa rasmi awe raisi. Uraisi wa Mwinyi ulikuwa accident baada ya kugoma kuchomoa jina lake kumpisha Salim Ahmed Salim - na baada ya wajanja kumwondoa Sokoine kimaajabu; uraisi wa Kikwete ulilazimishwa baada ya kutishia angegombea na upinzani na kuiangusha CCM ikiwa wangemweka Salim Ahmed Salim au Mwandosya; uraisi wa Magufuli alikuwa accident baada ya mgongano wa Kikwete kumtaka Membe na wajumbe kumtaka Lowasa. Hakuna raisi wa kupangwa Tanzania, ilitokea mara moja tu kwa Mkapa, na yeye bila Nyerere Mrema angekuwa raisi.
Ina maana hao wajanja waliomwondoa Sokoine kimaajabu April 1984 walishajua mapema kwamba Nyerere alikuwa na mpango wa kung'atuka Novemba 1985?
 
Kama unaongelea aliyosema kwa wafanya kazi wake wa wizara ya mambo ya ndani, lengo lilikuwa ni mbali zaidi. Amejionyesha wazi jinsi gani yeye ni kiongozi bora zaidi hasa katika kushughulika na mambo ya kimataifa, kuifanya Tanzania iheshime nk. Huyu sio yule mtu anaesema nimeokotwa jalalani, ndio maana nikasema huwa anaamua kujishusha ili akwezwe
Kabudi amehojiwa na Zuhura Yunusi yule mwandishi wa BBC swahili kwe tv inaitwa tanzanite online

ameonyesha hawezi kumudu jaziba yake anashindwa interview mara ya pili huyu hajamasta kwenye wizara yake anabebwa tuu

Hulka yake ya ubabe, maneno yasiyona busara na kuendekeza jazba kunamwonyesha jinsi anavyopwaya.
 
si bora hata lukuvi, huyo kabugi na mimacho yake hata akigombea nani atampigia kura?
 
Kumfananisha Magufuli na salakasi za Mzee wetu wa Msoga wakati wa kumtosa Mwandosya ni kituko ainasafu zao kiuongozi hazishabihiani.

Wakati JK alikuwa mnafiki kwa kuwapaka mafuta kwa mgongo wa chupa asiowataka. JPM hamung'unyi maneno wala kukupa matumaini makubwa ili hali anajua sio chaguo lake. Wasio mfahamu wanadhani huu ni udhaifu au "ushamba" la! hasha hiyo ndio namna yake aliyojipambanua nayo na ikampa kura 12m.
Siasa za Magufuli amezipambanua kiuwazi kila mahali ili asikupotezee muda kuunda makundi au mkururo unaweza kuundwa na viongozi aliowataja ingawa nashawishika kuamini target ya ujumbe alikuwa Kabudi, maana ndio alishaanza kuwashawishi baadhi ya makatibu wakuu... (Wizara nazihifadhi) kuwa anachokishauri kwa mheshimiwa hakipingi! Huu ndio udhaifu wa Kabudi pia anapenda madaraka kwa njia za kubebwa na kulaghai.

JPM kama Mwenyekiti wao wa chama kusema kwake ni kufikisha ujumbe kwenye kambi zote zinazoanza kujiuunda.

Pia fitina zilizokuwepo kwenye baraza lililopita zimesababisha JPM kuwaambia wazi mawaziri waliopita kwa wasiende kwa waganga ilikupata uwaziri maana yake ni moja tu ndani yake kuna wezi na wabadhirifu, kuna waroho wa madaraka na wahudumu uchumi.

Haki ya kikatiba ya raia wa Tanzania mwenye sifa kuomba ridhaa na kuchaguliwa ipo ila ikiwa haki hiyo inatishia utulivu na amani ndani ya chama... Ni wajibu wa chama kutupia mwenyekiti kutuliza hali.

Kabudi na Lukuvi wakiona wamebanwa ili hali uwezo na uhitaji wa wananchi upo kwao sio lazima wabaki CCM ili kuweza wa marais.
 
Acha waambiwe maana hawana msaada wowote kwa taifa
Acha kudaganya umma

Wewe hujui faida na misaada tunayopata kwa wafadhilo, wahisani na wawezeshaji wabia wa maendeleo.

Labda haujui mifumo ya uendeshaji wa nchi maskini
 
Kumfananisha Magufuli na salakasi za Mzee wetu wa Msoga wakati wa kumtosa Mwandosya ni kituko ainasafu zao kiuongozi hazishabihiani.

Wakati JK alikuwa mnafiki kwa kuwapaka mafuta kwa mgongo wa chupa asiowataka. JPM hamung'unyi maneno wala kukupa matumaini makubwa ili hali anajua sio chaguo lake. Wasio mfahamu wanadhani huu ni udhaifu au "ushamba" la! hasha hiyo ndio namna yake aliyojipambanua nayo na ikampa kura 12m.
Siasa za Magufuli amezipambanua kiuwazi kila mahali ili asikupotezee muda kuunda makundi au mkururo unaweza kuundwa na viongozi aliowataja ingawa nashawishika kuamini target ya ujumbe alikuwa Kabudi, maana ndio alishaanza kuwashawishi baadhi ya makatibu wakuu... (Wizara nazihifadhi) kuwa anachokishauri kwa mheshimiwa hakipingi! Huu ndio udhaifu wa Kabudi pia anapenda madaraka kwa njia za kubebwa na kulaghai.

JPM kama Mwenyekiti wao wa chama kusema kwake ni kufikisha ujumbe kwenye kambi zote zinazoanza kujiuunda.

Pia fitina zilizokuwepo kwenye baraza lililopita zimesababisha JPM kuwaambia wazi mawaziri waliopita kwa wasiende kwa waganga ilikupata uwaziri maana yake ni moja tu ndani yake kuna wezi na wabadhirifu, kuna waroho wa madaraka na wahudumu uchumi.

Haki ya kikatiba ya raia wa Tanzania mwenye sifa kuomba ridhaa na kuchaguliwa ipo ila ikiwa haki hiyo inatishia utulivu na amani ndani ya chama... Ni wajibu wa chama kutupia mwenyekiti kutuliza hali.

Kabudi na Lukuvi wakiona wamebanwa ili hali uwezo na uhitaji wa wananchi upo kwao sio lazima wabaki CCM ili kuweza wa marais.
Kwa hiyo alichosema Magufuli dhidi ya Lukuvi na Kabudi ndio msimamo wa CCM yote? Au ni kwamba unachosema ni kuwa anachosema Magufuli CCM lazima wafuate wapende wasipende?
 
Kabudi amehojiwa na Zuhura Yunusi yule mwandishi wa BBC swahili kwe tv inaitwa tanzanite online

ameonyesha hawezi kumudu jaziba yake anashindwa interview mara ya pili huyu hajamasta kwenye wizara yake anabebwa tuu

Hulka yake ya ubabe, maneno yasiyona busara na kuendekeza jazba kunamwonyesha jinsi anavyopwaya.
Nakubali kabisa. Tena Kabudi ni aina ya watu ambao akiwa raisi atajua kwamba yeye ni raisi kwa kuwa anawazidi Watanzania wote akili!
 
Ina maana hao wajanja waliomwondoa Sokoine kimaajabu April 1984 walishajua mapema kwamba Nyerere alikuwa na mpango wa kung'atuka Novemba 1985?
Hewaaa! Actually, kuna watu walimfuata Nyerere kumwambia Sokoine alikuwa hajafa bado, na alikuwa ameuwawa "kimazingira". Hata walimwambia wangeweza kumrudisha na itabidi wafanye haraka kabla waliomchukua hawajamzuru zaidi au kumwondoa akili.

Kuna watu wenye dawa sijui, siku ya kuangalia maiti walisema walikuwa wanamwona yuko hai na wanashituka sana - kama unaweza kuupata huo mkanda utafute!

Wakamwambia kuwa waliofanya hivyo wanajulikana, na kwamba walimfuata Nyerere kumwambia Sokoine alikuwa anavuka mipaka, alitaka kuwaweka ndani mawaziri, na hivyo walihitaji kumdhibiti. Nyerere akawaambia kama mnaweza kumdhibiti mdhibitini, na wao wakaelewa aliwapa go ahead kumwondoa. Sasa aliyesema Sokoine alihitaji kudhibitiwa alikuwa mtu wa karibu sana na Nyerere. Nyerere akauliza, ina maana so and so anahusika pia? Wakajibu ndio. Nyerere akakasirika mno. Huyo so and so alipoenda kujieleza kwa Nyerere alifukuzwa kama mbwa!

Nyerere akawauliza, na tukimrudisha, baada ya kuitangazia dunia kuwa Waziri wetu Mkuu amekufa kwa ajali na tukapokea na salamu za rambirambi, tutaiambia nini dunia, na watatuoana sisi ni taifa la watu wa aina gani?

Akawaambia kama hajafa kabisa basi mmalizieni ili asiumizwe zaidi.
 
Hewaaa! Actually, kuna watu walimfuata Nyerere kumwambia Sokoine alikuwa hajafa bado, na alikuwa ameuwawa "kimazingira". Hata walimwambia wangewea kumrudisha na itabidi wafanye haraka kabla waliomchukua hawajamzuru zaidi au kumwondoa akili.

Wakamwambia kuwa waliofanya hivyo wanajulikana, na kwamba walimfuata Nyerere kumwambia Sokoine alikuwa anavuka mipaka, alitaka kuwaweka ndani mawaziri, na hivyo walihitaji kumdhibiti, akawaambia kama mnaweza kumdhibiti mdhibitini, na wao wakaelewa aliwapa go ahead kumwondoa. Sasa aliyesema Sokoine alihitaji kudhibitiwa alikuwa mtu wa karibu sana na Nyerere. Nyerere anasema ina maana so and so anahusika pia? Wakajibu ndio. Nyerere akakasirika mno. Huyo so and so alipoenda kujieleza kwa Nyerere alifukuzwa kama mbwa!

Nyerere akawauliza, na tukimrudisha, baada ya kuitangazia dunia kuwa Waziri wetu Mkuu amekufa kwa ajali na tukapkea na salamu za rambirambi, tutaiambia nini dunia, na watatuoana sisi ni taifa la watu wa aina gani?

Akawaambia kama hajafa kabisa basi mmalizieni ili asiumizwe zaidi.
Hii chai tamu. Mhudumu aniongezee vitumbua viwili.
 
Kwa hiyo alichosema Magufuli dhidi ya Lukuvi na Kabudi ndio msimamo wa CCM yote? Au ni kwamba unachosema ni kuwa anachosema Magufuli CCM lazima wafuate wapende wasipende?
Sina hakika kama msimamo wa mwenyekiti ndio wa chama... ila nililo na uhakika nalo mwenyekiti akisema wajumbe hawana utamaduni wa kumpinga. Muda ni jibu zuri utayaona.
 
Siku Magufuli alipotamka hadharani kwamba Kabudi na Lukuvi hawatagombea Urais kwa sababu ya umri wao mkubwa, wengine walicheka wakiichukulia kama ni kauli ya ghafla. La hasha, hii ilikuwa ni kauli ya kimkakati ambayo Magufuli alikuwa ameitafakari na kupanga kuisema kabla hata ya kuingia Uchaguzi Mkuu.

Ni kauli ambayo iliwashangaza sana Kabudi na Lukuvi, kuwashitua, kuwakatisha tamaa na hatimae kuwaudhi sana. Ilibidi tu wajichekeshe mbele za watu.

Magufuli ameitoa kauli hiyo akiwa amesoma wazi nia za Kabudi na Lukuvi kutaka kuwa Marais wajao. Ukiangalia kwa makini, Kabudi na Lukuvi wamekuwa waaminifu sana kwa Magufuli, wakiwa nyuma yake kwa 100%, wakimpamba kila wanapopata nafasi, na lengo lao ilikuwa kupata kuungwa mkono na Magufuli ili kuwa Rais awamu ifuatayo. Kuna wakati mtu kama Kabudi anajitoa kabisa maarifa na akili (wisdom and intelligence) ili mradi tu ajiweke upande wa Magufuli na Magufuli amuone ndio Waziri anaefaa kuwa Rais ajaye.

Sasa kwa kauli hii Magufuli amefanya kosa kubwa sana. Ametangaza vita na mgogoro ndani ya CCM katika suala la Rais atakaemrithi. Magufuli ameshaanza kumpigia debe "kijana" anaetaka amrithi, kijana ambae Magufuli ataweza kumtawala (kum-influence) kirahisi wakati amemaliza awamu hii. Na watu wanajua ili Magufuli awe na "mrithi" wa kumtawala, lazima awe ni kijana wake mtiifu kabisa kama vile Makonda, au kijana wa kutoka kanda ya ziwa.

Sasa ndani ya CCM kuna watu wameanza kuliona hilo na hawataki kabisa! Kuna watu wanaona Lukuvi au Kabudi ndio Mawaziri "wenye hekima na busara" wanaofaa kumrithi Magufuli.

Magufuli amekuwa na haraka mno kuanzisha vita ya wa Rais ajae, akidhani kuwakatisha tamaa mapema Kabudi na Lukuvi itasaidia kuwaondoa uwanja wa mapambano. Magufuli alipaswa ajifunze toka kwa Kikwete, ambaye alijua kabisa Mwandosya alitaka kuwa kumrithi kiti cha Urais, na Kikwete akajifanya kumuunga mkono Mwandosya hadi dakika za mwisho kabisa ndio akatoa majina yake mfukoni. Mwandosya akawa amepigwa knock out kwa " sucker punch" hakuamini betrayal ya Kikwete! Sidhani hata kama hata wanasalimiana hadi leo. Kikwete mtoto wa mjini, Magufuli mtu wa kuja, ndio tofauti zao.

Sasa athari za Magufuli kuonyesha karata zake mapema ni kwamba ile support aliyopata toka kwa Kabudi na Lukuvi katika awamu ya kwanza hataipata tena! Hilo ndilo kosa kubwa Magufuli amefanya. Sasa Kabudi na Lukuvi hawatampta tena ile 100% waliyompa huko nyuma. Kibaya sana kinachoweza kutokea ni kwamba wataunda makundi yao ndani ya CCM ya kuwa support, lengo likiwa kupanda mbegu ndani ya watu wa CCM kwamba Magufuli ni kiongozi asie na hekima hata kumuunga mkono juu ya chaguo lake la Rais ajae itakuwa ni kosa kubwa!

Kwangu mimi, Hotuba ya Kabudi aliyotoa kwa wafanya kazi wa mambo ya ndani ina kila namna ya viashiria kwamba ameanza mapambano na kujitofautisha ili watu waone anaweza kuwa Rais wa namna gani!

Yajayo ndani ya CCM yatafurahisha sana. Mpambano ndio kwanza unaanza!
Thubutu yao...kwani hawapendi kutangulia kwa malaika?
 
Hewaaa! Actually, kuna watu walimfuata Nyerere kumwambia Sokoine alikuwa hajafa bado, na alikuwa ameuwawa "kimazingira". Hata walimwambia wangewea kumrudisha na itabidi wafanye haraka kabla waliomchukua hawajamzuru zaidi au kumwondoa akili.

Wakamwambia kuwa waliofanya hivyo wanajulikana, na kwamba walimfuata Nyerere kumwambia Sokoine alikuwa anavuka mipaka, alitaka kuwaweka ndani mawaziri, na hivyo walihitaji kumdhibiti, akawaambia kama mnaweza kumdhibiti mdhibitini, na wao wakaelewa aliwapa go ahead kumwondoa. Sasa aliyesema Sokoine alihitaji kudhibitiwa alikuwa mtu wa karibu sana na Nyerere. Nyerere anasema ina maana so and so anahusika pia? Wakajibu ndio. Nyerere akakasirika mno. Huyo so and so alipoenda kujieleza kwa Nyerere alifukuzwa kama mbwa!

Nyerere akawauliza, na tukimrudisha, baada ya kuitangazia dunia kuwa Waziri wetu Mkuu amekufa kwa ajali na tukapkea na salamu za rambirambi, tutaiambia nini dunia, na watatuoana sisi ni taifa la watu wa aina gani?

Akawaambia kama hajafa kabisa basi mmalizieni ili asiumizwe zaidi.
Hichi kisa kina chekesha sana
 
hiiiii (in magu voice) kutatokea surprise kubwa sana hadi watu watashangaa,majina yapo mfukoni bado wanabodi ngojeni kidogo vuteni subra mtajionea wenyew tu
 
Back
Top Bottom